Freeman Mbowe, Mnyika na Viongozi CHADEMA wakutana na Rais Samia na Viongozi wa CCM Ikulu ya Chamwino - Dodoma leo 20/5/2022

Freeman Mbowe, Mnyika na Viongozi CHADEMA wakutana na Rais Samia na Viongozi wa CCM Ikulu ya Chamwino - Dodoma leo 20/5/2022

Matendo yao ACT ndio yanawaweka kwrnye hiyo Category. Chadema iko very clear. Umeona tukioa la kina Mdee?? Hatulei ujinga sisi na hii ndio sababu ya watanzania kutuamini.
Matendo kama yapi

Maana hata akikutana na Raisi bado Zitto ataambiwa kafata maslahi na uzuri hyo mijadala ipo humu pia

Tatizo siasa zetu za Tanzania kuna kakikundi kanajihesabia haki zaidi ya wengine

Hyo ipo CCM,Chadema,ACT n.k kila kimoja kinajiona chenyewe ndio kina haki zaidi ya kingine

Ndio maana hata wakifika kwenye uchaguz huwa wanaungana kinafiki majimbo hawaachiani kiukwel ukwel wanafanyiana figisu kwa kuweka wagombea wawili eneo moja.
 
Unadhani akili za Lisu ni kama za kabudi? Watu wanatofautiana sana tena sana kufikiri. Kama umesoma some history of science, Albert Einstein alipopendekeza theory of relativity, wharping of spacetime and the like dunia nzima ya Scientists haikumuelewa. But later walimshangaa kwa kiwango alichokuwa nacho baada ya kumuelewa. Na mpaka leo hakuna mwanadamu kama yeye kwa akili alizokuwa nazo.
Likewise Tanzaia, kuna wachache kama 0.000000000000000000000000001 wana uwezo wa kufikiri sawasawa
Sawa kila mtu ana akili zake alizopewa na mungu, ila kisiwe kigezo cha kudharau wengine, wako wengi tuu wenye akili sema hawaongei usione lissu ana akili sana kuliko wengine, watu wametulia tuu huko sio waropokaji, wako magineus wengi tuu tz ila sio waongeaji
 
Zitto hata kabla ya kukutana na rais alishawekwa kundi la wasaliti hivyo akikutana naye huo ni muendelezo tu wa usaliti ambao uko ndani yake kitambo, learn how to differentiate things.
Na uzuri hii nchi huwa tunapeana shutuma bila ushahidi

Hadi leo Dk.Slaa anaitwa msaliti ila ukimuuliza mtu alisaliti nini ngonjera zinakuwa nyingi

Lowasa alipewa shutuma za kila namna je ilikuwaje

Vyama vya upinzani kutuhumiana ni kawaida yao tena hata bila ushahidi wao huwa wanasambaza propaganda na kuacha wale wanaopenda maneno bila ushahidi waendelee nayo

Zitto aliwahi kusema Nimrod alimpatia Mbowe pesa ili asiweke mgombea kwenye jimbo husika je tumuamini kisa kasema bila ushahidi

Ukiniletea ushahidi wa Zitto Kabwe kufanya usaliti kwa Chama chake basi cha zamani takushukuru saaana.
 
Dudumizi lazima unune sana ukimuona Heche Ikulu🤣🤣

Muachage dharau.
Jamaa amesababisha chawa wake mtumie muda mwingi kumtetea yeye, badala ya kutetea chama. Lisu, Lema na misimamo yao wote chali. Hizi ndio siasa za Tanzania aisee 😂😂😂🤣🤣
 
Jamaa amesababisha chawa wake mtumie muda mwingi kumtetea yeye, badala ya kutetea chama. Lisu, Lema na misimamo yao wote chali. Hizi ndio siasa za Tanzania aisee 😂😂😂🤣🤣
jana umelala na viatu.
 
To open up a new chapter as a nation haijawahi kuwa dhambi...

Hili kama ni kweli bac ni jambo jema kwa kila mwenye pumzi..

Narudia tena Political reconciliation ndiyo njia pekee ya kujenga taifa imara lenye umoja na nguvu kiuchumi kisiasa na kiutamaduni.

Nchi haiwezi kujengwa na mawazo ya upande mmoja.
Hivi CHADEMA wanafanya reconciliation gani na Serikali?
 
Unachosema ni sahihi lakini bahati mbaya sana mkuu hutoi alternative wanafanye nini badala yake.
Chadema wanaangalia na aina ya jamii tuliyonayo. Mbali na maridhiano njia pekee ni maandamano na kufanya nchi isitawalike. Yuko wapi mwananchi wa kufanya hayo? Wazee wa nchi wapo kimya,wamejaa unafiki,wananchi wanalalamika kichini chini. Sisi wachache mimi na wewe tumejificha kwenye keyboard. Mbowe afanye nini zaidi ya kutumia fursa ya kukaa meza moja.
Kukaa meza moja pia haimaanishi kusaliti misisimamo bali kueleza misimamo badala ya kutunishiana misuli kwenye majukwaa. Utatuna msuli jukwaani lakini ili unayemtunishia akupate vizuri inabidi akusikilize ukiwa kwenye utulivu na umweleze kwa ufasaha.

