Godbless Lema ukimbizi: Kaingia jela ya kufikirika

Godbless Lema ukimbizi: Kaingia jela ya kufikirika

Mawazo ya kijinga eti Mchaga,mbona tunayo majinga majinga mengi tu hapa mjini ?
Hayo majinga majinga mko nayo Unguja au huko chamani mnako yajenga?

kwani Lema amependa, yeye kuwa mkimbizi?
Au nanyi mnapenda, na haya ni mashauzi?
achaneni na u nunda, tukae tuchape kazi,
Lissu Lema wamekwenda, wengine wasijekwenda.
 
MATAGA ni Mapsychopath kwa kweli,
Mmemkosa Lema kumuua, mnakosa na raha kabisa.
Lema akili kubwa Mungu amemponya kawapiga chenga ya mwili.
Mmebaki karagwe sasa mnataka kula damu ya baba Askofu. Mlaaniwe MaCCM wote.
 
Nafikili tusimbeze mh lemma,wenda nyuma yake yapo makubwa ambayo hatujui,safari yake TOKA tz to kenya then canada,wenda anayo mazito anayoyajua
Namhurumia sana Godbless Lema.
Kaingia jela ya kufikirika, jela ambayo ni yeye mwenyewe atajua ni kifungo cha miaka mingapi na atatokaje kwa msamaha wake mwenyewe.

Mbaya zaidi familia nzima imemsindikiza jela hiyo ya kufikirika.

Lema ata enjoy miezi michache ya kwanza huko Canada, pamoja na familia.
Baada ya hapo ndipo ataelewa uzuri na utamu wa Tanzania, maji ya kunywa bure, hewa bure, shule karo za watoto karibu na bure, chakula unarudi kutoka Moshi na mikungu miwili ya ndizi bure!
Mbge ndo usiseme!

Tuliokaa nje muda kidogo tunaelewa jinsi matatizo tuliyo nayo, yalivyotukomaza na kuishi nayo kama ndugu.

Nampa pole Lema maana alisema wanataka kumuua.
Bado angeweza kubaki na kutatua hilo fumbo na shinikizo.

Tanzania ni nzuri!
 
Future nzuri ? Mbona watoto wa Kambona hawajapata future nzuri ?
Kwa hiyo unataka kusema watoto wa lema walikua wanasoma kayumba ambapo elimu ni bure? Kwa ninavyojua mimi elimu ya canada public schools are free, na public schools zina ubora kuliko hata feza ambayo ndio tunaiona bora hapa bongo

Watoti wake watapata elimu bora, exposure na watakua future nzuro, hayo mengine mataga muendelee kutunga tu
 
Kila nchi unao matajiri na maskini, kama unafikiria kila mtu huko Ulaya au Canada ni tajiri wewe bado sana tu. Pole sana.
Mkuu 'Jidu', mbona unaturudisha tulikokwishatoka wewe na mimi siku nyingi humu JF. Tulishaelezana kwa uwazi kabisa kila mmoja wetu anakosimamia, halafu leo unanigeuza tena na kuniita "mpenzi wa chama na mlengo fulani"?

Ngoja nirudie kwa kifupi ili kukukumbusha: ushabiki wangu ni Tanzania pekee. Niliwahi kuwa shabiki wa CCM kilipokuwa chama cha wakulima na wafanya kazi na sio kile kilichowahi kuwepo kikiwa "Chama cha Huyu Mwenzetu" na wala siyo hiki "Chama Kilichobinafsishwa kwa mtu mmoja." Mbali na hivyo, sijawahi kuwa shabiki wa chama chochote kati ya hivi vipya. Unapoona tunafanya utetezi juu yao, sio kwa sababu ni 'wapenzi' au 'wanazi'; bali tunasikitishwa na maonezi wanayofanyiwa wao wakiwa ni waTanzania wenzetu. Hili ndilo linalotuumiza.

Wewe ni msahaulifu kiasi hiki kweli, kwamba unasahau yote na leo unanipakazia, ati "wew ni mpenzi wa chama na mlengo fulani"? na wakati huo huo unasahau uliyoungama mbele yangu wakati ule; na huku leo unageuka jiwe la chumvi, eti "nashabikia siasa kwa unazi tu", hata sijui huko ndio kufanya nini?

