God's Conscience vs Free Will: Je, Mungu anajua hatima ya wanadamu itakuwaje?

God's Conscience vs Free Will: Je, Mungu anajua hatima ya wanadamu itakuwaje?

Hello y’all..

NB
: Naomba moderator mada hii msiihamishie jukwaa la dini maana huko itakosa wachangiaji na lengo langu la kutaka kujuzwa jambo hili halitatimia and that will leave me frustrated and bums me out, Natuamaini mtatii takwa langu hili. Ahsanteni.

Binafsi kiimani ni muumini wa kanisa Katoliki kwa kuzaliwa na kubatizwa, pia ninaamini na kuisadiki kanuni ya imani yangu katoliki isemayo “Nasadiki kwa Mungu baba mwenyezi muumba mbingu na dunia na kwa Yesu Kristu Bwana wetuu….” Self-schemas: katika sayansi ya utambuzi (Cognitive science) inasema kwamba schemas huelezea muundo wa mawazo au tabia ambazo hupanga aina za taarifa na uhusiano kati ya taarifa hizo. Lakini inaelezwa pia kwamba ni muundo wa akili kupokea taarifa na kuzichambua..taarifa hizo ndio huleta maarifa ya kumuwezesha mtu kutambua self-concept.

Self-Concept ni i hatua ambapo mtu anaweza kufafanua kua yeye ni nani hasa au ni hali ambapo mtu anakua ameweza kujitambua . Self-Concept imeundwa na Self-Schemas, past self (Kutambua wapi ulipotoka) present self (Kutambua wapi ulipo) na Future self (Kutambua wapi utakapokua baada ya hapa ulipo). Toka nilipoanza kutambua Self Concept yangu Nimekua na swali ambalo kwakweli pamoja na kuisadiki imani yangu hii na kupokea ya Sakrament takatifu ya Communion swali hilo limekua mwiba mchungu na kikwazo kikubwa katika imani yangu hii na Mungu kwa ujumla.

Toka nilipoanza kujitambua nimejaribu kuwashirikisha watu wenye uelewa jambo hili ila bado sijapewa majibu thabiti….natumaini hapa JF nitapewa maelekezo vyema , mnivumilie kama maelezo yatakua marefu maana hua siwezi kuelezea kwa ufupi but it worth your time.

The One above all, In-Betweener and The One bellow all.

Monotheism
ni imani ya kua kuna Mungu mmoja pekee ambae aliumba ulimwengu na vyote vilivyomo. Watu wanao amini katika imani hii ni wafuasi wa dini zilizotokana na Ibrahim ambae anachukuliwa kama baba wa imani ambazo ni Judaism, Ukristo,uislam, mandaeism ,Rastafarian na Bahai. Mungu wa imani hii ndio huyu tunayemfahamu mimi na wewe ambae ana sifa kuu tatu ambazo ni yupo kila mahali, anajua kila kitu, na anaweza kila kitu. Omni ni neno la kilatini lenye maana ya yote au kila kitu na Sciens ni neno la kilatini likimaanisha kujua(conscious)……. Moja kati ya sifa kuu tatu za Mungu nilizotaja hapo juu ni Omniscience ikimaanisha kwamba Mungu anajua yote yaliyopita,yaliyopo na yajayo.

The Great Chain of Being ni mchoro au nadharia ambayo inaonyesha kwamba maisha ya mwanadamu yapo kwenye ngazi /mtiririko Fulani ambapo juu kabisa anaanza Mungu,wanafuta malaika, kisha mwandamu, wanafuta wanyama,mimea halafu chini kabisa yupo shetani. Mungu ni the one above all, mwanadamu ni aliyekati /in-betweener na shetani ni the one below all. Unajua mwanadamu ni kiumbe kamili na mwenye hadhi kubwa kuliko viumbe wote walioumbwa na mungu kuzidi hata malaika ndio maana kuna malaika wanafanya kazi kwa wanadamu ya kutulind, Moja kati ya utajiri na kitu kikubwa alichonacho mwanadamu hakuna kiumbe kingine anacho ni uwezo wa kuchagua na kuamua Kuishi vile atakavyo yeye yaani Free Will….Katika Great chain of being mwanadamu amewekwa katikati (In-Betweener) maana yeye ameumbwa na roho isiyokufa (immortal) na mwili ambao unaokufa (mortal) hivyo inamuwezesha yeye kuishi duniani au mbinguni . Mwanadamu kwakua ana roho yenye uungu na mwili wa kibanaadamu amepewa chaguzi la yeye kuweza kuishi Uungu kwa kutenda mema maishani mwake au ushetani kwa kutenda ubaya maishani mwake. Kwakua mwanadamu ana free will uamuzi ni wake ni kuchagua kwenda kwa The One above all au kwa the one bellow all.

