Freeman Mbowe atuhumiwa kwa Ugaidi na kupanga njama za Kuua Viongozi wa Serikali

Freeman Mbowe atuhumiwa kwa Ugaidi na kupanga njama za Kuua Viongozi wa Serikali

Baada ya upekuzi wa Polisi kukamilika nyumbani Kwa M.Kiti Mbowe, tumepokea taarifa za kushtua na kushangaza kuwa Polisi wamemwambia kuwa ataunganishwa kwenye kesi ya Ugaidi na watuhumiwa walioko gereza mojawapo DSM. Tutaendelea kutoa taarifa za kina hapo baadaye.

View attachment 1862953

====

UPDATES;

=====

TAARIFA KWA UMMA

JESHI LA POLISI LAMTUHUMU MWENYEKITI WA CHAMA
MHE.FREEMAN MBOWE NA "MAKOSA YA UGAIDI"

Mwenyekiti wa Chama Taifa Mhe. Freeman Mbowe alifikishwa Dar es Salaam jana majira ya saa tatu usiku chini ya ulinzi wa Polisi , walimpeleka nyumbani kwake Mikocheni Kwa ajili ya kumfanyia upekuzi ambao ulichukua takribani saa mbili na nusu.

Baada ya upekuzi huo Polisi waliondoka na Kompyuta mpakato (Laptop) na Vishikwambi (tablets) za watoto wake, Kompyuta mpakato moja ya kwake na modem ya Internet Kwa ajili ya uchunguzi wao.

Leo majira ya saa Saba mchana Polisi walimfikisha Mhe. Freeman Mbowe Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano na kuchukua maelezo yake.

Polisi walitaka maelezo kutoka Kwa Mhe. Freeman Mbowe kuhusiana na kosa waliloliita 'KULA NJAMA ZA KUTENDA KOSA LA UGAIDI'

Baada ya maelezo hayo ya Polisi Mhe. Freeman Mbowe alitumia haki yake ya kisheria na aliamua kutokutoa maelezo yoyote Polisi kwa mujibu wa Sheria. Baada ya maelezo hayo Polisi wamemrejesha Mhe. Freeman Mbowe katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay ,Jijini Dar es Salaam.

Aidha , viongozi wengine waliokuwa wanashikiliwa Mkoani Mwanza wameendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi na baadhi yao walifanyiwa upekuzi nyumbani kwao na vyumba vya hotel ambako walikuwa wameshukia .

Waraka wa Mbowe kwa Watanzania
Mwenyekiti Taifa Mhe. Freeman Mbowe ametuma waraka kwa Watanzania kama ifuatavyo;
"Hatimaye madai ya Katiba Mpya yamenisababishia kesi ya ugaidi, nipo tayari kwa mashtaka ya kuchongwa siogopi. Ninaamini Dunia itaujua ukweli wa kile kinachoendelea Tanzania na kile tunachokipitia Watanzania. Lakini pia itajua ukweli juu ya makosa haya ya kuchongwa.

Natoa wito kwa watanzania kuendeleza mapambano, haki hutafutwa” Mhe.
Freeman Mbowe.”

Imetolewa leo Alhamisi tarehe 22 Julai, 2021.

John Mrema
Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje.

=====

UPDATE:

View attachment 1863559
View attachment 1863560
huyu mama akianza kufanya mambo kama ya jiwe atafia madarakani na yeye

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu mama amejua kuchemsha. Kumbe waliomdoubt tangu mwanzo walikuwa na point aisee. Amejua kutushangaza. Mambo gani ya hovyo hivi!!
 
Nasikitika nilimpa Imani kubwa Sana Mama.Yanayojiri ni kinyume chake.
 
4) Kutunga katiba zinazowalinda na kuwapa madaraka makubwa watawala kuliko wananchi

Serikali chini ya Samia Suluhu Hassani na CCM hakika ni "dola ya kigaidi"...

Kinachoendelea sasa ni STATE SPONSORED TERRORISM dhidi ya wapinzani wa dola ya kigaidi la Tanzania...

Hii "dola ya kigaidi" au "kikundi cha serikali ya kigaidi" kikishajitungia katiba ya kulinda maslahi yao, hujitamba na kujinadi kuwa hiyo ni katiba ya wananchi wanayoikubali na hutumia njia zote za kigaidi kuilinda na ku - suppress kila sauti ya kukosoa ubovu wa katiba hiyo...

