Freeman Mbowe: Rais Samia Suluhu anateswa na kivuli cha Magufuli

Freeman Mbowe: Rais Samia Suluhu anateswa na kivuli cha Magufuli

..Mbowe anatakiwa kuuma na kupuliza.

..kwa maoni haya naona kama ameuma bila kupuliza.

..Kuna wana-ccm ambao wanapinga azma ya Rais Samia Suluhu kuboresha mazingira ya kisiasa nchini.

..Ni vizuri Mh.Mbowe na viongozi wa CDM wasizungumze kwa namna ambayo inamvunja moyo Rais Samia ktk kuleta maridhiano ya kisiasa nchini.

..Kwa kifupi sijayapenda maoni ya Mh.Mbowe.
Mimi nadhani anachokifanya Mbowe ni kumhakikishia kuwa kuna watu wanamfuatilia kwa makini matendo yake na asi wa take for granted. Kwa upande mwingine msimamo na matamshi ya Mbowe yanamjengea legitimacy katika chama chake kama mrithi wa JPM. Kwa CCM wengi adui namba moja ni Mbowe na angeonyesha kuwa anamkubali kwa aina yeyote Mheshimiwa Rais wetu ungewafanya wamtilie mashaka, kwa maneno mengine ingekuwa ndio busy la kifo kwake. Wapambe wako wengi ( Zitto n.k.) Mbowe hahitajiki kujiunga nao. Huu msimamo unawajenga wote wawili, Mbowe kama mpinzani asiyetetereka na Mheshimiwa Rais kuwa yeye ni mrithi sahihi wa Mwendazake.

Amandla...
 
Hapo sasa Dj Mbowe atashangaa anataka kucheza na Mama atashangaa ajawaita kwenye kikao wakashindwa kutoa ya moyoni
 
Sasa Mkuu ikiwa Mama anasema anafuata nyayo za Magufuli aliyekimbiza wawekezaji lakini wakati huohuo anataka kurudisha imani ya wawekezaje wewe unaelewa nini ?
Sharti ni kwamba asigeuke nyuma lakini kelele ni nyingi za huyooo huyoooo! Hicho ndicho kivuli but SASHA is detemined, deliverables shall speak.
 
Sasa Mkuu ikiwa Mama anasema anafuata nyayo za Magufuli aliyekimbiza wawekezaji lakini wakati huohuo anataka kurudisha imani ya wawekezaje wewe unaelewa nini ?


Hamjui siasa?
Unataka mama aende bungeni aseme Magufuli alifukuza wawekezaji?
 
Sometimes naona kizunguzungu jinsi wanasiasa walivyo hawaeleweki wanataka nini utafikiri wanatumwa kuzingua tu
 
Mbowe ulishapitwa na wakati wewe kaa pembeni achia wengine waongoze cdm umekuwa mbinafsi sana tu na hujitambui.

Chama kipokipo tu hakina mbele wala nyuma usifikiri utatoka kwa kutaka kumpotosha Mh Rais SSH.

Mh Rais kaujua ukweli wa mawazo na matamanio ya Watanzania wengi anao waongoza. Hotuba yake leo Bungeni imedhihirisha hilo. Lazima auishi ukweli huo na sikufuata mambo ya genge flani ambalo kimsingi ni cartel ya kuibia nchi kwa mgongo wa uongozi wa kisiasa.

Mbowe haja kosea kazi bado iko kweli maana Watanzania wa leo sio mandondocha tena wa kupelekwa pelekwa na mijizi na mafisadi.

Mh Rais kahutubia sahihi na bila kumungunya maneno kaamua kudemka kwa kufuata mirindio ya upepo wa kisiasa unaovuma kwa nguvu hapa nchini kipindi hiki.
Ulitaka Mbowe afanye nini wakati mijizi iliiba kura na bunduki zinazonunuliwa kwa Kodi zetu..aaarrggghhh
 
Mimi napendekeza kwamba tumpe mama Samia nafasi. Hayo machache anayosema, mfano kukutana na vyama vya upinzani, Magufuli hakuwahi kuyafanya. Alifanya tu usanii wa kuwaita baadhi ya viongozi, kukidhi malengo yake ya kisiasa. Mheshimiwa Mbowe uliomba Rais akutane na viongozi wa CHADEMA. Tumieni kwanza hiyo fursa, kisha ndipo hukumu itolewe.
Sioni kama SSH ana uhuru kihivyo. Lakini ukweli hasa utajidhihirisha. Kwa sasa tumpe nafasi acheze kete zake
 
Huyu Dj anajua kuwa na yeye ni dikteta au kwa vile Chadema hawamwambii ukweli? sifa moja ya madictator kung'ang'ania madarakani

Sitaki kuamini kama Chadema wote hawana akili mwenye akili ni Mbowe tu lakini kumbukeni Mbowe ni Binadamu kuna siku atakuwa hayupo leo JPM hayupo lakini CCM ipo na inapata mwenyekiti mwingine kwa amani kabisa kila mtu akitabasamu kwa maana utaratibu ulishatengenezwa siku Mbowe akiondoka tutashuhudia ugomvi na kugombea madaraka ndani ya Chadema .
Amini sasa
Chadema Wote hawanaga akili
 
Mimi napendekeza kwamba tumpe mama Samia nafasi. Hayo machache anayosema, mfano kukutana na vyama vya upinzani, Magufuli hakuwahi kuyafanya. Alifanya tu usanii wa kuwaita baadhi ya viongozi, kukidhi malengo yake ya kisiasa. Mheshimiwa Mbowe uliomba Rais akutane na viongozi wa CHADEMA. Tumieni kwanza hiyo fursa, kisha ndipo hukumu itolewe.
Sioni kama SSH ana uhuru kihivyo. Lakini ukweli hasa utajidhihirisha. Kwa sasa tumpe nafasi acheze kete zake
Sawa mkuu
 
Hawa wanasiasa wawili wanaokuwa na tabia ya kujinasibu kuwa wao mabingwa wa uzandiki wa siasa za hapa Tanzania mbona wako Kimya?

Au ndio wanaunga juhudi kimyakimya maana tumeshuhudia miaka mitano chini ya hayati JPM wakiburuzwa na kugarazwa kama kambale kwenye matope.
Wajinga kumbe bado mpo ee? Badilikeni mfikie mahali mjue umuhimu wa upinzani katika nchi.
 
Labda atabadilika baada ya miezi michache ya kuwepo Ikulu lakini kwa mwendo huu matumaini makubwa niliyokuwa nayo kwake ya kuongoza nchi kwa kuheshimu Katiba, haki, usawa na sheria za nchi yamefifia.
Sioni dalili ya kupata katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi kabla ya 2025.
Nyumbu bwana! Kwa hiyo mnategemea rais wa ccm siku moja atawapa katiba mpya na hiyo tume huru. Hamkuona nguvu ya ccm pale yule mzee wa Msoga alipokaribia kuwapa katiba mpya!

Acha mwenyekiti wenu wa kudumu aendelee kuwayumbisha.
 
Back
Top Bottom