Fuvu na Mifupa(Skull and Bones) Jamii ya Siri ya Kishetani inayoongoza Matukio ya Duniani

Fuvu na Mifupa(Skull and Bones) Jamii ya Siri ya Kishetani inayoongoza Matukio ya Duniani

Sasa kama wanasiri ww umewajuaje?na uhakika gani unachokisema nichaukweli ikiwa ni siri hapo nachanganyikiwa
 
Novus ordo Seclorum...

Order out of chaos,New world order,New order of ages n.k....

Inatumika kwa namna tofautu tofauti sana lakini hapo kwenye hiyo yako imetumika hiyo ya order out of chaos,wanaleta vurugu mahali ili kuleta matokeo wayatakayo.....

Mfano wa hili ni vita viwili vya dunia,vita ya Iraq,Afghanistan,WTC attack,ISIS war,Syrian war,Congo war,Somali war,na vita vingine vyote vinavyoendelea duniani iwe vya nchi na nchi au vya wenyewe kwa wenyewe vyote vimetengenezwa na hawa watu ambao kila mmoja anawaelewa kwa namna tofauti kulingana na ufahamu wake wa amambo yanavyoendelea duniani...

Hatujachelewa sana tunaweza kujua mengi bado...
Kaka nimekuelewa sana.swali hivi tukishayajua haya tutafanyaje maana wao ndo wanaongoza ulimwengu.je kunambadala wa kupingana nao?
 
Nitajitahidi kufupisha kwa namna nitakavyoweza ili nisiandike maandishi mengi japokuwa siyo jambo zuri maana kuna mengine hutayajua...

Bara la Atlantis ni bara lililokuwa kwenye bahari ya atlantic baina ya bara ulaya na Amrerica ya kaskazini.Bara hili lilijulikana kama kitovu cha maendeleo duniani na wakati huo dunia ilikuwa na maendeleo makubwa mara kumi ya sasa.Jambo hili linafichwa sana kwa sababu maalum.Bara hili waliishi magiant [Nephilims] ambao waliendesha utawala duniani utawala ambao ulimuumiza sana binadamu wa kawaida.Kulikuwa kukifanyika kafara za binadamu na viungo vya binadamu vilikuwa vikitumika kwa shughuli mbali mbali za nguvu za giza.Ilifikia mahali damu ya binadamu ilikuwa ikitumika kama kinywaji cha kawaida kwa hawa viumbe..

Unaweza kujiuliza hawa Nephilim ni nani au akina nani.Nephilims ni viumbe ambao walikuwa nusu binadamu na nusu malaika ambao walipatikana baada ya malaika waasi kufanya ngono na wanawake wanadamu.Malaika waasi ndiyo waliowafundishwa wanadamu elimu za unajimu,utoaji wa mimba,kutengeneza silaha na teknolojia nyinginezo ambazo ni za hali ya juu sana.Binadamu baana ya kupata ujuzi huu walianza kuuana wao kwa wao na ndipo Mungu alipoingilia kati na kuleta gharika lililowasambaratisha viumbe wote na kuwasalimisha walioingia kwenye safina...

Maisha ya wakati huu yalikuwa ya kishetani haswa.ni maisha ya kutisha sana maana binadamu alikuwa akiishi kama vile mbuzi leo maana alikuwa akiwindwa vilivyo hadi pale ambapo Mungu alipoamua kuingilia kati.Anayetaka kulirudisha bara hili na ustaarabu ule ni Semjaza,miongoni mwa malaika wakuu walioasi wanataka kuuleta ufalme wao hapa duniani wakishirikiana na binadamu wachache wasiojua ukweli na wanaoujua wachache sana lakini kwa umakini na udanganyifu mkubwa sana wa kisayansi....

Wanataka watawale dunia na jambo hili litatokea siyo miaka mingi kutokea sasa maana wanamalizia tu na wanataka kuwaleta tena hao malaika kutoka walipo kupitia kinachoendelea kule kwenye mitambo yao ya LHC [Large Hadron Collider] kwenye project yao maarufu ya Cern ambapo wanataka kufanya kitu ambacho dunia haitakuja kusahau kamwe...