Haya yanayoendelea sasa dhidi ya CHADEMA na wafuasi wao na m/kiti wao taifa Ndugu Freeman Aikael Mbowe ni ugaidi wa kidola moja kwa moja
 
Bila kumwaga damu, hakuna mabadiliko kamwe. We are stuck with CCM na polisi wao.
100%Yaliyojiri kwa Mrema,Seif na Mahita makondena ya visu,Mabomu ya Arusha,Slaa kutegeshewa vitu hotelini,Lissu kupigwa lisasi na sasa Mbowe nani atafuata?
Je,nisuluhisho?
 
Tatizo ni viongozi wetu. Tangu akina Maalim, Mrema (enzi hizo), na sasa akina Mbowe, hakuna anayetaka kumwaga damu. Na CCM wataendelea daima dumu. Hawatabadilika. Walimfanyia uhuni Maalim from 1995 hadi kifo chake. Akina Mbowe wasitegemee mabadiliko bila kumwaga damu. Wakenya walikwisha mwaga damu na kupata katiba yao.
Natamani kila mtanzania asome hii comment yako.
 
Nimepima maelezo ya msemaji wa polisi na Mbowe mwenyewe, nimetafakari Sana.

Ila kwangu nimeamua kumwamini Mbowe na kumpuuza huyu polisi. Kuna sababu nyingi Sana za kumuamini Mbowe, hata mtoto angeamini tu.

Pole sanaMbowe, umefanyiwa ugaidi ma magaidi, tunajua. ila Sasa unaitwa gaidi wewe.

Lala kwa taabu huko uliko ila tunakuombea Sana huwezi dhurika na hao mawakala wa magaidi wanaokulinda kwa bunduki zetu.
 
Ndugu, mimi mtu akijisifia kwa "ubakaji" wa demokrasia na "uharamia" wa "uchafuzi" wa serikali za mitaa wa 2019 na "uchafuzi" mkuu 2020,huyo huwa namuweka kwenye kundi la "vibogoyo" wa akili.
Hivi hawa wanapropaganda wa CCM siku hizi wanasomeshwa wapi!!??
Hawana propaganda za Romania.
Hawana propaganda za Soviet.
Hawana propaganda za Israel.
Wa wapi hawa!?
Uchaguzi upi ulimchagua magufuli? Mwananchi yupi? Kura zipi? Tume upi? Hakuna uchaguzi Tanzania kilichofanyika ni CCM kuulawiti kuubaka kuunajisi uchaguzi mkuu kwa njia haramu za kishetani t
 
Nimepima maelezo ya msemaji wa polisi na Mbowe mwenyewe, nimetafakari Sana.

Ila kwangu nimeamua kumwamini Mbowe na kumpuuza huyu polisi. Kuna sababu nyingi Sana za kumuamini Mbowe, hata mtoto angeamini tu.

Pole sanaMbowe, umefanyiwa ugaidi ma magaidi, tunajua. ila Sasa unaitwa gaidi wewe.

Lala kwa taabu huko uliko ila tunakuombea Sana huwezi dhurika na hao mawakala wa magaidi wanaokulinda kwa bunduki zetu.
Hivi mtaendelea kuwafanya vijana WAJINGA mpaka lini?!!!

Hivi humu barani afrika siasa zinarahisishwa kiasi mfanyavyo?!!

Ingekuwa ni rahisi BOBI WINE angekuwa Prezooo...

Ingekuwa ni rahisi Raila Odinga angekuwa ni Prezooo....

Ingekuwa ni rahisi MR SLIM asingekuwa hadi Sasa.....

Mungu amrehemu Marehemu mama ASHA BAKARI aaamin...alisema nchi haitoki kwa makaratasi 🤣

MNAPOPAMBANA NA WENYE NGUVU ZA M
KIUTAWALA MSITAKE HURUMA KWETU ,KATU HATUTOLIA KAMA HAJI MANARA KWA MASHABIKI WA SIMBA!

#KaziIendelee
#NchiKwanza
#AmaniKwanza
 
Acha kufata upepo
Achana nae huyo,ni mshabiki ila sio mchambuzi wa siasa za tz tangu mfumo wa vyama vingi hasa kinapotokea chama chenye hoja na nguvu na hakinunuliki.

Mbowe ni Gaidi hata akawezesha wabunge 19 waapishwe na serikali ikaona sawa.Kwanini usiamini UGAIDI.
MUNGU NDIO HAKIMU KWA TZ.
 
Back
Top Bottom