Data: Bei za mafuta DRC, Burundi, Rwanda, Zambia ziko chini

Data: Bei za mafuta DRC, Burundi, Rwanda, Zambia ziko chini

Uko sahihi kabisa, tunasema serekali ipunguze matumizi yasiyo ya lazima, mfano hayo mashangingi ya nini wakati hali ni ngumu? Bunge linaendelea kukaa kwanini wakati hawana jipya wanalojadili, kwani kila kitu cha serekali wanapitisha kwa 100%. Rais naye kila siku kiguu na njia na msafara kama anaelekea peponi. Kwanini mambo hayo yasipungue au kusimama kabisa?
Wivu tu unakusumbua[emoji23][emoji23]
 
Waache watambe tu hata enzi za yule muovu mlitamba sana, kutesa kwa zamu na tutaupiga mwingi hadi tufidie gepu lote alotupiga yule muovu.
Bora yule muovu aliewakata mikono wezi 200 na ku favour wanyonge million 59.8 kuliko malaika anaekumbatia wezi 200 na kunyanyasa wanyonge million 59.8
 
Dah jamani hii vita ya ukraine imetukalia vibaya sisi tu au hawa jirani zetu wao wanachimba mafuta? si wanapitisha mafuta hapahapa bandarini kwetu jamani?

Tunaongelea vita lakini hawa jamaa wa Drc congo wana vita na waasi miaka 25 sasa , tunahitaji maombi maalumu nchii hii hali tete sana

View attachment 2214602

View attachment 2214603
Tuqchane na data za kwenye makaratasi tuje kwenye uhalisia..

Je umeona madereva wanaoishi maeneo ya mipakani wakivuka mpaka kwenda kujaza mafuta Nchi hizo jirani?

Maana kipindi Mafuta yamepanda tukiona kule Tunduma,Namanga nk madereva wa Tanzania wqkienda kujaza mafuta huko,sasa mbona saizi hawavuki? Kwamba hawataki bei za chini za mafuta?

Namba na uhalisia huwa hazidanganyi kama siasa za Jiwe.
 
chawa ,embu kuweni na huruma basi jamani, khaaa ni kodi inapatikana tu kwenye mafuta? ili ku maintain life style ya kulamba asali ya maboss zenu...huu ni ubinafsi wa hali ya juu ,kikosi kazi mmejazwa social media kila platform kuwakumbusha wanuka majasho kwamba ni haki yao kupigika na kuishi maisha magumu..laana iwe kwenu
Kutesa kwa zamu, harudi tena yule, mkiambiwa katiba mpya ndio dawa mnajifanya hamuelewi sasa isomeni namba.
 
Wewe jamaa ndy Hamnazo kabsaa..kumbe Rea serkali inatulamba kotekote, mana wananchi tukinunua umeme tu...umelambwa hela,halafu hili la kuwekwa makodi mengi si ndy waoo?kwanini waliweka makodi mengi kwenye bidhaa mkakati kama hyoo? Kuna majizi manyonyaji yanatupopoa wananchi bila huruma hapa. Kwa nchi nilizotembea hii nchi ndy inakodi nyingi sana. Serikali inakusanya hela nyingi sana ila znaenda mifukoni mwao hawa WAJANJA. mafuta futa kodi halaf punguza mianya ya Upigaji basi.
Bila kusahau na mishahara ipunguzwe kwa kila idara za nchi serikali na binafsi.
 
Swala la wizi lipo duniani kote, hata huko china m'badhirifu wa fedha za uma ananyongwa lkn bado wapo wezi,
Tatizo mkiona miradi imepungua kasi mnalalamika mkiambiwa mlipe kodi mnahisi mnaonewa,

Mbona magu alituingizia kodi za magari kwenye mafuta hamkulalamika hivi? Yaani magari yote sasa hivi hayalipi kodi kila mwaka mzigo wote tulibebeshwa wananchi maskini kwa kua aliogopeka hakuna aliepiga kelele kukemea lile leo wamenogewa ndio mnatokwa povu[emoji23][emoji23]
Mama piga kazi adi mafuta yafike elfu 6 na huko ili mjue sisiemu sio chama kinachofaa kuongoza nchi.
Aliingiza shilingi ngapi mzee mbona unaongea kama choko wewe?