View attachment 503610 View attachment 503611
LHC

Sananda ni kiumbe wa roho ambaye anajifananisha na Yesu,picha inayotumika kwenye makanisa na ambayo watu wanaamini kuwa ni ya Yesu ni ya Sananda,kuna mengi kumhusu huyu lakini kwa hapa inatosha kusema hivyo.Watu wanadai ni picha ya Cecare Borgia lakini ukweli ni kwamba ni picha ya Sananda.Kiumbe huyu ni miongoni mwa wale malaika waasi na huyu atatumika kudanganya watu wakati watakapo fake ujio wa Yesu.....

View attachment 503607 View attachment 503608 View attachment 503609 View attachment 503609
Sananda...

Sanat Kumara ni Azazel ambaye hujulikana kama Satan Kumara maana jina lake la kwanza limebadilishwa tu herufi.Huyu inasemekana ni Shetani mwenyewe au ni second in command kwenye himaya yao hawa malaika waasi....

Nadhani nimekupa mwanga angalau kidogo....
Mimi nimeelewa kwasababu najua kidogo kuhusu Cern na nephilis .....ila mtu asiye na msingi atakuwa amepotea kama hapo pa picha.....Thanks Eiyer
 
Naomba unisaidie tofauti ya Freemason, Illuminati na hawa Skull & bones?
Sijajua haswa unahitaji tofauti ipi lakini kama unahitaji tofauti ya kimsingi hakuna labda ya kiutendaji...

Nasema tofauti ya kimsingi hakuna kwasababu waliounda Illuminati ndiyo waliounda Freemason lakini kwa malengo tofauti.illuminati ndiyo baba yao na ndani ya Illuminati ndiyo kuna hivyo vyama vya siri...

Ndani ya Illuminati kuna vyama vidogo vidogo vya siri vilivyoundwa kwaajili ua kusimamia maeneo specific.Mfano Skull & Bones wao jukumu lao ni kusimamia masuala ya vyuo.Freemason masuala ya kiimani,hawa wana jukumu la kusimamia maeneo yote ya kiimani yawe wanavyotaka wao....

Lakini,siyo kila mwanachama wa Skull & Bones ni mwanachama wa Illuminati bali wale wa rank ya juu tu ndiyo wanaounda Illuminati.Illuminati ina watu maalum 300 ambao ndiyo hukutana kupokea maelekezo ya |kamati kuu" ya watu 13 ambayo hii hupokea maelekezo kutoka kwa Pindar ambaye ndiye mkuu wake ambaye yeye ni mjumbe kwenye "kamati" nyingine.....

Kwa mfano huwezi kuwa 33 degree Freemason bila kuwa mwanachama wa kamati ya watu 300.Hakuna mwanachama wa juu wa Illuminati mwanamke.Vyama vyote vya siri vipo ndani ya Illuminati lakini hawataki hilo lijulikane kabisa ili kuwahadaa watu...

Chati hii hapa chini itakusaidia kuelewa ninachokuelekeza..

illuminati chat 1.jpeg
 
mimi naona kama kuna Ibada inayoweza kumpa mtu utajiri, haiba,kukubalika na jamii, power na mali halafu usidhuruke mwili wala kudhuru wengine inafaa. Bora tu hao kwa sababu kila binadamu anataka afya, utajiri, madaraka , mali, haiba na kukubalika. Maisha ni hapa hapa duniani kwingine ni imani tuu.
Tusikijua ni kwamba tunadhani vyote hivyo vinapatikana hivi hivi tu...

Dunani kuna pande mbili,either uwe kwa Mungu au upande mwingine na kila upande una namna yake ya kupata mafanikio....

