Dkt. Mwigulu: Kiswahili kitumike katika usaili wa Watumishi Serikalini

Dkt. Mwigulu: Kiswahili kitumike katika usaili wa Watumishi Serikalini

Ina maana mtu akikuuliza utakayofanya juu ya au kuhusiana na taaluma yako utashindwa kumwelezea kweli? Yaani utashindwa kujieleza kuwa nafanya au nitafanya hivi na vile? Labda umekariri tu na hujui unachokifanya au utakachofanya sambamba na taaluma yako.
Kama naweza kwa ung'eng'e nitashindwaje kwa lugha yangu adhimu niliyozaliwanayo..? Ila Binafsi Interview inayohusiana na professional husika kwa Kiswahili haimake sense..
 
Hiki ndo Kingereza unachovimbia.!!
Mimi sijasema kuwa najua kingereza mkuu sababu hyo lugha nimejifunzia ukubwani.. Ila mtu yeyote akiongea namuelewa na nikiulizwa swali siwezi kushindwa kujibu kwa sababu ya lugha ni ya kingereza, nitajipiga broken hivyohivyo Ila naamini muuliza swali atakuwa amejua kuwa nimemuelewa na nimemjibu LABDA kama hicho kitu sikijui kabisa maana unaweza kuulizwa swali kwa Kiswahili kama Hilo swali hulijui basi utashindwa kujibu Ila sio kwamba kiswahili/lugha hujui(Na ndo maana saili kama zinazofanywa PSRS wanaangalia zaidi CONTENT, unauliza swali toa ushirikiano ukimaliza unaamsha). kwahyo hata kama hapo nimeandika broken Ila mtu anayejua basi anajua kuwa nilikuwa na maana gani.. hiyo ndo point nazungumzia
 
Kufundisha iwe lugha hii hii ya kingereza tu maana kiswahili kufundishia kigumu nyie hebu fikiria
"Beautiful with a brain" itafsiri kwa kiswahili uone..

Kiswahili ni lugha ambayo misamiati yake mingi haijitoshelezi kabisa, na mnyambuliko wake haueleweki..

Hapo kwenye usaili ni sawa hata wakiuliza kwa kiswahili sababu nadhani unaulizwa tu kuhusu yale utakayoyafanya ukipewa kazi na malengo yako pia vitu kama hivyo basi..
 
Hii imekaa vizuri wengi wanashindwa kufanya interview sababu ya mkinzano na ujuzi mdogo wa kingereza

Haijakaa vizuri. Hatulazimiki kujua lugha moja tukasema basi. Elimu tuliyoopata imetolewa katika Kiingereza!! Ujuzi tulioupata umefundiswa kwetu katika Kiingereza.

Tusitumie udhaifu wa kutojua Kiingereza kukifanya Kiswahili kishike hatamu!! Taifa hili halifanyi mambo yake peke yake - kwa kushikilia Kiswahili huku tukijionesha tumepata maarifa kwa Kiingereza halafu Kiingereza kikatushinda - tunaonesha hatuna maarifa (waliopata ajira nje na mbali na eneo la Kiswahili wanatambua hili)!

Tufundishwe lugha zote mbili na tuzijue kwa ufasaha. Zipo nchi ni mfano!!! Tubadili mfumo na kuanza Kiingereza toka shule ya msingi - ingekuwa hivo tusingezungumzia hili.

Udhaifu wetu kwenye Kiingereza isiwe ndio ishara kwamba Kiswahili ni bora huku tumepewa maarifa kwa Kiingereza!!!
 
Wapwa hii kauli ya waziri mwenye dhamana kuhusu kutumika kwa kiswahili katika usahili imekaaje?itatiliwa uzito au bado kiingereza kitaendelea kutumika?
 
Haijakaa vizuri. Hatulazimiki kujua lugha moja tukasema basi. Elimu tuliyoopata imetolewa katika Kiingereza!! Ujuzi tulioupata umefundiswa kwetu katika Kiingereza.

Tusitumie udhaifu wa kutojua Kiingereza kukifanya Kiswahili kishike hatamu!! Taifa hili halifanyi mambo yake peke yake - kwa kushikilia Kiswahili huku tukijionesha tumepata maarifa kwa Kiingereza halafu Kiingereza kikatushinda - tunaonesha hatuna maarifa (waliopata ajira nje na mbali na eneo la Kiswahili wanatambua hili)!

Tufundishwe lugha zote mbili na tuzijue kwa ufasaha. Zipo nchi ni mfano!!! Tubadili mfumo na kuanza Kiingereza toka shule ya msingi - ingekuwa hivo tusingezungumzia hili.

Udhaifu wetu kwenye Kiingereza isiwe ndio ishara kwamba Kiswahili ni bora huku tumepewa maarifa kwa Kiingereza!!!

Umeandika mengi yasiyo na maana. Ujuzi ata ufundushwe kwa lugha za kikabila hauwezi kufa kisa umekutana na matumizi ya lugha mpya.

Lugha itatumika kujielezea wakati wa kufanya usaili kueleza wewe ni nani, umefanya nini, unafahamu nini, utasaidia nini.

Kama wewe ukishindwa wapo watakao weza. Kama vile wewe ulivyokua unaweza kingereza wengine wakawa wanashindwa
 
Kiswahili ndio lugha yetu inatambulika SADC na Umoja wa Afrika. Wazri wa fedha ahoji sababu ya kufanya usaili wa watumishi wa serikali kwa lugha ya kiingereza na kushindwa kukipa nguvu Kiswahili.

Ameshauri kishwahili kitumike katika usaili
Hii ni sawa sina pingamizi hata kidogo
 
Kwani wamesoma kwa kutumia kiswahili??

Masomo yote ni kiinglish isipokua lugha ya kiswahili.

It doesn't make sense at all.
Hapana mkuu makazini kinatumika kiswahili 80% hakuna sababu ya kufanya interview kwa kiingereza
 
unaweza kuwa na uwezo lakini lugha ikakupiga chenga .
watoto wengi wa English medium wanapata kazi kichwani 0 kinachowabeba ni kujua kiingereza Basi.
Kujieleza kaa kiingereza kusiwe kigezo Cha KUPATA KAZI
 
Itakuwa bora zaidi maana watu watafunguka na kuonesha ubora wao vyema. Ni katika lugha yako pekee ndio unaweza ukaeleza kwa kina na wanaokusikiliza wakakuelewa vyema na wala sio kwa lugha ya kigeni.

Tunashuhudia hata mashuleni na vyuoni Walimu wakitaka kufundisha kwa kina lazima atumie Kiswahili na hapo ndipo wanafunzi huelewa zaidi na umakini huongezeka mara dufu.

Naamini tutakuwa na uhuru kamili pale tutakapo tumia lugha yetu kwenye kila idara.
 
Hii imekaa vizuri wengi wanashindwa kufanya interview sababu ya mkinzano na ujuzi mdogo wa kingereza
Mfano unaulizwa law kiswahili wewe umesoma fizikia? Unajibu ndiyo

Unaulizwa elezea fizikia ni nini kwa kiswahili.Kama mtu hajafeli hugo interview kuliko.angehojiwa kiingereza
 
Back
Top Bottom