Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli: Bunda walijichanganya wenyewe, Utawapelekeaje Barabara watu wanaokutukana?

Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli: Bunda walijichanganya wenyewe, Utawapelekeaje Barabara watu wanaokutukana?

Nilikuwa nacheki mubashara naona kuna muda aliposkia na kuona mafuriko ya lisu mbeya akatoka jukwaani kwenda maliwato,

Lisu unamlaza mtu na viatu kitandani
Hahahahhha !!! Yaani jamaa anasema ni sawa kupapendelea chato!!! Haya ni maneno ya kusema kwenye kampeni kwa kweli???? Sasa naamini kuwa Lissu anamlaza huyu mzee na viatu!!!
 
Hahahahaha !!! Baba ingawa upo kikampeni ila haya ya huyu mzee Embu yakemee kama unavyomkemea Gwajiboy!!!

Kwa sasa sitoweza kabisa 'Kumsema' Rais na Mwenyekiti wangu Taifa CCM kwani nina 'Jukumu' Kuu la Kuhakikisha kuwa anashinda huu Uchaguzi.
 
Sasa hivi GENTAMYCINE nipo 'Kikampeni' zaidi Mkuu, hivyo nakuomba tu 'tuvumiliane' kidogo kwani siwezi Kuacha Rais wangu Magufuli asishinde.

Ni haki yako kabisa na inaheshimiwa, na hiyo ndio demokrasia ambayo jiwe imemshinda kuikubali. Tetea mgombea wako uwezavyo hakuna mwenye tatizo kabisa na hilo. Tena hata ukiweza badili kabisa avator yako uweke lile shati lako la mgomba.
 
Kwanini unaamini hivyo?
Hili sio swala la Imani, hata Mbowe anajua huu ukweli.. ni mashabiki tu mliojaa hisia mnaoamini Lissu anaweza kuwa Raisi wa Tanzania. Hii nchi inaongozwa na System, usipokubalika kwenye system huwezi kuwa Raisi. Kuna miiko ya System Lissu ameshaikiuka na hafai tena Milele. Ndo maana nikasema sio tu 2020 but NEVER.Kama una ndugu yako aliye sehemu nyeti serikalini siku moja kwenye kipindi hiki cha kampeni muulize atakuelezea vizuri.
 
Kwa sasa sitoweza kabisa 'Kumsema' Rais na Mwenyekiti wangu Taifa CCM kwani nina 'Jukumu' Kuu la Kuhakikisha kuwa anashinda huu Uchaguzi.

Uko sahihi kabisa, japo hategemei kushinda kwa kura yako, zaidi ya mbeleko ya tume ya uchaguzi na vyombo vya dola. Hizi kampeni ni ili ionekane kashinda kwa kura, ila matokeo tayari ameshapanga yaweje.
 
Uko sahihi kabisa, japo hategemei kushinda kwa kura yako, zaidi ya mbeleko ya tume ya uchaguzi na vyombo vya dola. Hizi kampeni ni ili ionekane kashinda kwa kura, ila matokeo tayari ameshapanga yaweje.

Sasa kama umeshajua kuwa CCM itashinda au imeshashinda mbona unasumbuka na kuteseka nayo hivi Mkuu? CCM itatawala 'Tanzania' hii Milele.
 
quote

Huyu jamaa asipoangalia anaweza kosa kura hata za wajinga anaowategemea

unquote

😄😄😄😄
 
Naona mnatumia JF kujipa moyo.Yaan hata kura mil 2 hampati.Pole sana ndugu
Hatuwachukii watu wa ccm wala Jiwe. Tunachukia na kucukizwa na matamshi yanayokinzana na sheria za uchaguzi toka kwa wana ccm hasa Jiwe. Ukiweka siasa pembeni utagundua kuwa huyu Mgombea wenu anamatatizo fulani. Hafai kuwa Kiongozi. Mnambeba tu kwakuwa ni wa chama chenu cha kijani.

Ninyi ccm hata angesimamishwa Musukuma na std 7 yake kuwa mgombea mngempamba tu. Ccm kwa sasa mmeishiwa pumzi tunasubiri tu Jiwe apige puuu jukwaani. Hapo ndipo akili zitawakaa sawa.
 
