DCI Wambura: Uchunguzi umebaini Hamza alikuwa gaidi wa kujitoa mhanga
Mimi sijui chochote na Sina Elimu yeyote ya kupambanua Mambo zaidi ya kuzozana na akina fulani hapa Ila kwa maelezo haya ya DCI hapa tumepigwa mchana kweupe, huhitaji kidgree Cha chuo Cha Amazon Ila narudi Tena kusema tumepigwa hakuna mtu humo
 
Aisee siwez kubisha sana..lakini kwa mtanzania tu aliyekulia katika mazingira ya kitajiri hawez kuwa anajua kushika bunduki vile na kujiamini kiasi kile kwa umri ule...palikua na namna..na inawezekana kabisa ametuma salam kwa wenzake..inaweza kuwa mwanzo wa ugaid tanzania au mwisho wa ugaid inategemea tu na vyombo vya usalama vitakavyolimaliza hili
Aisee siwez kubisha sana..lakini kwa mtanzania tu aliyekulia katika mazingira ya kitajiri hawez kuwa anajua kushika bunduki vile na kujiamini kiasi kile kwa umri ule...palikua na namna..na inawezekana kabisa ametuma salam kwa wenzake..inaweza kuwa mwanzo wa ugaid tanzania au mwisho wa ugaid inategemea tu na vyombo vya usalama vitakavyolimaliza hili
Mbowe nae si gaidi,kwa hio nae anaweza akabeba bunduki vile na kupambana na mapolisi kwa style ya Hamza?
 
Hapa tumepigwa! Yani mualifu kajichunguza mwenyewe na tutegemee aje na majibu yakuwa yeye alikosea? Mungu awalaze mahali pema hamza na vijana wa Siro..... Wale jamaa wakujitoa muhanga huwa wanatafuta sehemu sehemu yenye wingi wa watu!' sasa najiuliza huyu gaidi hamza kwann alidili na police tu? Manake hapo kuna jambo lazima na police walikuwa kwenye position yakuweza kupiga miguu ili wasipoteze ushahidi!!! Ila naisi kule kumpiga risasi nyingi nikupoteza ushahidi na kama ujuavyo kosa siku zote linakuwa la marehemu.....!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Hilo swali la kwanini aliwinda police tu jamaa wanajifanya Kama hawalioni.Wanaruruka tu Kama maharage ya mbeya yanapotaka kuiva.
 
Nilijua tu majibu yatakuwa ya namna hii.

Mnakanusha kuwa hakuwa anamiliki migodi halafu mnakiri kuwa alikuwa na migodi.
 
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Camillius Wambura amedai kuwa uchunguzi uliyofanywa na Jeshi la Polisi umebaini kwamba Hamza Mohammed alikuwa gaidi wa kujitoa mhanga.

Hamza aliuawa na polisi Agosti 25, mwaka huu baada ya kuwaua kwa risasi askari wanne, watatu kati yao wa polisi na mmoja wa kampuni binafsi ya ulinzi jirani na ulipo ubalozi wa Ufaransa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza leo Alhamisi Septemba 2, 2021 jijini Mwanza na waandishi wa habari Wambura amesema uchunguzi huo ulijikita katika mambo makuu matatu ambayo ni kutaka kutambua Hamza Mohammed ni nani, nini kilimsukuma Hamza kwenda kufanya tukio lile na kutaka kutambua mshiriki mwingine katika tukio hilo.

Wambura amesema katika uchunguzi huo polisi imebaini kwamba Hamza alikuwa akiishi kisiri huku akiwa amegubikwa na viashiria vyote vya ugaidi.

"Amekuwa akijifunza mambo mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii ambayo kwa kipindi kirefu amekuwa akijifunza mambo ya kigaidi kwa kuangalia mitandao ambayo inaonyesha matendo ya Al-Shabab na makundi kama ISIS yanayoendelea na wagaidi wengi hujifunza kupitia mitandao hiyo," amesema Wambura.

Amesema kwamba kitendo alichokifanya Hamza kilikuwa ni cha ugaidi wa kujitoa mhanga.

"Tabia na matendo ya Hamza aliyapata kupitia mawasiliano aliyokuwa nayo na watu wanaoishi katika nchi zenye matendo ya kihalifu ikiwemo ugaidi hasa wa kupitia mtandao yanayojulikana kama "Radicalisation through social media)," amesema Wambura.