Free Will is illusion (?)

Kuna mada Fulani niliwahi kusema kwamba tukio la kuumbwa Adam na eva hadi kufukuzwa eden linapinga uwepo wa Mungu kwa kupinga sifa tatu alizonazo Mungu kwamba anaweza yote,anajua kila kitu na yupo kila mahali… ndio maana mimi hua nalichukulia kama lugha ya picha tu na sio tukio halisi na kama kweli ni kweli lilitokea kama lilivyoelezewa kwenye kitabu cha mwanzo basi linaonyesha Mungu hafai kupokea sifa tunazompa. Kama anajua kila kitu je wakati anamuumba adamu bila Eva hakujua kwamba adamu hatapata uhitaji wa kua na mwenza? Yupo kila mahali jewakati adam na eva wamekula tunda hakuwepo pale walipojificha hadi aanze kuuliza wako wapi? Alikua hajajua juu ya tukio la adam kula tunda maana lilimuudhi kwelikweli like he didn’t know a thing from a first place.

Mungu anajua kila kitu kutuhusu sisi wanadamu, anajua kesho nitakua wapi,nitakula nini na nitakufa lini...pia ametupa uwezo wa kuchagua kuishi ville tupendavyo bila yeye kutuingilia(free will) sasa hapa ndio kuna msingi mkuu wa mada yangu ambapo imekua ikinitatiza sana jambo hili. Je kwakua Mungu anajua kila kitu, Je anajua kama mimi nitakua mbaya au mwema? Je anajua kwamba mimi nikifa nitakua wa mbinguni au wa motoni? Na kama anajua nikifa nitafikia motoni je mimi naweza kubadirisha nisiende motoni? Kumbuka kwamba kama nitaweza kubadirisha nikaenda mbinguni badala ya motoni basi Mungu anakua hajui kila kitu kuhusu mimi…Pia kama anajua moja kwa moja nitaenda motoni basi wanadamu hatuna uhuru wa kuchagua kufanya yale tupendayo. Mungu kama anajua tutachagua kufanya kitu Fulani kwa uhuru basi huo sio uhuru tena bali tunapangiwa yale ya kuchagua hivyo free will hatuna its illusion na kama Mungu hajui kama nitachagua jambo Fulani kwa uhuru basi anapoteza sifa ya kujua kila kitu toka kwangu.?


Kuna phrase protestant wanapenda kusema kwamba sisi wakatoliki hatujui kusoma na kuielewa biblia, naamini name ni mmoja wapo nisiojua kusoma biblia. Hivyo basi napenda kuwaalika wale wote wenye uelewa juu ya jambo hili. Naombeni mnijuze kama Mungu anajua hatima yangu na hukumu yangu siki ya mwisho na kama anajua je naweza kubadirisha? Kama mchezo kautengeneza yeye na sharia za mchezo kazitengeneza yeye je wachezaji wanawezaje kua huru?

Vinjii…
Mada hizi za kumuuliza Mungu nyingi huletwa na wakristo mna dini yao haina mafundisho sahihi
 
-Kama nitajitambua nitawezaje kuishi heaven kwa raha huku wazazi na ndugu zangu wapendwa nimewashuhudia wakienda kuchomwa moto?

-Labda siku hiyo tutakua hatutambuani, kama hatutambuani it means hata mimi sitajitambua. Sasa kama mimi sitajitambua nitajuaje kama ni mimi ndio niko peponi au motoni? (Kumbuka kama nikijitambua sitafurahia kwenda heaven wakati my wife and any of my kids they're suffering in hell)
Tutajitambua vizuri kabisa na tutatambuana vizuri tu.

