Dodoma: RC Antony Mtaka amchana Waziri wa Elimu kuhusu mwisho wa Watoto kusoma kuwa ni saa tisa
Kisiasa huyo Mkuu wa mkoa kakosea sana. Alichofanya ni utovu wa nidhamu kwa serikali na Chama Cha Mapinduzi. Sema huyo RC ana nguvu kubwa sana ya umma nyuma yake... kumtumbua kizembe inaweza leta mtikisiko. Waziri angetulia zake na kufanya mambo yanayomhusu. Hii kuingilia hadi watoto wasomeje ni upumbavu kwa hadhi ya waziri.... waziri adili na mambo ya madawati, mitaala, maslahi ya walimu na mambo mengine ngazi ya kitaifa. Kambi za wanafunzi ni jambo dogo mno. Tusubiri uamuzi wa Mwenyekiti wa CCM (Rais wa JMT) katika hili.

..Augustino Mrema naye alijiona ana nguvu sana akatofautiana na msimamo wa serikali, Rais Mwinyi wala hakupoteza muda kumuondoa.

..Huyu asipochukuliwa hatua itajenga mfano mbaya na nidhamu inaweza kutoweka ktk wateule wa Raisi.
 
Kuna ulazima gani wa kumshambulia waziri na familia yake? Kuwa realistic hakuondoi utu brother. Vipi kama wewe ni kiwete nikikuita wewe kiwete njoo hapa? Si realistic? Kwanza kiuongozi huwezi kumzodoa boss wako hadharani namna ile.

Zipo channel za kuchallenge mambo ya utawala! Huu ujasiri si wa bure, Ndalichako ndiye waziri mwenye dhamana ya elimu na aliyemteua ndiye mwenye responsibility ya kumuwajibisha na si huu uhuni.

Kwahili hastahili hata kuomba radhi bila kujivua ukuu wa mkoa maana ameongea kwa msisitizo na kurudia mara nyingi akijua anachofanya.

Wewe unajua, mwambie mtu hapo Chadema amkosoe Mbowe hadharani uone kama atabakia salama! Kuna miiko ya uongozi na Mtaka hajakosea tu bali amekoroga sifa yake njema tuliyomsifia muda mrefu.
Mkoa fulani ukifeli analaumiwa Waziri au Mkuu wa Mkoa?.
 
Swala la Elimu yetu kufanywa kama mpira wa danadana na kila mmoja kuwa anachezea, ni makosa makubwa sana, mwongozo wa pamoja uko wapi?

Napingana na huyo mkuu wa mkoa wenu pendwa, Inakuweje awe na mpango wa kivyake vyake?

Mkuu wa mkoa wa Songea naye awe na matakwa yake, na wa mikoa mingine, tutakuwa taifa la aina gani?
We pingana naye sisi tunaenda naye
 
..Nakubaliana na wewe kwamba RC Mtaka hakutakiwa kumshambulia Waziri Ndalichako waziwazi kana kwamba hawatumikii serikali moja.

..Mtaka angeweza kuwaambia waalimu na wanafunzi waendelee na kambi zao za mafunzo ya ziada, na yeye kama RC wao atakwenda kuzungumza na Waziri wa Elimu ili kuweka mambo sawa.

..Mambo ya international school, sijui gari yenye kiyoyozi, etc etc hayakupaswa kuzungumzwa na RC mwenye heshima zake kama Mh.Mtaka.
Umeiweka vizuri
Ujumbe ulikuwa mzuri
Maneno sio
 
Mtaka Hana adabu kabisa. Nigelikuwa Samia I would have fired him immediately. Angelitafuta forum ya staha kusema aliyoyasema na si kubwatuka mbele za wazazi kumdhalilisha mteule mwenzake. Mtu anaweza kugeneralise kuwa the gov is disunited in it's dealings Amesema màneno ya kishenzi akiwa part of the government machinery.

Hafai kukalia ofisi ya umma.
Ndio hujawa Samia!
 
Safi Sana Mh MTAKA ,mawaziri wanajikuta Sana ,na kwenye elim wametuvuluga Sana
Mawaziri mara nyingi ni kama hujiamulia baadhi ya mambo, sitasahau JJ Mungai akiwa Waziri wa Elimu walivyoruhusu Physics na Chemistry kuwa somo moja eti wakaliita Phys-Chem.