Dhana ya maisha ni hapa duniani ililetwa na hawa hawa tunaowazungumza hapa ili uione dunia ni ya maana sana na ufanye chochote kile ili uendelee kuishi na kupata utajiri.Lakini ukweli ni kinyume kabisa maana tamaa ya maisha ndiyo iliyozaa utumwa na mabaya mengine yote yanayomharibu binadamu....

Kama utajua tu kuhna zaidi ya maisha haya tamaa yako na maisha haya taratibu itaanza kupungua na kuchukulia kawaida kabisa na utawashangaa wanaofikia hadi kuua ili wapate mali...

Wake up...
 
Mkuu away from Google una source yeyote ile inaweza upload
Vyanzo vyote vipo kwenye internet lakini unapaswa utumie muda sana kutafuta maana siyo vyote vinapatikana kiurahisi tu....

Kuna habari zingine za uongo pia hivyo ni kuwa makini na uvumilivu na taratibu utaanza kuona mengi yakijifunua tu kadiri unavyotafuta....
 
Yale Nomaa Apo Pako na Bonesmen wakutosha Very smart H.Bush, H.Taft,W.bush hao ni Maraisi ninaowajua waliotokea Skull and bones
 
Nimrodi ni mjukuu wa Ham mtoto wa Nuhu.Alikuwa ni mtuhodari sana na muwindaji mahiri sana.Vyanzo vingine vinaeleza kwamba,kwasababu ya watu kuanza kuenea baada ya gharika na wanyama kuazaliana kuliibuka kitisho kwa binadamu wa eneo la Babeli la kudhuriwa na wanyama wakati na Nimrod alikuwa akipambana na wanyama vilivyo na kuwa mtu muhimu sana katika jamii iliyomzunguka...

Alianza kua mtawala wa Babel hadi Ninawi na maeneo mengine ya jirani.Alimuoa Semiramis ambaye vyanzo vingine vinasema kwamba alikuwa ni mama yake.Alianzisha dini ya kuabudu sayari ambayo ilikuwa maarufu sana maeneo mengi ya dunia baadaye.Imani hii aliipata baada ya kuwasiliana na viumbe wa roho ambao ni wale malaika walioasi.Dini hii ilikuwa maarufu sana katika Babeli....

Baada ya watu kuwa wengi aliamua kujenga mnara ambao kama itatokea tena gharika basi watu wasife.Alijenga mnara mkubwa sana ambao ulikuwa ni mnara mrefu zaidi duniani kwa wakati ule.Pia hakutaka watu wasambae duniani kote bali wabaki pale pale ili kujenga jamii moja na yenye nguvu ikiwa na dini moja.Maelekezo yote haya aliyapata kutoka kwa malaika waasi ambao alikuwa akiwasiliana nao kwa njia mbali mbali kama vile maono na ndoto....

Dhana hii ya kuunda jamii moja yenye nguvu inayozungumza lugha moja na yenye dini moja ndiyo ipo hadi leo na ndiyo maana hata jengo la umoja wa ulaya limejenga likionekana halijamaliziwa wakimaanisha kudhamiria kukamilisha alichoshindwa kukikamilisha Nimrod.Pia,kitendo kilichotokea sept 11 kule Marekani ni ishara ya kuondoa mamlaka mbili zilizokuwa zikishindana na kubakisha moja ya shetani na ndiyo maana likajengwa jengo moja tu na likaitwa One World Trade center...

Turudi kwa Nimrod..
Babu yake ambaye ni Ham hakufurahishwa na imani hii,aliamua kumuua mwanae huyu na kumkatakata vipande vipande na kuvisambaza katika maeneo yote aliyokuwa akitawala Nimrod na kutoa agizo kuwa yoyote atakayeendelea kufanya ibada alizokuwa anazifanya Nimrod basi atafanywa kama kiongozi wao alivyofanywa...

