Elon Musk Anakuja na Usafiri wa Kuzunguka Duniani Kote Ndani ya Saa Moja! Unaweza kufanya Kazi Marekani Ukitokea na Kurudi Da es Salaam Kila Siku!

Elon Musk Anakuja na Usafiri wa Kuzunguka Duniani Kote Ndani ya Saa Moja! Unaweza kufanya Kazi Marekani Ukitokea na Kurudi Da es Salaam Kila Siku!

Huyo jamaa hamna kitu, yuko overrated sana. Ameshakuja na blah blah kibao za kiuvumbuzi lakini kiuhalisia hakuna kitu kinachofanikiwa.
Kiufupi Elon Musk ni muongo muongo, mjanja mjanja na mwizi kimtindo.
Mhh tajiri namba moja duniani ndo awe muongo muongo??? Na wanasema anaweza akawa ndio trillionaire wa kwanza duniani?? Sidhani kama unayosema ni kweli
 
Huyo jamaa hamna kitu, yuko overrated sana. Ameshakuja na blah blah kibao za kiuvumbuzi lakini kiuhalisia hakuna kitu kinachofanikiwa.
Kiufupi Elon Musk ni muongo muongo, mjanja mjanja na mwizi kimtindo.
no!! anachofanya ni kuwekeza kwenye tech. nimeona clip moja inasema trump labda ni time traveller na hii ni kweli kuwa amerithi notebook za Nicola tesla na inasemekana 99% haijaea public je kama trump ndio qnampa hizo note book mask anaimplement hizo creation.? dunia hii ina mambo meng ya kielem.wengine tuko obsessed na uchawi.na tumeusoma.huko dogon tribe wajomba wana data za nyota toka enz na enz na hajawai rusha rocket ila may be wnaaenda usiku na nyungo?
 
Ni ujinga kuamini Elon Musk anaweza kugundua vitu vipya tofauti tofauti vya kisayansi. Elon Musk hana akili hizo wala uwezo huo. Yeye amewekeza pesa zake nyingi kwenye project za kitafiti na kuzalisha bidhaa na huduma za kiteknolojia zilizotokana na gunduzi za watu wengine hususani young scientists.

Elon musk yuko overrated
Huyu ni Thomas Edison
 
Kuna watu wameletwa dunian kama wakombozi wengine wanasindikiza
Huku kwenye kusindikiza ndiko kwenye umati mkubwa zaidi. Tutoke huko mkiani tuanze mdogo mdogo, hata kama tunaanza na magari ya mbao. Au turushe vishada vyenye abiria mmoja au wawili kwa kuanzia.
 
Huyo jamaa hamna kitu, yuko overrated sana. Ameshakuja na blah blah kibao za kiuvumbuzi lakini kiuhalisia hakuna kitu kinachofanikiwa.
Kiufupi Elon Musk ni muongo muongo, mjanja mjanja na mwizi kimtindo.
Ila katajirika sana kwa vitu ambavyo ni vya kweli. Lakini pia kumbuka kuwa kila jambo huanzia na wazo, hata kama kwa sasa linaonekana haliwezekani.

Je, umeona TEHAMA ilivyo na maajabu? Miaka michache iliyopita ilikuwa kama uongo au ndoto za Alinacha kutuma barua Marekani kwa selundu tu! Sasa si ndoto tena, bali uhalisia!
 
Na watanzania wengi sio tu wasindikizaji...tunazuia hata wanasindikiza.
Tumezoea rushwa, fitna, uchawi na roho mbaya kwa wanaopambana ili tukae sawa.
Wajinga wamekaa siti za mbele karibu kwenye kila kitu. Tunaishia kudanganyana tu
Hilo ni tatizo kubwa sana na kizingiti kikubwa kwa maendeleo yetu. Tuna vijana wabunifu wengi, badala ya kuwasaidia na kuwatia moyo, tunaweka kauzibe, chuki na kebehi. Tuache kabisa hii dhambi kwa vijana wetu ili tupate akina Elon Musk wa kwetu - hata kama ni wa mchongo!
 
