Dkt. Mwigulu: Chanjo za Corona zimefanyiwa utafiti nchi za baridi zitawafaaje watu wa Dar es Salaam?

Dkt. Mwigulu: Chanjo za Corona zimefanyiwa utafiti nchi za baridi zitawafaaje watu wa Dar es Salaam?

Akizungumza katika kipindi cha Clouds 360, Waziri Dkt. Mwigulu Nchemba amesema watanzania wanapaswa kujiuliza chanjo za watu wa nchi zenye baridi zinawezaje kuwasaidia watu wa Dar es Salaam kwenye joto.

Mwigulu amesema ndio maana watu waliotoroka wakaenda kuchanja kimya kimya zinawaletea matatizo.

Chanzo: Clouds 360

Maendeleo hayana vyama!
Awataje waliotoroka na kuchanjwa kimyakimya na Sasa wamepata matatizo.
 
Hvi NIMRI wanafanya nn au nao wanajifukiza? Kwa nn maghufuli asiifute NIMR na kuwafukuza wote kazi ...mpak sa hv hawajaonyesha effort yyte ya wao nao kutafta chanjo ...wamekaa tu kusikiliza matamko ya Wana siasa
Wametengeneza malimao na pilipili NIMRCAF. Wanasayansi Hawa wameendelea Sana.
 
Kama ni joto, Chanjo imetengenezwa kulingana na joto la binadamu. Joto la binadamu ni moja, haijalishi upo Sweden au upo Tz. Kwa hiyo anataka kusema hiyo chanjo itawafaa watu wa Makete, Longido, Mafinga na sehemu kama hizo?
 
Mimi sikatai madhara ya Chanjo iliyoharakishwa kama ilivyofanyika na inavyoendelea kufanyika hata sasa kwa ugonjwa wa Corona. Hata hivyo, siwezi kukubaliana kuwa kwa kuwa majaribio yamefanyika nchi za baridi ndiyo iwe sababau ya msingi ya kukataa chanjo. Viongozi wetu watumieni Wataalamu wa Sayansi za Afya katika kutoa hoja zinazogusana na sayansi. Chanjo zote katika nchi yetu tangu uhuru zimetoka na zimefanyiwa utafiti huko huko katika nchi za baraidi na bado zilitufaa na zimeendeleea kutufaa hata sasa, Chanjo ya surua, pepopunda na kadhalika. Hazikutafitiwa Dar es Salaam hata mojawapo! Hatukuzikataa kwa sababu tafiti zake zilifanyika nchi za baridi. Zipo sababu za msingi na maana zaidi ya kukataa au kuchelewa kuzikubali chanjo za Corona kwa sababu nyingi za kisayansi, lakini si kwa sababu dhaifu ya mahali zilipofanyika tafiti zake. TUKUMBUKE, miaka ya 1980's kulikuwa na mradi mkubwa sana wa chanjo chini ya Wizara ya Afya ambao uliitwa "Cold Supply Chain" ambao ulitulazimu sehemu zisizokuwa na umeme yalinunuliwa MAJOKOVU YA MAFUTA YA TAA ili kuhakikisha Chango zinakuwa kwenye ubaridi unatakiwa muda wote. Kisayansi, hata chanjo ikitafitiwa na kutengenezwa Dar es Salaam, BADO ITAHITAJI KUTUNZWA KWENYE UBADIRI UNAOTAKIWA KWA AINA YAKE YA CHANJO. Ninaomba kuwasilsha,
 
Akizungumza katika kipindi cha Clouds 360, Waziri Dkt. Mwigulu Nchemba amesema watanzania wanapaswa kujiuliza chanjo za watu wa nchi zenye baridi zinawezaje kuwasaidia watu wa Dar es Salaam kwenye joto.

Mwigulu amesema ndio maana watu waliotoroka wakaenda kuchanja kimya kimya zinawaletea matatizo.

