Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Yote kheri safari njema mzee, kina sisi tutasimama na upinzani mpaka CCM itoke madarakani....Aluta continua.
 
Ama kweli mzee kabanwa kila sehemu,mme wa mwanae leo mwaka wa ngapi sijui yupo Lumande. But why wanatangaza ndani ya kipindi cha msiba wa Taifa?
Mkuu wewe na uelewa wako unasema tuna msiba wa Taifa? Tafadhali!
 
Wimbo ulianza kwa chadema, hakuna kupinga. Kila pembe ilikuwa ni "Lowassa fisadi, Lowassa fisadi" alipokosa kuteuliwa kuwania urais wa tiketi CCM akajitoa CCM na kuhamia chadema, akapewa nafasi ya kugombea urais kwa tiketi ya chadema, ghafla chorus ya "Lowassa fisadi, Lowassa fisadi" ikawa inaimbwa na wana CCM.

Sasa karudi CCM nani ataiimba chorus hiyo?

Siasa ni mchezo mbaya sana.
 
Kama jinsi wote tunavyokumbuka mshike mshike kati ya lowasa na Dr slaa kipindi cha 2015 .

Hawa watu walikuwa ni sawa panya na nyau ndani ya nyumba.

Dr slaa alikuwa haungani na cdm kumkaribisha manywele chamani na ndio akachukua uamuzi wa kukaa kando na siasa.

Kwani mzee manywele alikuwa akihusishwa na ma issue ya ki fisadi ambayo hadi leo hayajapatiwa majibu pamoja na mahakama ya mafisadi kufunguliwa.

Sasa leo hii mzee manywele kaamua kumfuata mzee Dr slaa huko huko aliko,hahahaha patamu hapa.


Je kwa kitendo hiki cha mzee manywele kumfuata mzee slaa ccm ,slaa atachukua uamuzi gani?

Kama kweli mzee slaa ni mzalendo ni basi afanye maamuzi magumu yakurudi cdm kwani mbaya wake karudi ccm

Tofauti na hapo wananchi hawatamuelewa kabisa Dr slaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa Amerejea Rasmi CCM Leo.

Amepokelewa Lumumba Makao Makuu Madogo Ya Chama Cha Mapinduzi Na Katibu Mkuu Dr Bashiru Ally.

Aidha, katika mapokezi hayo walikuwepo Rais Magufuli, Rostam Aziz, Mzee Phillip Mangula, Waziri Mkuu Majaliwa Kassim, Humphrey Polepole n.k



View attachment 1035375

View attachment 1035448

Unaweza soma pia:

Edward Lowassa na Frederick Sumaye mbioni kurejea CCM - JamiiForums

Edward Lowassa: Wanaodhani nitarudi CCM wanapiga porojo na kuota ndoto - JamiiForums

Lowassa hana namna zaidi ya kuipigia magoti CCM, Mkwewe Sioi Sumari mpaka sasa yupo lockup - JamiiForums

Hongela mzee wetu umetambua ukweli na umerudi nyumbani, ni heri umeachana nao wazandiki karibu karibu nyumbani
 
Back
Top Bottom