Droo ya Hatua ya Makundi CAF: Yanga yapangwa na TP Mazembe, Simba wapangwa na Raja Casablanca

Alafu ndugu zangu Simba hivi hamjui kama nanyie mnapangwa mda sio mrefu na nyie ndio mnabalaa zaidi maana target yenu ni nusu fainal ili Hali mna kikosi kibovu sana kuwahi kutokea toka Dunia iumbwe..

Hizi nguvu mnazotumia kuwananga Yanga kwann msingezitumia kumwomba Allah ili awanusuru na droo ngumu itakayowatia aibu ya mwaka Kwa vipigo mnavoenda kukutana navyo[emoji848][emoji848][emoji848]
 
Amka utajinyea
 
Kwamba mtu mmoja tu kachezesha droo ya kombe la luza, nawaona watu wanne kwenye kombe la wanaume.
 
Ila kusema ukweli Simba awamu hii hatuendi robo fainali, hatuna timu imara ya ushindani.

Timu nyingi ziko vizuri kuliko sisi japo tutajitetea kwa maneno mengi ila ukweli ndo huo, hatuwezi tembelea historia ya nyuma ambako tulikuwa na timu yenye ushindani na morali ya hali ya juu.

Kwa sasa tunagombana huko ndani mambo hayako sawa na mwezi February sio mbali ambako tutaanza kunyolewa na mabeberu yaliyowekeza cash tofauti na sisi wazee wa akina bhebhe wanasusa susa mithili ya mwali mwenye mimba changa
 
Mkuu ilikuwaje ukawa miongoni mwa mbumbumbu wakati unazo akili nyingi kiasi cha kuona huu ukweli?? Ushauri wangu hebu ondoka kwenye iyo timu kabla hawajakuambukiza Umbumbumbu hao watu
 
Mkuu ilikuwaje ukawa miongoni mwa mbumbumbu wakati unazo akili nyingi kiasi cha kuona huu ukweli?? Ushauri wangu hebu ondoka kwenye iyo timu kabla hawajakuambukiza Umbumbumbu hao watu
Ukweli unakuweka huru, mwaka huu hata huku kwenye ligi ya NBC tukiwa mikoani ni tiamaji tiamaji, Simba mwendo tumeumaliza.
Atakayebisha analeta ushabiki lakini hali inayoendelea ni ngumu kwetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…