God's Conscience vs Free Will: Je, Mungu anajua hatima ya wanadamu itakuwaje?

God's Conscience vs Free Will: Je, Mungu anajua hatima ya wanadamu itakuwaje?

Mawazo ambayo hayana uhalisia sioni sababu ya kuyazingatia
Una haki ya kufanya hivyo.

Lakini laiti kama ungeweza ukiwa hivyohivyo mtu mzima na kujiwezesha kufikiri kama huyo mtoto ungetoboa. In fact hakuna njia nyingine zaidi ya hiyo ya kuchukua baadhi ya sifa za mtoto katika kuuelewa uhalisia.
 
Sio mimi bro, historia inaonesha hivyo;

Mungu ni mkubwa na sisi kwa akili zetu tunamuelewa kulingana na uwezo wetu kwa wakati huo. Akili inavyopanuka unamjua Mungu zaidi naamini hivyo. Na ndivyo ilivyo anyways.
Umesema Mungu anabadilika badilika na historia ndio inavyosema

So kumbe tuipuuze biblia kwakua imeandika uongo?

Melach 3:6

“For I the Lord do not change; therefore you, O children of Jacob, are not consumed​


Hebrew 13:8

"Jesus Christ is the same yesterday and today and forever"​

 
Ndiyo, kinadharia chance ipo kiuhalisia haipo wala. Rejea mfano wangu wa mwanajeshi wa kawaida vs yule mwanajeshi mkubwa na mzalendo damu, ambaye hata identity yake amejipiga chapa ya nchi yake ndani kwa ndani
Kwa hiyo huku duniani kuna uovu wa kinadharia?
 
Una haki ya kufanya hivyo.

Lakini laiti kama ungeweza ukiwa hivyohivyo mtu mzima na kujiwezesha kufikiri kama huyo mtoto ungetoboa. In fact hakuna njia nyingine zaidi ya hiyo ya kuchukua baadhi ya sifa za mtoto katika kuuelewa uhalisia.
Hakuna njia ni kwasababu unachokielezea hakipo kihakisia na ndio maana imekuwa ngumu ku avoid contradictions
 
Umesema Mungu anabadilika badilika na historia ndio inavyosema

So kumbe tuipuuze biblia kwakua imeandika uongo?

Melach 3:6

“For I the Lord do not change; therefore you, O children of Jacob, are not consumed​


Hebrew 13:8

"Jesus Christ is the same yesterday and today and forever"​

I agree the Lord do not change It is our understanding of Him that changes. Not Him.

Kwani wapi nilisema Mungu anabadilika?
 
I agree the Lord do not change It is our understanding of Him that changes. Not Him.

Kwani wapi nilisema Mungu anabadilika?
Uliposema kadri unavyozidi kumuamini ndivyo picha yake inavyozidi kubadilika

Kwa hiyo nikufate wewe au biblia?
 
Kwa hiyo huku duniani kuna uovu wa kinadharia?
Basi bro sio lazima nibishe tu.

Mbinguni chance ya kufanya uovu ipo kinadharia na kiuhalisia. Uridhike. Ukiwa mbinguni unaweza kuamua kuwa mwovu na kukataa kuwa mtii ukiamua. But why on eart.... no why on heaven would you do that!? Binafsi nashindwa kuimagine.

Nisije nikawa nakufukuza mbinguni bila kutarajia maana hupendi kufungwa na kukosa uhuru wako wa kufanya 'mema au mabaya'.

Siachi kusisitiza kuwa hadi ukafika mbinguni, jua akili yako na utashi wako umeshajiamulia kuwa wewe ni sehemu ya ufalme wa Mungu na ndivyo ulivyo sasa sijui ni nini kikubadilishe kwa kweli sijui!!
 
Basi bro sio lazima nibishe tu.

Mbinguni chance ya kufanya uovu ipo kinadharia na kiuhalisia. Uridhike. Ukiwa mbinguni unaweza kuamua kuwa mwovu na kukataa kuwa mtii ukiamua. But why on eart.... no why on heaven would you do that!? Binafsi nashindwa kuimagine.

Nisije nikawa nakufukuza mbinguni bila kutarajia maana hupendi kufungwa na kukosa uhuru wako wa kufanya 'mema au mabaya'.

