Harmonize sio authority yoyote katika uislamu.
Harmonize alisha ukana uislamu kwa vitendo tangu alipo ingia kwenye kazi ya muziki kwa sababu kwa mujibu wa mafundisho ya dini ya kiislamu muziki ni haramu kama ilivyo nyama ya nguruwe .
Kwa hiyo kwa hermonize kuingia kwenye muziki tayari ameshajitoa kwenye uislamu.
Harmonize kasema kwamba kwa miaka 30 aliyo ishi duniani anadhani kwamba huenda Mungu ni mwanamke.
Harmonize was talking about a personal experience that he had with God.
Kwa mambo mema na mazuri ambayo Mungu amemtendea yeye kama yeye katika maisha yake Binafsi basi ameshawishika kuamini kwamba huenda Mungu akawa ni mwanamke...
Harmonize ameutathmini upendo ambao Mungu amemuonyesha kwenye maisha yake kisha akaufananisha na upendo wa mama yake mzazi.
Sasa ana kosa gani akisema kwamba ana amini kwamba huenda Mungu ni mwanamke?
Harmonize sio wa kwanza kutoa kauli hii hata Shaggy aliwahi kuimba kwenye wimbo wake " strength of a woman" kwamba anafikiri huenda Mungu akawa ni mwanamke.
Kitu kimoja ambacho nimegundua kuhusu viongozi na walimu wa dini zenu kuu mbili ukristu na uislamu ni kwamba these guys have got a very little and limited understanding about God. They think they know everything about God. Halafu wamemuwekea Mungu mipaka kwa maana ya kwamba wanaamini Mungu hawezi kuwa hivi wala vile. To them Mungu anaweza kuwa vile tu alivyo elezewa kwenye vitabu vyao na sio tofauti na hapo.
Yani wamemfunga Mungu kwenye vitabu vyao.
Kwa upande wa wakristu Mungu kwao alipewa majina tofauti tofauti kwa nyakati tofauti based on the personal experiences that he had with those people.
Mfano aliitwa Mungu wa Ibrahim kwa sababu ya his experience with Abraham.
Aliitwa Mungu wa Isaka kwa sababu ya his experience with Isack.
Aliitwa Mungu wa Yakobo kwa sababu ya his experience with Jacob.
Tundu Lissu alivyo shambuliwa kwa risasi mwaka 2017 na kisha aka survive watu wengi walisema ni Mungu ndio alimuokoa. Kama Lissu angeishi in Biblical times huenda leo tungekuwa na Mungu wa Tundu Lissu. Mungu mwenye kuokoa na hatari mbaya.
Je kwako wewe Binafsi based on your personal experience with God Mungu ni nani kwako? Mungu wako angeitwa nani? Mungu wa Likud angeitwa nani?
Kwa Harmonize yeye based on his personal experience with God kwake yeye Mungu ni Mama kwake ( mwanamke)
Kwa upendo ambao Mungu amemuonyesha Hermonize yeye anamfananisha Mungu wake na mama yake.
Jamani hivi duniani kuna kiumbe mwenye upendo wa kweli kama Mama?
Hata wewe Dr. Sule anae kupenda kuliko chochote ni Mama yako.
Hata wewe Dr. Sule ukiambiwa uchague kitu kimoja kati ya Mungu wa kwenye kitabu chako na mama yako mzazi alie kuzaa utamchagua mama.yako.
Chid Benz aliwahi kuongea point moja kubwa sana akasema.mama zetu ndio Mungu zetu. Hawa ndio walio tuumba kwenye mafumbo yao. Tunatakiwa kuwatazama kama.miungu.
Hata Mtume Muhammad (pbuh) aliwahi kuulizwa na swahiba wake " nifanye nini ili niende mbinguni"
Majibu ya mtume yalikuwa :
1. Mpende mama ako.
2. Mpende mama ako.
3. Mpende mama ako.
Mtume hakusema " mpende Mungu wako" la hasha. Alisema " mpende mama ako"
Uislamu unatuelekeza mama.ndio pepo yako.
Harmonize yupo sahihi sana kuliko Dr. SULE.
UPENDO WA MUNGU NI SAWA NA UPENDO WA MAMA.
Kama Hermonize angekuwa ni shekhe na akasema maneno hayo kama.shekhe ungeweza kumchallenge kidogo kwa sababu mashekhe na wachungaji/ mapadri huwaga hawana tumiagi fikra zao huru ktk kutoa maoni kuhusu Mungu . Wao huwa wana quote kilicho andikwa kwenye vitabu vyao.
Harmonize sio shekhe ndio maana ametumia mawazo yake Binafsi.
So Dr. Sule na wote mnao mtukana hermonize stop being selfish. Acheni kutaka kila mtu akiamini kile mnacho kiamini nyinyi.
Kwa hiyo Hermonize yupo sahihi kabisa..
1. Uislamu una taratibu zake.
2. Dhambi kwenye uislamu Zina madaraja tofauti.
3. Kuwa muislamu ni kuwa na shahada mbili. Kwa maana yake halisi. Kwamba jambo lolote la ibada hutamfanyia mwingine yeyote ispokuwa Allaah. Na lazima uamini Muhammad ni mja na mtume wa Allaah. Si mwana wa Allaah wala mshauri wa Allaah. Yeye ni mwanadamu kama wengine. Ila yeye aliletewa ufunuo. Hivyo, kwakuwa yeye aliletewa ufunuo ndiye aliyetufundisha ibada,na jinsi ya kuitekeleza. Maana ya shahada ya pili ni kuwa,sitafanya ibada yeyote ila Kwa muongozo na kumuiga Muhammad.
Kwa maana hiyo muislamu ni yule anayeyafuata hayo kikamilifu.
Kinyume na hivyo unaweza ukatoka kwenye uislamu au ukahukumiwa kuwa si muisla. Na hili la kuhukumiwa lina taratibu zake. Na wanaoweza kutoa hukumu hiyo ni wanachuoni wakubwa waliobobea kwenye ilmu.(Kwa maana hiyo, Sule amekosea kutoa hukumu wakati yeye si mwanachuoni)
Wasio wanachuoni nafasi yao ni kukumbisha,kunasihi na kufundisha.
Harmonies sio mwanachuoni. Anapewa dharura ya ujinga. Hajui uzito wa maneno aliyoyasema. Atabaki kuwa ameasi Kwa kutenda dhambi kubwa hadi pale taratibu zitakapokamilika na kupelekwa suala lake Kwa wanazuoni.
Ama suala la muziki ni kweli ni haramu. Lakini halimtoi mtu kwenye uislamu.
Ama hadithi uliyoitaja kwamba ni mafundisho ya Mtume,si sahihi.
Bali Mtume aliulizwa kuhusiana na baba na mama, nani afanyiwe wema zaidi?
Akajibu,
Mama yako mara tatu ndio akajibu "baba yako" kwamaana mama anastahili kufanyiwa wema mara tatu zaidi ya baba.
Hivyo, Kwa mujibu wa Sheria ya kiislamu, konde boy kafanya kufru ila hajatoka kwenye uislamu hadi aukane uislamu mwenyewe au ahukumiwe na wanazuoni kwamba si muislamu.
Muhimu utambue kwenye uislamu Kuna kufanya tendo la kufru na Kuna kukufuru. Kama Ilivyo unaweza kufanya tendo la ushirikina na kuwa mshirikina. Ni vitu tofauti.