Kitu kimoja ni kwamba hata hapa duniani, kadri unavyozidi kuwa na upendo, kupanua wigo wako wa upendo ndivyo 'attachment yako' kwa ubinafsi inavyozidi kupotea. Namaanisha mtu asiye na regard na mwingine bali yeye tu anao upendo sifuri. Lakini atakayempenda ndugu wa damu tu huyo anao upendo assume wa moja. Yule atakayeongeza na upendo kwa kila jirani yake huyo labda anao wa elfu na akizidisha hadi akapenda nature na mawe na fisi na majani na swala huyo anaelekea upendo infinity, upendo ambao ni upendo wa kimungu anayependa hadi magalaxy mazimamazima!

So mtu kujimilikisha 'ooh huyu mke wangu nampenda' au 'mtoto wangu ningependa kuwa karibu naye na sio mtu baki katika kula raha' hapo bado unakuwa na ego attachment kujimilikisha vitu/watu.
Angalia mfano wa Yesu aliwapenda jirani zake kwa kiwango cha kimungu na ndio maana hata ndugu zake hadhi yao ilikuwa sawa na wooooote wanaolishika na kulifuata mapenzi ya Baba. Nadhani hii ndiyo kiashiria cha 'kujikana nafsi yako' yaani kutokuwa na ubinafsi bali kujawa na upendo. Upendo haubagui, hautafuti vya kibinafsi etc etc
 
wapi ulichagua kuzaliwa, unafikiri ungepewa nafasi ya kuchagua ungechagua kuzaliwa maxingira uliyopo. Why ulikuwa walia ulivyozaliwa tu
Kisayansi kulia wakati wa kuzaliwa ni ishara ya uhai, pia ni matokeo ya reaction inayosababishwa na kubadilika kwa mazingira ya mtoto kutoka tumboni hadi duniani.

Hauchagui mahali ama mazingira ya kuzaliwa kwa kuwa Mungu anakupa akili na utashi the moment anapokuumba. And just like personality; intellect and will develop in the course of time.

Ndio maana tunaamini athari (consequence) ya maamuzi yetu inategemea na levels za uelewa wetu juu ya jambo husika.

Atakavyohukumiwa shetani si sawa na atakavyohukumiwa Baba Mtakatifu au atakavyohukumiwa Padre wa kawaida au tutakavyohukumiwa sisi au watakavyohukumiwa wapagani.

Kila mmoja atahukumiwa kulingana na level yake ya uelewa wakati anafanya maamuzi husika. Luka 12:48


- wapi ulichagua kuwa muumini wa dini unayoabudu. Jee wazazi wako wangekuwa dini tofauti na yako uliyonayo sasa hivi, ungekuwa na dini hii unafikiri?
Ndiyo, kuna watu wengi wamezaliwa na wazazi wapagani ila wao wamekuwa Wakristu.

Kuna watu wengi wamezaliwa na Wakristo ila wao wameamua kuwa Wapagani.

Kuna watu wengi tu wamezaliwa dini A nao wameamua kubadili na kuwa dini B.

Wanatumia freewill zao watakavyo.



- kwa wale walio na magonjwa ya kurithi, hivi kuna sehemu walichagua kuwa nayo au the whole sequence of events was predetermined from moment their parents fall in love to moment they conceive.
Magonjwa hayahusiani moja kwa moja na mtu kuwa mwema ama muovu.
 
Did you use your freewill to write this comment, or you were programmed to write it?
As I said there is no freewill at all, it is just an illusion

Free will haipaswi kuwa na mipaka, na kwa perception ya kimungu, hiyo comment sijaandika kwa utashi wangu na nilikuwa sina uwezo wa kuepuka kutoiandika. ikiwemo na hii nayoandika sasa

Ephesians 1:11


11 All things are done according to God's plan and decision; and God chose us to be his own people in union with Christ because of his own purpose, based on what he had decided from the very beginning.

Ikiwa kila kitu ni mipango ya Mungu utasemaje tuna freewil?

Kama tuna free will kivipi kila jambo liwe ni sehemu ya mipango yake?
 
Kwa hiyo Mungu alidhamiria kabisa kumuumba Shetani ili kuleta balance, sasa kwa nini shetani alaumiwe wakati kumbe yeye aliumbwa ahamasishe ubaya ili alete balance?
Mungu hakumuumba shetani, ila Malaika mwema kabisa anayeitwa Lusifa. Kila alichokiumba Mungu kilikuwa chema (Mwanzo 1:31).

Shetani ni matokeo ya uamuzi wa malaika mwema Lusifa kuamua kuwa muovu.