Chanzo: Clouds 360

Maendeleo hayana vyama!
Mwigulu acha siasa.Tunaka wanasayansi wetu watueleze ki-utafiti kwamba hizo chanjo zina madhara gani?Mbona wanasema tuu hazifai ila hawesemi utafiti wao unaonyesha mapungufu gani kwenye hizo chanjo.

Ndiyo maana tunaishia kusema habari za kisayansi zinashughulikiwa kisiasa.Tunaye waziri wa afya .atoe tamko kwamba kutokana na utafiti uliofanywa kwenye chanjo hizo,matokeo yanonyesha hazitafaa kwenye maeneo ya joto kama Dar es salaam ila zitafaa maeneo ya Bariki kama Arusha,njombe na Lushoto.

Hayo aliyoonge mwigulu ni matakataka kama mengine.

Wanasayansi wetu mko wapi?Mbona kimya?Au nyinyi wote mlisomea tiba lishe?
 
Tujiulize kama chanjo yao ni real sio feki kwa nini waliopata chanjo nchi zao wanawazuia wasisafiri kwenda nchi zenye Corona au zilizokataa chanjo?

mtu ukipata chanjo iwe a ndui au yellow fever ruksa kusafiri nchi yeyote hata iwe na huo ugonjwa.

wazungu wanaogopa nini si waruhusu watu wao waliochanjwa kwenda popote na ndege zao zianze kuruka kama kawaida kwenda popote duniani.

Hizo chanjo zao feki serikali ikomae hivyohivyo hakuna kuzipokea.Wazungu wasitufanye watanzania mabwege

Hakuna kupokea chanjo yao hata wakiileta bure
 
Akizungumza katika kipindi cha Clouds 360, Waziri Dkt. Mwigulu Nchemba amesema watanzania wanapaswa kujiuliza chanjo za watu wa nchi zenye baridi zinawezaje kuwasaidia watu wa Dar es Salaam kwenye joto.

Mwigulu amesema ndio maana watu waliotoroka wakaenda kuchanja kimya kimya zinawaletea matatizo.

Chanzo: Clouds 360

Maendeleo hayana vyama!
Sisi wa mikoani ya Iringa, Njombe, Mbeya na Kilimanjaro au Arusha.
Hatuhusiki etu
 
Tujiulize kama chanjo yao ni real sio feki kwa nini waliopata chanjo nchi zao wanawazuia wasisafiri kwenda nchi zenye Corona au zilizokataa chanjo?

mtu ukipata chanjo iwe a ndui au yellow fever ruksa kusafiri nchi yeyote hata iwe na huo ugonjwa.

wazungu wanaogopa nini si waruhusu watu wao waliochanjwa kwenda popote na ndege zao zianze kuruka kama kawaida kwenda popote duniani.

Hizo chanjo zao feki serikali ikomae hivyohivyo hakuna kuzipokea.Wazungu wasitufanye watanzania mabwege

Hakuna kupokea chanjo yao hata wakiileta bure
Sawa tengenezeni chanjo yenu kama hiO za wazungu ni feki


Halafu msizuie watu kuchanja. Watu wachague wenyewe kama wachanje au wasichanje.
 
Sawa tengenezeni chanjo yenu kama hiO za wazungu ni feki


Halafu msizuie watu kuchanja. Watu wachague wenyewe kama wachanje au wasichanje.
Ulaya na Marekani wamechanja watu wao kinachowafanya wawazuie watu wao kusafiri na ndege zao kuruka kwenda pipote duniani hata nchi zenye corona au zilizokataa chanjo ni nini? Hawaiamini chanjo yao? kama hawaiamini sisi ndio tuiamini?
 
Joto la binadamu ni 36.9oC bila kujali yupo wapi.
 
Ile chanjo inaingia mwilini kwenye joto la binadamu ambapo wote average joto ni sawa regardless unaishi wapi. Mbona ARVs, chanjo za homa ya ini, yellow fever, polio, surua, pepopunda etc zinatoka huko huko kwenye baridi?

Huyu bora angekuwa anaongelea mambo ya uchumi aliyosomea. Vitu vingine awaachie Wataalamu husika.
 
Back
Top Bottom