Dkt. Mwigulu: Kiswahili kitumike katika usaili wa Watumishi Serikalini

Dkt. Mwigulu: Kiswahili kitumike katika usaili wa Watumishi Serikalini

Kiswahili ndio lugha yetu inatambulika SADC na Umoja wa Afrika. Wazri wa fedha ahoji sababu ya kufanya usaili wa watumishi wa serikali kwa lugha ya kiingereza na kushindwa kukipa nguvu Kiswahili.

Ameshauri kishwahili kitumike katika usaili
hoja zake ni za ovyo vovyo sana.Kiswahili tayari kina nguvu za kutosha.Watu wanapaswa wafahamu kingereza zaidi ili waweza kujiuza katika masoko ya dunia.Dunia ni kijiji na hakuna faida ya kuishi kama kisiwa.Atuondolee hayo mawazo ya mwendazake
 
Kiswahili ndio lugha yetu inatambulika SADC na Umoja wa Afrika. Wazri wa fedha ahoji sababu ya kufanya usaili wa watumishi wa serikali kwa lugha ya kiingereza na kushindwa kukipa nguvu Kiswahili.

Ameshauri kishwahili kitumike katika usaili
na watoto wote wa watumishi wa Serikali wasomeshwe kwa kiswahili katika shule zetu za umma ili tuenzi lugha yetu ya kiswahili inayokua kila kukicha katika ukanda wa SADC.

Mtumishi yoyote wa umma atakayebainika anasomesha watoto wake shule za Private kwa lugha ya kigeni basi huyo anakizana na Sera yetu ya kukuza kiswahili na si Mzalendo.
 
Haijakaa vizuri. Hatulazimiki kujua lugha moja tukasema basi. Elimu tuliyoopata imetolewa katika Kiingereza!! Ujuzi tulioupata umefundiswa kwetu katika Kiingereza.

Tusitumie udhaifu wa kutojua Kiingereza kukifanya Kiswahili kishike hatamu!! Taifa hili halifanyi mambo yake peke yake - kwa kushikilia Kiswahili huku tukijionesha tumepata maarifa kwa Kiingereza halafu Kiingereza kikatushinda - tunaonesha hatuna maarifa (waliopata ajira nje na mbali na eneo la Kiswahili wanatambua hili)!

Tufundishwe lugha zote mbili na tuzijue kwa ufasaha. Zipo nchi ni mfano!!! Tubadili mfumo na kuanza Kiingereza toka shule ya msingi - ingekuwa hivo tusingezungumzia hili.

Udhaifu wetu kwenye Kiingereza isiwe ndio ishara kwamba Kiswahili ni bora huku tumepewa maarifa kwa Kiingereza!!!
Asante kwa maelezo mazuri.

Wenzetu Rwanda wapo viziro katika kinywarwanda na French na sasa wameanza kukimasta ata kiingereza.Mambo ya kung"ang'ania kiswahili ni ya kijima
 
Ina maana mtu akikuuliza
utakayofanya juu ya au kuhusiana na taaluma yako
utashindwa kumwelezea kweli?
Yaani utashindwa kujieleza
kuwa nafanya au nitafanya hivi
na vile? Labda umekariri tu na
hujui unachokifanya au
utakachofanya sambamba na
taaluma yako.
Et hawezi kujieleza kwa kiswahili kisa kuna baadhi ya maneno ya kiingereza hajui kiswahili chake au tafsiri yake kwa kiswahili.

Ni hoja ya ajabu kweli.
 
Basi na sisi mtu anapokwenda kuhojiwa kuhusu kazi ajieleze kiswahili.kama ana uwezo anao tu.
kiingereza kisiwe ndo kigezo Cha KUPATA kazi.
Kuna watoto nawajua kichwani 0.lakini kinachowabeba ni kujua kiingereza na wameajiliwa serikalini
Wewe unayeshindwa kujieleza kwa kiingereza unaonekana 0.
Kwanini kijana ashindwe kujieleza kwa lugha aliyofundishiwa?

O-level, A-level, chuo kikuu kote kinatumika kiingereza.

Kijana aliyepita kote huko akifundishwa kwa kiingereza, kutoa kisingizio cha kufeli usaili kisa lugha ni uzembe na mtu huyo hafai.
 
Basi na sisi mtu anapokwenda kuhojiwa kuhusu kazi ajieleze kiswahili.kama ana uwezo anao tu.
kiingereza kisiwe ndo kigezo Cha KUPATA kazi.
Kuna watoto nawajua kichwani 0.lakini kinachowabeba ni kujua kiingereza na wameajiliwa serikalini
Wewe unayeshindwa kujieleza kwa kiingereza unaonekana 0.
Sidhani

Shule za msingi wote darasa la saba hupewa mitihani mmoja wa taifa uwe umesoma kwa kiingereza au kiswahili

Wa kiingereza hupewa mitihani kwa kingereza alichosomea na aliyesoma kiswahili hupewa mtihani ule ule

Kaangalie matokeo ya darasa la Saba kitaifa shule ambazo huongoza kitaifa ni shule za msingi za kiingereza
 
Wengi watataka kuhojiwa kiingereza .

