God's Conscience vs Free Will: Je, Mungu anajua hatima ya wanadamu itakuwaje?

God's Conscience vs Free Will: Je, Mungu anajua hatima ya wanadamu itakuwaje?

Mungu anajua hatma kwasababu yupo nje ya time dimension. Hivyo yeye anakuona mwaka 2000, anakuona mwaka 2022 na anakuona mwaka 2040 (mfano tuu).

Hajakupangia wala haku control ila anakuona unavyofanya maamuzi yako na unavyovuna matokeo yake.

Hata hivyo ameweka njia ambayo ukichagua kuifuata unapata matokeo mazuri wakati wote.
Je mleta maada, wakati unajiuliza uwezo wa Mungu na Uhuru wa kuchagua. Je umejiuliza maswali haya mawili?. 1. Je ni kweli tuliumbwa na Mungu?. 2. Kama ni kweri kwa Nini alituumba?. Kama hatujaumbwa na Mungu maada hiii Haina maana. Sasa kwa umuhimu wa maada hii ni kwanza lazima tukiri tuliumbwa na Mungu. Sasa kwa Nini alituumba?. Kwa wakatoliki jiubu huwa tumpende, tumujue na tumutumikie ( kwa kifupi Yeye anatafuta recognization only).
Kwa Kuwa binadamu tunamwili na hivyo unatuongonza kwenye matakwa ya mwili ( Tamaa za mwili, Tamaa za Mali na tafasiri zetu binafisi kukwepa uhalisia). Sasa hapa kwa Kuwa lengo lake ni recognization ndiyo maana kaweka kitu kuomba msamaha kwake. Binadamu ni Roho iliyofunikwa na mwili na Roho ndiyo uungu wetu hivyo sisi tunaweza kutumia Roho zetu Kuwa na Mungu au tukazichafua tukawa kwa shetani. Sasa hoja ya uwezo wa uungu ipo ndani yetu na ndiyo inayotunza history ya mema na mabaya yote . Maana ya free will ni kuchagua Kuwa kwa Mungu ama kwa shetani. Ukichagua kwa Mungu maana yake umechagua kutumia nguvu za uungu ulio nao hapo Sasa binadamu wewe unakuwa na nguvu za Mungu na ushetani haukusogelei Tena. Maana yake uwezo wa kujikinga na mabaya utakuwa nazo na Mungu atakuwa ndani yako. Mleta maada God blesses are always there , the issues we opt to use or to damp?. Huenda nimeongea kwa kifupi Sana Hoja nzituo niulize kivingine nikujibu.
 
Kujua kwa jambo kuna kuzuia nini weww kufanya unachotaka ? Shida yenu wote wanao pinga hii "free will" hawaonyeshi uhusiano wa kujua na kufanya matendo.

Katika Uislamu kuna baadhi ya makundi yalikuwa yanaitwa Jahmiyah na Jabriyah, hawa walikuwa wanajinasibu ya kuwa wao ni Waislamu, katika istilahi ya Kiislamu tunaziita "Firaq" hawa katika itikadi zao walikuwa wanasema au kuamini ya kuwa "Mwanadamu hana uhuru wa kuchagua, yaani ni kama vile ua au jani linalo au lililo pulizwa na upepo" lakini wote walio kuwa na imani hiyo hawaonyeshi popote uhusiano wa kujua na ufanyaji matendo. Hili ni tatizo la kulazimisha mambo na kutofikiria mambo kwa undani.

Unakuaga na logic za kidini sana ila sisi tulikua tunaamin ivo ivo sasa kama anajua itazuia nn mm kufanya nafny sabab alijua nitafnya
 
Nakubaliana na wewe hakika hapa ndo pana utata. Mi nadhani hutajitambua kabisa kwa sababu hutakumbuka kabisa ya duniani. Mind inaikomind brain kufanya vitu. Na kumbukumbu zipo kwa brain zimetunzwa. Wanasayansi walishadhibitisha ubongo ndio unaotunza kumbukumbu. Ni baada ya jamaa mmoja kupoteza sehemu ya ubungo wake katika ajali, ikawa kuna vitu anakumbuka ila vingine hakumbuki kabisa.

Ila tumetoka mbali sana ni karne ya juzi tu hapa watu wa kisomo walikuwa wakidhania moyo ndo unatunza kumbukumbu.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] et watu wa visomo
 
fre will is illusion

Ambao mnadhania kuna free will mnijibu haya.