Hivyo, Mungu hakuumba na haumbi uovu ama waovu. Ni sisi ndio tunaamua kuwa wema ama waovu.

NB: Uovu ni terminology tu inayotumika kuelezea vitu au watu wasio wema. In fact, evil do not exist but merely a terminology that depicts the absence of good and goodness.


Mbona wakati wana wa Israel walipikuwa wanatenda hiyo iitwayo dhambi alikuwa anaona na alikuwa akikasirika sana?
Aliona na hakuingilia uamuzi wao. Na hiyo ndio freewill, upo huru kuamua chochote. Changamoto inakuja kwenye matokeo ya uamuzi wako.

Vipi kuhusu Daudi kuzini na mke wa mwanajeshi wake na utamu ukamkolea akaamua asuke mpango wa kumuua huyo mjeshi ili amchukue kabisa mke wa huyo jamaa mbona alimuona hadi akamtuma nabii kwenda kumweleza ni jinsi gani yeye (Mungu) amekasirika...?
Mungu aliona yote lakini hakuingulia, maana hajihusishi na kuingilia uhuru wa watu. Na hiyo ndio freewill yenyewe tunayoiongelea.

Unakuwa huru kufanya uamuzi huru. Mungu anachokifanya ni kukupa taarifa zote ili ufanye informed decision na uwe tayari kuwajibikia matokeo ya uamuzi wako - bila kujali kama ni mema ama maovu.


Mnona kaini alipomuua nduguye Abeli
Bado Mungu hakuingilia uamuzi wa Kaini, maana Kaini pia alikuwa na freewill.

Mifano yote uliyoitoa inathibitisha Mungu haingilii uamuzi wetu. Ni sisi ndio tunaamua hatma yetu.

Yeye anatusaidia kutupa taarifa zote muhimu ili tufanye informed decision na tuwajibikie consequences zake.
 
Safi sana, safi sana umereinforce point moja ilikuwa inapelekea watu kumuona Mungu isivyo. Kumuona kama vile yeye ndio anaye'dictate' hali zetu huku duniani. Wakati kumbe ni matokeo ya chaguzi zetu wenyewe ndiyo tunajiumbia dunia zetu.

Mtu akisoma kwa bidii na akaelewa kinamna fulani yeye mwenyewe mwisho wake atapata ufaulu fulani sambamba na alivyofanyafanya. Yaani ni kama automatically hivi.

Pia hata kuishi baadaye katika ufalme wa mbingu au ufalme wa shetani inawezekana hakuna kiumbe kutoka nje kinachokuja kukuambia wewe nenda huku au nenda kule. La!. Itakuwa ni mtu mwenyewe tu mfano akijifanya mbinafsi mwovu mwishoni atachaguachagua hadi kujikuta na washirika wenzie wenye tabia hizo baada ya kufa. Ukizungukwa na watu wabinafsi na waovu mara nyingi inamaanisha 'hell' hata kama upo wapi. Fikiria wewe uwe tajiri sehemu iliyozagaa 'ma-panya road' je utafaidi?

Lakini pia fikiria mfano ukafanya fikira na maamuzi yako ya kijamaa/communal ukapenda ushirikiano na upendo usio wa kibinafsi, upendo wa kimungu. Halafu mwishoni ukajitengenezea uhusiano wa karibu na marafiki wa namna hiyo mkajikuta wote baada ya kufa mpo katika dunia yenye watu wenye utashi huru/freewill lakini wote mna maamuzi ya kiupendo kwa kila mmoja wenu. Ndugu yangu hiyo mojakwa moja ndiyo tafsiri ya kuuishi ufalme wa mbinguni. Fikiria labda mazingira ambapo hata nyumba yako imebomolewa na upepo ukiwa haupo upo safarini, utarudi na utakuta vyombo vyako vi salama [tena hata kukuta wamekurekebishia wanakijiji!] Na siku nyingine ikimtokea mwingine wewe na wanakijiji wenzio mtashirikiana kumjengea 'victim mpya'. So kazi zitaendelea, hakuna kupumzika mbinguni wala jehanamu, lakini kwa mbinguni zitaleta raha mno kuzishiriki maana ni za upendo.

