Fei Toto agonga mwamba TFF, bado ni mali ya Yanga

Fei Toto agonga mwamba TFF, bado ni mali ya Yanga

Muuza Kangala

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2021
Posts
1,242
Reaction score
4,813
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mira wa Miguu Tanzania (TFF) imekutana leo tarehe 2 Machi, 2023 kwa ajili ya kusikiliza pamoja na mambo mengine shauri la mapitio (Review) ya uamuzi wake wa tarehe 9 Januari 2023 kati ya Feisal Salumu na Klabu ya Young Africans kama yalivyowasilishwa na muombaji Feisal Salum dhidi ya Klabu ya Young Africans.

Baada ya kusikiliza hoja za mawakili wa pande zote mbili Kamati imeona kuwa shauri hilo la mapitio (Review) halina msingi wa kisheria kushawishi

Kamati kubadili maamuzi yake yaliyotolewa awali hivyo imetupilia mbali shauri hilo.

Sababu kwa undani za uamuzi huo zitatolewa kwa pande zote mbili zinazohusika katika shauri hilo siku ya Jumatatu 6 Machi, 2023.

E13575C7-00C0-4FBC-9E67-D574260485C0.jpeg
 
Taarifa iliyotolewa na TFF imeeleza kwamba mzee wa Ugali na sukari ameangukia pua

Hii ni baada ya TFF kukosa msingi wa kisheria wa kubadili uamuzi wake wa awali

Sasa ni hiyari yake kusuka au kunyoa, bali nawaomba viongozi wa Yanga wamhurumie huyu kijana aende atakako, kumkomoa haitasaidia chochote.

Yanga Mshahara wenu mdogo sana, mwacheni huyo kijana akale Ugali na mboga sasa, milion zenu hizo 4 zinatosha unga, sukari na mkaa tu.

b16c33a3-3c34-402c-b775-292ddb8d8762-jpeg.2535203
 
Haya ale fedha alizotaka kuzitumia kuvunja mkataba, asubiri 2024 aondoke zake bure. Akiendelea kulipwa mshahara huku achezi itapendeza. Au aende mbele kupigana zaidi, binafsi namtakia kila la heri na hili lipite na afanikiwe vita yake ya maslahi.

Kwa upande wa Yanga sioni ushindi wowote wakibaki nae au wakimwachia, labda itokee timu imlipie dau kubwa kuliko alilotoa wakati akivunja mkataba au wampe adhabu ya kutokumlipa mshahara au sehemu ya mshahara, si mchezaji wao, ngoja tuone watakachomfanya.
 
Marejeo ya kesi ya Feisal vs Yanga yametolewa na TFF kupigilia msumari kwenye kaburi la Mla UGALI na SUKARI
20230302_195648.jpg
 
Sababu za undani zitatolewa kwa wahusika wa shauri hilo

Yale yale kufanya mambo gizani kuwaficha watu wasiweze kukosoa endapo kuna ukiukwaji wa sheria umefanyika
 
Kuna ule msemo wa sisi wanasheria " ignorance of the law is not an excuse before the court of law"

Kwa wale mbumbumbu.....mliokimbia shule ....Ina maanisha kutokujua Sheria siyo utetezi mbele ya mahakama

Sasa mama mtu alitaka public sympathy [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Uonevu tu. Waweke hoja zilizobishaniwa na rejea za vifungu kila mtu aone.
Ulikuwepo mle ndani wakati wansfanya review? Au ndio nyie wanasheria mnaoishia kupiga kelele himu huku mkimjaza upepo mla ugali kwa sukari ili apotee kwenye medani za soka. William Mshumbusi na denooJ vipi mlienda kwenye kusikiliza review?
 
Anapewa mil 4,anakula ugali na chumvi then alikuwa na uwezo wa kulipa 110m Yanga bila kufuata utaratibu na kwenda Dubai kutrain na trainer mkubwa anao watrain wachezaji wanaocheza ligi kubwa ulaya.

Hamna logic kabisa, bi mkubwa alizani ana mtetea mwanae kumbe kamwaribia.
 
Back
Top Bottom