- wapi ulichagua kuzaliwa, unafikiri ungepewa nafasi ya kuchagua ungechagua kuzaliwa maxingira uliyopo. Why ulikuwa walia ulivyozaliwa tu

- wapi ulichagua kuwa muumini wa dini unayoabudu. Jee wazazi wako wangekuwa dini tofauti na yako uliyonayo sasa hivi, ungekuwa na dini hii unafikiri?

- kwa wale walio na magonjwa ya kurithi, hivi kuna sehemu walichagua kuwa nayo au the whole sequence of events was predetermined from moment their parents fall in love to moment they conceive.

Yes dini pia n uongo
 
Freewill ipo kwenye uhuru tuliopewa wa kufanya maamuzi ya ama kuwa wema ama wabaya.

Kwamba, Mungu hatakaa aingilie uhuru wa uamuzi wote unaoufanya mpaka utakapokufa.

Amekupa mamlaka ya kujichagulia hatma yako - uwe mwema ama mbaya.

So hajui kesho yetu?
 
As I said there is no freewill at all, it is just an illusion

Free will haipaswi kuwa na mipaka, na kwa perception ya kimungu, hiyo comment sijaandika kwa utashi wangu na nilikuwa sina uwezo wa kuepuka kutoiandika. ikiwemo na hii nayoandika sasa

Ephesians 1:11


11 All things are done according to God's plan and decision; and God chose us to be his own people in union with Christ because of his own purpose, based on what he had decided from the very beginning.

Ikiwa kila kitu ni mipango ya Mungu utasemaje tuna freewil?

Kama tuna free will kivipi kila jambo liwe ni sehemu ya mipango yake?

Huenda mungu hakumuumba shetani
 
Unashindwa kuelewa jambo

Ni kwamba katika concept ya freewill na dhana ya Mungu mjuzi wa yote, muweza wa yote na mwenye upendo wote.

Tunasema freewill ni illusion kwasababu kila kitu kilipangwa though the choice may seem very free for you but in reality you're choice cannot be otherwise
Jibu swali nililo kuuliza, kujua kwa Mola, kupanga mambo kuna uhusiano gani na wewe kushindwa kufanya unachokitaka ?
 
Hapa ndipo unapojichanganya
Hakuna sehemu niliyo jichanganya, ni wewe kutokuelewa jambo husika.
Kuomba kwako dua kutakuwa ni kitu kipya kitachoweza kubadilisha maono ya Mungu?
Si kitu kipya sababu Allah anajua kila kitu "in general" na anajua kila kitu "in details".

Anajua mja wangu atatoka hapa ataenda pale ? Atafanya kadha ? Atakosea ataomba msamaha, nitambadilishia nilichompangia sababu atafanya jambo fulani. Jambo rahisi sana hili.

Mimi nasubiri mnionyeshe uhusiano wa kujua kwake Allah ana kuzuia nini weww kufanya unachotaka ?

Kwanini una akili na kwanini una matashi na kwanini una uwezo wa kufanya jambo fulani na kuacha jambo fulani ?
Kuomba kwako msamaha nako sio kwa utashi wako, na hata ukibadilishiwa hiyo itaonekana hivyo katika perception yako lakini uhalisia ni kuwa yeye ndiye alitaka iwe hivyo
Ni utashi wako ndiyo maana unajua hapa umekosea na hapa unatakiwa ufanye kadha wa kadha.
 
Jibu swali nililo kuuliza, kujua kwa Mola, kupanga mambo kuna uhusiano gani na wewe kushindwa kufanya unachokitaka ?
Weka umakini sio kila jibu linaanza na neno "kwasababu"

Nimekuambia hakuna freewill ya mtu kuchagua anachotaka kwasababu choice iko fixed haina option nyingine

Choice ikiwa fixed unapataje uhuru wa kufanya unacho kitaka?
 
Hakuna sehemu niliyo jichanganya, ni wewe kutokuelewa jambo husika.

Si kitu kipya sababu Allah anajua kila kitu "in general" na anajua kila kitu "in details".

Anajua mja wangu atatoka hapa ataenda pale ? Atafanya kadha ? Atakosea ataomba msamaha, nitambadilishia nilichompangia sababu atafanya jambo fulani. Jambo rahisi sana hili.

Mimi nasubiri mnionyeshe uhusiano wa kujua kwake Allah ana kuzuia nini weww kufanya unachotaka ?