Kwa hiyo hata kama Scars alivyopendekeza kuwa na mbinguni napo tutaendelea na kuhustle kinamna fulani afahamu utofauti mkubwa uliopo kati ya; watu wanaohustle kati ya mijitu mibinafsi, na wanaohustle kati ya watu waupendo kuna utofauti mkubwa sana mfano wa hell and heaven figuratively and literally too! Kila mtu kutokana na namna anyoiona sahihi anajielekeza .anakokupenda mwenyewe. Mungu anajua kuwa njia ya upendo ni nzuri, ila mwanadamu akimsisitizia kwamba njia ya ubinafsi ndio yenyewe sasa. Akajitia u-much-know basi Mungu humruhusu aendage huko maana ndiko atakakofaidi kwa mujibu wake yeye mwanadamu. Huo ni upendo mkuu sana!

Upendo ni pale unao uwezo na utashi kufanya lolote, lakini unaamua kutumia uwezo huo kwa uamuzi huru wako kuyafanya matakwa/mapenzi ya yule unayempenda. Mungu anatupenda sana mazee
Umeielewa vizuri sana. Wengi tunamlaumu Mungu kwa matokeo ya uamuzi tulioufanya badala ya kuuwajibikia.
 
Mimi kuna rafiki yangu kutokana na kumjua yeye na demu wake niiliwahi kumtabiria kuwa haitopita muda fulani lazima wataachana ,sababu za kuachana na aina gani ya mwanaume atakaye mfuata na nikampa na muongozo wa kufanya kuepusha hilo jambo lkn akanipuuza siku baada ya siku kadhaa kila kitu nilichokisema kilitimia kila kitu mpk muda jamaa aliniona mimi mtu wa ajabu lakini siku mlazimusha na tahadhari nilimpa na nikajua matokeo kutokana na uzoefu wangu mpk akawa akipatwa na majambo yake aninifata nimpe muongozo.
 
Freewill haipo kwasababu Mungu ndiye anayetengeneza fate

Refer kwa kisa cha yuda kumsaliti yesu, Yuda hata kabla hajazaliwa alikuwa amekwisha andaliwa kutimiza mpango wa Mungu

Kwa maana ya kwamba hakuwa na freewill yeyote ya kuweza kuepuka usaliti

Mungu alimuumba Yuda akiwa tayari msaliti angali yupo tumboni, hakuwa na option ya kuepuka na kwamba usaliti ule aufanye zakayo au mtu mwingine yeyote.

Sasa kama mtu hufanya kile ambacho ameumbiwa aje afanye utasemaje kuwa ni freewill?

Mbali zaidi kwanini mtu ambaye anafanya kile alichoumbiwa aje afanye, aje kuadhibiwa tena?
Huwaga najiuliza Yuda sana kimaelezo Yuda alikua ashaandaliwa sikuona kosa !!
Lakini niliwahi kupewa jibu kwamba Mungu ametoa uwezo wa kusamehe yaani kutubu hivyo basi hata kama kuna maandiko tunapaswa kutimiza tunapewa nafasi kurudi kundini…
 
Kila uamuzi unaofanyika huambatana na matokeo yake.

Kwa mfano; ukiamua kusoma kwa bidii kuna matokeo yake kama ambavyo ungeamua kutokusoma.

Kinachotokea baada ya wewe kuchagua kuwa mwema ama muovu ni matokeo ya uamuzi na uchaguzi wako.

Na kwa kuwa Mungu anatupenda sana, akatupa akili, utashi na dhamiri ili zitusaidie kufanya informed decisions.

Mungu anatupenda sana aisee.
Unakakubali kuwa kila jambo hutokea kwasababu au kuna bahati mbaya?
 
Twende taratibu..
Mungu anajua yote, sivyo.?
Hii inamaanisha kuwa ana uwezo wa kuona yote kabla hata hayo yote hayajaanza kutokea.

Kabla mimi sijazaliwa alishajua kuwa mimi nitakuwaje kwa kuwa yeye ajua yote, then huo utashi huru nautoa wapi wakati mimi naishi kile ambacho kilionekana kabla ya hata mimi kuwapo?
Naam, twende taratibu, utaelewa.

Ni kweli kabisa Mungu anajua yote kabla hata haujaumbwa. Anajua kabisa utakuwaje, utaishije, na utakufaje. Anajua yote.

Freewill haihusiani na yeye kujua yote. Freewill is all about Mungu kutupa uhuru kamili wa kuchagua tuwe akina nani, tuishi vipi na ama tuwe wema ama wabaya.

