LGE2024 Freeman Mbowe akamatwa na Jeshi la Polisi akielekea Mbozi mkoani Songwe

LGE2024 Freeman Mbowe akamatwa na Jeshi la Polisi akielekea Mbozi mkoani Songwe

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Nimesoma heading tu, Ila nauliza kwa mwaka anatakiwa akamtwe mara ngapi?
 

Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Mheshimiwa Freeman Mbowe amekamatwa na Jeshi la Polisi katika mapori ya HALUNGU akiwa njiani anaelekea Mbozi kwenye Kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa baada ya kutoka Mlowo ambapo mkutano wale ulizuiwa na Jeshi la Polisi kwa Kutawanya Watu kwa mabomu ya machozi

Magari yameharibiwa kwa kuvunjwa Vioo,Watu waliokuwa katika msafara wa Mbowe wamepigwa vibaya mno,wamepoteza simu na fedha.

Polisi wamempakia Mheshimiwa Mbowe katika Defender na Kutoweka naye pasipo Julikana.

Viongozi wengine waandamizi wamekamatwa na Kupakiwa katika gari tofauti na ile iliyombeba Mheshimiwa Freeman Mbowe.

Pia soma
- LGE2024 - Polisi watawanya Mkutano wa Mbowe kwa Mabomu. Kosa kaingilia ratiba ya ACT-Wazalendo

======

UPDATES

=======

TAARIFA KWA UMMA

Jeshi la Polisi leo tarehe 22 Novemba,2024 katika Pori la Halungu lililopo Wilaya ya Mbozi wamevamia Msafara na kumkamata Mwenyekiti wa Chama Taifa Mheshimiwa Freeman Mbowe pamoja na Viongozi mbalimbali aliokuwa ameambatana nao .

Msafara wa Mwenyekiti wa Chama Taifa ulikuwa umeshafanya Mikutano ya kampeni katika Kata ya Itaka,Kijiji Cha Itewe na Kata ya Halungu Mjini.

Awali mkutano wa kwanza uliokuwa ufanyike katika mji wa Mlowo uliozuiliwa na Polisi pamoja na wenyeji wetu ambao ni Chama Cha ACT Wazalendo kutualika kushiriki kwenye mkutano wa pamoja ila Polisi walikataa na kutawanya wananchi Kwa mabomy ya machozi .

Kabla ya kuwakamata walifuatwa na gari ya Polisi ambayo ilikutana nao njiani na hivyo iligeuza na baada ya mwendo kidogo walikuwa njia imefungwa na gari za polisi ndipo walipofungua milango Kwa nguvu na kuanza kuwashambulia waliokuwa kwenye Magari hayo na kuwakamata Kwa nguvu.

Waliokamatwa ni :
1. Mhe.Freeman Mbowe
2. Mhe. Joseph Mbilinyi - Mwenyekiti Kanda ya Nyassa
3. Mhe. Pascal Haongo- Mbunge wa Mbozi mashariki Mstaafu
4. Mwenyekiti wa Chama Cha ACT Wazalendo Wilaya ya Mbozi
5. B Appolinary Boniface - Mkuu wa Digital platform
6. Paul Joseph - Afisa habari Kanda ya Nyassa
6. Calvin Ndabila - Afisa habari Kanda ya Nyassa
7. Mdude Nyagali - Mwanaharakati na mwanachama wetu
8. Wasaidizi wa Mwenyekiti wa Chama Taifa Bwire,Adamoo na Lingwenya

Jeshi la Polisi wameondoka na viongozi wetu na hajajasema wanawapeleka wapi na mpaka Sasa hatujui wanashikiliwa wapi na Kwa sababu gani.

Chadema Kwa hatua ya Sasa tunasema yafuatayo;

1. Tunalaani kitendo hiki kwani kinaonyesha wazi kuwa ni mkakati wa Polisi kuhujumu kampeni za chama chetu Kwa kushirikiana na CCM
2. Polisi wawaachie mara Moja na bila masharti yoyote ili waendelee na ratiba ya Mikutano ya Kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
3. Wanachama na Viongozi wetu waendelee na kampeni za kuondoa CCM madarakani .
4. Tunaialika jumuiya ya kimataifa kuja kushuhudia uvunjifu wa Haki za kidemokrasia Kwa vyama vya upinzani nchini katika uchaguzi huu unaoendelea nchini .

Imetolewa Leo Ijumaa tarehe 22 Novemba, 2024

John Mrema - Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje
Ndiyo maana mimi binafsi nimeamua sitapiga kura katika uchaguzi wowote utakaofanyika chini ya katiba hii, tume hii na OR Tamisemi ni kupoteza muda na nguvu bure
 

Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Mheshimiwa Freeman Mbowe amekamatwa na Jeshi la Polisi katika mapori ya HALUNGU akiwa njiani anaelekea Mbozi kwenye Kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa baada ya kutoka Mlowo ambapo mkutano wale ulizuiwa na Jeshi la Polisi kwa Kutawanya Watu kwa mabomu ya machozi

Magari yameharibiwa kwa kuvunjwa Vioo,Watu waliokuwa katika msafara wa Mbowe wamepigwa vibaya mno,wamepoteza simu na fedha.

Polisi wamempakia Mheshimiwa Mbowe katika Defender na Kutoweka naye pasipo Julikana.