Kwanini una akili na kwanini una matashi na kwanini una uwezo wa kufanya jambo fulani na kuacha jambo fulani ?

Ni utashi wako ndiyo maana unajua hapa umekosea na hapa unatakiwa ufanye kadha wa kadha.
Mungu akijua utaenda kushoto, hapo una uchaguzi wa kufanya unachotaka ukaenda kulia?

Kama huna option hiyo utasemaje una uhuru wa kufanya unachotaka wakati choice ilishakuwa fixed kabla hata hujazaliwa?

1653756785086.png
 
Nitajibu;

Ndiyoni freewill ni kuchagua mema na yasiyo mema kwetu, kuchagua kwenda left ama right wewe tu na utaendelea kuyapata matokeo kadri ya unavyochagua.

Ndiyo, ubaya ni matokeo ya makosa katika chaguzi zetu, na mda mwingine unatufunza kuwa njia ile ya mwanzo sio sahihi, tubadilike/tubadilishe.

Na ipo popote utakapokuwa utakuwa na freewill [hadi levo fulani za mbinguni] kulingana na mazingira utakayokuwapo [mfano huwezi kuamua tu kupaa ukiwa duniani], free will ni sifa zetu wanaadamu na baadhi ya viumbe wengine wa Mungu. Ndiyo maana kuna mahala Yesu alisisitiza sana kuwa tutumie utashi wetu kuyafanya mapenzi ya baba wa Mbinguni. Kumbe hata yeye angeweza kutotii kukinywa kikombe kama angeamua hivyo ila akaamua kutumia utashi wake kukubali kuyatenda mapenzi ya Baba yake. Maana huo ni mfano mzuri wa kujitoa kwa upendo kusema ukweli hata kama maisha ya matatani.
Maelezo mengi mpaka nimeshindwa kujua umejibu wapi swali langu

Peponi kuna freewill au haipo?
 
Mungu anajua kila kitu kutuhusu sisi wanadamu, anajua kesho nitakua wapi,nitakula nini na nitakufa lini...pia ametupa uwezo wa kuchagua kuishi ville tupendavyo bila yeye kutuingilia(free will) sasa hapa ndio kuna msingi mkuu wa mada yangu ambapo imekua ikinitatiza sana jambo hili. Je kwakua Mungu anajua kila kitu, Je anajua kama mimi nitakua mbaya au mwema? Je anajua kwamba mimi nikifa nitakua wa mbinguni au wa motoni? Na kama anajua nikifa nitafikia motoni je mimi naweza kubadirisha nisiende motoni?
Unachanganya kati ya foreknowledge, kujua kitu kabla hakijatukia na kufanya kitukie.
Ukiwa na utashi maana yake unaamua utafanya nini. Mungu anajua kuwa katika kuutumia utashi utautumiaje.

Mfano, kabla X hajazaliwa, Mungu anajua matendo yake yote atakayoyafanya na kuwa atakufa akiwa anafanya ujambazi na kuwa atahitimisha safari yake motoni. Mungu anajua kwa sababu kila sekunde anajua jamaa atafanya uchaguzi gani. Mungu kujua uchaguzi ambao X ataufanya kwa utashi wake (X) hajahusika kumfanya X afanye ujambazi. Ni uchaguzi binafsi wa X ambao Mungu aliujua kabla hajaumbwa kwa sababu Omniscience inajumlisha na foreknowledge.

Wengi hujichanganya hapo!
Mfano ambao sio mkamilifu ila utafaa kukusaidia kuelewa ni huu.
Fikiria una mtoto wako. For some reason ukajua kuwa kesho ataiba sukari. Je ni wewe ndiye umesababisha aibe kwa sababu unajua kuwa ataiba sukari?

Kuongezea kwenye haya, Mungu hujua tutakachochagua na ndio maana hutuletea watu wa kutuhubiria habari njema ili kutupa nafasi. Na anajua wangapi watazipokea nafasi hizo na wangapi watazikataa. Ili siku ikifika wasiseme haukutupa nafasi!

Hope hizo nafasi utazitumia vyema ikiwemo hii!

Kumbuka kwamba kama nitaweza kubadirisha nikaenda mbinguni badala ya motoni basi Mungu anakua hajui kila kitu kuhusu mimi…
Mungu anajua maamuzi yako yote na utakavyoishia. Ni kama uone mkanda wa video mpaka mwisho halafu muwe mnaangalia na wengine. Hakuna kinachobadilika. Sema mfano huu sio mkamilifu kwa sababu Mungu hana mfanowe. lakini utakupa picha!

