Uchaguzi 2020 Dkt. Bashiru: Wanaotegemea Tume Huru iwape ushindi wanajidanganya! Tume haipigi kura

Uchaguzi 2020 Dkt. Bashiru: Wanaotegemea Tume Huru iwape ushindi wanajidanganya! Tume haipigi kura

Mmawia

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
122,494
Reaction score
96,074
Binafsi nimeshindwa kumuelewa kabisa huyu bwana mkubwa wa CCM.

Maneno aliyo yaongea na elimu aliyo nayo sidhani kama vinaendana.

HOTUBA YA DR. BASHIRU KWA UFUPI

CCM inatoa salamu za mwaka mpya 2020, niwahakikishie watanzania kuwa tutaongoza siasa safi,ni mwaka wa kuheshimu maoni na uamuzi wa Umma, na tutashinda kwa kishindo kwa kuwa wananchi walihitaji huduma ya maji, elimu bure, afya na sasa wanapata huduma hizo,wananchi sio wanafiki.

CCM inapingana na udhalilishaji unaojitokeza ktk chaguzi, Wanawake kabla ya kugombea wanaitwa majembe, wakichukua fomu za kugombea wanaanza kuchimbwa na kupewa kashfa,wanajazwa hofu na wanaogopa, awamu hii CCM haitakubali wanawake wadhalilishwe na haki ni lazima itendeke kwa wote.

Wapo wanaolilia tume huru iwasaidie kupata ushindi, tume haipigi kura bali inasimamia uchaguzi, chama kisicho na wapigakura kisitegemee tume iwape ushindi, CCM imetafuta wapigakura kwa kutoa elimu bure, afya, maji na barabara, wao waseme wapiga kura wamewapataje.

Wenyeviti wa vijiji na mitaa, ninyi ni wajumbe wa vikao vya CCM kwenye Matawi na Kata, mtusaidie kupata wagombea bora, ikiwa mnaona kuna watu wanawazidi nguvu na kupendekeza wagombea wasio na sifa kwa maslahi yao, leteni taarifa haraka kusaidia Chama.

bashiru.jpg
 
huyu Mwalimu Wangu tangu amekalia hicho kiti na Akili imehama kabisa mungu amsaidie kwa kweli, Mkate wa Kila siku unapokuwa unapatikana bila taabu hata akili huwa inagoma kufikiri, huyu kwenye midahalo pale Nkuruma ndio alikuwa anazungumzia haya mambo ya Demokrasia, Haki na Tume huru leo gafla hata haoni maana ya Tume kisa amepewa shavu, Eeeh Mungu Tunusuru
 
Polepole aliwahi kusema CCM tume ikiwa huru ni wepesi sana,ila baada ya kuanza kuendeshwa kwny V8 aisee ukimuuliza swali lolote lile utasikia stigler's,SGR,elimu bure.

Full stop.
huyu Mwalimu Wangu tangu amekalia hicho kiti na Akili imehama kabisa mungu amsaidie kwa kweli, Mkate wa Kila siku unapokuwa unapatikana bila taabu hata akili huwa inagoma kufikiri, huyu kwenye midahalo pale Nkuruma ndio alikuwa anazungumzia haya mambo ya Demokrasia, Haki na Tume huru leo gafla hata haoni maana ya Tume kisa amepewa shavu, Eeeh Mungu Tunusuru

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndiyo hapo kila mtu anamshangaa sana kwa hizi kauli zake ambazo kimsingi hazilingani na daraja alilo nalo kielimu.
huyu Mwalimu Wangu tangu amekalia hicho kiti na Akili imehama kabisa mungu amsaidie kwa kweli, Mkate wa Kila siku unapokuwa unapatikana bila taabu hata akili huwa inagoma kufikiri, huyu kwenye midahalo pale Nkuruma ndio alikuwa anazungumzia haya mambo ya Demokrasia, Haki na Tume huru leo gafla hata haoni maana ya Tume kisa amepewa shavu, Eeeh Mungu Tunusuru

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi nimeshindwa kumuelewa kabisa huyu bwana mkubwa wa ccm.

Maneno aliyo yaongea na elimu aliyo nayo sidhani kama vinaendana.
View attachment 1310741

Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli mtu ukisha kuwa ccm unakuwa takataka. Bashiru umebadilika kabisa, akili iko wapi uliyokuwa nayo UDSM! Mavi ya kunya yamekuondolea akili kabisa Unakula na kunya kesho, akili imehama! Huoni umuhimu wa tume huru ya uchaguzi? Una wapiga kura wote, wakakuchagua nikakataa kukutangaza, kura zina maana gani?
 
Back
Top Bottom