Freeman Mbowe atuhumiwa kwa Ugaidi na kupanga njama za Kuua Viongozi wa Serikali

Freeman Mbowe atuhumiwa kwa Ugaidi na kupanga njama za Kuua Viongozi wa Serikali

Huu ujinga wote wanaopanga wana mkataba na mungu? Wataishi milele? Magufuli alifanya vyote vibaya leo hayupo hata yeyote afanyae mabaya ipo siku atakwenda tu
Hata myie mnaofanya "mema" muda wenu ukifika na nyie mnakwenda tu.

Msitishe watu na kifo
 
Hata mahakama ya uhalifu wa kimataifa ICC sasa wanaanza kuangazia hilo taasisi za haki za binadamu zote wameona uonevu mateso waliofanyiwa wananchi kule mwanza, hii inaenda kumletea chuki kubwa Mama na itaharibu mazuri machache aliyokuwa kaanza kuyafanya
Potelea nyanda za juu kusini.

Sisi kazi inaendelea huku
 
Pesa ya walipa kodi zinatumika hovyo kukandamiza demokrasia kwa njia haramu za kishetani, wametumia gharama kubwa kumsafirisha mbowe tokea mwanza hadi huko Dsm kwenda kusachi nyumbani kwake ni Aibu iliyoje
Amani ndio jambo ambalo hatuwezi ku-compromise. Tunataka Watanzania waishi kwa amani ndani ya nchi yao.

Kwahiyo, tutatumia gharama yoyote kama taifa kuilinda amani yetu. Hatavumiliwa yoyote yule anaetaka kucheza na amani yetu
 
Vurugu zipi? Wananchi wapi unawasemea? Hivi Unafikiri wananchi ni wapumbavu kama wewe? Wananchi wanaona wanaujua ukweli acha kuendekeza njaa zako kujinufaisha kupitia uonevu unyanyasaji uovu mateso ya kishamba kwa chadema
Yaani mateso kila siku ni kwa Chadema tu??
 
Nchi ilikuwa imeanza kwenda vizuri lakini wajinga wachache kwa masilahi yao badala ya masilahi ya kitaifa wameamua kumshauri mama afanye udikiteta wapate kutimiza lengo lao, mama kuwa makini na washauri wako maana sasa wanaenda kukuharibia sifa zako zote
Tulivyokuwa tukiwaeleza kwamba muwe na adabu si mlisema mtamnyoa mama???

Haya sasa kazi kwenu
 

CCM ya sasa inachafua taswira ya Tanzania,ni muda sasa tuchukue hatua,mimi naanza kwa kususia system zao za kodi...sitatumia miamala ya simu kutuma hela,

Nawapa notice wapangaji wangu wanaofanya kazi jeshi la polisi,sitashirikiana na mwanaccm yoyote ktk shughuli za kijamii. Nafikiria hatua zaidi...
 
Nchi ilikuwa imeanza kwenda vizuri lakini wajinga wachache kwa masilahi yao badala ya masilahi ya kitaifa wameamua kumshauri mama afanye udikiteta wapate kutimiza lengo lao, mama kuwa makini na washauri wako maana sasa wanaenda kukuharibia sifa zako zote
Kwani mama ni mtoto mdogo anashauriwa vibaya akubali kila kitu msimdharau hivyo. Please!
 
Washauri wa mama acheni kumpotosha apate kuja kuwa Rais mwanamke wa kwanza Tanzania ambaye amekosa utu na haki za binadamu
Acha dharau apotoshwe yeye mtoto mdogo. Huyu ni Rais ana uwezo mkubwa kuliko unavyofikiria wewe.
 
Ukishika mkia wa mnyama mkali lazima akushughulikie. Ukikaribishwa sebuleni usifanye haraka kutaka kuingia chumbani bali subiri ukaribishwe chumbani baadaye. Vingenevyo unaweza ukafikiriwa kwamba wewe ni mwizi kumbe siyo. Hekima inatakiwa unapotekeleza- mikakati ya kukabiliana na adui/mshindani wako. Amemlazimisha mama kwenda maili nyingi. Ajiandae !
[emoji106]
 
Ukishika mkia wa mnyama mkali lazima akushughulikie. Ukikaribishwa sebuleni usifanye haraka kutaka kuingia chumbani bali subiri ukaribishwe chumbani baadaye. Vingenevyo unaweza ukafikiriwa kwamba wewe ni mwizi kumbe siyo. Hekima inatakiwa unapotekeleza- mikakati ya kukabiliana na adui/mshindani wako. Amemlazimisha mama kwenda maili nyingi. Ajiandae !
Mnamwita Mama amewazaa?
Yule ni Raisi wa wote.Nyie mna Mama sisi tuna Mungu.
 
Viongozi wa chadema mipango yao ya siri inafahamika
kwa sasa hakuna tena siri maana Makamanda wengi wa ukweli wapo nje ya Chadema na wanajua mikakati na figisu zote zinazo fanywa na viongozi wa chadema.
Polisi inataarifa zote za muhimu kupitia Makamanda wazalendo wa Taifa.
 
Mie sielewi nini kingeharibika, iwapo wangefanya kongamano lao la katiba? Hakuna jambo lolote lingetokea, hakuna sheria iliovunja, mambo mengine mnayakuza bure, eti polisi anasema awajui kama mkutano ulitaka kufanyika ni wa adhara au wa ndani! Inabidi tuwaelimishe polisi maana ya mikutano na aina na tofauti kati ya adhara na ndani!
 
Back
Top Bottom