Huoni ilisaidia kiasi gani, imagine gari iliopaki unahesabiwa hujalipa fee ya barabarani jamaa akaamua kuweka TZS50 iwe kama mchango kwenye mafuta which means ni siku ukiendesha gari ukaenda sheli kujaza wese ndio unalipia hio 50 tsh.

Hata muongee utumbo kiasi gani Magu aliwa outsmart watanzania wengi vilaza. Ndio maana mlimuua kumamaq zenu ila ukweli utabakia ukweli.
 
Hii sio dharula mzee, hata USA bei iko juu, hii ishu ya bei iko Dunia nzima kutokana na uhaba wa bidhaa yenyewe. Bei ya mafuta ni kitu kinachopanda na kushuka, huwezi toa kodi eti kisa mafuta yamepanda, kodi itaendelea kukusanywa vile vile.

Mtakubali kupunguzwa mishahara au kupunguzwa dawa na vifaa tiba hospitalini pia??

Tunapaswa kutoa elimu juu ya namna uchumi unaenda, hili si suala la CCM au CHADEMA au ACT ni national matters, hivyo lazima tuelewe chanzo chake na effect yake. Ni suala la muda tu kila kitu kitarudi kwenye hali yale ya kawaida.

Tusiwe watu wa kulalamika sana, Price ya mafuta sio kwamba ifanane kwa nchi zote, hata hapa Afrika mashariki, bei ya mchele iko tofauti baina yetu, ni kutokana na uwekezaji nk.

Kwa mfano Kenya wao hutumia kiasi kikubwa mno cha mafuta ukilinganisha na sisi hivyo lazima watapata punguzo la bei as we know kadiri unavyonunua mzigo mkubwa ndipo disccount hupatikana.
Hujui unachoandika japo unaonekana una confidence sana.

Kama hii hali ya uhaba wa mafuta sio ya dharura ni kitu gani? simply, unasema sio dharura ili kuficha uozo wa serikali kwenye kukabiliana na hii hali.

Zile nchi wanaoona hii hali ni ya dharura wao tayari wameshatenga kiasi fulani cha pesa kwa ajili ya kukabiliana nayo. Hawa hawajapunguza vifaa tiba wala mishahara ya wafanyakazi kwenye nchi zao, ni viongozi wanaojielewa tofauti na haya maboga yetu.

Wewe unapewa option za kukabiliana na hali hiyo hapa kwetu kwasababu mpaka sasa serikali yetu bado imelala, unasema kodi lazima iendelee kukatwa, na mashangingi lazima yaendeshwe, poor you!.

Hii yako ni thinking ya kifisadi kabisa, na sitashangaa kama upo huko wizarani kwenye ile bodi ya wezi.
 
Bora yule muovu aliewakata mikono wezi 200 na ku favour wanyonge million 59.8 kuliko malaika anaekumbatia wezi 200 na kunyanyasa wanyonge million 59.8
Wezi gani aliowakata mikono? Zaidi ya kutesa na kuwapeleka kusikojulikana,
Siasa mbaya sana mliaminishwa kuna mafisadi na mahakama yake yaja lkn hata mahakama yenyewe haikuonekana, hakumfunga hata mmoja kwa ufisadi afadhali hata kikwete aliwafunga kina yona basi mramba
 
Mkuu unaandika content nzito mno ambayo watanzania wengi aidha kwa kutokwenda shule au kwa ujinga wa kuzaliwa hawaelewi.

Mpuuzi mmoja anakuambia eti mbona nchi x au y ni bei rahisi kuliko sisi na yanapita kwetu.
Haangalii kodi tulizoziweka humo ili kukimbiza miradi ya REA na Reli na TARURA
Mtu huyo huyo kesho kodi hiyo ikiondolewa na miradi ya REA na Reli ikafia mbali ataandika tena kulalamika

Kwa muktadha huo kuna sehemu nilikuwa nakubaliana na Magufuli, kwamba ng'ombe kama hawa ni wa kuburuza tu watake wasitake.
Wakati mheshimiwa anahojiwa na Tido,alikiri mwenyewe kuwa miradi ya REA itaendelea ila kwa kasi ndogo,na wewe unasema tuendelee kulipa Kodi ya REA kwenye mafuta ili miradi yake iende kasi,
Kama miradi ya REA inatarajiwa kwenda kwa kasi ndogo kwanini Kodi yake kwenye mafuta isiondolewe ibaki ile tunayotozwa kwenye umeme
 
