Gharama za kumuuguza Mzee zinaongezeka. Sisi tumeshachoka kwa kweli. Bora tu achukuliwe

Gharama za kumuuguza Mzee zinaongezeka. Sisi tumeshachoka kwa kweli. Bora tu achukuliwe

Kibinadamu sio rahisi mkuu, haya mambo unaweza kumlaumu lakini likiwa kwako ndio utaelewa anachoongea.

Hawa ni wazee wetu, tunawapenda sana, tunawahudumia kwa dhati ya mioyo yetu na uwezo wetu, lakini kuna sehemu ubinadamu unachukua nafasi yake, madhaifu yetu yanadhihirika pale unapoona kazi unayoifanya haina faida(mzee haponi na rasilimali zinaisha). Achana na kuuguza, ni kazi kuliko kazi ila tummies nguvu, tusimlaani kwa sababu ndio jukumu lake kwa sasa.
Ayubu Alirudishiwa Kila Mali mara Mia.

Hudumieni huyo Mzee.
 
Kama unewahi kuuguza wala huwezi kushangaa maneno ya huyu jamaa, unajua kuna ile kumpeleka mtu hospitali, anapata vipimo, anaganyiwa procedure zote, analazwa a few days na kutoka.

Njoo scenario nyinhine, amelala tu, ni vipimo tu, majibu hayaeleweki, Doctor anatoa kipimo kimoja tu ndugu mnaambiwa hiki ni 1,200,000 mchange kama ndugu, keshokutwa kuna kipimo kingine, costs za hospitali zinaongezeka, baada ya mwezi mnapewa gharama mnashika kichwa, ukute sasa familia ndio hizi za kwetu...aaagr.

Tumtie moyo, tusimlaani hata kidogo. Anayeumwa na anayeuguza wote wanahitaji kutiwa moyo.
 
Hoja hupingwa na hoja lete aya inayopinga aliyoyatoa huyo member ikiwa wewe unaijua dini kuliko yeye.

Mtu yeyote anweza kuwa alhaji akishaenda ku hiji makka ,mtu yeyote anaweza pia kuwa mufti maana ni nafasi ya uteuzi wa kiserikali na haizingatii elimu ya dini .

So usitumie hayo kama chaka la kujifichia pinga hoja kwa hoja
Unatumia IDs nyingi. ila nimeepuka tu mjadala wa kidini hapa maana kuna mambo sisi wenye hekma tunayaacha hatujazi watu ambao si sehemu yao hapo. hakuna kitu ambacho huwa najaribu kwanza kuepuka kama kuanza mchambulia mtu dini hasa ya uislamu. naifahamu sijakariri. naifahamu kwa ukaribu sana...sisi ni baadhi ya watu ambao marhamu sheikh yahya alikuwa anakuja mpaka nyumbani kukaa kuongea na mzee habari za dini ya kiislamu. nami nimesoma tena kwa kusoma Mombasa na Lamu... ila mwishowe nimebaki na akili zangu timamu.
 
Mtoa mada huyo ni baba yako au kuna taarifa uliwah kupata kuwa wewe sio mwanaye au hayo ni mawazo ya mkeo....Kumbuka na wewe ni mzazi na <b> hujui utaishia wapi</b>
 
Kuna kipindi pia aliumwaaa.... tukafikia hatua tukasema bora tu arudishe number maana sasa inakuwa changamoto kwetu. Akaja akapona. Shida ikawa pale pale. Hakuna afadhali akiwa mzima shida akiugua shida. Ni msumbufu sana.

Sasa this time anaumwa tena. mwezi wa 3 huu amelala tumehamisha hosp zote. Tunagharamia ukimwangalia age yake nayo imeenda sana. 90 plus. Anataka aendelee kuishi kufanya nini hapa duniani? Sasa tunatumia pesa ambazo zingesaidia wajukuu wake kumtibu mgonjwa mbaye kwa kweli ameshakula chumvi ya kutosha hapa duniani. Mwisho wa siku tunamuona tu kama chuma ulete. Maana kila pesa zetu zinaenda kwenye matibabu yake. Meno yake yameshatoka, anaishi kwa shida. Anaanikwa tu juani kama mjusi ila bado anataka aendelee kuishi. Unajiuliza aishi kufanya nini hapa duniani? Mbona alishamaliza kila kitu?

