..Augustino Mrema naye alijiona ana nguvu sana akatofautiana na msimamo wa serikali, Rais Mwinyi wala hakupoteza muda kumuondoa.

..Huyu asipochukuliwa hatua itajenga mfano mbaya na nidhamu inaweza kutoweka ktk wateule wa Raisi.
Mhe. Jokakuu hata mimi nimetangulia kusema kwamba huyo RC kakosea. Mamlaka za uteuzi ndo zenye kauli ya mwisho. Ila tukubaliane kuwa Mtaka anakubalika sana.
 
..Augustino Mrema naye alijiona ana nguvu sana akatofautiana na msimamo wa serikali, Rais Mwinyi wala hakupoteza muda kumuondoa.

..Huyu asipochukuliwa hatua itajenga mfano mbaya na nidhamu inaweza kutoweka ktk wateule wa Raisi.
Tumsamehe. Nafikiri lipo jambo lilimtokea maana kwa jinsi alivyo ni ajabu kutoa lugha zisizo za kiungwana kiasi kile kama vile ana ugomvi binafsi.
 
Huu uongo mmeutoa wapi? Hiyo nguvu ya umma mtaka kaipata lini? Mbona Kama huyu mtu mnamuabudu sana?
Sio hiyo nguvu ya umma ya CHADEMA. Hizi za Mtaka ni zile halisi sio hizo nguvu za KVANT za chadema
 
Mtaka ana hoja, tatizo kuu ni yale mashambulizi kwa boss wake tena very personal. Mtaka si mtu wa mambo hayo, nafikiri lipo jambo.
 
Waziri yupo sahihi,

Muda wa kazi wa Serikali ni saa tisa na nusu.

Waziri kafuata sheria ya kazi ilivyo.

Kinyume na hapo ni fujo.

RC amemkosea heshima Waziri.

Hakupaswa ajibu.Angepiga kimya na akaendelea na mipango yake kimya kimya tu.
Ubinafsi wenu ndio unaowafelisha watoto wa masikini,na agenda zenu ni kutaka watoto wenu tu ndio wawe wasomi, selfish katika ubora wenu
 
Hapa nimekukubali mkongwe. BTW ameomba radhi kiungwana. Tusahau tusonge mbele. Ni mtu mwema na mchapakazi.

..kama ameomba radhi basi naunga mkono RC Mtaka asamehewe.

..wahenga walisema, " we learn from our mistakes. "
 
Mtaka tumemsifia sana sasa kalewa sifa! Anajiona very exceptional
Mtaka ni mjita,anatokea kabila moja na
Mtaka kakosea sana
 
Nijenge hoja kwa mtu mpumbavu?
 
Mhe. Jokakuu hata mimi nimetangulia kusema kwamba huyo RC kakosea. Mamlaka za uteuzi ndo zenye kauli ya mwisho. Ila tukubaliane kuwa Mtaka anakubalika sana.

..wamesema ameomba RADHI.

..hilo ni jambo la kiungwana.

..litamsaidia yeye Mtaka kuwa makini zaidi.

..pia atakuwa ameonyesha mfano mzuri kwa walioko chini yake, na wananchi kwa ujumla.

..binafsi ningefurahi kama RC Mtaka angekwenda kuomba msamaha mbele ya wale wanafunzi aliwaambia wampuuze Waziri wa Elimu.
 
Yaani Mtaka alete impact gani acheni masihara
 

Badala ya kujadili swala la msingi tunataka kujadili nani mkubwa zaidi. Yaani hapa yunatakiwa tuangalie maslahi ya watoto kwanza. Nakumbuka wakati nikiwa Ilboru pale wote tuliwekwa sawa bila kijali wewe ni mtoto wa nani lakini siku hizi shule ni kwa matabaka na viongozi wengi watoto wao hawako shule za kata. Wakati wetu watoto wa wakulima, mawaziri, mabalozi, viongozi wa mikoa tulikuwa kitu kimoja. Hii imesababisha watoto kujiamini mtaona watoto wa wakulima pale Ilboru kama Lissu na Nyalandu wametoka kama sio washamba kwasababu ya kuwachanganya .
 
Mkuu wa mkoa ulipaswa kwenda kuzungumza na waziri faragha sio public kama hivyo. Hapo umekosea mkuu.

Mkuu wa mkoa anapata nguvu wapi ya kupinga maagizo ya Waziri jamani.

Tena maagizo ya waziri wa elimu jamani tena mbele ya wanafunzi kweli.

Waziri hawezi kuwa chanzo cha mkoa wako kuwa wa mwisho. Kwani Mikoa yote ni ya Waziri, na katika hiyo mikoa lazima mmojawapo uwe wa mwisho na mwingine uwe wa, kwanza hata kama yote ikifaulu vizuri.

Mkoa ukiwa wa mwisho wa kuulizwa ni wahusika wa mkoa huo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…