Utashi huru unaupata kwa kuwa Mungu amekupa uhuru kamili wa kufanya uamuzi uwao wote.

Look; Mungu anajua kila kitu lakini hajakupangia chochote. Mungu anajua matokeo ya uamuzi utakaoufanya lakini hajakupangia ufanye uamuzi wowote. Amekuacha wewe uamue.

Kwa kuwa anajua kila kitu, amekupa akili na utashi ili vikusaidie ufanye uamuzi sahihi ukiwa na taarifa zote (informed) za uamuzi unaochagua kuufanya na matokeo (consequences) yake.
 
Huwaga najiuliza Yuda sana kimaelezo Yuda alikua ashaandaliwa sikuona kosa !!
Lakini niliwahi kupewa jibu kwamba Mungu ametoa uwezo wa kusamehe yaani kutubu hivyo basi hata kama kuna maandiko tunapaswa kutimiza tunapewa nafasi kurudi kundini…
Mungu ndiye anayepaswa kuomba msahama kwa Yuda kwa kumuumba na hali ya usaliti kwa kusudio maalumu ambapo Yuda hakuwa na option ya kuepuka
 
Ndio mkuu upo sahihi Mungu hatuamulii wapi pa kwenda ila swaki la Muhimu ni je Mungu anajua mimi nitachagua Uzuri au ubaya??
Hilo ameliwekea siku ya hukumu ,ila uwezo WA kujua anao , alishaamua amekupa uchaguzi , so in between hapo utamua mwenyew hatma yako ambayo itajulikana siku ya hukumu
 
As I said there is no freewill at all, it is just an illusion

Free will haipaswi kuwa na mipaka, na kwa perception ya kimungu, hiyo comment sijaandika kwa utashi wangu na nilikuwa sina uwezo wa kuepuka kutoiandika. ikiwemo na hii nayoandika sasa

Ephesians 1:11


11 All things are done according to God's plan and decision; and God chose us to be his own people in union with Christ because of his own purpose, based on what he had decided from the very beginning.

Ikiwa kila kitu ni mipango ya Mungu utasemaje tuna freewil?

Kama tuna free will kivipi kila jambo liwe ni sehemu ya mipango yake?
First of all, freewill haina mipaka, not even God can intervene.

Waefeso 1:11
na ndani yake sisi nasi tulifanywa urithi,
huku tukichaguliwa tangu awali sawasawa na kusudi lake yeye,
ambaye hufanya mambo yote kwa shauri la mapenzi yake.


Hapa Mtume Paulo anaelezea namna Mungu aliye huru anavyotumia uhuru wake kutusaidia tuendelee kuwa wema.

Yaani kama ambavyo mimi nina freewill kwa mambo yangu, na ambavyo wewe ulivyo na freewill kwenye maamuzi yako, ama ambavyo mtu mwingine yeyote alivyo na freewill kuamua mambo yamhusuyo; Mungu naye ana freewill.

Na ameamua kuitumia freewill yake kuwa mwema na kusaidia wanadamu kuwa wema kama yeye alivyo.

Hayo ndiyo mapenzi yake aliyoamua kuyachagua, kama ambavyo sisi nasi tuna mapenzi yetu tunayoyachagua.
 
Mimi kuna rafiki yangu kutokana na kumjua yeye na demu wake niiliwahi kumtabiria kuwa haitopita muda fulani lazima wataachana ,sababu za kuachana na aina gani ya mwanaume atakaye mfuata na nikampa na muongozo wa kufanya kuepusha hilo jambo lkn akanipuuza siku baada ya siku kadhaa kila kitu nilichokisema kilitimia kila kitu mpk muda jamaa aliniona mimi mtu wa ajabu lakini siku mlazimusha na tahadhari nilimpa na nikajua matokeo kutokana na uzoefu wangu mpk akawa akipatwa na majambo yake aninifata nimpe muongozo.
Pamoja na kujua kila kitu lakini haukuingilia uamuzi wake. Ndivyo afanyavyo Mungu. Anajua kila kitu, anaweza kila kitu na yupo kila mahali ila haingilii uamuzi wetu.
 