Siachi kusisitiza kuwa hadi ukafika mbinguni, jua akili yako na utashi wako umeshajiamulia kuwa wewe ni sehemu ya ufalme wa Mungu na ndivyo ulivyo sasa sijui ni nini kikubadilishe kwa kweli sijui!!
Mbinguni tutaenda kufanya nini?
 
Uliposema kadri unavyozidi kumuamini ndivyo picha yake inavyozidi kubadilika

Kwa hiyo nikufate wewe au biblia?
Fuata ukweli bro. I only appeal to sense.

Angalia mfano Yesu alivyokuja kuweka sawa mambo ya sheria na mambo ya sabato. Hakusema nifuateni mimi, au yafuateni maandiko. Bali yeye aliweka logic mezani na akawaacha watu wafuate chenye mantiki zaidi. Nimechagua kumuiga kwa kufuata mantiki au sense.

Tena uzuri sasa hivi wote tuna Roho mtakatifu, na Msaidizi aliyeahidiwa pia anatushuhudia kwa hiyo tuna sababu zaidi za kutumia utashi wetu.
 
Kuna kitu kimoja cha ajabu kwa watu wazima, ukiona unaelimika na kufurahia elimu mpya, ujue hata sio mpya kweli. Ni kitu ulikuwa unachontangu mwanzo sema tu kuna jamaa kaamua kukiweka katika maneno.

So unaresonate nacho. Kwa mantiki hiyo naamini unajua na tunakaribisha maoni yako pia[emoji111]
Hahaha mhmh mkuu, maarifa ni muhumi na hatufanani kwenye ubebaji wa taarifa ya maarifa ni hiyo hutokana na uzoefu wa mtu binafsi kupenda kujifunza, unaambiwa hata kama jambo unalijua basi jifanye ndiyo unajifunza kuna vitu vipya pia hutavipata kama ukiona unajua kila kitu, shehe usijinyime kujifunza, elimu haina mipaka wala muda kila siku tunajifunza,

Nitachangia pia yangu usihofu
 
Mungu na wanadamu.
Tuendelee kukosoa ilhali majibu yapo peupe..... Tuangamie coz we gat wrong knowledge na tunahisi tupo sawa.
Ni Kama tunekaa mahali taa imezimwa na hatuoni vilivyotuzunguka ila kadri tunavyozidi kuwasha taa tunazidi kuona vilivyotuzunguka.
 
Basi bro sio lazima nibishe tu.

Mbinguni chance ya kufanya uovu ipo kinadharia na kiuhalisia. Uridhike. Ukiwa mbinguni unaweza kuamua kuwa mwovu na kukataa kuwa mtii ukiamua. But why on eart.... no why on heaven would you do that!? Binafsi nashindwa kuimagine.

Nisije nikawa nakufukuza mbinguni bila kutarajia maana hupendi kufungwa na kukosa uhuru wako wa kufanya 'mema au mabaya'.

Siachi kusisitiza kuwa hadi ukafika mbinguni, jua akili yako na utashi wako umeshajiamulia kuwa wewe ni sehemu ya ufalme wa Mungu na ndivyo ulivyo sasa sijui ni nini kikubadilishe kwa kweli sijui!!
Kwa maana hiyo mbinguni kuna uroboti kwakua umefungwa usiweze kuamua zaid ya kinadharia tu?
 
Fuata ukweli bro. I only appeal to sense.

Angalia mfano Yesu alivyokuja kuweka sawa mambo ya sheria na mambo ya sabato. Hakusema nifuateni mimi, au yafuateni maandiko. Bali yeye aliweka logic mezani na akawaacha watu wafuate chenye mantiki zaidi. Nimechagua kumuiga kwa kufuata mantiki au sense.

Tena uzuri sasa hivi wote tuna Roho mtakatifu, na Msaidizi aliyeahidiwa pia anatushuhudia kwa hiyo tuna sababu zaidi za kutumia utashi wetu.
Hapa unakuwa umeandika nini?

Umeandika kutetea kuwa Mungu habadiriki au umezidi kusisitiza kuwa anabadilika ili nijue biblia imepotosha?
 
Ebhana kuna jibu limepatikana hapa. Jibu zuri sana see nimelipenda:

Ni kwamba mbinguni itakuwa ni kumsifu na kumtukuza Mungu na kumtumikia. Mzungu mmoja akatahayari akauliza je hali ya kusifu Mungu/kitu kilekile siku nzima na siku zote milele haitaboa sasa? Itachosha.