Suala hili liliwafanya wakazi wa Babel wakaogopa lakini kwa muda tu.Mkewe Nimrod ambaye ni Semiramis alikusanya vipande vya mwili wa mumewe na kuvizika lakini kiungo cha uzazi cha Nimrod hakikupatikana na Semiramis akasema kuwa Nimrod amepaa kwenda kuishi juu na alama yake ni jua [Sun] na tangia hapo alama ya Jua ikawa ni alama ya Nimrod na akaanza kuabudiwa kama mungu na ndipo ibada ya kuabudu jua ilivyoanza na ikaonekana kuwa kiungo cha uzazi ni kitakatifu hivyo wakakitengenezea alama ya kukiheshimu kama alama ya imani yao na ndipo ilipotengenezwa Obelsk..

Obelisk hizi zipo maeneo mengi sana duniani kama vile St. Peter's square kule Vatican,Washingnton DC,Paris,Ufaransa na maeneo mengi kuonesha ni imani gani waliyonayo...

Baada ya miaka kupita Semiramis alipata ujauzito kwa namna ambayo hadi leo haijulikani lakini yeye akasema kwamba alikuwa amekwenda kumtembelea Nimrod mawinguni na akampatia ujauzito kwa njia ya ajabu hivyo hata atakachokizaa kitakuwa ni kitakatifu.Baada ya muda alimzaa mwana aliyejulikana kama Tamuz....

Tamuz,kama alivyokuwa "baba yake" naye alikuwa muwindaji mahiri sana lakini alikuja kuuawa na nguruwe pori siku ya ijumaa na waumini wa dini ile wakaamua kila ikifika ijumaa hiyo kwenye mwaka walikuwa hawali nyama kabisa kuenzi kifo cha Tamuz.Tamuz alichukuliwa kama |mwana wa mungu" [son of god] kwasababu ya maelezo ya mama yake ambaye alisema kuwa alikwenda mawinguni na kupewa ujauzito na Nimrod hivyo naye wakawa wanamuabudu...

Semiramis alikuja kufa na waumini wake waliamini naye kama ilivyokuwa Nimrod alikuwa ameenda kuishi na mumewe mawinguni na kuanzia hapo alama yake ikawa ni mwezi,mwezi ukawa kama mke na jua likawa kama mume kwakuwa lilikuwa linawakilisha watu hao muhimu mawili katika imani ya Babeli na ndipo ilipozaliwa ibada ya kuabudu vitu hivyo na kuviweka kwenye majumba ya ibada.....

Walitengeneza utatu wao ambao ulikuwa ni wa Nimrod,Semiramis na Tamuz,semiramis akajulikana kama malkia wa mbingu [queen of heaven]

Baadaye ilipoanguka mamlaka ya Babeli imani hiyo ilisambaa duniani kote na watu hao watatu walikuwa wakiabudiwa kwa majina tofauti tofauti.Mfano kule Misri waliitwa Isis [Semiramis] Osiris [Nimrod] Horus [Tamuz]....

Ni hayo kwa ufupi sana mkuu...
Mkuu Wangu Eiyer naomba kuuliza tena usinichoke,ni huyu Pindar na yule black Pope nani zaidi?...pia huyu Pindar anaonekana kwa macho?..na hiyo Atlantic mpya wanaijenga duniani hapa hapa tunapoishi?
 
Mkuu Wangu Eiyer naomba kuuliza tena usinichoke,ni huyu Pindar na yule black Pope nani zaidi?...pia huyu Pindar anaonekana kwa macho?..na hiyo Atlantic mpya wanaijenga duniani hapa hapa tunapoishi?
Vatican ni taasisi ya kidini iliyoko chini ya Illuminati kwenye mwamvuli wa Freemason ambapo wanahakikisha inakuwa kama watakavyo wao,hili liko hivyo kwa dini zingine zote unazozijua wewe na madhehebu yote unayoyajua wewe hivyo Pindar ndiyo mkuu wao wote....

Pindar ni binadamu mwenye DNA ya reptilian ambaye anaonekana kama binadamu wa kawaida tu na anaishi kama wengine hivyo anaonekana kabisa lakini kumjua ndiyo mziki wenyewe...