Wewe fikiria unaulizwa wewe kama Mkuu wa kitengo cha ajira leo ndio umemwajiri kazi Mkerengeza Mwandamizi.Utampangia majukumu gani huyo Mkerengeza Mwandamizi uliyemajiri ?

Hilo swali lazima ufeli sababu hata humjui huyo anayeitwa Mkerengeza ni mtu wa fani gani
Kabisa Mkuu,nimeshindwa kuelewa hapa,Elimu yetu haijatuandaa kujua kiswahili,watuache tu hivi hivi
 
Fafanua kidogo, unamaanisha uelewa wa hizo fani hauna maneno ya kiswahili? Maana kwenye usaili tunataka kujua ni nini unachokijua kuhusu kazi unayoiomba, sasa ukisema unaweza kuyasema hayo kwa lugha moja, ina maana umekariri au???? Au ni wapi sijakuelewa.



JESUS IS LORD
Ngoja nikupe mfano huu ameusema jamaa mmoja hapo,
 
Fafanua kidogo, unamaanisha uelewa wa hizo fani hauna maneno ya kiswahili? Maana kwenye usaili tunataka kujua ni nini unachokijua kuhusu kazi unayoiomba, sasa ukisema unaweza kuyasema hayo kwa lugha moja, ina maana umekariri au???? Au ni wapi sijakuelewa.



JESUS IS LORD
Wengi watataka kuhojiwa kiingereza .

Wewe fikiria unaulizwa wewe kama Mkuu wa kitengo cha ajira leo ndio umemwajiri kazi Mkerengeza Mwandamizi.Utampangia majukumu gani huyo Mkerengeza Mwandamizi uliyemajiri ?

Hilo swali lazima ufeli sababu hata humjui huyo anayeitwa Mkerengeza ni mtu wa fani gani
 
Watu wanafikiri wanakosa ajira kwasababu ya lugha ajira hakuna pia kiswahili ni kigumu sana kuliko kingereza
Upo sahihi Mkuu, tatizo ni ajira,Yani nafasi kumi tunaomba watu elfu nne,hapo hata kuwe na interview za kisukuma na kimasai mtu anakosa tu ajira
 
Kwa wale tulioishi South Africa, mtakubaliana na mimi kuwa wao kwenye Saili zao unachanganya English na Lugha yako ya asili ili kueleweka vyema.

Hata hapa ni sawa tu, hata usome nn huwezi kushindwa kuelezea namna gani hiko kitu kinafanya kazi kwa kiswahili, otherwise uwe umekariri maneno bila kujua maana yake.

Kiswanglish kitatumika katika kuelezea kitu kwa ufasaha.
 
Hiyo ni hotuba ya bajeti au ni hotuba ya Waziri Mkuu, wizara ya elimu au wizara ya utamadumi? Na hao watoto wetu wakishindwa kwenye usaili tutaomba na lugha yetu ya asili iwemo! Waendelewa hiyo huita "competition towards the bottom." Sawa na kupunguza kiwango cha ufaulu ili wanafunzi wengi wafuzu mitihani. Hivi Watanzania tunafikiri kweli!

Sent from my ONEPLUS A5000 using JamiiForums mobile app
Hapo sasa, anatwaga kote kote pamoja na wateuliwa. Swali dogo tu. Usaili kwa lugha ya kiswahili unasaidia vipi kuinua uchumi wa taifa au ajira kwa vijana wengi wanaoranda randa mitaani na vyeti vyao.
 
u
Kuna kitu amekisema kina ukakasi mbaya sana: kusamehe kodi kwa nyasi bandia kwa viwanja vya michezo/mpira kadhaa kama Arusha, Mwanza, Mbeya n.k. Maana yake ni kwamba ccm inaweka nyasi bandia viwanja vyake bila kulipia kodi.
umeona vyema!
 
Hapo sasa, anatwaga kote kote pamoja na wateuliwa. Swali dogo tu. Usaili kwa lugha ya kiswahili unasaidia vipi kuinua uchumi wa taifa au ajira kwa vijana wengi wanaoranda randa mitaani na vyeti vyao.
wako watu wenye uelewa mkubwa na wangefanya makubwa katika kuitumikia taifa lakini Lugha iksababisha washindwe kupata fursa.
 
Haliwezekani kingereza ndio I we lugh ya kusaili watu wanasiasa Ni wajinga Sana wanatufuruga tu
 
Hapana, kiingereza kiendelee kutumika kwa usaili wa wasomi wa ngazi ya degree kwenda juu!
... ni njia sahihi kabisa ya kujua kama kuna chochote ndani ya fuvu husika!
 
Waziri wa feza ametoka wapi na interview za utumishi wanae wanasoma feza boys je yey atakubali mwanae afunfishwe kwa kiswahili
Nchi hii unafiki umejaa hasa wa viongozi

Wabunge wote,viongozi wa Serikali na mahakama watoto wao wanasoma English medium halafu kinafiki wanasisitiza kiswahili mbona hawapeleki watoto wao shule za kiswahili? Hata wakifaulu kwenda sekondari za Serikali hawataki wanapeleka shule private

Kuondoa unafiki shule zote za Serikali zibadilishwe kuwa English medium
 
Back
Top Bottom