Dkt. Mollel: Ni ujinga Waziri kutoa Data za Walioathiriwa na Corona kila siku. Bei ya chanjo ni Tsh 400,000

Dkt. Mollel: Ni ujinga Waziri kutoa Data za Walioathiriwa na Corona kila siku. Bei ya chanjo ni Tsh 400,000

Yuko sahihi, kwani kuto kutanganza data hadharani pia ni mbinu mojawapo ya kupambana na matatizo ya Corona.

sio kila mtu mwenye changamoto ya upumuaji basi ana zushiwa kuwa anaumwa corona, bali matatizo ya upumuaji yanaweza pia kusababishwa na magonjwa ya moyo, pumu, nimonia, sukari, n.k.
ni vyema wagonjwa wote wenye magonjwa sugu na ambao wanapaswa kuhudhuria kliniki wafanye hivyo badala ya kubaki nyumbani.

Lengo ni kuokoa maisha ya watu wote na haswa wenye changamoto sugu za kiafya na sio kuwatisha kwa matangazo ya vifo.

Hakuna mpika data yoyote anayejaribu kuhadaa umma kuwa mambo ni mazuri, ambaye atakuwa tayari kutoa data za ukweli kila mara. Na isitoshe serikali hii ni ya vitu zaidi kuliko watu.
 
Abaki kwenye fani yake ya dentistry yawaachie md specialist wa internal medicine na nyinginezo watoe mchakato wa magonjwa.
Hakuna awezaye kujibu kisayansi hoja zake za kisayansi. Katumia data kuhusu matatizo ya upumuaji kuwa yapo hata kabla ya Corona na yalishika namba 2 duniani kwa kusababisha vifo.
 
Kwahio dunia nzima ni wajinga?

Ni ujinga na kukosa busara na hekima kuita wengine wajinga, kila mtu anafanya kila anachokiona ni sawa / kuita wengine wajinga sababu wanafanya tofauti na wewe ni ujinga. Kila mtu ana mbinu zake heshima kitu cha bure.
 
Statistics zinasaidia kujua ukubwa wa janga, umri gani wameathirika zaidi na walindwe vipi. Kama ugonjwa utaendelea basi litakua na ukubwa gani na watu wangapi wanakadiriwa kuupata na Serikali isaidie vipi. Hili ni janga la dunia we owe this to the world. Lazma ije isemwe this tragedy claimed how many lives, dunia ilijikingaje na inaelekea kuumaliza vipi.

Je unadhani zile chanjo za polio na kifua kikuu zinakuja kiholela? Wanakadiria nchi kwa mwaka wanazaliwa wangapi, wangapi wanakadiriwa kupata chanjo na ugonjwa umeshuka kwa kiasi gani??

Kwani statistics za waliokufa kwa malaria mamilioni kwa dunia nzima kuna mtu anaamka tu halafu anaitaja??? In general statictics zinakusaidia pia wewe na Serikali yenu mtapewa msaada wa chanjo kwa kiasi gani.
Kansa pia inaua na takwimu zinatolewa.

Mtu akasema kumbe ndo maana ilianza na taarifa ya mapapai kukutwa na korona kisha ziii. Vita ya uchumi ina mbinu nyingi kweli.
 
... Mbowe na genge lake ndio waliosaini mkataba wa WHO.

Your too political than a scientist
Can you re-define yourself.
Hivi ndo vichwa vinaleta matatizo kwa kuingiza siasa kwenye sayansi.
Jifanyie factory default labda utarudi kwenye normal thinking.
 

Attachments

  • gwaji.jpg
    gwaji.jpg
    38.6 KB · Views: 1
Yuko sahihi, kwani kuto kutanganza data hadharani pia ni mbinu mojawapo ya kupambana na matatizo ya Corona.

Sio kila mtu mwenye changamoto ya upumuaji basi ana zushiwa kuwa anaumwa corona, bali matatizo ya upumuaji yanaweza pia kusababishwa na magonjwa ya moyo, pumu, nimonia, sukari, n.k.

ni vyema wagonjwa wote wenye magonjwa sugu na ambao wanapaswa kuhudhuria kliniki wafanye hivyo badala ya kubaki nyumbani.