Huyo jamaa hamna kitu, yuko overrated sana. Ameshakuja na blah blah kibao za kiuvumbuzi lakini kiuhalisia hakuna kitu kinachofanikiwa.
Kiufupi Elon Musk ni muongo muongo, mjanja mjanja na mwizi kimtindo.
Unamuitaje muongo ilihali kazi zake zinaonekana? Anaweza akashidwa jambo and yet akaibuka na lingie la maana zaidi.
Elonana projects kibao zipo pending na nyingine aliachana nazo.
Inawezekana wewe unamsubiri amalizie ambacho ameshaachana nacho au alichoweka pending, unatakiwa uelewe, kuna pengine yanahitaji scientic approval na mengie ya mgogolo kisheria.
 
Ugunduzi si masuala ya simba na Yanga kwamba unasema leo linakuwa kesho, inawezekana wanasayansi wakapanga jambo leo likatekelezeka miaka 10 au 20 baadae.

Musk yupo vizuri, napenda anavyowaza nje ya box na haamini katika kushindwa.
Uko sahihi kabisa! Hakuna kinachoshindikana chini ya mbingu tukiwa na fikra pevu na chanya. Tuko hivi tulivyo kulingana na tunavyofikiri.
 
Huku kwenye kusindikiza ndiko kwenye umati mkubwa zaidi. Tutoke huko mkiani tuanze mdogo mdogo, hata kama tunaanza na magari ya mbao. Au turushe vishada vyenye abiria mmoja au wawili kwa kuanzia.
Mkuu na hapa sasa ndipo kuna changamoto ukianza kuunda tu wenye mamlaka wanakwambia huna leseni mara ni hatar kwa usalama wa raia
 
Sisi labda tukune nazi...!

Ukiona watu wazima(sio kichaa) anaharibu miundombinu ya SGR ili akauze kama vyuma chakavu, ujue huku bado Mungu yuko kazini anaumba.
Eeh Mungu tupishie mbali huu uhaini, uhalifu na uharibifu
 
Uchafu kama huu inabidi uwepo ili wenye akili waweza kutumia akili zao. Kila wakiangalia nguchiro kama hizi wanapata ari ya kujituma zaidi ili vizazi vyao visije kuwa kama hao ng'ombe.
Ameni, na iwe hivyo kwa hakika. Nguchiro waje waishe kabisa vizazi vijavyo.
 
Mungu fundi mwaisa ona ameumba jitu lina akili hadi zinamwagikaaa..

Imagine genius mmoja tu huyu anasumbua dunia je wangekuwa 100 hawa dunia isingekalika sijui tungekuwa naishi Pluto huko..

Mwacheni Mungu aitwe Mungu.
Momumo, naloli mwaisa. Hata Biblia inasema wakati wa mwisho maarifa yataongezeka. Danieli 12:4
 
Mtu ni kapuku wa kutupwa ambaye hata kiwembe tu cha kunyolea mavuzi yake ameshindwa kubuni ila yuko busy anamponda tajiri wa Dunia, "eti Elon hamna kitu pale."
Pathetic.
Yes, so pathetic! Na inashangaza sana kuchukia wanaoendelea badala ya kuwakubali na hata kuwaiga au kujifunza kutokana na mafanikio yao. Mungu atusamehe kwa hakika.
 
Huku kwenye kusindikiza ndiko kwenye umati mkubwa zaidi. Tutoke huko mkiani tuanze mdogo mdogo, hata kama tunaanza na magari ya mbao. Au turushe vishada vyenye abiria mmoja au wawili kwa kuanzia.
Ngoja kwanza tumalize kujenga matundu ya vyoo mashuleni. Uchaguzi wa 2025 itakuwa ni Kwa ajili ya kuomba kura ili tukamilishe Ujenzi wa vyoo Kwa level ya lenta, 2030 ni uchaguzi Kwa ajili ya kuomba kura ili tupauwe vyoo vilivyojengwa, 2035 ni uchaguzi Kwa ajili ya finishing ya vyoo.


BTW, yule jamaa wa Tunduma aliyetengeneza helicopter aliishia wapi?
 
Back
Top Bottom