Michango yako humu JF inajieleza yenyewe; na ya kwangu inajulikana bila kificho; halafu leo unageuka na kunipaka matope?

Hayo ya ulaya, sio peke yako umeishi huko, kama kweli umewahi kuishi huko. Kuishi ulaya sio hoja, unaweza ukaishi huko na ukawa 'miserable' kama unaamua kujiweka jela mwenyewe. Kama hayo ndiyo maisha uliyoishi, usidhani kila mtu anayekwenda huko anayaishi kama wewe ulivyoyaishi.
Huko kutokuwa na 'noti' sio huko tu, hata hapa kama huna noti maisha yatakufanya uonekane kama "takataka" kama ulivyoandika mwenyewe. Kuwa "takataka" kunatokea mahali popote, iwe ulaya au hapahapa. Na mbaya zaidi ni kuwa "takataka" huku ukiwa mateka!

"Paradiso" ya kuwekwa 'mateka'. Hiyo paradiso yako ni ya ajabu. Tanzania ingekuwa 'paradiso' sana, licha ya umaskini unaowakabili wananchi wetu, kama kusingekuwepo na haya ya kufanywa mateka ndani ya nchi yetu wenyewe.
 
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16] Jitahidi uache bangi kabla haijaingia kwenye ubongo
[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]huo ndio ukweli mkuu.
Mchaga hazuiliki kufikia ndoto zake.
Ukimwekea vikwazo unampa akili zaidi.
Lema atarudi akiwa mupya kabisa.
Angekuwa mmakonde, mzaramo au mgogo ningemhurumia but mchaga ni Mwisraeli bro
 
Namhurumia sana Godbless Lema.
Kaingia jela ya kufikirika, jela ambayo ni yeye mwenyewe atajua ni kifungo cha miaka mingapi na atatokaje kwa msamaha wake mwenyewe.

Mbaya zaidi familia nzima imemsindikiza jela hiyo ya kufikirika.

Lema ata enjoy miezi michache ya kwanza huko Canada, pamoja na familia.
Baada ya hapo ndipo ataelewa uzuri na utamu wa Tanzania, maji ya kunywa bure, hewa bure, shule karo za watoto karibu na bure, chakula unarudi kutoka Moshi na mikungu miwili ya ndizi bure!
Mbge ndo usiseme!

Tuliokaa nje muda kidogo tunaelewa jinsi matatizo tuliyo nayo, yalivyotukomaza na kuishi nayo kama ndugu.

Nampa pole Lema maana alisema wanataka kumuua.
Bado angeweza kubaki na kutatua hilo fumbo na shinikizo.

Tanzania ni nzuri!
Tanzania nzuri kwa watawala tu ndugu
 
On the basis of matibabu ya muda mrefu na some EU countries kama una kiasi fulani cha pesa, unaweza kuomba residence permit or golden visa.

Process ya Belgium hii hapa

Tundu Lissu hahitaji matibabu ya muda mrefu ya kuishi Belgium. Matibabu ya kitu gani yanayomlazimisha kuishi Belgium?


Vilevile Tundu Lissu hana kiasi cha pesa cha kumfanya epewe residence. Mtu anayepewa residence on the basis of kiasi cha pesa ni kwa misingi kuwa atawekeza na kutengeneza ajira. Tundu Lissu hana pesa hizo.
 
MATAGA ni Mapsychopath kwa kweli,
Mmemkosa Lema kumuua, mnakosa na raha kabisa.
Lema akili kubwa Mungu amemponya kawapiga chenga ya mwili.
Mmebaki karagwe sasa mnataka kula damu ya baba Askofu. Mlaaniwe MaCCM wote.
Mkuu hakuna nchi yenye sera za kuua raia wake.
Wakimalizika wataua nani?
Lema angejiwekea utaratibu kuwa siasa si uadui.
Mbona Msigwa ana undugu hata na Rais?
Wanaoua ni wahalifu kama wahalifu wengine, wakipatikana Pilato anawahusu.
 
Hayo majinga majinga mko nayo Unguja au huko chamani mnako yajenga?

kwani Lema amependa, yeye kuwa mkimbizi?
Au nanyi mnapenda, na haya ni mashauzi?
achaneni na u nunda, tukae tuchape kazi,
Lissu Lema wamekwenda, wengine wasijekwenda.