Kuhusu taarifa zinazodai kwamba Hamza aliwashambulia askari hao kwa sababu walimdhulumu madini yake, Wambura amekanusha na kusema katika uchunguzi huo wamebaini kwamba Hamza hakuwa na madini wala fedha katika mazingira yale.

"Hamza hakuwa na madini wala pesa na hakuwa katika nafasi yoyote ya kumiliki madini wala pesa mbali ya kwamba watu wengi wameongea kwamba alikuwa anamiliki migodi ya madini kule Chunya na maeneo ya Makongolosi uchunguzi wetu umebaini hali hiyo ya maisha ilikwisha simama muda mrefu," ameongeza Wambura.

Wambura ameongeza kuwa taarifa ya uchunguzi huo pia imebaini kwamba Hamza alikuwa kwenye kundi la magaidi wanaoamua kuifia dini.

Chanzo: Mwananchi
Definition ya "kuishi kisiri siri" inasemaje?
 
Matangazo mengine ni kuichafua nchi tu, nadhani Tz saizi tunashida ya lidashipu
 
Nilijua tu majibu yatakuwa ya namna hii.

Mnakanusha kuwa hakuwa anamiliki migodi halafu mnakiri kuwa alikuwa na migodi.
Natamani kujua hio office ya CCM aliwajengea lini ili nijue anaposema jamaa mambo ya madini alikua ametoka tangu zamani alimaanisha zamani ipi?
 
Hili nalo mmeamua kujichafua ili mpate kwa kumukamatia mbowe munaamua kuuaminisha umma kua kuna ugaidi tanzania yani hamuelewi tu nyie ccm kweli????
Kuna kazi maalum aliyopewa Hamza na lile kundi lililoratibu kesi ya Ugaidi Kwa Mbowe. Hamza kakosea au kaamua Kwa makusudi kutekeleza tofauti na makubaliano yao. Polisiccm sio wakumuamini hata kidogo.

Tujiulize kwanini tukio lile linalosenwa na Polisi ni la kigaidi lilifanyikia mbele ya ubalozi wa Ufaransa?? Tujiulize pia kwanini Polisi hao hao wameshindwa kufanya uchunguzi dhidi ya shabulio la Mh Lissu? Wakati ule walisema hawakupewa ushirikiano na Dereva wa Mh Lissu. Je ni nani aliyewapa ushirikiano kwenye tukio la Hamza??

Polisiccm endeleeni kujianika mkishakauka tutawaanua.
 
kweli alikuwa gaidi kwa uchunguzi ulio ona vip hujatuambia bastola alitoa wapi
pia ailkuwa anaishi kwa siri
kama aliishishi kwa siri ujumbe wa chama fulani aliuupataje? mbona picha na clip zake ziko mitandaoni huo usiri ni upi si mlisema mkazi wa upanga? au ok ngoja tuamini tulio wapa zamana
 
Mjumbe wa mkutano Mkuu wa CCM ngazi ya wilaya, Hamza (R. I. P) bado naamini umekufa na siri nzito sana kuhusu kitu kati ya wewe na Jeshi la polisi.
Narudia kutazama ile video clip, kwa hekima anaitazama daladala iliyojaa raia abiria wenye hofu kubwa. Anaiacha, anakwenda katikati ya barabara anaanza kuongoza magari yapite haraka. Anachagua kushughurika na askari tu!

Magaidi Duniani wa kujitoa muhanga wasinge acha ile daladala vile maana njia pekee kwao kutuma ujumbe kwa Serikali huwa ni kuua innocent souls ili mamlaka zipakazwe tope la lawama.

Kesi ya Zombe na wenzake, Tume ya polisi ilikuja na matokeo kwamba wale wafanya biashara walikuwa MAJAMBAZI. Baada ya kelele nyingi ikaundwa Tume Huru ya majaji ikabaini hawakuwa MAJAMBAZI.

Polisi yajichunguza!
 
Hilo halina Ubishi.
Hamza alikuwa Gaidi namba 2.
ndio maana karibia wafuasi wote wa Chadema walimtangaza Hamza kama shujaa wao, inathibitisha kuwa Chadema wanaunga mkono kwa 100% vitendo vya kigaidi.
 
Back
Top Bottom