FT: Namungo FC 0-3 Simba SC | NBC PL | 19.02.2025

FT: Namungo FC 0-3 Simba SC | NBC PL | 19.02.2025

Leo nataka kushuhudia kwa macho yangu maigizo ya Bongo muvi. Yaani Mgunda huyu huyu kocha wetu wa akiba, akubali timu yetu kufungwa! Hata sare tu haipo kwenye mechi ya leo.

Kwa wale wazee wa kubet, hakika leo ni siku yenu ya kuvuna hela. Mpe Simba mazima hata milioni 2. Na hutojutia.
 
sikufuatilia ratiba rasmi ya bodi ya ligi,niliandika kimazoea. Samahani,turudi kwenye uzi wetu.
Huna unachokijua kichwa chako kimejaa funza hata mpira wenyewe umeanza kufuatilia juzi tu.
 
Simba vs Namungo ya mgunda. Tff na TAKUKURU fuatilieni kwa ukaribu
Naunga mkono hoja. Leo kuna timu inaenda kupewa pointi 3 na magoli ya kutosha, bure kabisa! Ni vizuri Takukuru wakawahi eneo la tukio.
 
Halafu unaanzishaje uzi timu haikuhusu??? Kutuletea nuksi tuu
yeyote anaweza kuanzisha uzi mkuu,ili mradi tu ukidhi vigezo na uwawahi wenzio, sasa natangaza vita,nitakuwa silali mpaka nihakikishe nakuwa wakwanza kila mchezo wa NBC PL hasa mechi za SIMBA na YANGA
 
mengine mkuu tunayaleta kwa lengo la kuufungua macho uma katika maswala magumu yanayowakabili. Mimi nikaona nijivike uhusika wa kumchukia mdingi ili ujumbe ufike kiurahisi. Sijui umenielewa The Legacy ?
Una laana ya baba ako ndo maana hata tarehe za mechi unasahau.
 
Tumebishana sana jana baadae ikabidi nikae tu kimya maana kila mtu akawa ananishambulia Mimi nikajiuliza tu swali mbona ni rahisi tu kujua ratiba kupitia Instagram pages za Azam Tv, timu husika na hata bodi ya ligi, kwanini mtu anakua na haraka ya kuja kupost bila kujirudhisha kwanza?!, Hilo nalo hadi tusubiri wachambuzi kweli?!...end of the day uzi wa hiyo mechi ukafutwa nadhani walijua kuna kitu hakipo sawa
Halafu hawa mazombi wanaokimbilia kupost live updates za mechi hua wala hawatoi time to time updates, unashangaa tu wanaweka full time results. Hopeless kabisa... kuna mwamba mmoja anaitwa Vicenzo nadhani ndo hua anatoa updates.... Hawa wengine magamblish tu..
 
Naunga mkono hoja. Leo kuna timu inaenda kupewa pointi 3 na magoli ya kutosha, bure kabisa! Ni vizuri Takukuru wakawahi eneo la tukio.
Yasipopatikana hayo magoli ya kutosha tukufanyaje?
 
Misimu mitatu mfululizo simba hajawahi kushinda majaliwa stadium dhidi ya namungo wanakuwaje ndugu?
Ni vile tu hambebeki wakati fulani. Ila mwaka huu nadhani mnajitahidi kubebeka. Imagine kwenye mechi 20, penati 16! Na leo tunategemea ziongezeke tena ili Ateba aongoze kwenye ufungaji bora.
 
Back
Top Bottom