Ndio manake kwa raha zetu, mlitutesa sana
kikosi kazi mko bize kuharibu hii mijadala ya wanuka jasho kwa kila mbinu naona umehamia plan b sasa...hayo mambo yenu ya sukuma gang,msoga gang, mchambawima gang ni upuuzi wenu nyie hapa najadili upeo mdogo wa jinsi nchi hii inavyoendeshwa , hii ni dharura lakini watu wanaona poapoa tu yaani
 
Zanzibar nao wanachukua kutoka nigeria kupitia angola!? Maana degree zetu za ufugaji nyuki hazijuwi lolote.
Kwa Hawa watetezi wa huu upandaji Bei mafuta hakuna hata mmoja anaweza elezea suala la zanzibar..mkitoa mifano ya Kenya,Rwanda,Burundi,DRC ni wanakuja Kama nyuki utasikia tunatofautiana sijui Kodi,Mara bandari wanayochukulia, ila ukigusa mfano was zanzibar,hakuna anaejibu,mnawachosha tu maana ni Kama wamekariri majibu
 
1 Litre of Petrol

1.Total cost CIF to Dar port 1,162
2. Wharfage 20.5
3. Railway devl levy 19.4
5. Customs processing fee 6.0
5. Weights & measures fee 5.6
6. TBS charge 10.0
7. TASAC fee 8.7
8. EWURA fee 9.0
9. Fuel making 16.0
10. Demurrage costs 8.0
11. Surveyors cost 8.00
12. Financial cost 17.0
13. Evaporation losses 6.5
14. Fuel levy 513.00
15. Excise duty 479.0
16. Petroleum fee 180.0
17. Oil marketing companies 163.0
18. Charges to executive agencies 6.0
19. Service levy to LGA 6.7
20. Retailers margin (profit) 210.5
21. Transport charges (local) 50.5

Total Levy 1,743.4
Plus TC 1,162

Total cost 2,905.4 @Wabunge wetu,huo mzigo wa 1,743.4 yote mlaji wa mwisho,Wananchi wenu wanakwenda kulipa kwa kila lita moja ya mafuta, yaani kodi ni kubwa kuliko bei halisi ya mafuta🤣 Tanzania nchi yaanguu..!
 
Dah jamani hii vita ya ukraine imetukalia vibaya sisi tu au hawa jirani zetu wao wanachimba mafuta? si wanapitisha mafuta hapahapa bandarini kwetu jamani?

Tunaongelea vita lakini hawa jamaa wa Drc congo wana vita na waasi miaka 25 sasa , tunahitaji maombi maalumu nchii hii hali tete sana

View attachment 2214602

View attachment 2214603
Tatizo ni tozo nyingi kwenye kila lita ya mafuta.
 
wewe na wewe umeandika utumboo. Wenzetu hawana bandar bdo bei iko chini. Kwaiyoo wakichukulia kenya na angola ndo bei iwe chini.

Kama ndo hvyoo mafuta na sisi tuchukulie kenya na angalo hiyo bandar tufugie mbuzi.
Bajeti ya Tanzania tokea enzi za baba wa Taifa inategemea mafuta ya petroli , vinywaji vyenye kilevi na soda ,kwahiyo serikali ikipunguza kodi kwenye petroli itakuwa imepunguza mapato yake. Vita ya Ukraine na Urusi inachangia upandaji wa bei ya mafuta kwa sababu ya vikwazo. Kampuni kubwa za petroli duniani ni za nchi za magharibi - ambazo kwa wakati huu hazinunui wala kuuza mafuta ya Urusi. Hii inasababisha uhaba wa Petroli duniani- kwahiyo bei katika soko la dunia inapanda. Vile vile kampuni yoyote ile ya mafuta itakayokutwa inakiuka vikwazo hivyo itapigwa faini kubwa na kutengwa na mataifa ya Marekani na Ulaya. Nini kifanyike kupunguza ukali wa bei ya mafuta 1) Tuombe vita hii ya Urusi imalizike haraka, 2) Serikali na watu binafsi tubane matumizi ya mafuta, 3) Serikali ikubali kusamehe pato lake la kutoka kwenye petroli na kusimamisha miradi mingine ambayo haina uharaka-kwamfano uhamiaji wa kwenda Dodoma na kadhalika.
 
Back
Top Bottom