Droo ya Hatua ya Makundi CAF: Yanga yapangwa na TP Mazembe, Simba wapangwa na Raja Casablanca

Ukiachilia mbali kipigo kinachoenda kuwapata huko nje ya nchi, sidhani kama mtaweza kupeleka timu.

Bus lenu limewashinda kukomboa, nauli za ndege mtaziweza?
Mambo yote yanafanyika kimahesabu

Wote hao wana point 9 zetu kwa mkapa

Kati ya hao kuna natafuta mmoja wa kutoa sare naye kwake ikiwezekana na kipigo kabisa

Baada ya hapo hata unifunge goli 5 haiwezi fanya nisipite

Ni swala la hesabu tu
 
Ukweli unakuweka huru, mwaka huu hata huku kwenye ligi ya NBC tukiwa mikoani ni tiamaji tiamaji, Simba mwendo tumeumaliza.
Atakayebisha analeta ushabiki lakini hali inayoendelea ni ngumu kwetu.
Mpira ni dakika 90, ndugu.
Kwani nani alijua kuwa Ihefu ikiwa timu ya mwisho kwenye NBC, ingeifunga YANGA? ( Timu yenye uwekezaji mkubwa).
 
Yanga na Simba wamepangwa na timu za kawaida wakaze mwendo
Hususani Yanga

Tp Mazembe ya saizi haieleweki inacheza nini yani tia maji tia maji tu

Hao watunis nao inaonekana ni clone ya Club Africain, huyo mwingine ndio simjui hata rekodi yake

Ila upande wa Simba naye muheshimu ni Raja Casablanca tu kuwa atanisumbua, hao wengine waliobaki ni vipigo tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…