Dubai: Rais Samia ashuhudia utiaji saini wa Mikataba ya Uwekezaji ya thamani ya Trilioni 17

Dubai: Rais Samia ashuhudia utiaji saini wa Mikataba ya Uwekezaji ya thamani ya Trilioni 17

Sawa ila tunaomba utukumbushe ile mikataba ya kikwete na raisi wa china ni upi umetekelezwa maana nasikia ilikua ishirini na zaidina tuakaambiwa itaibadilisha tanzania lakina maisha ndo yanazidi kua magumu.
Mmoja ulikuwa ni makubaliano ya kujenga SGR. Bahati Mbabane sehemu ya kipande kile alikuja kupewa Mturuki na JPM ila mchina still kapewa Mwanza -Isaka

Bandari ya Bagamoyo serikali imesema majadiliano yameanza upya so tusubiri
 
Jamani amkeni amkeni
Huko dubai mambo ni moto balaa! Leo hii Rais wa JMT Mhe Samia Suluhu Hassan ameshuhudia utiaji saini wa mikataba zaidi ya 30 ya uwekezaji Tanzania yenye thamani ya fedha za Tanzania zaidi ya Trilioni 14 na itakayotoa ajira kwa Watanzania za moja kwa moja zaidi ya laki 2.

Mikataba iyo inahusu maeneo ya Kilimo, Madini, Biashara, Utalii na Uzalishaji wa Viwanda

Hongera sana Mhe. Rais kwa jitihada hizi. Mungu akubariki kwa kweli. Haya ndo maendeleo tunayotaka Watanzania

Kutoka Nyasa, ziwani
Lord denning
Fedha za kuja kuwateketeza Wamasai Ngorongoro hizo
 
Angeweka Saini Ujenzi wa Reli ya Mtwara Hadi Mbaba bay, au Reli ya Mpanda-Karema, Tabora-Kigoma katika viwango vya Reli za meme ningeona mama kaupiga mwingi lakini hiyo miradi ya kilimo, Madini nk ni pesa za watu kuweka mifukoni huku miradi ikinunuliwa magari tu refer kilimo kwanza
Akiweka mikataba iyo bado utalalamika mikopo
 
Jamani amkeni amkeni
Huko dubai mambo ni moto balaa! Leo hii Rais wa JMT Mhe Samia Suluhu Hassan ameshuhudia utiaji saini wa mikataba zaidi ya 30 ya uwekezaji Tanzania yenye thamani ya fedha za Tanzania zaidi ya Trilioni 14 na itakayotoa ajira kwa Watanzania za moja kwa moja zaidi ya laki 2.

Mikataba iyo inahusu maeneo ya Kilimo, Madini, Biashara, Utalii na Uzalishaji wa Viwanda

Hongera sana Mhe. Rais kwa jitihada hizi. Mungu akubariki kwa kweli. Haya ndo maendeleo tunayotaka Watanzania

Kutoka Nyasa, ziwani
Lord denning
Si muna wa tu kana warabu nyinyi muna sema wataurejesha utumwa
 
Hii nchi fursa ziko nyingi sana. Ilikosa mtu anayeaminika tu ambaye akishawishi watu wanashawishika kweli
Tuwekane sawa, hata mama hakugombea urais au kwa lugha nyimgne alikuwa namba 2 hadi katiba ilivyoelekeza vinginevyo.
Sasa ukisema namba 2 hakuwa na ushawishi wa kushawishi mambo itakuwaje kwa hawa wengine akina waziri au katibu kata?

Na kama nje ya watu millioni 60, waliojitokeza kuigombea hiyo nafasi hakuwemo kuna haja ya kuendelea kuamini hizi ngonjera za 'haijawahi kutokea' au tumuachie mwalimu mkuu ambaye ni muda atueleze?
Katiba mpya ndio inaweza kutupa picha nzuri ya haya mambo na kutuondolea mashaka hata pale yasipokuwepo. Mfano mikataba mingi nchi hii iliyoingia huwa inashangiliwa lakini mwishoni ndipo tunasikiaga habari za makinikia, gesi kuuzwa, makaa ya mawe, Loliondo kuwa na masafa yake ya mawasiliano au ajira ambazo watu wanalipwa Tsh. 3,000/- kama ujira wa siku nzima
 
Tuwekane sawa, hata mama hakugombea urais au kwa lugha nyimgne alikuwa namba 2 hadi katiba ilivyoelekeza vinginevyo.
Sasa ukisema namba 2 hakuwa na ushawishi wa kushawishi mambo itakuwaje kwa hawa wengine hadi katibu kata?

Na kama nje ya watu millioni 60, waliojitokeza kuigombea hiyo nafasi hakuwemo kuna haja ya kuendelea kuamini hizi ngonjera za 'haijawahi kutokea' au tumuachie mwalimu mkuu ambaye ni muda atueleze?
Kwani kwa Tanzania kuna mtu mwenye maamuzi kuzidi Rais? Unadhani angefanyaje?
 
Heko Samia Suluhu Hassan, ina heri miguu yako.

