Dawa ya mtu aliyeziba masikio ni kumuwekea loud speaker, kazi iendelee

Serikali haitarudi nyuma nyie endeleeni kujadili
Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
Tunashida kubwa, hawa usalama wa taifa kazi yao ni kubinya pumb.u za watu tu. Mambo magumu kama haya wanajifanya hawayaoni, ni kama wameapa kulinda serikali na sio Nchi.
 
Tunashida kubwa, hawa usalama wa taifa kazi yao ni kubinya pumb.u za watu tu. Mambo magumu kama haya wanajifanya hawayaoni, ni kama wameapa kulinda serikali na sio Nchi.
 
Watanzania wengi wajinga mnapiga kelele bila uelewa mngesubiri utekelezaji muone kwa vitendo.
If a thing does not add up with others on paper then forget it, as it won't work on the ground!!! This is not a myth but a reality!! Mwenye masikio asikie!!!!
 
Na hicho ndicho kinaniumiza, tumeachiwa mzigo mkubwa wa madeni kwa mikopo matrillion ya kurmdeleza bandari, lakini gawio la faida za bandari tutapewa 0% ??!!!
Sio 0% tu. Ili mkataba mama usimame,Serikali yetu ina ulazimu kujikita kubadilisha sheria zinazogusa ushuru na forodha au kuwapatia Incentives au kusamehe kodi kwa masuala mbali mbali yatakayogusa Uwekezaji wao kupitia HGA. Mfano magari yao ya miradi, Mishahara ya wale 60 if not 99% ya mejimenti!! Tunaweza fanya ulinganishi wa hili shauri na lile la Disney na jimbo la Florida ambapo kampuni lile limekuwa kama Serikali ndani ya Serikali- Hatari sana.
 
Ni hatari sana kuziba masikio Ukiwa unatembea Kwa miguu njia ya mwendo Kasi😳😳😳😳
 
Wahini Mahakamani Ili upotoshaji ukome
 
Amezungukwa na wapiga dili Kama akina Rostam, na mbumbumbu Kama akina waitala, nape na wengineo
 


Swali

"Hivi Baba akiuza Kiwanja cha familia, akachukua hela za watu, akaja kuwashirikisha, mkakataa, unafikiri atasikiliza hoje zenu?"
 
Tunachotaka ni ufanisi bandarini nchi isonge mbele hatuwezi kucheleweshwa na hizo blaa blaa zenu
 

Watz tuelewe.

Hadi sasa hakuna mkataba. Bali makubaliano kati ya nchi na nchi.
Kwa maana ya states.

Mkataba utakuja kati ya tpa na dpw.

Hivyo hakuna accountability yyt ambayo mama anapaswa kuwajibika.

Kwa ufupi Mama anapaswa kujosolewa kwa kuwa yeye ni accountable.

Lkn kuna mwenye responsibility hamtaki aguswe.

1. Mwanasheria Mkuu.
2. Baraza la mawaziri

Kama kweli tunahitaji kuingozwa kwa utawala wa sheria hawa ndio wanapaswa kujibu hoja hizi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…