Full Time: Young Africans 4 - 0 Tanzania Prisons | NBC premier league | KMC Complex| Disemba 22, 2024

Full Time: Young Africans 4 - 0 Tanzania Prisons | NBC premier league | KMC Complex| Disemba 22, 2024

Yanga hii sasa ni ya moto sana na ina mambo mengi mazuri, km kucheza kwa spidi , fitness imerudi, kutengeneza nafasi za kufunga, kukaba kwa nguvu kitimu kipindi cha kwanza na kila mechi kufanya sub 5 kuweka nguvu mpya na kwa muda sahihi. Maua mengi kwa Ramovic

Bado timu ina shida kupasua ngome za wapinzani kupitia katikati , Aziz Ki ni mzito kutoa pasi, timu kuridhika baada ya kufunga, kuacha kukaba kwa nguvu kipindi cha pili, wachezaji wengi kupenda mno kurudisha nyuma mpira, na baadhi ya nyakati baadhi ya wachezaji kulazimisha kufunga badala ya kutoa assist, leo Mudathir kazingua sana katuboa sana kama angempa pasi Dube lilikuwa goli la wazi la nne, kwani Muda ana shida gani aambiwe kutoa assist si lazima afunge ye si striker, Pacome anao anao sana badala ya kutoa assist watu wafunge sijui alikuwa anaenda wapi na mpira wenzake washafungua ye yumo tu. Akumbushwe.

Otherwise Yanga inarudisha makali yake kwa kasi.

Maandalizi ya kuifunga Simba yaanze sasa.
1000205115.jpg
 
Malalamiko fc mmeanza!!!
Hahaha msimu huu malalamiko fc wanajulikana mbona, tena walianza mapema sana hata kabla ligi haijaanza, mwanzoni timu zilikuwa zinaikamia sana utopolo ila baada ya ushindi wa jana tutarajie mashambulizi kuhamia unyamani
 
Hawa prisons walichofanya leo ni kulegeza ili kesho kutwa wakikutana na simba wakamie, yani leo ukiangalia ni kama hawakutaka kujichosha kabisa hakuna mashambulizi wala kukaba wanatunza nguvu zao kwa ajili ya kesho kutwa, yani ni kama timu za ligi kuu ghafla zimeswitch kutoka kuiogopa na kuikamia yanga hadi kuiogopa na kuikamia simba dooh
hata yanga pia katunza nguvu kwa ajili ya nyau ko hii inaitwa collaboration
 
Leo wamefunga goli la mkono na wanashangilia.
Ulitakaje kwani bwana mbumbumbu? Tulishakubaliana kwamba atutoitaji malalamiko ya namna yoyote yale kutoka umbumbuni kwakuwa wakati yanga imeyumba kidogo mlifunga mabakuri yenu na kufurahia,,sasa Kila timu ishinde mechi zake inavyoweza tutaona mwisho wa msimu timu Bora ni ipi itayobeba ndoo!
 
Back
Top Bottom