Demokrasia haileti maendeleo ila udikteta ndio unaleta maendeleo?

Demokrasia haileti maendeleo ila udikteta ndio unaleta maendeleo?

U.S.A, Canada, Ulaya hawa maendeleo yao kwa kiasi kikubwa yamechagizwa na shughuli za ukoloni na utumwa na nafikiri wafahamu yale watumwa waliyokuwa wakitendewa ni kinyume kabisa na vitabuni demokrasia inavyo elekeza.
Umekuwa mwongo kupindukia.

Niambie nchi kama Norway, Finland, Sweden, Singapore, Malaysia, Switzerland, Denmark, Australia, Japan, yalimfanyia utumwa au ukoloni nchi gani?
 
Ulaya yote nchi za EU zimeendelea. Zipo karibu 30. Kule USA zote zilizoendelea ni za kidemokrasia.

Angalia Russia na utajiri wote ule waliko. Wanazidiwa maendeleo na nchi ndogo walizozitawala kama Poland.

Nenda kule Asia ya Japan, Taiwan, Hongkong , Malaysia nk.
Udikteta ni laana. Huwezi kupata maendeleo kwa kuwategemea madikteta. Ili maendeleo yapatikane unahitaji ushiriki mkamilifu wa umma katika shughuli za kiuchumi. Utawala ni regulator tu. Udikteta unaua morali ya ushiriki wa umma katika ujenzi wa uchumi. Udikteta unaua mchango wa mawazo, mipango na usimamizi kutoka kwa wananchi, na hivyo kutegemea fikra za mtu mmoja ambaye kwa vyovyote, hana uwezo kuuzidi umma wote.
 
Hizo nchi za Asia zimepita katika historia ya kutisha ya madikteta katika historia ya nchi zao
Ndiyo maana wakati wa udikteta zilikuwa duni kama ilivyo North Korea mpaka leo.
 
Naomba mnisaidie wadau ni nchi gani duniani imepiga hatua za maendeleo ya kiuchumi kwa sababu ya demokrasia?
Hata tulipokuwa watoto tulikuwa tunafokewa na mara nyingine kuchapwa na wazazi wetu ili tuwe watoto waadilifu !
Vivyo hivyo tulipokuwa shuleni tukisoma tulikaripiwa na mara nyingine tulikula mboko ili tuwe wanafunzi wazuri waadilifu na wenye kufanya vizuri kwenye masomo na maisha mengine kwa ujumla !!
Hali kadhalika katika Nchi zote zilizoendelea tunazozifahamu Tawala zao za mwanzo mwanzo zilikuwa ni za kidikiteta dikiteta ili kuwaweka watu kwenye mstari ili wawe waadilifu na wazalendo kwa Nchi zao !

Wenye elements za upigaji wataipinga hii ideology 😅😅🙏🙏🙏
 
Taiwan ilikuwa chini ya udikteta wa KMT chini ya Chiang Kai-Shek na mwanae kwa miongo mingi tu. Korea kusini iliweza pita mikono ya military dictatorship, Japan imefanya udikteta wa kifalme ndani na nje ya mipaka yake wakati wa mchakato wake wa maendeleo kuhusu Hongkong ilikuwa mikononi ya ukoloni wa Uingereza
Argument yako ni baseless. Kama udikteta unaleta maendeleo, basi nchi zilizodumu kwenye udikteta miaka yote ndiyo zingekuwa na maendeleo makubwa kuyazidi mataifa yote.

Unapotaja nchi ambazo labda awali zilikuwa kwenye dictatorship rule, baadaye zikabadilika na kufuata demokrasia, na sasa zimeendelea, utakuwa unaunga mkono kuwa demokrasia ina mchango mkubwa katika maendeleo. Labda kama ungesema kuwa nchi hizo ambazo zamani zilipokuwa zikiongozwa kidikteta zilikuwa na maendeleo, lakini baada ya kukumbatia demokrasia, maendeleo yake yamekuwa duni au yanaporomoka.