Sasa inafikia kipindi tunasema bora tu akapumzike nasi tupumzike kidogo maana atatufilisi kwa kweli. Mimi nimeshauza gari moja, nimechukua mkopo, nimekuwa sasa nina madeni ile mbaya. Kwa mabro wengine nao.. ishakuwa shida. Maana tulishampeleka mpaka India kipindi fulani. Wakatwambia kwa huu umri asifanyiwe hayo matibabu maana kinga zake nazo zimekosa nguvu. So alilazwa tu akipewa madawa miezi mitatu. Gharama kubwa ilikuja kwetu. Akarudi amekuwa tia maji tia maji kama gari la mkaa trip moja shamba nyingine gereji.

Ila bado mbishi sana, bado anataka atibiwe na kupelekwa hosp za gharama, sasa mzee si atatuacha watoto wake tumefilisika halafu ndo afe? Hapo tutakuwa tumefanya nini? Nahitaji ushauri wenu kwa kweli hili jambo limenifika hatua nimechoka sana. Sipendi unafiki... hii hali ni ngumu sana maana sasa hata ukiona simu toka kwa ndugu unashindwa kupokea maana huchelewi kuambiwa sasa tuchangie kila mtu atoe 700,000 kuna vipimo na matibabu flani tena yanatakiwa.
Pole sana kwa kuuguza ila unapouguza usitazame kile utoacho kama unacho toa kama huna basi usimsimange mgonjwa bali muombe Mungu akusaidie pale unapokuwa na uzito akufanyie wepesi,Ila heshima ya wazazi wetu inatakiwa iwepo wangali wapo hai ama wametangulia mbele ya haki,
 
Ayubu Alirudishiwa Kila Mali mara Mia.

Hudumieni huyo Mzee.
Hizo ni habari za Ayubu, njoo kwenye uhalisia wa dunia ya leo utaniambia, tuwaombee wazee wetu wawe na maisha mazuri na mwisho wao uwe mzuri. Ikiwezekana kuwe na bima ya afya ya wazee ili kupunguza machungu ya kuuguza na kumaliza rasilimali zote za familia.

Kuna ndugu yangu wa kule Kijichi, mzee alilazwa Agha Khan just three weeks kwa shida ya figo, hapo kabla walishatoa mapesa kama yote, by the time anafariki deni lilikuwa 40m.
 
Biblia imeandika mwisho wa kuishi ni miaka 75 sasa huko kwingine anatafuta nini, mkuu kwani hakuna daktari umpe dili?
 
Mimi mpaka hapo sijaona ustaarabu wako pia. Mimi nimeongea uhalisia ulivyo. Kila mtu ni mzee na marehemu mtarajiwa. So hi haitoi kibali cha mtu kuwa mnafiki na mpuuzi. Kuna haja gani kutumia chakula cha wazima kumpa mtu ambaye hatoweza kuwa mzima? Wafe wote? Miaka 90 plus unadhani ni michache? Na hali yake si nzuri. Unadhani kuna mtu ataishi milele?

Wengine kwenye familia zao hawana Wazee hata WA miaka 80 hivyo hawawezi kuelewa unazungumzia Jambo gani.
 
Miaka ya nyuma kidogo early 2003 brother'angu alikuwa na frame ya biashara mitaa ya Kariakoo kwenye jengo la hawa waarabu wapemba wenyewe wanajiita Wayemen so mimi nilikuwa naenda kushinda pale kusaidia saidia kazi,huyu mzee alikuwa na mdogo wake alikuwa anasumbuliwa sana na nyonga na pressure.

Kuna siku huyu mdogo maradhi yake yalimng’ang‘ania akalazwa Muhimbili ndugu wakachoka wakamrudisha home wasubiri afe sasa ipo siku hali ilibadilika kwa macho ya kibinadamu wakaona huyu kesho hafiki,ilikuwa asubuhi huyu kaka mtu tukawa tumekaa nae nje kwenye bench tunakunywa kahawa akawa anawataarifu kwa simu ndugu zao walioko Zanzibar kwamba wajiandae muda wowote watakuwa na safari ya kuvuka bara kuja kuzika,siku zikaenda mara tukaanza kumuona Sharifu anatoka nje kuota jua,mara akarudi kuishi kwake na akawa anaendelea na kazi zake kama kawaida(alikuja kuugulia kwa kaka yake kwa sababu miezi saba iliyokuwa imepita nyuma alimzika mkewe).

Sasa siku moja asubuhi kufika pale eneo tukakuta turubai tukasema Sharifu atakuwa ameondoka,mara tunamuona Sharifu na ndugu zao wengine wanaratibu msiba kuuliza wanasema mzee Omar ambaye alikuwa mzima zaidi ya mzima amefariki ghafla na huyu Sharifu tulikuja kumzika miaka miwili mbele,binadamu hakuna mwenye haki ya kujadili uzima au kifo cha mwenzake as long as yeye mwenyewe hayuko guaranteed na kile kitamjia dk 30 zinazokuja mbele yake.
 
