Benjamini Netanyahu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2014
- 95,871
- 116,627
Ukiwapa pesa CCM inakuwa mhisaniKama maisha ya kumiliki pesa na madini yalikuwa ya muda mwingi uliopita vipi zile pesa alizotoa kuisaidia CCM mwaka jana mwishoni (200ml) alizitoa wapi?
Aisee siwez kubisha sana..lakini kwa mtanzania tu aliyekulia katika mazingira ya kitajiri hawez kuwa anajua kushika bunduki vile na kujiamini kiasi kile kwa umri ule...palikua na namna..na inawezekana kabisa ametuma salam kwa wenzake..inaweza kuwa mwanzo wa ugaid tanzania au mwisho wa ugaid inategemea tu na vyombo vya usalama vitakavyolimaliza hili
Mbowe nae si gaidi,kwa hio nae anaweza akabeba bunduki vile na kupambana na mapolisi kwa style ya Hamza?Aisee siwez kubisha sana..lakini kwa mtanzania tu aliyekulia katika mazingira ya kitajiri hawez kuwa anajua kushika bunduki vile na kujiamini kiasi kile kwa umri ule...palikua na namna..na inawezekana kabisa ametuma salam kwa wenzake..inaweza kuwa mwanzo wa ugaid tanzania au mwisho wa ugaid inategemea tu na vyombo vya usalama vitakavyolimaliza hili
Hiyo haibadili usomali wake,wala utamaduni wake.Huyu kazaliwa bongo na siyo Somalia
Hilo swali la kwanini aliwinda police tu jamaa wanajifanya Kama hawalioni.Wanaruruka tu Kama maharage ya mbeya yanapotaka kuiva.Hapa tumepigwa! Yani mualifu kajichunguza mwenyewe na tutegemee aje na majibu yakuwa yeye alikosea? Mungu awalaze mahali pema hamza na vijana wa Siro..... Wale jamaa wakujitoa muhanga huwa wanatafuta sehemu sehemu yenye wingi wa watu!' sasa najiuliza huyu gaidi hamza kwann alidili na police tu? Manake hapo kuna jambo lazima na police walikuwa kwenye position yakuweza kupiga miguu ili wasipoteze ushahidi!!! Ila naisi kule kumpiga risasi nyingi nikupoteza ushahidi na kama ujuavyo kosa siku zote linakuwa la marehemu.....!!!!
Sent using Jamii Forums mobile app
Definition ya "kuishi kisiri siri" inasemaje?Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Camillius Wambura amedai kuwa uchunguzi uliyofanywa na Jeshi la Polisi umebaini kwamba Hamza Mohammed alikuwa gaidi wa kujitoa mhanga.
Hamza aliuawa na polisi Agosti 25, mwaka huu baada ya kuwaua kwa risasi askari wanne, watatu kati yao wa polisi na mmoja wa kampuni binafsi ya ulinzi jirani na ulipo ubalozi wa Ufaransa jijini Dar es Salaam.
Akizungumza leo Alhamisi Septemba 2, 2021 jijini Mwanza na waandishi wa habari Wambura amesema uchunguzi huo ulijikita katika mambo makuu matatu ambayo ni kutaka kutambua Hamza Mohammed ni nani, nini kilimsukuma Hamza kwenda kufanya tukio lile na kutaka kutambua mshiriki mwingine katika tukio hilo.
Wambura amesema katika uchunguzi huo polisi imebaini kwamba Hamza alikuwa akiishi kisiri huku akiwa amegubikwa na viashiria vyote vya ugaidi.
"Amekuwa akijifunza mambo mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii ambayo kwa kipindi kirefu amekuwa akijifunza mambo ya kigaidi kwa kuangalia mitandao ambayo inaonyesha matendo ya Al-Shabab na makundi kama ISIS yanayoendelea na wagaidi wengi hujifunza kupitia mitandao hiyo," amesema Wambura.
Amesema kwamba kitendo alichokifanya Hamza kilikuwa ni cha ugaidi wa kujitoa mhanga.
"Tabia na matendo ya Hamza aliyapata kupitia mawasiliano aliyokuwa nayo na watu wanaoishi katika nchi zenye matendo ya kihalifu ikiwemo ugaidi hasa wa kupitia mtandao yanayojulikana kama "Radicalisation through social media)," amesema Wambura.
Kuhusu taarifa zinazodai kwamba Hamza aliwashambulia askari hao kwa sababu walimdhulumu madini yake, Wambura amekanusha na kusema katika uchunguzi huo wamebaini kwamba Hamza hakuwa na madini wala fedha katika mazingira yale.
"Hamza hakuwa na madini wala pesa na hakuwa katika nafasi yoyote ya kumiliki madini wala pesa mbali ya kwamba watu wengi wameongea kwamba alikuwa anamiliki migodi ya madini kule Chunya na maeneo ya Makongolosi uchunguzi wetu umebaini hali hiyo ya maisha ilikwisha simama muda mrefu," ameongeza Wambura.
Wambura ameongeza kuwa taarifa ya uchunguzi huo pia imebaini kwamba Hamza alikuwa kwenye kundi la magaidi wanaoamua kuifia dini.
Chanzo: Mwananchi
Taarifa hizi zifike kwa mabalozi wote kuwa Tanzania kwasasa ni kitovu cha Ugaidi.
Polisi wameweka alarm kuhusu Chadema tuIle intelijensia ya polisi ya fujo kwenye mikutano ya CHADEMA ilikuwa wapi mpaka Hamza akawa gaidi na huku ni mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM wilaya?
Natamani kujua hio office ya CCM aliwajengea lini ili nijue anaposema jamaa mambo ya madini alikua ametoka tangu zamani alimaanisha zamani ipi?Nilijua tu majibu yatakuwa ya namna hii.
Mnakanusha kuwa hakuwa anamiliki migodi halafu mnakiri kuwa alikuwa na migodi.
Hapo wapo active vibaya snPolisi wameweka alarm kuhusu Chadema tu
Sawa mkuuHiyo haibadili usomali wake,wala utamaduni wake.
Kuna kazi maalum aliyopewa Hamza na lile kundi lililoratibu kesi ya Ugaidi Kwa Mbowe. Hamza kakosea au kaamua Kwa makusudi kutekeleza tofauti na makubaliano yao. Polisiccm sio wakumuamini hata kidogo.Hili nalo mmeamua kujichafua ili mpate kwa kumukamatia mbowe munaamua kuuaminisha umma kua kuna ugaidi tanzania yani hamuelewi tu nyie ccm kweli????