Kuna tatizo gani asipokuwa rais? Nchi hii ina miaka 60 toka uhuru, na raia 59m+, idadi yote hiyo ya watu, ni watu watano tu wamekuwa marais. Hivyo hakuna tatizo kwani kwa ratio hiyo kuwa rais sio uwezo bali ni bahati. Tunachotaka ni ashindwe kihalali tu basi. Na uzuri kampeni hizi zimeonyesha kuwa ccm haina uwezo wa kushinda kihalali kwa kura zaidi vya 55%, na zama za ccm kuwa chama pekee zimeshapita na hazitakaa zirudi tena. Kinachofuata ni ccm kutolewa madarakani kwa amani, au kinyume chake muda si mrefu.
Mtarudi na kelele za tume muda sio mrefu. CCM hata ichokwe vipi haitaondolewa na upinzani huu wa akina Lissu na Mbowe.
 
Hili sio swala la Imani, hata Mbowe anajua huu ukweli.. ni mashabiki tu mliojaa hisia mnaoamini Lissu anaweza kuwa Raisi wa Tanzania. Hii nchi inaongozwa na System, usipokubalika kwenye system huwezi kuwa Raisi. Kuna miiko ya System Lissu ameshaikiuka na hafai tena Milele. Ndo maana nikasema sio tu 2020 but NEVER.Kama una ndugu yako aliye sehemu nyeti serikalini siku moja kwenye kipindi hiki cha kampeni muulize atakuelezea vizuri.

Huo ushindi wa kupewa na system Lisu hahitaji, Magufuli ndio anauhitaji ushindi wa mezani, maana hana ushawishi wala mvuto kwa wapiga kura. Tutampa Lisu kura zetu, yeye Magufuli angojee kutangazwa kwa mbeleko ya system. Ila hata hao system watajua kuwa enzi za ccm kutawala nchi hii zimeshapita. Na hao system waendelee kuomba wananchi kuwa makondoo, vinginevyo wakiamua kukaza kutatokea machafuko na mauji ya kutosha.

Ukitaka kujua ccm sio chama cha kizazi hiki, angalia ccm imefanya siasa miaka mitano peke yake, kila uchaguzi wameunajisi, lakini ndani ya mwezi tu, tayari watu wamerudi kwenye uhitaji wao wa mabadiliko. Peleka ujumbe huu kwenye vikao vya mboga mboga kuwa kila kitu kina kizazi chake, na ccm sio chama cha kizazi hiki bali cha kizazi kilichopita, ndio maana kinatumia nguvu kubwa kubaki madarakani, kuliko ushawishi wa kisiasa.
 
Kuna ile kauli ya mama mmoja Mzanzibari aliongelea swala la kuwapa nchi wapinzani kwa kutumia vikaratasi sijui kama mnaisikiliza bado. Nadhani yule aliongea ukweli
 
Naona mnatumia JF kujipa moyo.Yaan hata kura mil 2 hampati.Pole sana ndugu
Acha waendelee kujipa matumaini hewa nawakati Mikutano ya mgombea wao Shinyanga, Tabora, na Dodoma ilibuma hadi ikawapelekea kuanza kuahariri picha.
 
Sehemu pekee nchini Tanzania ambapo waweza kudhani Lissu atakuwa Raisi wa nchi hii ni Jamii Forums
Hao watu wa JamiiForums wameshuka kutoka mbinguni?

Humo mitaani watu huwa hawatumii Jamiiforums kumbe?

Heheheee... na zile nyomi kule kwa ground nazo ni za Jamiiforums?

Mimi nafikiri, mtu pekee hapa ambaye ni delusional ni wewe!
 
Huyo mgombea wenu sasa anawafanya hata wale wajinga waliokuwa wanam support kumgeuka.

Kwa haya maneno nawaambia mtashangazwa hiyo October 2020 mkiona Lissu anampiga vibaya huyu mtu wenu kwenye Sanduku la kura!!
Mbona mama yako ni mjinga lakina bado anaendelea kumsapoti .

Yaani vijana wa bavicha shida tupu.
 
Sasa kama umeshajua kuwa CCM itashinda au imeshashinda mbona unasumbuka na kuteseka nayo hivi Mkuu? CCM itatawala 'Tanzania' hii Milele.

Nani amekuambia ccm itashinda, ccm itatangazwa washindi na sio kushinda. Hapa tunachofanya ni kupush mkapewe huo ushindi wa mezani na sio wa kura. Ccm kutawala milele sio shida maana sio chama cha siasa, bali ni kikundi cha dola kilichojivika koti la chama cha siasa. Hivyo kwetu tunachukulia ccm kutawala, ni kama nchi iliyopinduliwa na jeshi.
 
Back
Top Bottom