Familia yake wanataka kunitolea mahari

Familia yake wanataka kunitolea mahari

"Watoto wote nilikuwa naishi nao kwangu, huku tukisaidizana malezi. Yeye alishaoa kama miaka mitatu nyuma".


"wazazi wake wakasema niwakabidhi watoto wawalee hadi hapo nitakapo kuwa sawa".

Nimejifunza kuwa, ni kweli kwa 101%, single mother hawaachani na watu wao. Kuoa single mother tegemea mikiki mikiki kama hii.

Hebu fikiria sasa ndio umemuoa halafu mwenzio anakua na stress za mwenzie kama hivi.

Ovyo kabisa
🤣🤣 Kwahiyo ulitaka nimfute kwenye malezi ya watoto wake?toka tuachane sijawahi kujuana naye kimwili zaid ya maslah ya watoto tu 🙏
 
Mkewe anajua kuwa jamaa alishazaaga watoto kabla hajamuoa🙏
Usikubali familia ikulipie mahali. Tafakari haya;

1. Hujui msimamo wa baba wa watoto wako

2. Unujua msimamo wa jamaa yako wa sasa kuhusu hilo?

3. Huko unakolipiwa mahali, unaenda kuolewa mke wa pili?

4. Mke aliyeko huko kwa baba wa watoto wako, anajua chochote juu ya jambo hilo?

5. Mke anayeishi naye baba wa watoto wako, anajua uwepo wa watoto wako?
 
[emoji1787][emoji1787] Kwahiyo ulitaka nimfute kwenye malezi ya watoto wake?toka tuachane sijawahi kujuana naye kimwili zaid ya maslah ya watoto tu [emoji120]
Sio hivyo mkuu, ila najaribu kuvuta picha mm ndio nimeoa mwanamke wa aina yako. Yaana mara uende nyumbani kwa mzazi mwenzio kuona watoto, mara mtoto kaumwa mmekutana hospital, siwezi kwakweli.
 
Najua kwa sasa unaweza kuwa mbali nae ila si milele, iko siku utarudi tu kwake kupasha kiporo.
Haipo hiyo najiheshimu na tushakuwa watu wazima sasa,tunafocus kuwapatia watoto malezi Bora kwa wote kuwajibika🙏
 
Hahah siendi kwake,naenda kwao,yani mengi yanafanyika kupitia wazazi wake na ndugu zake,mie Sina hata namba yake ya simu 🙏
Sio hivyo mkuu, ila najaribu kuvuta picha mm ndio nimeoa mwanamke wa aina yako. Yaana mara uende nyumbani kwa mzazi mwenzio kuona watoto, mara mtoto kaumwa mmekutana hospital, siwezi kwakweli.
 
Huwezi kushika watoto na bwana mwingine! Ukiamua kuwa na mahusiano mengine, achana na idea ya kuishi na hao wanao. Kama kuishi na watoto hao ni lazima achana na mwanaume mpya. Choice zipo mbili tu. Hakuna ya tatu kuwachanganya wote itakuwa mtihani utakaopata F tu
Ila nashauri watoto wake kwa bibi,ili kila mmoja awe na uhuru wa kuwaona wanae,kwa sababu wakikaa kwa baba,mama yao mzazi hatapata uhuru wa kuwaona wanae kwa kuhofia ugomvi na mke mwenzake.Na baba pia hatoweza kwenda kuwaona watoto wake ikiwa watakuwa wanaishi na mama yao mzazi na baba wa Kambo. But all in all natamani kusingekuwa na kuachana Hasa kwa watu waliozaa watoto,ni huzuni sana,watoto wanateseka vibaya mno pasipo na sababu,na since watu wakiachana lazima kuwe na maumivu.
 
