Dkt. Philip Mpango: Narudi kuchapa kazi, Mungu amenivusha. Leo siku ya 3 sijatumia mtungi wa Oxygen

Dkt. Philip Mpango: Narudi kuchapa kazi, Mungu amenivusha. Leo siku ya 3 sijatumia mtungi wa Oxygen

Amevuka hizi wiki mbili mlizomzushia kifo.

Ni kweli, japo alishuhudia wapinzani wakiuliwa na kupewa vilema ili ccm ikae madarakani kwa shuruti. Bora yeye kazuishiwa vifo, wapinzani wameuwawa kabisa ili ccm itangazwe washindi.
 
Mbona bado mgonjwa?? Tens sana tu! Iko wazi kwamba hao walioko pembeni yake wako hatarini, maana anakohoa tu uncontrollably!! hivi sisi huwa tunatumia nini kufirikiri?? hata tu mask ,, kama act of kindness (kulinda wengine)?? politics, na uchoyo!
 
Hawa ndio PhD holder tulio nao Tanzania.

Sishangai Msukuma anavyo watukana bungeni na wao kushangilia wakati wana tukanwa...
Hivi wengi inawezekana hamjui hiyo hapo mkononi mwake ni IV line ya kuwekewa dawa. Sasa kama mtu ana IV line maana yake ni kwamba bado anapata matibabu na Mpango bado ana IV line mkononi.
 
Amerudi KUCHAPA KAZI Kama alivodai
Back to ICU
Sijui kwanini hakujionea huruma! Alikuwa anaongea huku anahema juu juu ili TU kumfurahisha mkuu. Too bad

Mungu amsimamie apone.

Haikupaswa kutusuta walimwengu kabla hajapona vizuri.
 
Ni kweli, japo alishuhudia wapinzani wakiuliwa na kupewa vilema ili ccm ikae madarakani kwa shuruti. Bora yeye kazuishiwa vifo, wapinzani wameuwawa kabisa ili ccm itangazwe washindi.
Hii imekaa sawa? Inaingia vipi?
 
Amezungumza na waandishi wa habari akiwa hospitali ya Benjamin Mkapa Dodoma leo tarehe 23 Febr 2021, live kupitia TBC.

Amesema alikuja hapo hospitalini akiwa na mtungi wa Oxygen. Amekuwapo kwa zaidi ya wiki mbili. Na leo ni siku ya 3 hajagusa mtungi wa Oxygen, anapumua mwenyewe.

Tunafurahi sana kuona amepona.

Binafsi nafurahi zaidi kwa ushuhuda wake wa kwamba amepona kwa tiba rasmi za hospitali, na si kwa mambo ya kujifukiza na kupiga nyungu. Huu ni ushuhuda kwamba hizi ndizo huduma tunazopaswa kuzieneza kwa wote na kuhimiza wananchi wazitumie, na siyo kutupoteza kwa mambo ya nyungu.

Amesifu excellent professionalism ya madaktari wetu. Naomba ujumbe huu uwafikie wale wanasiasa wote wanaobeza madaktari wetu na kuwadhalilisha, na ujumbe uwafikie pia wale wanaohimiza uganga wa jadi. Mheshimiwa amekiri kuwa hii sekta inastahili kupewa kipaumbele zaidi.
Mkuu umeongea NENO...
 
Sijui nini kinaendelea katika dunia hii ya Tanzania? Kuna ulazima gani huyu mzee wa watu kuzungumzishwa katika vyombo vya habari. Kuna jambo linatafutwa. Bado mgonjwa huyu saa 48 ni chache sana.
 
Waziri wa fedha na mipango Dkt. Philp Mpango amesema anarudi kuchapa kazi baada ya mkono wa Mungu kumvusha na ugonjwa uliomkumba mpaka akalazwa.

Waziri Mpango amesema haya (Nukuu) - Narudi kazini na kazi ndogondogo nimekwishaanza za kulitumikia Taifa. Watanzania tuendelee kumwomba Mungu kwa kila mmoja na imani yake na atatuvusha. Amenivusha mimi na wengine ninaowaacha hapa atawavusha.

