Dkt. Philip Mpango: Narudi kuchapa kazi, Mungu amenivusha. Leo siku ya 3 sijatumia mtungi wa Oxygen

Dkt. Philip Mpango: Narudi kuchapa kazi, Mungu amenivusha. Leo siku ya 3 sijatumia mtungi wa Oxygen

Jambo la kheri ni kwamba anapata nafuu, nafurahi kuona na kusikia hivyo japo ningefurahi zaidi kama angetahadharisha kuhusu COVID ili wengine nao wachukue tahadhari, angalau ushuhuda wake ingesaidia wengi.

Suala ninaloliona hapa ni kwamba ukimsikiliza sana Dr. Mpango ni kama anasisitiza zaidi tiba ya (Kisayansi) hospitalini japo anagusia gusia mambo ya vyungu, all in all ndugu zangu, tuchukue tahadhari, hatujui mpango kaawacha wangapi bado wapo kwenye mitungi hapo hospitalini, tuwaombee wapone maisha yaendelee.
 
Kwani kuna Corona au anataka tu kumuumbua boss wake. anyway i just wish him a very quick recovery.! Tunaamini atakuwa balozi mzuri kwa wanaobeza kuwa tatizo la corona halipo nchini
 
Kumbe alikuwa anaumwa kweli? Nilijua mijamaa ilikuwa inazusha tu.

Mshukuru sana Mungu, usije ukakufuru ukamshukuru yule jamaa yetu kama walivyofanya wale vigogo wa Pentekoste.
Aisee!
 
Bado anaongea kwa taabu, sijui kwanini wamemruhusu kuongea na waandishi.

Ameongea kwa huzuni sana kuhusu waliofariki, nimeona kama machozi yamemlenga lenga.
Tatizo lilikukuta ndiyo utajua ugumu wake lakini bila hivyo watabakia kushabikia tu
 
Waziri wa fedha na mipango Dkt. Philp Mpango amesema anarudi kuchapa kazi baada ya mkono wa Mungu kumvusha na ugonjwa uliomkumba mpaka akalazwa.

Waziri Mpango amesema haya (Nukuu) - Narudi kazini na kazi ndogondogo nimekwishaanza za kulitumikia Taifa. Watanzania tuendelee kumwomba Mungu kwa kila mmoja na imani yake na atatuvusha. Amenivusha mimi na wengine ninaowaacha hapa atawavusha.

Nilikuwa nafungua mitandao, ni mambo ya ajabu sana. Nimeonja upendo mkubwa sana kwa wananchi wa Tanzania na wananchi wenzangu wa Buhigwe, wawe na amani na muda si mrefu nitakwenda kuwatembelea

Madaktari, manesi, wataalamu wa viungo, mpaka wahudumu nawashukuru sana kwa huduma nzuri mlizonipa katika kipindi chote. Ni vijana lakini wanafanya kazi kubwa sana"

Natoa pole sana kwa familia zilizopoteza wapendwa kwa wiki mbili nilizokuwa hapa na nyumbani. Ningeshiriki msiba wa Maalim Seif, Balozi John Kijazi na jana nimempoteza mwalimu wangu wa pekee, Profesa Benno Ndulu na mdogo wangu Atashasta Nditiye"

Kulikuwa na vishawishi, hamia Dar es Salaam, hamia huku nikasema hapana, hospitali ni nzuri kabisa na wataalamu walioiva. Sababu ya kukimbilia Ulaya, haipo. Tuboreshe vya kwetu na kwa nafasi aliyonipa Rais, nitamshauri kuboresha zaidi



Ikumbukwe watu wasio wema walizua taarifa za uongo kuwa amefariki baada ya kulazwa. Na tarifa hizo za uongo zilidai amefariki kwa ugonjwa wa Covid 19.

Dkt. Mpango alituma sms kwa mkuu wa nchi yetu kuwa amewasamehe waliomzushia uongo kuwa amekufa.Sasa wakimuona sijui watajisikia vipi. Aibu kubwa kwa wanafiki. Zaidi soma Dkt. Philip Mpango: Mimi ni mzima, walionizushia kifo nimewasamehe
Kwani alipatwa na nini? Mbona mafumbo mafumbo?
 
Hayo yote ni bure bila msaada wa Mungu.

Nae amesisitiza Mungu kamponya, wangapi kwan wanafia mhimbili au India!!?
 
Waafrica hawajaizingatia corona
In short Corona Africa imepotea njia
 
ukiumwa usiiingie mitandao ya kijamii kuna mapepo kazi yao kukuombea kifo.
 
Hizi siasa hatari sana mtu ulikuwa ICU kwenye koma situation siku unachomolewa oxygen unatoka mkuku kwenda kuongea na media bila hata kupumzisha misuli ili tu ku prove mtu wrong.
Mpango anawapenda watanzania,anataka kyshare nanyi exprience,,that is why?
 
Duu! Kwa hiyo kila mtu anatakiwa anunue mtungi wake wa oxygen kwa kujihami?
Hivi hiyo mitungi inauzwa pesa ngapi mkubwa,halafu kumbe asingekuwa na mtungi wake wa oxygen sasa hivi angekuwa anacheza karata na akina Kijazi huko kuzimu kwa waiba kura
 
Hivi hiyo mitungi inauzwa pesa ngapi mkubwa,halafu kumbe asingekuwa na mtungi wake wa oxygen sasa hivi angekuwa anacheza karata na akina Kijazi huko kuzimu kwa waiba kura
Una roho ya kichawi.
 
Baada ya kushindwa kuficha korona sasa wagonjwa wanaandaliwa press conference. Ila watanzania.wenye utimamu wameshajielewa, hata viongozi wa dini hawapo upande wa waficha maradhi. Failed leadership
 
Back
Top Bottom