Lengo ni kuokoa maisha ya watu wote na haswa wenye changamoto sugu za kiafya na sio kuwatisha kwa matangazo ya vifo.
Misplaced argument!! Magonjwa yote uliyotaja ikiwemo na corona hutolewa data. Kinachotakiwa ni kutoa hizo data kwa vyombo husika, hata kama itakuwa mara moja kwa mwezi. Kama hujui hili basi wewe ni layman - data za kila siku zinaonesha upimaji na kwa kuwa upimaji unapaswa kufanyika kila siku wanakwepa hitaji hilo. Lakini kama Dr. Mollel anasema data huwasilishwa kwa mwezi - sio vibaya. Tatizo ni kutowasilishwa kabisa ili kuleta picha kuwa vifo vyote havina uhusiano na covid-19!!
 
Hakuna mpika data yoyote anayejaribu kuhadaa umma kuwa mambo ni mazuri, ambaye atakuwa tayari kutoa data za ukweli kila mara. Na isitoshe serikali hii ni ya vitu zaidi kuliko watu.
Serikali hii ni ya vitu zaidi kulilo watu! Hauna aibu?
 
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya Jinsia Wazee na Watoto amesema watu wengi wanasema Tanzania haitoi data, ambapo amesema data haina haja ya kutangazwa kila siku na Waziri, utakuwa ni ujinga mtupu.

Amesema Data huwa inataka uchakataji ili kujua tatizo ya magonjwa yanayosababisha vifo na kujua namna ya kuyakabili.

Kwa kipindi cha karibuni kumekuwa na taharuki ambayo imesababisha kila anayefariki kupakaziwa amekufa kwa #CoronaVirus hivyo inahitajika uchakataji kujua waliopakaziwa

Amesema ili kutoua watu, mtu akienda hospitali huwa wanasema ana matatizo ya kupumua ili kwanza kujua kama anashindwa kupumua kwa tatizo la presha, nimonia, sukari au bakteria.

Msikilize:


View attachment 1709630
Hivyo yeye Mh.Naibu Waziri ambaye ni Dr kitaaluma hafahamu kuwa kuhuisha taarifa/takwimu katika jamii inaweza kuwasaidia wengine kuchukua tahadhari zaidi,kutathmini ukubwa wa tatizo na kusaidiana kulitokomeza!Viongozi wote hata wanataaluma wasomi wanashindwa kujisimamia kuiwezesha jamii kupata uelewa mpana wanafanya siasa nyepesi nyepesi kwenye serious issues.
Sasa hivi hata watoa huduma za afya kama Madaktari,Manesi nk wanasita kuandika even provisional Diagnosis wanataja Symptoms&Signs of it?What a tragedy!
Dr.Mollel aje na takwimu,mikakati na raslimali zinazohitajika kukabili COVID 19 aache siasa.Anawalindaje watoa huduma kwa kuwapatia Uhuru wa kuelimisha jamii na kutoa Diagnosis bila kuzuiliwa ili waongeze ufanisi.
 
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya Jinsia Wazee na Watoto amesema watu wengi wanasema Tanzania haitoi data, ambapo amesema data haina haja ya kutangazwa kila siku na Waziri, utakuwa ni ujinga mtupu.
Tutamfute mtu au kaburi la aliyetuloga tukamuombe AU tukaliombe msamaha!
Only ni Tz, huwezi kukuta lugha kama hii dunia nzima.
 
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya Jinsia Wazee na Watoto amesema watu wengi wanasema Tanzania haitoi data, ambapo amesema data haina haja ya kutangazwa kila siku na Waziri, utakuwa ni ujinga mtupu....

Ugonjwa unapogeuzwa mtaji wa kisiasa mbona inakuwa shughuli?

Anatumia nguvu nyingi Mollel. Ni nini kinafichwa?
 
Back
Top Bottom