Nilikuwa nafungua mitandao, ni mambo ya ajabu sana. Nimeonja upendo mkubwa sana kwa wananchi wa Tanzania na wananchi wenzangu wa Buhigwe, wawe na amani na muda si mrefu nitakwenda kuwatembelea

Madaktari, manesi, wataalamu wa viungo, mpaka wahudumu nawashukuru sana kwa huduma nzuri mlizonipa katika kipindi chote. Ni vijana lakini wanafanya kazi kubwa sana"

Natoa pole sana kwa familia zilizopoteza wapendwa kwa wiki mbili nilizokuwa hapa na nyumbani. Ningeshiriki msiba wa Maalim Seif, Balozi John Kijazi na jana nimempoteza mwalimu wangu wa pekee, Profesa Benno Ndulu na mdogo wangu Atashasta Nditiye"

Kulikuwa na vishawishi, hamia Dar es Salaam, hamia huku nikasema hapana, hospitali ni nzuri kabisa na wataalamu walioiva. Sababu ya kukimbilia Ulaya, haipo. Tuboreshe vya kwetu na kwa nafasi aliyonipa Rais, nitamshauri kuboresha zaidi



Ikumbukwe watu wasio wema walizua taarifa za uongo kuwa amefariki baada ya kulazwa. Na tarifa hizo za uongo zilidai amefariki kwa ugonjwa wa Covid 19.

Dkt. Mpango alituma sms kwa mkuu wa nchi yetu kuwa amewasamehe waliomzushia uongo kuwa amekufa.Sasa wakimuona sijui watajisikia vipi. Aibu kubwa kwa wanafiki. Zaidi soma Dkt. Philip Mpango: Mimi ni mzima, walionizushia kifo nimewasamehe
Kama tumefika huku, basi tumepoteza muelekeo kama nchi. Maana hii ni hatari sana, huyu mh bado anaumwa haikuwa sahihi kabisa kumleta kwenye vyombo vya habari. Hata kama tunataka kuwaonyesha "mabeberu" kwamba maombi yamejibiwa lakini huyu mh bado anahitaji muda.
Daktari anae simamia matibabu yake ilitakiwa awajibike kwa kuhatarisha maisha ya mgonjwa anae mtibu.
Kwa sababu anafahamu kwamba mh alikuwa anatumia mtungi (oxygen) kumsaidia kupumua, hii maana yake ni kwamba wasiojulikana wameharibu mapafu hali inayopelekea mtu kupata tatizo la changamoto ya upumuaji.
Ikifikia mtu akiwekewa mtungi (oxygen) ina maana kati ya asilimia 1 adi 30 ya mapafu yake imeathirika, na hata kama wasiojulikana wametoka/wamedhibitiwa lakini ile athari/uharibifu waliofanya haindoki nao pamoja. Hivyo mgonjwa bado anahitaji uangalizi wa hali ya juu badala yakumuhangaisha kwenye vyombo vya habari.
Ndio maana mabeberu baada ya kugundua athari zinazo achwa na wasiojulikana hasa kwa wale waliofikia kutumia mtungi (oxygen) wameamua kuanza kinga kwa wazee, lengo lao sio kwamba wakipata maambukizi watakufa, bali lengo nikuwahi kuwalinda wasihathirike. Maana hata wakipona kwa wasiojulikana lakini athari zake mtu anaweza kuhitaji huduma ya mapafu katika uhai wake wote ulio baki, na athari zinazoachwa na wasiojulikana hazimo kwenye mifumo ya bima, ni jukumu la serikali kupitia mpango wa dharura na kwa kuwa gharama yakumtibu mtu mmoja kwa mwaka mzima ni kubwa kuliko gharama inayotokana na vifo vya watu 10 kwa mwaka mzima ndio maana wanamuangalia mtu kwa ukaribu zaidi adi afya yake kuimarika badala ya kumkimbiza kwenye vyombo vya habari.
Hivyo waliofanya ama kushirikiana na mh kufanya maamuzi yakuzungumza na vyombo vya habari na daktari wake kuruhusu hilo, wote kwa pamoja wamefanya jambo ambalo ni hatari sana kwa afya yake na ni hatari pia kwa taifa kutokana na nafasi yake.
 
sasa hao walio hapo pembeni ... duuuuuh Mungu awasaidie. Pole mzee wetu Mpango. Mungu aendelee kukupigania.
 
Back
Top Bottom