Ukimbizi ametaka,kavuka boda kwa gari,
Hapakuwa na mashaka,wala hakuna ghururi
Kasubiriwa kuvuka,afanye yake jeuri,
Kayakimbia madeni,Mkimbizi siyo lema
 
Namhurumia sana Godbless Lema.
Kaingia jela ya kufikirika, jela ambayo ni yeye mwenyewe atajua ni kifungo cha miaka mingapi na atatokaje kwa msamaha wake mwenyewe.

Mbaya zaidi familia nzima imemsindikiza jela hiyo ya kufikirika.

Lema ata enjoy miezi michache ya kwanza huko Canada, pamoja na familia.
Baada ya hapo ndipo ataelewa uzuri na utamu wa Tanzania, maji ya kunywa bure, hewa bure, shule karo za watoto karibu na bure, chakula unarudi kutoka Moshi na mikungu miwili ya ndizi bure!
Mbge ndo usiseme!

Tuliokaa nje muda kidogo tunaelewa jinsi matatizo tuliyo nayo, yalivyotukomaza na kuishi nayo kama ndugu.

Nampa pole Lema maana alisema wanataka kumuua.
Bado angeweza kubaki na kutatua hilo fumbo na shinikizo.

Tanzania ni nzuri!
Theory mbovu uliyonayo canada ata enjoy sana sema alivyowasaliti watu wa Arusha kuwa atawakomboa baadae akaondoka vile sijapenda ata kidogo lakini yeye kama yeye anaenda kuishi maisha ya kifalme
 
Namhurumia sana Godbless Lema.
Kaingia jela ya kufikirika, jela ambayo ni yeye mwenyewe atajua ni kifungo cha miaka mingapi na atatokaje kwa msamaha wake mwenyewe.

Mbaya zaidi familia nzima imemsindikiza jela hiyo ya kufikirika.

Lema ata enjoy miezi michache ya kwanza huko Canada, pamoja na familia.
Baada ya hapo ndipo ataelewa uzuri na utamu wa Tanzania, maji ya kunywa bure, hewa bure, shule karo za watoto karibu na bure, chakula unarudi kutoka Moshi na mikungu miwili ya ndizi bure!
Mbge ndo usiseme!

Tuliokaa nje muda kidogo tunaelewa jinsi matatizo tuliyo nayo, yalivyotukomaza na kuishi nayo kama ndugu.

Nampa pole Lema maana alisema wanataka kumuua.
Bado angeweza kubaki na kutatua hilo fumbo na shinikizo.

Tanzania ni nzuri!
Acha uongo. Wataka kusema eti tanzania ni pazuri kuishi kuliko Canada?
 
Tundu Lissu hahitaji matibabu ya muda mrefu ya kuishi Belgium. Matibabu ya kitu gani yanayomlazimisha kuishi Belgium?


Vilevile Tundu Lissu hana kiasi cha pesa cha kumfanya epewe residence. Mtu anayepewa residence on the basis of kiasi cha pesa ni kwa misingi kuwa atawekeza na kutengeneza ajira. Tundu Lissu hana pesa hizo.
So, ina maana unataka kusema Lissu kupewa ukimbizi? Wakati mwenye alishasema ana kibali cha kuishi Ubeligiji?
 
mchaga ..uchaga uchaga uchaga..what is uchaga by the way..who the hell are you in Tz..foolish comment ever..we are not entertaining tribalism here in tz..No one should be regarded as superior than the rest, we are all equal..
Ahsante.
 
Ukimbizi ametaka,kavuka boda kwa gari,
Hapakuwa na mashaka,wala hakuna ghururi
Kasubiriwa kuvuka,afanye yake jeuri,
Kayakimbia madeni,Mkimbizi siyo lema
Je Lema si mkimbizi, wewe msajili wao?
mmezidi ubazazi, mwawakimbiza makwao,
kwani ya nini makazi, si bora ya roho zao?
Yu eni hechi si ara, wajua ni mkimbizi!

(UNHCR = "Yu eni hechi si ara" wanayo orodha ya wakimbizi. Jiridhishe Lema hayumo.)
 
Back
Top Bottom