Tupatie mfano wa nchi iliyodumu katika udikteta ambayo inaendelea kwa kasi.

Tupatie mfano wa nchi iliyokuwa ya kiditeta iliyokuwa na maendeleo makubwa wakati wa udikteta, lakini baada ya kufuata demokrasia, maendeleo yake yamekuwa duni.

Tupatie mfano wa nchi iliyokuwa ya kidemokrasia ambayo ilikuwa na maendeleo duni, lakini baada ya kukumbatia udikteta imepata maendeleo makubwa.

Kudai kuwa nchi ambayo ni ya kidemokrasia na ina maendeleo makubwa sasa, eti ni kwa sababu misingi yake ilijengwa na udikteta ni nadharia duni kabisa. Ni sawa mtu awe maskini wakati alipokuwa mvivu wa kufanya kazi, baadaye akaachana na uvivu, akawa anafanya kazi kwa bidii, akapata maendeleo, halafu mtu atokee aseme kuwa eti maendeleo aliyoyapata huyo mtu kwa kufanya kazi kwa bidii yamekuja kwa sababu ya misingi iliyojengwa na uvivu aliokuwa nao zamani.
 
U.S.A, Canada, Ulaya hawa maendeleo yao kwa kiasi kikubwa yamechagizwa na shughuli za ukoloni na utumwa na nafikiri wafahamu yale watumwa waliyokuwa wakitendewa ni kinyume kabisa na vitabuni demokrasia inavyo elekeza.
Usa na Canada kamwe hazijawahi kuitawala nchi yeyote Ile duniani. Ulaya nchi zao bado zingine ni kingdoms

Sent from my CPH1937 using JamiiForums mobile app
 
na huu ndio ukweli...dunia hii ina wenyewe ukiwagusa hao wenyewe ndio utajua kama kuna democracy au akuna...ila haki na waambia hakuna democracy....!​

Demokrasia ipo, ila inaweza isiwepo kwenye fikra zako.

Demokrasia haimaanishi uhuru wa kufanya kila kitu, mema na mabaya. Wewe uchukue kisu ukamchome mwenzio afe, halafu ukikamatwa na kuhukumiwa kunyongwa, halafu utasema hakuna demokrasia?

Uovu au kufanya mambo yaliyozuliwa ni jamij husika kupitia mifumo ya kidemokrasia, siyo sehemu ya demokrasia.
 
Title imetoa conclusion, content inatuuliza kutoa proof.

Nadhani ungefanya tu research mkuu kabla ya kuanzisha thread ili at lease uongeze nyama
Singapore. Ilifanikiwa na kiobgozi wake aliitwa dikteta.
Nafikiri mkisema demokrasia ni kwamba hata Tanzania ipo. Pengine nzuri kuliko ya Marekani, tatizo ni utekelezaji tu.
Nchi kama Marekani, wakosoaji wanawekwa ndani bila kupelekwa mahakamani. Ukija kwenye udikteta ndo kabisa tunachanganya kwa kufata Wazungu wanavyotwambia. Kwa maana ya wamagharibi, kwamba eti Mugabe alikuwa dikteta na Mobutu alikuwa mwanademokrasia kwa vile alikuwa mtu wao!! Labda mbadilishe mtumie neno "Ubabe" "utemi"
Wazungu walitudanganya eti nchi zetu haziendelei kwa sababu hatuna utawala bora, hatuna uwajibikaji, hatukusanyi kodi, hatudhibiti mapato, hatulindi rasilimali, katokea JPM kufanya yote hayo hawamtaki, kwa sababu kazuia wao kutuibia, hataki kuwakopa, hataki wawekezaji uchwara, hatoi vibali vya kazi kiholela. Wakampa majina kibao na mwisho akapotea. Wanakuwa hawamaanishi, ni janja tu ya kutukeep busy na sera zao zisizotekelezeka.
 