Sijui walikuwa wanafikiria nini??

Ifikie wakati Elimu isifanyiwe mzaha na Wanasiasa.
 
Waziri hajatoa agizo kwa feelings zake, ipo miongozo ya elimu. Badala ya kushambulia mtu angejikita kwenye mabadiliko kisera na nafasi hiyo anayo. Lakini pia anaweza kuwasiliana na waziri au hata Rais kwa marekebisho kama ana hoja.

Kwanini amdhalilishe waziri? Unajua matokeo ya kauli zake ikiachwa namna hii bila kuwajibika?

Nimesema wewe unajua vyema, Mbowe hata kama akiongea jambo hadharani akakosea kuna mtu pale ufipa anaweza kutoka hadharani kumkosoa akabaki salama? Uongozi una miiko yake lakini tukienda hivi mawaziri wataachia wakuu wa mikoa wafanye wanalotaka.

Mama Samia anapaswa kunyoosha rula. Huu ni utomvu wa nidhamu anapaswa kuchukua hatua ili viongozi waheshimiane otherwise tutasikia mengine na mwisho serikali kuwa dhaifu.
Mkuu 'MTAZAMO', leo umetoka vizuri sana na kueleweka vyema, at least na mimi kuhusu hayo uliyoandika hapo juu.

Pamoja na kukubaliana na wewe, nakataa hiyo dhana unayoitetea kutokana na mazoea mabaya ambayo tumekwishayashuhudia hapa nchini.

Unalotetea hapa ni kulinda uozo uleule unaoendelea wa kuabudu viongozi hata kama wanafanya mambo ya kipuuzi. Tumefika hatua sasa ya kukataa, hata kama ni hadharani kama alivyofanya Mtaka. Mambo ya kufunikafunika unayoyatetea ndiyo yaliyotufikisha hapa. Unafiki ndio umekuwa sifa ya kuonekana kuwa kiongozi mzuri!.

Ni wakati sasa, kiongozi anayejuwa anakerwa na jambo, aliseme waziwazi, tuondokane na hii tabia mbovu ya kulalamikia pembeni.

Namuunga Mtaka mkono, na kama Samia anachembe yoyote ya uongozi ndani yake, angeanzia hapa kukataa unafiki kwa kumuunga mkono Mkuu wa mkoa wake.
 
Jamaa kaongea ukweli kabisa, mawaziri wengi wanaongozwa na matamko toka juu tu.
Wadau mnasema angetafuta namna ya kumjibu amjibu vipi sasa kama hoja za watu wa chini hasikilizwi. Wacha awaambie wananchi wake.

Mliosoma izo private sio rahisi kumkubali huyu RC, matamko ya viongozi yanaathiri sana elimu ukizingatia hapa nchini kila mkoa ni tofauti na mkoa mwingine kwahiyo strategy zilizotumika mkoa huu si rahisi kutumika na kiufasaha mikoa mingine pia. Mikoa ingeachiwa walau nafasi ya kutatua matatizo yao kulingana na changamoto zilizopo
[emoji106][emoji106]. Mkoa wa Njombe wana mkakati huo wa kambi toka miaka mingi unaitwa "UWANJO". Msingi wa kambi hizi ni kuwa Wanafunzi ambao ni senior pamoja na walimu wa shule husika husaidiana kuwaanda wanafunzi wanaojiandaa kufanya mitihani ya Form IV.
Wanafunzi wa Vyuo Vikuu na walimu wa shule husika husaidiana kuwaanda wanafunzi wanaojiandaa kufanya mitihani ya Form VI.
Hivyo RC Mtaka yuko sahihi kabisa. Anaanzisha kitu ambacho mikoa mingine kilishaanza miaka mingi iliyopita.
 
Mawaziri mara nyingi ni kama hujiamulia baadhi ya mambo, sitasahau JJ Mungai akiwa Waziri wa Elimu walivyoruhusu Physics na Chemistry kuwa somo moja eti wakaliita Phys-Chem.

Sijui walikuwa wanafikiria nini??

Ifikie wakati Elimu isifanyiwe mzaha na Wanasiasa.

..shule ya msingi phys-chem-bio yamechanganywa na kuitwa SAYANSI.
 
Back
Top Bottom