Ila nashauri watoto wake kwa bibi,ili kila mmoja awe na uhuru wa kuwaona wanae,kwa sababu wakikaa kwa baba,mama yao mzazi hatapata uhuru wa kuwaona wanae kwa kuhofia ugomvi na mke mwenzake.Na baba pia hatoweza kwenda kuwaona watoto wake ikiwa watakuwa wanaishi na mama yao mzazi na baba wa Kambo. But all in all natamani kusingekuwa na kuachana Hasa kwa watu waliozaa watoto,ni huzuni sana,watoto wanateseka vibaya mno pasipo na sababu,na since watu wakiachana lazima kuwe na maumivu.
Kuna wakati kija wangu alimweleza kaka yake kuwa, ananichukia kwa vile siishi na mama yake. Ni maumivu ajabu ila utamu wa K unaleta madhara makubwa na vidonda kwa watoto visivyoponyeka.

Huyu Ironbutterfly kitu hajui ni kuwa mtopto akiwa wa kiume, hataki amuone mama na mwanaume mwingine ambaye si baba yake. Akiwa na mwanaume mwingine, atataka kurudi kwa baba. Kama hao watoto ni wa kike, wao huwa hawana tatizo kuishi na baba wa kambo.
 
Mkuu kwanza ondoa hiyo fikra ya kwamba hao ni wanao tu.Hilo litakusababisha ufanye maamuzi ya kibinafsi yatakoyoathiri mahusiano yaliyopo na kuleta migogoro na hata kuwaathiri watoto.

Hao ni watoto wenu,wewe na mzazi mwenzako.Hivyo,katika kuamua lolote litakalowahusu watoto,kila mmoja ana nguvu sawa na mwenzake

Na watoto(bila ya kujali umri wao) wanahaki ya kuishi popote ambapo ni pazuri kwa ustawi wao,haijalishi kwa mama au kwa baba na hata nje ya baba na mama.

Hivyo,jadiliana pamoja na mzazi mwenzako,weka matamanio yako pembeni,uelewe nia yake,mueleze mawazo yako...na wote amueni jambo moja,tena bila kuvutana au kulumbana.

Yote hayo yanayotokea sasa,jua chanzo ni maamuzi ya kutokuwa pamoja,hivyo tumia akili sana kufanya maamuzi yako,mgogoro ulio katika nafsi yako au zenu msiuingize kwa watoto na kuwafanya nao waanze kuchagua na kubagua kwamba kule ni kuzuri huku kubaya.

Hilo la mahari,jadiliana na upande wa uliopendekeza hilo ujue nia yao kabla ya kuamua chochote,kuna mambo lazima yafanyike yanayowahusu watoto na mwenza wako wa sasa lazima akubaliane nayo,likiwemo pale ukiwa na watoto mzazi mwenzako ana haki ya kuja kuwaona na kuwatembelea.
Ushauri mzuri sana huu,muhusika uchukue na uufanyie kazi kwa haraka
 
Mwanaume kulea mtoto wa mwanaume mwingine huwa ni kitendawili labda awe na matatizo ya uzazi.
Ishi humo afu baadae utakuja kuona matokea,labda baba yao awe amekufa.
 
Ohhh fidia ndio inakuwaje?
Sijasoma comment zote ila hiyo sio fidia ya kukuzalisha, kwa lugha ya kawaida hiyo ni kugomboa watoto. Kwahiyo haulipiwi wewe, wewe endelea tu na huyo mtu wako mpya na sioni haja ya wewe kuzuia hili.

Huyo mtu wako kama ana maarifa hawezi zuia hilo, wala hawezikua na wivu
 
Mwanaume kulea mtoto wa mwanaume mwingine huwa ni kitendawili labda awe na matatizo ya uzazi.
Ishi humo afu baadae utakuja kuona matokea,labda baba yao awe amekufa.
Ni kweli kwa asilimia kubwa ila wapo wanaume wenye mioyo yao na ni wazima tu na wanalea watoto ambao sio wa kuwazaa ila ni wachache sana,lkn pia ni heri baba wa Kambo kuliko mama wa kambo,Hawa ndo wabaya zaidi kipindi Cha kwanza watapretend kuwapenda watoto wa waume zao lkn badae wanaanza kuwanyanyasa.
 
Back
Top Bottom