Denmark Canada Sweden Finland Norway alimfanyia nani utumwa akawa na maendeleo.
Achana na chuki za panafricanist wameandika chuki nyingi kuliko ukweli halisi
Hizi nchi zote zilidaidika na wizi wa rasilimali kutoka afrika na faida kubwa ya mikataba ya kinyonyaji iliyopatikana baada ya nchi kubwa duniani kufaidika na kusaidia nchi nyengine kwa masharti nafuu
 
Soviet Union ilikuwa imeendelea na kuwa taifa kubwa na kuzalisha vita baridi kati yake na marekani
USSR ilikuwa duni sana kwenye human development index na hata kwenye GDP per capita. Kidogo kilichopatikana kiliishia tu kwenye kutengeneza silaha, sawa na ilivyo leo North Korea.

USSR yenyewe miaka ya 1990 ikiwa bunkrupt, iliamua kuomba msaada wa kiuchumi toka mataifa ya Magharibi.
 
Hizi nchi zote zilidaidika na wizi wa rasilimali kutoka afrika na faida kubwa ya mikataba ya kinyonyaji iliyopatikana baada ya nchi kubwa duniani kufaidika na kusaidia nchi nyengine kwa masharti nafuu
Raslimali walizopora hata robo hazifikii zilizobakia Africa.
 
Hapo kwenye demokrasia pia hawana. Mfano uingereza coz mfalme akisema waziri mkuu huyu simtaki basi hata kama kachaguliwa na wananchi, unaitishwa uchaguzi mwengine au anateuliwa mtu mwengine.
Marekani nako uchaguzi wao ni kichekesho, rais anaweza kushinda hata kama ana kura chache, kama akishinda kura nyingi kwenye majimbo fulani yenye watu weupe wengi au kura za turufu.
Mbona hatujiulizi kwamba hakuna rais atakaetoa maoni kupinga ushoga halafu akaachwa salama! Mfano Uganda, kama wazungu wanataka demokrasia na uhuru wa kujieleza si wamuache?
 
Umekuwa mwongo kupindukia.

Niambie nchi kama Norway, Finland, Sweden, Singapore, Malaysia, Switzerland, Denmark, Australia, Japan, yalimfanyia utumwa au ukoloni nchi gani?
Elimu yangu ndogo kabisa ya historia Japan kamtawala China miaka kibao kajichotea resources za kutosha.
 
Waafrika tuna shida gani hatuendelei ? Rasilimali tunazo hatusongi....Y?
 
Pia lazima tufahamu kati ya democracy na dictatorship kipi kianze. Nchi za magharibi zilianza na udikteta baada ya kupiga hatua katika nyanja za maendeleo na ustaharabu Wakashift kwenda Kwenye democracy.
Africa ni vice versa tumeanza na democracy 🤣🤣
Hakuna democracy kwenye jamii masikini na isiyostaharabika.
Misingi ya German ya Leo ilijengwa na Adolph Hitler.
Hii ndo ingekuwa hoja ya kujadili
 
Pia lazima tufahamu kati ya democracy na dictatorship kipi kianze. Nchi za magharibi zilianza na udikteta baada ya kupiga hatua katika nyanja za maendeleo na ustaharabu Wakashift kwenda Kwenye democracy.
Africa ni vice versa tumeanza na democracy 🤣🤣
Hakuna democracy kwenye jamii masikini na isiyostaharabika.
Misingi ya German ya Leo ilijengwa na Adolph Hitler.
Nchi karibu zote za kiafrika baada ya uhuru zilingia katika mfumo wa kidikteta isipokuwa afrka kusini na Botswana. Na zote zimekuwa na maendeleo duni isipokuwa Botswana na south Africa.
 
Nchi karibu zote za kiafrika baada ya uhuru zilingia katika mfumo wa kidikteta isipokuwa afrka kusini na Botswana. Na zote zimekuwa na maendeleo duni isipokuwa Botswana na south Africa.
Sahihi
 
Back
Top Bottom