Mwamba mmoja akaleta jibu tamu sana akasemaaa....... kwa mantiki hii;

Kwa kuwa Mungu ni mkubwa sana[infinity], na mwenye sifa zisizomithilika yaani kadri unavyomjua unazidi kufurahia na kujua kuwa hujui zaidi na kutamani kumjua zaidi yeye na sifa zake. Basi itahitaji muda mwingi usio na mwisho[eternity] ili kumjua kikamilifu Mungu asiye na mwisho [infinity]. Kwa hiyo tutaendelea kujifunza kuhusu Mungu, tukiishi uweponi mwake milele na milele na milele. Sifa tutazitoa, tutahimidi na kinamna fulani tutatumika katika ufalme wake.

Mfano unaambiwa kuna wale wazee sijui idadi ni watatu, 24 au kumi na mbili [au 144? sikumbuki!] wanaosujudu mbele zake. Ni kwamba kila siku, kila wakati wanaziona sifa mpya za Mungu wanaona rangi mpya na ndio maana wanaanguka na kusujudu kusema mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu. Jambo hilo haliwaboi maana ni kweli kila mara wanashuhudia sifa kuu mpya za Mungu. Kung fu panda alitumiaga neno ambalo litawafiti sana, wanapata 'Over-exposure to pure awesomeness' each and every moment.
 
Kwa maana hiyo mbinguni kuna uroboti kwakua umefungwa usiweze kuamua zaid ya kinadharia tu?
Hapana kaka hakuna uroboti, ukiwa huko unaweza kuamua kufanya uovu, unaweza kuamua kukaidi na kutokuwa mtii kwa Mungu ukiamua. Ukiweza sijui kinamna gani.

Kila nikiandika hiyo statement sitaacha kuweka msisitizo kuwa pamoja na kuwa unaweza kuamua kwenda kinyume hautakaa uamue hivyo wewe mwenyewe kwa kuwa wewe ni mwema na mtii [yaani muislamu] kwa Mungu. Na tayari unaishi katika utukufu wa Mungu ndani yake, na Mungu anaishi ndani yako sasa hayo mawazo ya kukaidi unayatoa wapi? Ego na pride/kiburi vinaweza kuwa vishawishi kutokea ndani yako lakini nisikatae sana. Ila tambua kuwa mpaka unafika mbinguni hivyo vitu umevimaster ujue. Sijui tu utaanzaje kukaidi ila mfano ukaamua kukaidi utaweza na utakufa nadhani automatically kama wengine waliokufa kabla.
 
Hapa unakuwa umeandika nini?

Umeandika kutetea kuwa Mungu habadiriki au umezidi kusisitiza kuwa anabadilika ili nijue biblia imepotosha?
Elimu inakua na utambuzi ni zaidi ya kujua tu kirahisi; Not simply knowing a fact but comprehending/asimilating it as we grow our understanding. Mungu habadiliki na biblia au msahafu wowote usomwe huku ukiwa na akili na upako pia ili kuelewa. Mimi si muumini wa kufata aya kwa aya au neno kwa neno maana nafahamu uelewa haufanyi kazi hivyo. Naamini maneno katika vitabu vitakatifu [na elimu yoyote ya ukweli] hayapotoshi yaninafundisha. Hatupaswi kukubaliana na kila kaandishi kama kalivyoandikwa tunapaswa kukaelewa mda mwingine hadi kujaribu kuvaa uhusika wa mwandishi na kujiuliza alikuwa anataka kufikisha ujumbe gani. Kuvaa uhusika wa waandikiwa kuona walichopaswa kuelezwa etc etc

Picha ya baba kwa mtoto inaweza kuwa baba ni mkali, mtoto huyohuyo akikua atajua kuwa baba ana upendo.

Picha ya pili ya upendo ni ukweli kabisa kama ambavyo picha ya kwanza ya ukali ilivyo ni ya kweli. Hakuna kinachomuua mwenzake wala hakuna wakati wowote huyu mtoto alikuwa muongo katika 'imani' yake.

Ila chekishia kitu kikubwa hapa ni kwamba; mtoto alipofikia hatua akamuelewa baba yake kuwa ni mwenye upendo aliielewa kwa uzuri zaidi hata ile picha/concept yake ya baba yake ni mkali mwenye kuadhibu aliyokuwa nayo mwanzo. Vyote ni ujuzi unaojenga ukweli mmoja mkuu kwamba hata kama alichukuliwa kama mkali alikuwa ni upendo all the way tangu mwanzo sema tu tulikuwa bado hatujakua kiakili na kung'amua vizuri tu.