Huwaga najiuliza Yuda sana kimaelezo Yuda alikua ashaandaliwa sikuona kosa !!
Lakini niliwahi kupewa jibu kwamba Mungu ametoa uwezo wa kusamehe yaani kutubu hivyo basi hata kama kuna maandiko tunapaswa kutimiza tunapewa nafasi kurudi kundini…
Maandiko gani yamemtaja Yuda kuandaliwa kumsaliti Kristo? Tuwekee hapa.
 
Japo mfano wako hauna uhalisia wowote, na hili nilishawahi kukukosoa katika uzi fulani, maana uliutoa mfano huu huu.

Allah anajua kila kitu "indetails" na "in general". Hili kwanza liweke akilini. Wewe na huyo muhusika nyote mlikuwa na "free will" ndiyo maana hukumuunga mkono kwa kile alichokifanya. Sasa Mola wetu hayo yote aliyajua na akaruhusu yakatokea, na angetaka yasitokee pia yasinge tokea.

Kujua kwa Mola mambo hayo yote hakukuzuii wewe kufanya unalo taka, mola alvyo tuumba akatupa uhuru wa kuchagua, hakuishia hapo akatupa akili za kujua zuri na baya, lenye hasara na manufaa. Wewe unapofanya ovu ujue muda huo hup ulikuwa na uwezo wa kufanya jema. Nikakutolea mfano mwepesi sana, leo hii wewe kwa kumjua vizuri mtu fulani, mfano akipata hela mtu fulani lazima atakunywa pombe, na kweli akipata hela anakunywa. Tofauti ya Mola wetu yeye anajua kabisa "indetails"

Sasa swali linakuja, kwa kile unachokihoji wewe na kutaka kiwe hivyo, kinaondoa kabisa suala la "free will". Ndiyo maana Mola wetu katika Qur'aan akasema ya wazi ya kuwa akatupa uwezo wa kusikia na kuona, kisha akatuacha tukipenda tutashukuru na tusipopenda tutakufuru, ila kila kitu amekuwekea wazi.

Lakini katika huko kukuwekea wazi, akakwambia hili baya usifanye na lile zuri fanya. Yaani sawa na kupewa mtihani wenye majibu tayari.
Kujua kwa Mungu mambo yote hata kabla sijazaliwa kunanizuia kufanya mimi nayo taka unless niwe na option ya kufanya kile ambacho yeye hajakiona au kwenda kinyume na alivyoona

Kupitia mfano wa calvin aliyeua makumi ya watu. Sasa kama mimi tu nimetengeneza madai lakini hakuna mtu yeyote rational ambaye ameweza kuniamini kuwa sihusiki na mauaji hayo aliyosababisha calvin na kuwa sikujua kitachokwenda kutokea baadaye

If this is what people would think about me, then what should we think about God?
 
Kujua kwa jambo kuna kuzuia nini weww kufanya unachotaka ? Shida yenu wote wanao pinga hii "free will" hawaonyeshi uhusiano wa kujua na kufanya matendo.

Katika Uislamu kuna baadhi ya makundi yalikuwa yanaitwa Jahmiyah na Jabriyah, hawa walikuwa wanajinasibu ya kuwa wao ni Waislamu, katika istilahi ya Kiislamu tunaziita "Firaq" hawa katika itikadi zao walikuwa wanasema au kuamini ya kuwa "Mwanadamu hana uhuru wa kuchagua, yaani ni kama vile ua au jani linalo au lililo pulizwa na upepo" lakini wote walio kuwa na imani hiyo hawaonyeshi popote uhusiano wa kujua na ufanyaji matendo. Hili ni tatizo la kulazimisha mambo na kutofikiria mambo kwa undani.
Kabla ya kuzaliwa kwako Mungu akijua utaua, una option ya kutoua?

Kama huna option ya kutoua utasemaje sijazuliwa kufanya nachotaka?
 
Kama waliweza kumsulubisha bila kuwa na ushahidi wa kweli, wangeshindwa vipi kumkamata bila hata ya usaliti wa Yuda?
Wangeshindwa kwa sababu walikuwa hawamjui ni nani, alikuwa sometimes anashinda maporini kusali. Afu pia ukisoma vizuri maelezo yanaonyesha kama hakutaka kukamatwa hivi. Maana pale yuda alivyokuja kuzuga kwa kumkisi, yesu akamkata kabda hajatoka karibu nae akwambia una msaliti mwana wa adamu kwa kumkisi.
 
Back
Top Bottom