Unaweza kukutana nayebarabarani ukamuona kama binadamu wa kawaida tu lakini huwezi kujua kuwa huyo ndiye Pindar....

Atlantis mpya itakuwepo hapa hapa duniani kama ilivyokuwepo ile ya kwanza.Hii ni mission ambayo ni LAZIMA ikamilike mkuu.Wapo wanaodhani kuwa ni AMERICA wengine wanadhani ni EU lakini America ndiyo inayoonekana ku match kwa haraka haraka lakini hakuna ukweli kwenye hili lakini kitu ambacho ninakijua ni kwamba wanatengeneza hii kitu hapa hapa duniani.....
 
Vatican ni taasisi ya kidini iliyoko chini ya Illuminati kwenye mwamvuli wa Freemason ambapo wanahakikisha inakuwa kama watakavyo wao,hili liko hivyo kwa dini zingine zote unazozijua wewe na madhehebu yote unayoyajua wewe hivyo Pindar ndiyo mkuu wao wote....

Pindar ni binadamu mwenye DNA ya reptilian ambaye anaonekana kama binadamu wa kawaida tu na anaishi kama wengine hivyo anaonekana kabisa lakini kumjua ndiyo mziki wenyewe...

Unaweza kukutana nayebarabarani ukamuona kama binadamu wa kawaida tu lakini huwezi kujua kuwa huyo ndiye Pindar....

Atlantis mpya itakuwepo hapa hapa duniani kama ilivyokuwepo ile ya kwanza.Hii ni mission ambayo ni LAZIMA ikamilike mkuu.Wapo wanaodhani kuwa ni AMERICA wengine wanadhani ni EU lakini America ndiyo inayoonekana ku match kwa haraka haraka lakini hakuna ukweli kwenye hili lakini kitu ambacho ninakijua ni kwamba wanatengeneza hii kitu hapa hapa duniani.....
Asee huyu Pindar huyu kumbe yuko hapa duniani? Mmmh huko anakoishi huko...naogopa hapo umetaja Vatican
 
Mara nyingi ukichimba sana unakuta unakufuru hata kile unachokiamini na hii ni kwa sababu unasoma hadi unafika sehemu hupati majibu yakinifu ya kutosha kueleza uhalisia. Propagamda juu ya matukio, uandishi wa vitabu mbalimbali vinavyoeleza uwepo wa Mungu, historia nzima ya waliyoviandika vitabu na namna bora fikirifu ya uandishi, uwepo wa makundi mbalimbali ya siri yanayoongoza dunia, dhana ya mwisho wa dunia na mambo mengi yanayoendana na hayo. Yanakupa wakati mgumu kuamini though biblia ambayo nayo iko katika mlolongo huo huo inakwambia imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana. Hapa ni kuendelea tu na unachokiamini.
 
Asee huyu Pindar huyu kumbe yuko hapa duniani? Mmmh huko anakoishi huko...naogopa hapo umetaja Vatican
Usiogope mkuu huo ndiyo ukweli wenyewe....

Ngoja nikuoneshe kitu hapa...

Tazama hizi picha...

vatican obelisk.jpeg
washingot obelisk.jpeg

St.Peter's square Washington D.C

msjid al huram obelisk.jpeg

Masjid al Huram

Halafu angalia hizi picha tena hapa chini...

vatican oval.jpeg
white house dome.jpeg

S.t. Peter's,Vatican White House,Washington DC,USA

masjid al aqsa.jpeg

Masjid al Aqsa

Mkuu,unadhani hayo yote yapo au yanafanana bahati mbaya? Hawa watu wana namna yao ya kujenga majengo ili yaonekane yanawakilisha kitu kimoja.Ikifikaga hapa ndipo watu wanaamua tu kuyakana haya mambo kwasababu yamegusa imani zao lakini hakuna aliyepona....

Hakuna haja ya kukana bali upende ukweli hata kama unakuumiza kwa kiwango gani....
 
Back
Top Bottom