DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali

DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali

Mungu amsaidie Mh Tundu Lisu apone arudi kulitumikia Taifa lake..mtetezi wa kweli wa haki zetu!
 
Subiri ujue amepigwa wapi hiyo risasi pia.. na acha kusingizia mamlaka wakati unajua na yeye ni msaliti na labda tapeli kwa anaowasaidia kuiba mali za nchi yetu.. pesa kala na ugumu wa serikali unaendelea kuwanyoosha wanaompa bahasha kuvuruga..
Wafuasi wa ccm hamtofautiani na viongozi wenu kwa roho za kikatili..weka uthibitisho hapa kuwa kaliibia taifa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Eeeh Mwenye Enzi Mungu twakusihi utende muujiza wa Uponyaji wa haraka Kwa mtoto wako Tundu Lisu , nakusihi Mungu mponye haraka mfanyie wepesi wa kupona Hata madaktari na wauguzi washangae Baba ili Utukufu wako uzidi kuinuliwa, na wale watesi waliotaka kumwangamiza waaibike kisha Wewe Ndiyo Ujue namna ya ambayo ni zaidi ya hizo bastola, eeh Mungu twakuomba utusikie [emoji24][emoji24][emoji24]
 
Huu mwanzo tu, tutarajie mengi yajayo kwani washachoka kuwekana mahabusu.

What goes around comes around
 
Hebu jiulize kwa nini watu humu ndani hawajafikiria sababu moja kati ya hizi ulizoorodhesha.............. Kwa sababu siku hizi imekuwa kawaida kwa mauaji ya ajabu ajabu kutokea, hakuna hatua za dhati kutafuta chanzo na wanaohusika.

Mara paaaap Tume ya Katiba anapigwa risasi. Watu wa assume unatafuta kiki na support ya kimataifa?

Yawezekana isiwe kama wengi tunavyofikiria lakini hali ya nchini sasa hivi hakuna aliye salama. Vyombo vinavyopaswa kutupa amani na ulinzi ndivyo vinavyotumika kutunyanyasa na kututesa.

Yawezekana ni
1. Wazee wa makemikia
2. Ugomvi wa madaraka ndani ya chama
3.Ugomvi wa madaraka ndani ya TLS
4. Wamedhurumiana na ACACCIA kwenye
5. Ugomvi wa mahusiano
6. Wapiga kura wake wana hasira na kushindwa kutekeleza ahadi
7. Kutafuta kiki na support za kimataifa
8. Mabepari wamempiga ili kuchochea vurugu
9......



Sent using Jamii Forums mobile app
 
d211975414e40891a7251e59ef944aff.jpg
 
"Naomba kabla sijaanza Mazungumzo yangu nimuombe Mkuu wa idara ya Usalama wa Taifa anaitwa Kipilimba au Inspekta Generali wa Polisi Simon Sirro, wale vijana ambao wamewatuma na kwa wiki tatu mfululizo wananifuata kila nilipo wanaotembea na gari ya Toyota premio namba T460CQV, jana niliwakaba Kanisani St. Peter's.
 
Back
Top Bottom