Ni kipi ambacho Chadema hawajafanya katika kutunisha misuli. Waliingia barabarani ikapalekea mauaji kesi ikawageuka na wananchi hawakuchukua hatua yeyote. Mbowe kakaa jela,Lissu kapigwa risasi mchana. Uchaguzi kura zimeibwa nk Wananchi walichukua hatua gani kali?

Naunga mkoni maridhiano kwa sababu hayupo raia wa kuingia barabarani kutumia nguvu ya umma
Issue sio lazima kuingia barabarani, mfano kususia bunge ilikuwa njia nzuri na tumeona walivyo panic mpk kwenda kutengeneza wasaliti kwa maslahi yao.
 
Na uzuri hii nchi huwa tunapeana shutuma bila ushahidi

Hadi leo Dk.Slaa anaitwa msaliti ila ukimuuliza mtu alisaliti nini ngonjera zinakuwa nyingi

Lowasa alipewa shutuma za kila namna je ilikuwaje

Vyama vya upinzani kutuhumiana ni kawaida yao tena hata bila ushahidi wao huwa wanasambaza propaganda na kuacha wale wanaopenda maneno bila ushahidi waendelee nayo

Zitto aliwahi kusema Nimrod alimpatia Mbowe pesa ili asiweke mgombea kwenye jimbo husika je tumuamini kisa kasema bila ushahidi

Ukiniletea ushahidi wa Zitto Kabwe kufanya usaliti kwa Chama chake basi cha zamani takushukuru saaana.
It's like you don't have clues whatsoever of the real games inside the political world, unadhani huo ni wizi wa maembe kwamba umtamkuta nayo kama kidhiti or you're just playing a mind game as the politicians do.
Hivyo vitu huwa based na circumstantial evidences, kama hauelewi mambo yanavyokwenda 'under water' then just go with the flow au waachie wajuvi wa mambo.
Traitors, back-bitters, snitches pamoja na hypocrites huwa haihitaji elimu yoyote kuwabaini lakini ukiwaangali na kuwafuatilia with open mind utawajua tu kwahivyo usishangae watu wakafanya vitu similar lakini vikapata mapokeo tofauti kwani 'the real intentions' ndiyo husababisha mapokeo tofauti.
 
Mkuu lakini hayo yameshafanyika. Chadema wamesusia chaguzi na bunge bila shaka unakumbuka. Lakini tazama pia impact ya kususia inavyokuwa haileti matokeo makubwa kwa sababu wako wapi wananchi wakususia drastically?

Baada ya kususia na kupaza sauti what next? Si inabidi mkae muweke hoja mezani? Kwa nini tusiamini pia hii meza wanayokaa ni impact ya kususia vikao vya kamati ya Zitto,bunge nk

Mkuu sipingi maelezo yako mazuri, lakini nikuambie kitu, hao viongozi wanachezewa shere, huyo mama anataka atawale bila kelele, na mengi ya madai ya msingi ya CDM hayatayanyiwa kazi, na akija kiongozi mwingine wa CCM hatatambua makubaliano hayo. Wanaccm wengi wenye maamuzi hasa huku bara hawako tayari kwa maridhiano, kwani maridhiano kwao ni kupoteza nafasi zao za ulaji. Simply sina imani ni hii miafaka, na mifano ninayo.
 
Wewe kama ulikuwa kwenye akili yangu. Hivi kwanini Mambo yaliyomo kwenye katiba yaombwe kama hisani toka kwa rais?

Kwa kufanya hivi vyama vya upinzani vinajifunga miguu na mikono vyenyewe. Maana vinapoenda ikulu kuomba hisani kwa Mambo ambayo ni haki ya kikatiba rais anqvimba kichwa

Kabisa, wameenda kutoa uhalali kwa mtu asiye na uhalali. Tunazijua haki zetu, kuminywa kwa haki zetu sio sababu ya kusurrender.
 
Ikulu tafuteni mpiga picha professional wa kiwango cha juu kabisa hii ni ikulu lazima kuwa na quality katika picha.
 
