Fredrick Lowassa: Kama sio Rais Samia, Baba asingefika juzi

Chadema watakuja kumponda huyo mtoto...na kutukana...wao walitaka kusikia lawama zinaenda Ccm na ikiwezekana Kwa Rais Samia
ChaDema wana wivu sana mtu akisifia au akisifia kwao wanaumia roho. Wataanza kumkashifu anayesifia.
 
Kwahiyo Mungu hakuwa na msaada wowote kwenye kuongeza siku za Lowasa.
 
Labda kwa vile alitoka kidogo chamani na kuelekea upinzani.
 
Sasa wewe unabishana na mtoto wa Marehemu? Wao ndio wanajua ipi ni stahili yao na kipi walisaidiwa
 
kwahiyo Mungu ameshindwa nguvu na Hangaya ?
Mbona amesema hiyo ni kazi ya Mungu ila alichosema inawezekana bila misaada ya Rais pengine hata hapo walipofika wasingefika kuna ugumu gani hapo wa kuelewa mbona ni lugha rahisi tu aliyotumia
 
Sasa kwa nini tunalalamika huduma mbovu za hospital zetu na kwanini wote wanaokufa hatusemi ni kazi ya Mungu ila ni uzembe wa Madaktari,Madereva,Polisi nk nk
Lazima tukubali vifo vingine ni kazi ya Mungu ila vingine ni ukosefu tu wa uwajibikaji tusimsingizie Mungu kila kitu
 
Sikujua kumbe Dr Samia ni daktari bingwa! Ni daktari wa magonjwa gani?
Maana kwa hela ndefu aliyokuwa nayo mzee Lowassa angeweza kutibiwa popote duniani ila wao wakaona atibiwe na huyo Dr Samia, jee ni bingwa wa nini?
Au huyo Fredrick anatumia kifo cha baba yake kukijengea mazingira ya uteuzi? Laana hizo, kama ndio lengo lake!

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Mbona amesema hiyo ni kazi ya Mungu ila alichosema inawezekana bila misaada ya Rais pengine hata hapo walipofika wasingefika kuna ugumu gani hapo wa kuelewa mbona ni lugha rahisi tu aliyotumia
angalia tuliyemquote aliandika nini
 
Uhai hauongezwi na figo Mungu akiamua hata upewe figo 20 unakufa saa hiyo hiyo.
Yaan ningekuwa dr walokole kama ninyi siwapi dawa na usiku nanyofoa mashine ya kuhema .nione ulaya wamejaa mashoga na mateja wanaishi wastan wa miaka
80 kisha zambia ambao ni taifa linaongoza kwa ukristo na maadili wastan wa kuishi miaka 52 .afu useme huduma nzuri mahospital haziongezi maisha
 
Sasa wewe unabishana na mtoto wa Marehemu? Wao ndio wanajua ipi ni stahili yao na kipi walisaidiwa
Hakuna anayebishana na mtoto wa marehemu kwa sababu stahiki za viongozi wakuu ziko wazi na zimeainishwa katika sheria ya " Political Service Retirement Benefits Act ya mwaka 2015 ( Cap.225. R.E.2015) ambayo inasema mtu aliyewahi kuwa Waziri Mkuu anastahiki zifuatazo:
1. Posho itakayofanana na 80% ya mshahara wa Waziri Mkuu aliyopo.
2. Gratuity itakayokuwa sawa na nusu ya pesa alizopokea kama mshahara wakati akiwa kazini.
Schedule C ya hiyo sheria inasema:
1. Yeye na mwenza wake watakuwa na pasi za kidiplomasia.
2. Atagharamiwa matibabu ndani na nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
3. Gari moja lenye uzito usio pungua tani 3 ambalo litakuwa linabadilishwa kila baada ya miaka mitano.
4. malipo yatakayotosha kulipa mishahara kwa wafuatao kwa kima cha chini:
a. Personal Assistant mmoja.
b. Mpishi mmoja.
c. Dobi mmoja.
d. Mfanyakazi wa ndani mmoja.
e. Shamba boi mmoja.
f. Dereva mmoja.
5. matumizi ya VIP lounge.
6. Gharama zote za kuzikwa.

Ibara ya 14 (2) inasema yeye na familia yake watapewa ulinzi wote unaostahili.

Sheria pia inasema kuwa wanaohusika ni wale wote waliowahi kuwa mawaziri wakuu bila caveats yeyote.
Mtoto wa marehemu anaweza kujua zaidi kuhusu utajiri na mali za mzazi wake lakini sio kwenye stahiki zake. Labda kama aliwahi kunyang'anywa kinyume na sheria na Rais akamrudishia.

Amandla...
 
ni vizuri ukweli usemwe bayana..
God bless Pres.Dr.SSH

gubu hazina maana sana 🐒

R.I.P Laigwanan comrade ENL
 
Mungu ndiye anajua utakufa saa ngapi sio huduma nzuri wala ulokole wala daktari.
 
Kuna sifa zingine hazina umaana, hoja ya Samia kusaidia kwa mgonjwa, yeye ndo anashikilia uhai?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…