Pia kama anajua moja kwa moja nitaenda motoni basi wanadamu hatuna uhuru wa kuchagua kufanya yale tupendayo.
Kila mwanadamu ametenda dhambi na amehukumiwa kwenda Jehanamu. Yesu ametoa nafasi kwa wanaotaka kulipiwa deni lao kumwamini. Mungu anajua kama utatumia utashi wako kuchagua kumwamini Yesu ama la! Na kwa sababu hiyo anajua kama uchaguzi wako ni wa Jehanamu ama mbinguni. Kumbuka kwenye hili Mungu sio bystander bali ndiye Jaji haswa na sheria anaijua vizuri.

Kwa hiyo huwezi kupewa utashi ukachagua kumkataa Mungu halafu ukienda Jehanamu useme haukuwa na uhuru wa kuchagua. Kama wanadamu tusingekuwa huru hakuna angekwenda Jehanamu. Mungu anataka wote tuione mbingu ila kwa sababu ya utashi wengi wataishia Jehanamu!

Mungu kama anajua tutachagua kufanya kitu Fulani kwa uhuru basi huo sio uhuru tena bali tunapangiwa yale ya kuchagua
Hapa sijui kama umetumia akili sawasawa kuwaza. Kama nikijua leo utaamua kuwa mwizi kesho maana yake hauko huru kwa sababu nimejua? Kwamba nimekupangia kwa kuwa nimejua utakachofanya?

hivyo free will hatuna its illusion na kama Mungu hajui kama nitachagua jambo Fulani kwa uhuru basi anapoteza sifa ya kujua kila kitu toka kwangu.?
Shida yako unachanganya mambo. Mungu kujua au kutojua utakachofanya kwa uchaguzi wako hakuna madhara kwenye utashi. Mimi nikijua ama nisjue kesho utaiba sukari haibadilishi uhalisia kuwa ulichagua kuba sukari!
 
Kwa hiyo nako peponi ipo possibility ya uovu kufanyika?
Ukifikia hatua upo peponi, upo Edeni, upo uweponi mwa Bwana unakuwa unaweza kuwa mwovu in theory. Lakini hapo upo tried and tested kiasi kwamba uovu kwako ni almost impossible.

Au tuseme kuna hatua fulani unaweza kufanya uovu ila kuna hatua unafikia kuwa mtakatifu kama Mungu mwenyewe alivyo mtakatifu mambo ya uovu yanakuwa kwako hayapo.

Sema kabla hujafikia utakatifu unaweza kukosea lakini kadri unavyoupunguza umbali wako wa kiroho kutoka pointi A[unyama] kupitia pointi BCD [Ubinadamu] hadi pointi X[Umungu]. Ndio umazidi kupunguza uwezekano wa kutenda dhambi hadi almost zero.

Nasema almost zero kwa kuwa kwa sisi hadi kumfikia Mungu kuna infinity hatuas. And that is a good thing😊
 
Ukifikia hatua upo peponi, upo Edeni, upo uweponi mwa Bwana unakuwa unaweza kuwa mwovu in theory. Lakini hapo upo tried and tested kiasi kwamba uovu kwako ni almost impossible.

Au tuseme kuna hatua fulani unaweza kufanya uovu ila kuna hatua unafikia kuwa mtakatifu kama Mungu mwenyewe alivyo mtakatifu mambo ya uovu yanakuwa kwako hayapo.

Sema kabla hujafikia utakatifu unaweza kukosea lakini kadri unavyoupunguza umbali wako wa kiroho kutoka pointi A[unyama] kupitia pointi BCD [Ubinadamu] hadi pointi X[Umungu]. Ndio umazidi kupunguza uwezekano wa kutenda dhambi hadi almost zero.

Nasema almost zero kwa kuwa kwa sisi hadi kumfikia Mungu kuna infinity hatuas. And that is a good thing😊
Nakukumbusha kuwa Freewill ni uchaguzi wa mema na mabaya

Bila freewill watu hawapo huru na hawana tofauti na humanoid robots

Hakuna jema linaweza tokea bila freewill kuhusika

Sasa kama peponi kuna freewill ni kwamba ipo chance ya uovu kufanyika peponi au haipo?
 
Back
Top Bottom