Wakati anaharibiwa shamba lake na kufukuzwa NHC maslahi yake yalikuwa wapi?. Hicho sio kikao Cha Mbowe, ni kikao Cha CCM na serikali pamoja na chadema. Turuhusu watu waongee kwanza baada ya muda mrefu.
Wewe bado kijana mdogo haujui misingi wala mfumo wa uanzishwaji wa vyama vingi. Uanzishaji wa vyama vingi ilikuwa geresha tu ya serikali ya wakati ule katika njia ya kutafuta kuvuta mpunga kupitia ufadhili wa nchi za magharibi. Ndio maana baada ya uanzishwaji wake kila chama kilipandikizwa watu wa mfumo ambao kazi yao itakuwa ni kurudisha nyuma juhudi za chama chochote kinachoonekana kuwa tishio la kweli kwa chama tawala. Tuliokuwepo toka enzi hizo tuliona kilichotokea kwa NCCR kupitia Mrema mwenyewe ambae alizima ndoto za wengi kwa kukisambaratisha chama. Ikaja CUF "wazee wa ngangari" ambayo ilipiganiwa mpaka watu kuuwawa kule pemba huku aliekuwa katibu mkuu wa chama hicho na aliekuwa mgombea uraisi wa Zanzibar mh Maalim Seif akiwa zake ughaibuni na familia yake wakila bata. Ikaja Chadema ambayo ilipamba moto mpaka watu wakaamini kuwa mwaka 2015 CCM ingemfia mikononi aliekuwa mwenyekiti wa chama hicho na raisi wa JMT wa wakati huo mh Kikwete. Kwa hali ya upinzani ilivyokuwa wakati ule Chadema chini ya ukawa iliyosheheni viongozi madhubuti waliokijenga chama kwa misingi ya kupambana na ufisadi, hakika chama kilikuwa tishio kweli kwa chama tawala, kwahiyo ikatumika ile ile mbinu iliyotumika kuuwa au kuvinyong'onyesha vyama vingine, mwenyekiti wa chama ambae mtu yeyote mwenye akili anaamini kuwa ni mtumishi wa siri wa mfumo akatumika kuhakikisha mgombea aliekatwa CCM makusudi anakuja ndani ya chama chake na yeye anamtengenezea mazingira mazuri ya kukisambaratisha chama kama vile kumpa nafasi ya kugombea huku akiamini kuwa nafasi hiyo ingekigawa chama na kumpa adui nafasi ya kutimiza malengo yake. Kweli jamaa akafanya kile alichofanya akishirikiana na mfumo kimya kimya, baada ya hapo chama kikafika hapa kilipo sasa. Swala la mashamba, hiyo huwa ni geresha inayotumiwa na wana mfumo. Yani wanaharibu shamba 1 hadharani, afu wanakupa mashamba 11 mafichoni ili watu wasije kushtuka kama unatumiwa nao. Kina Mrema wana mpaka makovu yaliosababishwa na kutupiana viti na wanachama wenzake akijifanya anapigania haki za chama kumbe sirini anapigania maslahi ya chama tawala, Lipumba ashawahi kuvunjwa hadi mkono katika maandamano ila ya sirini anayajua yeye na Mungu wake. Nafikiri mpinzani wa kweli ni Lisu tu ndo maana yalimkuta yale yaliomkuta, ila hawa wa mashamba sijui studio ya bilkanas ni geresha tu kwa wasiofahamu siasa za Tanzania.
 
Nyie mlitakaje kama mazungumzo hayapo? Vita au ugaidi?
Chama cha siasa kinapambana kwa hoja, na msipoelewana ndio yanakuja mengine kama ya kule Congo au Msumbiji.
Samia kesha gundua chama makini cha upinzani ni Chadema ndio maana kawaalika wazungumze, sio wale ambao unapingana naye lakini ukimlambisha sukari anasema Samia anashinda uchaguzi. Kwani ccm walikuambia wanamsimamisha?
Chawa mna kazi mwaka huu. Huku mnapambana kusafisha madudu ya mwenyekiti, huku mnapambana kusafisha madudu ya chama nk 😂😂😂
 
Issue sio lazima kuingia barabarani, mfano kususia bunge ilikuwa njia nzuri na tumeona walivyo panic mpk kwenda kutengeneza wasaliti kwa maslahi yao.
Mkuu nakubaliana na wewe,lakini wakishasusia mambo yanajipa yenyewe automatically? au inabidi sasa wakae wajiulize na kukubaliana waanzie wapi kurekebisha? Hoja nzuri zinazongumzwa majukwaani mwisho wa siku inabidi ziende mezani. Kumbuka kama rais ndiyo mtu wa kutoa maelekezo kwa vyombo vyake,iwe katiba au chochote,sasa mkimkimbia utasaidia nini. Yote hayo ya kususia yalifanyika kwa dikteta Magufuli,alitaka hata kukaa meza moja?

Simuungi mkono Samia,lakini hii ni fursa ya kusukuma hoja. Hata katika maisha ya kawaida,ipi ni fursa nzuri ya kumchana mtu anayekufanyia ubaya. Kukutana naye macho kwa macho na kunchana muafaka upatikane,au kumkwepa na kuendelea kutunisha msuli?
 
Wabunge wa Chadema kusamehewa...

Hivi Rais akiwa ikulu na akaamua kutoka point A to Point B humo humo ndani msafara lazima umfuate...
 
Back
Top Bottom