Viongozi wengine waandamizi wamekamatwa na Kupakiwa katika gari tofauti na ile iliyombeba Mheshimiwa Freeman Mbowe.

Pia soma
- LGE2024 - Polisi watawanya Mkutano wa Mbowe kwa Mabomu. Kosa kaingilia ratiba ya ACT-Wazalendo

======

UPDATES

=======

TAARIFA KWA UMMA

Jeshi la Polisi leo tarehe 22 Novemba,2024 katika Pori la Halungu lililopo Wilaya ya Mbozi wamevamia Msafara na kumkamata Mwenyekiti wa Chama Taifa Mheshimiwa Freeman Mbowe pamoja na Viongozi mbalimbali aliokuwa ameambatana nao .

Msafara wa Mwenyekiti wa Chama Taifa ulikuwa umeshafanya Mikutano ya kampeni katika Kata ya Itaka,Kijiji Cha Itewe na Kata ya Halungu Mjini.

Awali mkutano wa kwanza uliokuwa ufanyike katika mji wa Mlowo uliozuiliwa na Polisi pamoja na wenyeji wetu ambao ni Chama Cha ACT Wazalendo kutualika kushiriki kwenye mkutano wa pamoja ila Polisi walikataa na kutawanya wananchi Kwa mabomy ya machozi .

Kabla ya kuwakamata walifuatwa na gari ya Polisi ambayo ilikutana nao njiani na hivyo iligeuza na baada ya mwendo kidogo walikuwa njia imefungwa na gari za polisi ndipo walipofungua milango Kwa nguvu na kuanza kuwashambulia waliokuwa kwenye Magari hayo na kuwakamata Kwa nguvu.

Waliokamatwa ni :
1. Mhe.Freeman Mbowe
2. Mhe. Joseph Mbilinyi - Mwenyekiti Kanda ya Nyassa
3. Mhe. Pascal Haongo- Mbunge wa Mbozi mashariki Mstaafu
4. Mwenyekiti wa Chama Cha ACT Wazalendo Wilaya ya Mbozi
5. B Appolinary Boniface - Mkuu wa Digital platform
6. Paul Joseph - Afisa habari Kanda ya Nyassa
6. Calvin Ndabila - Afisa habari Kanda ya Nyassa
7. Mdude Nyagali - Mwanaharakati na mwanachama wetu
8. Wasaidizi wa Mwenyekiti wa Chama Taifa Bwire,Adamoo na Lingwenya

Jeshi la Polisi wameondoka na viongozi wetu na hajajasema wanawapeleka wapi na mpaka Sasa hatujui wanashikiliwa wapi na Kwa sababu gani.

Chadema Kwa hatua ya Sasa tunasema yafuatayo;

1. Tunalaani kitendo hiki kwani kinaonyesha wazi kuwa ni mkakati wa Polisi kuhujumu kampeni za chama chetu Kwa kushirikiana na CCM
2. Polisi wawaachie mara Moja na bila masharti yoyote ili waendelee na ratiba ya Mikutano ya Kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
3. Wanachama na Viongozi wetu waendelee na kampeni za kuondoa CCM madarakani .
4. Tunaialika jumuiya ya kimataifa kuja kushuhudia uvunjifu wa Haki za kidemokrasia Kwa vyama vya upinzani nchini katika uchaguzi huu unaoendelea nchini .

Imetolewa Leo Ijumaa tarehe 22 Novemba, 2024

John Mrema - Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje
Aisei! Hebu picha za magari yaliyoharibiwa vibaya? Waliojeruhiwa. Kimsingi, tunakubaliana umuhimu wa kuheshimu sheria.
 
Ndiyo maana mimi binafsi nimeamua sitapiga kura katika uchaguzi wowote utakaofanyika chini ya katiba hii, tume hii na OR Tamisemi ni kupoteza muda na nguvu bure
Ifike hatua tuwaachie CCM, Mbowe na Zitto uchaguzi wao!
 
Hii ya Zitto na hii taarifa ya Mrema....hapo ukweli ni upi? Kama nikweli Chadema ijirekebishe.
 

Attachments

  • IMG-20241122-WA0010.jpg
    IMG-20241122-WA0010.jpg
    474.1 KB · Views: 4
Tulionya humu kwamba Chadema inahitaji siku 7 tu kuteketeza ccm, nadhani mmeanza kuelewa
 
Hili ni trela,picha kamili ni hapo 2025 Mungu akijalia,imagine huu ni uchaguzi tu wa serikal za mitaa ambao hauna tija yoyote,huo wa ubunge madiwan na u prezdaa ndio mtashangaa
Wamekata wagombea karibia 65% ya wapinzani ila bado hawajiamni - hawana chama nimeamini
 
Pamoja na Mwenyekiti Freeman Mbowe wengine hawa hapa

Screenshot_2024-11-22-15-52-08-1.png


Shukrani kuu imwendee aliyerekodi tukio hili la kinyama lililokuwa na nia ovu, inaelezwa kwamba bila video kuvujishwa na msamaria mwema watuhumiwa hawa wangeweza kupotea milele

Screenshot_2024-11-22-15-01-46-1.png


Bila Polisi hakuna CCM
 
Back
Top Bottom