Kuna kipindi pia aliumwaaa.... tukafikia hatua tukasema bora tu arudishe number maana sasa inakuwa changamoto kwetu. Akaja akapona. Shida ikawa pale pale. Hakuna afadhali akiwa mzima shida akiugua shida. Ni msumbufu sana.

Sasa this time anaumwa tena. mwezi wa 3 huu amelala tumehamisha hosp zote. Tunagharamia ukimwangalia age yake nayo imeenda sana. 90 plus. Anataka aendelee kuishi kufanya nini hapa duniani? Sasa tunatumia pesa ambazo zingesaidia wajukuu wake kumtibu mgonjwa mbaye kwa kweli ameshakula chumvi ya kutosha hapa duniani. Mwisho wa siku tunamuona tu kama chuma ulete. Maana kila pesa zetu zinaenda kwenye matibabu yake. Meno yake yameshatoka, anaishi kwa shida. Anaanikwa tu juani kama mjusi ila bado anataka aendelee kuishi. Unajiuliza aishi kufanya nini hapa duniani? Mbona alishamaliza kila kitu?

Sasa inafikia kipindi tunasema bora tu akapumzike nasi tupumzike kidogo maana atatufilisi kwa kweli. Mimi nimeshauza gari moja, nimechukua mkopo, nimekuwa sasa nina madeni ile mbaya. Kwa mabro wengine nao.. ishakuwa shida. Maana tulishampeleka mpaka India kipindi fulani. Wakatwambia kwa huu umri asifanyiwe hayo matibabu maana kinga zake nazo zimekosa nguvu. So alilazwa tu akipewa madawa miezi mitatu. Gharama kubwa ilikuja kwetu. Akarudi amekuwa tia maji tia maji kama gari la mkaa trip moja shamba nyingine gereji.

Ila bado mbishi sana, bado anataka atibiwe na kupelekwa hosp za gharama, sasa mzee si atatuacha watoto wake tumefilisika halafu ndo afe? Hapo tutakuwa tumefanya nini? Nahitaji ushauri wenu kwa kweli hili jambo limenifika hatua nimechoka sana. Sipendi unafiki... hii hali ni ngumu sana maana sasa hata ukiona simu toka kwa ndugu unashindwa kupokea maana huchelewi kuambiwa sasa tuchangie kila mtu atoe 700,000 kuna vipimo na matibabu flani tena yanatakiwa.
Sasa unataka tukushauri ummalizie afe au???
Mzazi naye angesema amechoka heka heka zako asikuhangaikie hadi umri wa kujipambania ungepata hata hyo laki 7 unayochangia??
Niliuguza mama yangu hadi kufikia kuacha kazi pale alipozidiwa lakini sikuwahi kufikia kuwaza haya na kuyaleta kwa watu hadharani. Nia yangu nilijua siku moja ataamka ila hakuamka hadi nilipomzika 😭.
Usichojua ni kwamba Mungu Ana riziki ya kila mtu na kama unapata cha kumhudumia basi ujue hiyo ni riziki yake Mungu ameipitishia kwako.
Kuna baraka nyingi sana katika kumhudumia mtu asiyejiweza awe mzazi au mtu baki. Ila baraka ni nyingi zaidi kwa mzazi. Ninashuhudia kwa macho yangu. Baada ya msiba nilijua nitataabika sana ila kila ninapoona giza mwanga unakuja. Na Kila ninachokifanya kinafanikiwa mnoo ...radhi ya mzazi ni kitu cha kukiombea sana na kukifanyia jitihada ukipate kabla mzazi hajaondoka duniani.
 
Mimi mpaka hapo sijaona ustaarabu wako pia. Mimi nimeongea uhalisia ulivyo. Kila mtu ni mzee na marehemu mtarajiwa. So hi haitoi kibali cha mtu kuwa mnafiki na mpuuzi. Kuna haja gani kutumia chakula cha wazima kumpa mtu ambaye hatoweza kuwa mzima? Wafe wote? Miaka 90 plus unadhani ni michache? Na hali yake si nzuri. Unadhani kuna mtu ataishi milele?
Kwa hiyo unatakaje sasa,
Tumwambie Baba ako ajitoe Roho, tukupe mbinu ya kummaliza Baba ako au unataka nini hasaaa hebu funguka ewe Chizi Maarifa.
 
Back
Top Bottom