Mkusanyiko wa vitabu vya bibliani ni maktaba ya vitabu vinavyopishana kwa maelfu ya miaka. Akili ya kawaida inaniambia lazima nitashuhudia mageuko/evolution ya elimu kuhusu Mungu. Na ndicho tunachokiona agano la kale hadi injili hadi leo tunazidi kumjua Mungu vizuri zaidi na hatutaacha kumjifunza hadi mwisho...... sorry! hakuna mwisho ni MILELE. Tena ni milele na milele na milele.
 
Hapana kaka hakuna uroboti, ukiwa huko unaweza kuamua kufanya uovu, unaweza kuamua kukaidi na kutokuwa mtii kwa Mungu ukiamua. Ukiweza sijui kinamna gani.

Kila nikiandika hiyo statement sitaacha kuweka msisitizo kuwa pamoja na kuwa unaweza kuamua kwenda kinyume hautakaa uamue hivyo wewe mwenyewe kwa kuwa wewe ni mwema na mtii [yaani muislamu] kwa Mungu. Na tayari unaishi katika utukufu wa Mungu ndani yake, na Mungu anaishi ndani yako sasa hayo mawazo ya kukaidi unayatoa wapi? Ego na pride/kiburi vinaweza kuwa vishawishi kutokea ndani yako lakini nisikatae sana. Ila tambua kuwa mpaka unafika mbinguni hivyo vitu umevimaster ujue. Sijui tu utaanzaje kukaidi ila mfano ukaamua kukaidi utaweza na utakufa nadhani automatically kama wengine waliokufa kabla.
Nikiwa huko naweza kuua mtu na malaika pia endapo nitajisikia?
 
Elimu inakua na utambuzi ni zaidi ya kujua tu kirahisi; Not simply knowing a fact but comprehending/asimilating it as we grow our understanding. Mungu habadiliki na biblia au msahafu wowote usomwe huku ukiwa na akili na upako pia ili kuelewa. Mimi muumini wa kufata aya kwa aya au neno kwa neno maana nafahamu uelewa haufanyi kazi hivyo. Naamini maneno katika vitabu vitakatifu [na elimu yoyote ya ukweli] hayapotoshi yaninafundisha. Hatupaswi kukubaliana na kila kaandishi kama kalivyoandikwa tunapaswa kukaelewa mda mwingine hadi kujaribu kuvaa uhusika wa mwandishi na kujiuliza alikuwa anataka kufikisha ujumbe gani. Kuvaa uhusika wa waandikiwa kuona walichopaswa kuelezwa etc etc

Picha ya baba kwa mtoto inaweza kuwa baba ni mkali, mtoto huyohuyo akikua atajua kuwa baba ana upendo.

Picha ya pili ya upendo ni ukweli kabisa kama ambavyo picha ya kwanza ya ukali ilivyo ni ya kweli. Hakuna kinachomuua mwenzake wala hakuna wakati wowote huyu mtoto alikuwa muongo katika 'imani' yake.

Ila chekishia kitu kikubwa hapa ni kwamba; mtoto alipofikia hatua akamuelewa baba yake kuwa ni mwenye upendo aliielewa kwa uzuri zaidi hata ile picha/concept yake ya baba yake ni mkali mwenye kuadhibu aliyokuwa nayo mwanzo. Vyote ni ujuzi unaojenga ukweli mmoja mkuu kwamba hata kama alichukuliwa kama mkali alikuwa ni upendo all the way tangu mwanzo sema tu tulikuwa bado hatujakua kiakili na kung'amua vizuri tu.

Mkusanyiko wa vitabu vya bibliani ni maktaba ya vitabu vinavyopishana kwa maelfu ya miaka. Akili ya kawaida inaniambia lazima nitashuhudia mageuko/evolution ya elimu kuhusu Mungu. Na ndicho tunachokiona agano la kale hadi injili hadi leo tunazidi kumjua Mungu vizuri zaidi na hatutaacha kumjifunza hadi mwisho...... sorry! hakuna mwisho ni MILELE. Tena ni milele na milele na milele.
Kwa hiyo unafuta kauli yako ya kwanza kuwa Mungu anabadilika?
 
Back
Top Bottom