Vincenzo Jr
Platinum Member
- Sep 23, 2020
- 24,262
- 58,728
Hongera sanaNilikuwa siwezi kula mahindi ya kuchoma, siwezi kula maharage mfululizo, siwezi kula dagaa, siwezi pilipili,
Na maisha ya hapa nyumbani maharage ndio kwa sana,
Nilitumia kila aina ya dawa za kienyeji mfano mafuta ya kondoo, asali ya nyuki wadogo, juisi ya kabichi, maji ya vuguvugu kila asubuhi, na majanimajani naletewa nnayoambiwa , na kushauriwa kula kwa wakati kutoacha tumbo wazi,
mwisho nmepona sijui dawa iliyonponesha,, au kilicho ponesha , nakula vyote nlvyokuwa Sili, kinachomsumbua sasa ni kiungulia tu tena kinanisumbua nnapokula maharage alafu nisile tunda....
Namshukuru Mungu
Asante sana, hayo madonda ni mabaya sana sana..Hongera sana
Kabisa yaani mie vinanitesa sana 😭Asante sana, hayo madonda ni mabaya sana sana..
Pole sana😔 nayajua maumivu yake...afu unaambiwa kila aina ya dawa hadi unachanganyikiwa ..Kabisa yaani mie vinanitesa sana 😭
Asante sana 😭😭Pole sana😔 nayajua maumivu yake...afu unaambiwa kila aina ya dawa hadi unachanganyikiwa ..
Asante sana 😭😭
Unataka kusema, maziwa yanasaidia?Nadhani dawa ni maziwa mimi kazini muda wote nina chupa ya maziwa nusu lita kila siku the whole day nakunywa kama maji vile vidonda sijavisikia muda mrefu nahisi kupona
Jaribu dawa niliyotumia mm uone kama hauponaPole sana😔 nayajua maumivu yake...afu unaambiwa kila aina ya dawa hadi unachanganyikiwa ..
Usiku wa kuamkia tarehe 17 Mwezi November mwaka jana niliugua maumivu makali ya tumbo.Members humu kwema? Kwa ambaye amepata dawa ya vidonda vya tumbo anifahamishe vinanitesa sana, hapa mwili umeisha, nimeshatumia madawa ya kila Aina sasa umeshaangusha hata uchumi wangu, inshort ni maumivu usiku na mchana hakuna amani , mwenye kujua dawa anisaidie tafadhari
Brother asante sana pia pole sana , ulitumia Kwa muda Gani? Ratiba ilikuaje asubuhi , mchana na jioni au? Ulikuwa unatumiaje na Kwa muda Gani?Usiku wa kuamkia tarehe 17 Mwezi November mwaka jana niliugua maumivu makali ya tumbo.
Asubuhi nikajitosa moja kwa moja kwenda zahanati kupima.
Vipimo vikaja kama ifuatavyo View attachment 2976749
Kwa maelezo ya daktari ni kuwa nikisumbuliwa na magonjwa mawili. Vidonda vya tumbo na Typhoid.
Nilipata ukakasi kwenye Typhoid kwasababu circle yangu ya maisha nimekuwa mtu makini sana kwenye usalama wa vyakula na maji.
Nikaandikiwa dawa hapo kama shilingi 25K kwa ajili ya kutibu magonjwa yote mawili, lakini nikawajibu kuwa kwa saizi sina hela ngoja nikajipange.
Nilipotoka hapo nikachukua boda kwenda kwenye hospitali binafsi kwenda kupima tena kuhakiki.
Nilipofika pale nilichukuliwa vipimo vya damu na vipimo vilikuwa kama hivi.View attachment 2976752
Daktari akanipa ufafanuzi wa kinacho nisumbua akiniambia kuwa ni vidonda vya tumbo pekee, hakuna ugonjwa mwingine zaidi ya huo.
Dawa akaniandikia gharama zake kuwa ni 99,000 nikasema ngoja nikajipange.
Nikaongea na ndugu yangu akanipa ushauri wa dawa moja ambayo aliwahi kuitumia mke wake.
Dawa hiyo ilikuwa inajina linalofanana na "morpezoel"
Lakini mimi mwenyewe sikuacha kujiongeza. Nika Google nikakutana na link ya uzi wa mtu ambaye alitoa ushauri wa kutumia bamia kama dawa.
Bamia unaziloweka kwenye maji zinakaa kwenye maji kwa muda wa masaa 8 kisha unakunywa yale maji yake kwa kutwa mara mbili.
Kwa kufanya hivyo ndio nimejikuta nimepona vidonda vya tumbo.
Wiki Moja tu nilianza kuona changesBrother asante sana pia pole sana , ulitumia Kwa muda Gani? Ratiba ilikuaje asubuhi , mchana na jioni au? Ulikuwa unatumiaje na Kwa muda Gani?
Naomba namba zako za Simu kaka?Njoo kwangu.
Mm mwenyewe niliteseka sana.nilifikia hadi hatua ya kujisaidia blood clot.ila sasa niko poa nadunda vzr kbsa.njoo inbox kwa maelekezo zaidi
ost namba zakeMkuu usihangaike na hii kitu. Kuna jamaa yangu alinipa dawa free ikaniponya kabisa, naweza nikamuomba akusaidie na wewe.
Kama atakutoza haiwezi shilingi 5000. Nakutumia namba inbox.
Kama bado vinasumbua nicheki inboboKupona vidonda vya tumbo sio rahisi kwa sababu vipo ndani ya tumbo na tumboni kuna chemical na pia asilimia kubwa ya vyakula vina kemikal , ili upone lazima utafute namna ya kuepuka Vyakula vyenye kemikal na kula vyakula vyenye uwezo wa kukabiliana na acid ili vidondo vipate mda wa kupona.
Mkuu usihangaike na hii kitu. Kuna jamaa yangu alinipa dawa free ikaniponya kabisa, naweza nikamuomba akusaidie na wewe.
Kama atakutoza haiwezi shilingi 5000. Nakutumia namba inbox.
95% of my patients with PUD h pylori was negativeKinachosababisha vidonda vya tumbo ni Helicobacter pylori na sio stress wala aina ya chakula unachotumia.
Ninauza dawa za uhakika kutibu kabisa vidonda vya tumbo na kiungulia chote kinaisha.
Ukitumia hizi dawa unapona kabisa na utaweza kula chakula chochote ukipendacho.
Hii ni biashara, anayetaka aje PM