CC Crimea Stroke Kinuju YEHODAYA et al
Kila kitabu na zama zake.Magufuli ana yake mazuri alifanya ikiwemo kurudisha hadhi ya CCM iliyokuwa imepotea kabisa mtu akivaa nguo ya CCM ulikuwa unazomewa mitaani na alijenga miundo mbinu ya uhakika hadi uswahilini kulikokuwa kumesahaulika na kurudisha utendaji Kazi na uwajibikaji serikalini kujali wananchi wanyonge wa chini kabisa na umeme ulikuwa haukatiki hovyo

Magufuli alikuwa na mazuri yake kwa kitabu chake cha wakati huo .Samia naye anaandika kitabu chake Toleo lake
 
Jamani amkeni amkeni
Huko dubai mambo ni moto balaa! Leo hii Rais wa JMT Mhe Samia Suluhu Hassan ameshuhudia utiaji saini wa mikataba zaidi ya 30 ya uwekezaji Tanzania yenye thamani ya fedha za Tanzania zaidi ya Trilioni 14 na itakayotoa ajira kwa Watanzania za moja kwa moja zaidi ya laki 2.

Mikataba iyo inahusu maeneo ya Kilimo, Madini, Biashara, Utalii na Uzalishaji wa Viwanda

Hongera sana Mhe. Rais kwa jitihada hizi. Mungu akubariki kwa kweli. Haya ndo maendeleo tunayotaka Watanzania

Kutoka Nyasa, ziwani
Lord denning

Huo utapeli naufananisha na ule utapeli wa Obama alivyokuja Tanzania akatuadi power pool ya $7b.
 
Kwani kwa Tanzania kuna mtu mwenye maamuzi kuzidi Rais? Unadhani angefanyaje?
Sasa kama nchi yenye watu milioni 65 mwenye maamuzi ni mmoja tu kati yao na upatikanaji wake 'ahuhojiwi' na yeyote, unaona nini hapo? Kwamba hata maoni ya spika ambaye ni mhimili mmoja wapo yakitofautiana inabidi yatokee yaliyotokea. Rais ni binadamu na hata kama ni genius bado amezungukwa na watu dhaifu na wanaopigania matumbo yao badala ya wewe, mimi na Wamasai wa Ngorongoro, je katiba yetu inatuwezesha kumpata rais malaika na asiyekosea?

Naogopa kupinga kila kitu lakini ukweli ni kwamba yanayoendelea Dubai sasa tunayajua kupitia waliopo huko na hao ni waliomo kwenye delegation ambao daima hata yasiyo wanajitahidi yaonekane ndio. Ngojea wakija reporters huru tusiseme wametumwa
 
Jamani amkeni amkeni
Huko dubai mambo ni moto balaa! Leo hii Rais wa JMT Mhe Samia Suluhu Hassan ameshuhudia utiaji saini wa mikataba zaidi ya 30 ya uwekezaji Tanzania yenye thamani ya fedha za Tanzania zaidi ya Trilioni 14 na itakayotoa ajira kwa Watanzania za moja kwa moja zaidi ya laki 2.

Mikataba iyo inahusu maeneo ya Kilimo, Madini, Biashara, Utalii na Uzalishaji wa Viwanda

Hongera sana Mhe. Rais kwa jitihada hizi. Mungu akubariki kwa kweli. Haya ndo maendeleo tunayotaka Watanzania

Kutoka Nyasa, ziwani
Lord denning
Janga lingine la uharibifu wa mazingira laja na mengine mengi
 
Sasa kama nchi yenye watu milioni 65 mwenye maamuzi ni mmoja tu kati yao na upatikanaji wake 'ahuhojiwi' na yeyote, unaona nini hapo? Kwamba hata maoni ya spika ambaye ni mhimili mmoja wapo yakitofautiana inabidi yatokee yaliyotokea. Rais ni binadamu na hata kama ni genius bado amezungukwa na watu dhaifu na wanaopigania matumbo yao badala ya wewe, mimi na Wamasai wa Ngorongoro, je katiba yetu inatuwezesha kumpata rais malaika na asiyekosea?

Naogopa kupinga kila kitu lakini ukweli ni kwamba yanayoendelea Dubai sasa tunayajua kupitia waliopo huko na hao ni waliomo kwenye delegation ambao daima hata yasiyo wanajitahidi yaonekane ndio. Ngojea wakija reporters huru tusiseme wametumwa
Rais ni Taasisi
 
Kuna reformation kubwa sana Tanzania imefanya na inazidi kufanya ndani ya kipindi hiki kifupi hasa kwenye sheria za uwekezaji na kodi. Ndo mana naisi kuna kuongezeka kwa userious sana uwekezaji kuja Tanzania
Naomba sana hili jambo litokee haraka sana tuwe na sheria rafiki kuliko nchi yoyote maana nchi njia peke yakakutoka hapa ni private sector kukua. Kama hili linafanyika basi salute la lishukue muda mrefu. Kuna mtu alitaka kuwekeza hapa lakini kumtajia 45% tax alishtuka sana how comes na kibali chake sijui dola alfu naona nguvu zilimuishia kidogo anapenda kuja lakini kawa na mashaka kama njia sahihi.
 
Back
Top Bottom