God's Conscience vs Free Will: Je, Mungu anajua hatima ya wanadamu itakuwaje?

God's Conscience vs Free Will: Je, Mungu anajua hatima ya wanadamu itakuwaje?

Safi sana, safi sana umereinforce point moja ilikuwa inapelekea watu kumuona Mungu isivyo. Kumuona kama vile yeye ndio anaye'dictate' hali zetu huku duniani. Wakati kumbe ni matokeo ya chaguzi zetu wenyewe ndiyo tunajiumbia dunia zetu.

Mtu akisoma kwa bidii na akaelewa kinamna fulani yeye mwenyewe mwisho wake atapata ufaulu fulani sambamba na alivyofanyafanya. Yaani ni kama automatically hivi.

Pia hata kuishi baadaye katika ufalme wa mbingu au ufalme wa shetani inawezekana hakuna kiumbe kutoka nje kinachokuja kukuambia wewe nenda huku au nenda kule. La!. Itakuwa ni mtu mwenyewe tu mfano akijifanya mbinafsi mwovu mwishoni atachaguachagua hadi kujikuta na washirika wenzie wenye tabia hizo baada ya kufa. Ukizungukwa na watu wabinafsi na waovu mara nyingi inamaanisha 'hell' hata kama upo wapi. Fikiria wewe uwe tajiri sehemu iliyozagaa 'ma-panya road' je utafaidi?

Lakini pia fikiria mfano ukafanya fikira na maamuzi yako ya kijamaa/communal ukapenda ushirikiano na upendo usio wa kibinafsi, upendo wa kimungu. Halafu mwishoni ukajitengenezea uhusiano wa karibu na marafiki wa namna hiyo mkajikuta wote baada ya kufa mpo katika dunia yenye watu wenye utashi huru/freewill lakini wote mna maamuzi ya kiupendo kwa kila mmoja wenu. Ndugu yangu hiyo mojakwa moja ndiyo tafsiri ya kuuishi ufalme wa mbinguni. Fikiria labda mazingira ambapo hata nyumba yako imebomolewa na upepo ukiwa haupo upo safarini, utarudi na utakuta vyombo vyako vi salama [tena hata kukuta wamekurekebishia wanakijiji!] Na siku nyingine ikimtokea mwingine wewe na wanakijiji wenzio mtashirikiana kumjengea 'victim mpya'. So kazi zitaendelea, hakuna kupumzika mbinguni wala jehanamu, lakini kwa mbinguni zitaleta raha mno kuzishiriki maana ni za upendo.

Kwa hiyo hata kama Scars alivyopendekeza kuwa na mbinguni napo tutaendelea na kuhustle kinamna fulani afahamu utofauti mkubwa uliopo kati ya; watu wanaohustle kati ya mijitu mibinafsi, na wanaohustle kati ya watu waupendo kuna utofauti mkubwa sana mfano wa hell and heaven figuratively and literally too! Kila mtu kutokana na namna anyoiona sahihi anajielekeza anakokupenda mwenyewe. Mungu anajua kuwa njia ya upendo ni nzuri, ila mwanadamu akimsisitizia kwamba njia ya ubinafsi ndio yenyewe sasa. Akajitia u-much-know basi Mungu humruhusu aendage huko maana ndiko atakakofaidi kwa mujibu wake yeye mwanadamu. Huo ni upendo mkuu sana!

Upendo ni pale unao uwezo na utashi kufanya lolote, lakini unaamua kutumia uwezo huo kwa uamuzi huru wako kuyafanya matakwa/mapenzi ya yule unayempenda. Mungu anatupenda sana mazee
Free will ni uhuru wa kuchagua mema na mabaya, wote tunakubaliana na tafsiri hiyo.

Na kwamba ubaya unatokea kwasababu kuna freewill na bila freewill kusingekuwa na raha kwasababu watu wangeishi kama robots

Anyway. Peponi kuna freewill au haipo?
 
First of all, freewill haina mipaka, not even God can intervene.

Waefeso 1:11
na ndani yake sisi nasi tulifanywa urithi,
huku tukichaguliwa tangu awali sawasawa na kusudi lake yeye,
ambaye hufanya mambo yote kwa shauri la mapenzi yake.


Hapa Mtume Paulo anaelezea namna Mungu aliye huru anavyotumia uhuru wake kutusaidia tuendelee kuwa wema.

Yaani kama ambavyo mimi nina freewill kwa mambo yangu, na ambavyo wewe ulivyo na freewill kwenye maamuzi yako, ama ambavyo mtu mwingine yeyote alivyo na freewill kuamua mambo yamhusuyo; Mungu naye ana freewill.

Na ameamua kuitumia freewill yake kuwa mwema na kusaidia wanadamu kuwa wema kama yeye alivyo. Hayo ndiyo mapenzi yake aliyoamua kuyachagua, kama ambavyo sisi nasi tuna mapenzi yetu tunayoyachagua.
Ikiwa Mungu anafanya mambo yote kwa shauri na mapenzi yake, utasemaje una freewill ya kuchagua unachotaka?
 
Unakakubali kuwa kila jambo hutokea kwasababu au kuna bahati mbaya?
Tulikuwa na concept ya freewill, tukaingiza predestination; unataka tuongeze concept ya tatu - determinism? Mbona tutakesha sasa. 😁
 
Kujua kwa Mungu mambo yote hata kabla sijazaliwa kunanizuia kufanya mimi nayo taka unless niwe na option ya kufanya kile ambacho yeye hajakiona au kwenda kinyume na alivyoona
Wewe kwa mfano kama unajua Juma asiposoma atafeli na akisoma atafaulu kunamzuiaje Juma kusoma na akafaulu au kutokusoma na akafeli?
 
Kabla ya kuzaliwa kwako Mungu akijua utaua, una option ya kutoua?

Kama huna option ya kutoua utasemaje sijazuliwa kufanya nachotaka?
Kama Mungu anaingilia mambo ya wengine na kama hakuna freewill basi kusingekuwa na uovu.

Uovu upo kwa kuwa mnatumia freewill zenu kuamua kuwa waovu.

Hakuna anayekupangia.
 
Wangeshindwa kwa sababu walikuwa hawamjui ni nani, alikuwa sometimes anashinda maporini kusali. Afu pia ukisoma vizuri maelezo yanaonyesha kama hakutaka kukamatwa hivi. Maana pale yuda alivyokuja kuzuga kwa kumkisi, yesu akamkata kabda hajatoka karibu nae akwambia una msaliti mwana wa adamu kwa kumkisi.
You must be kidding! Yesu alifundisha maporini?

Luka 23:2
Wakaanza kumshitaki, wakisema, "Tumemwona huyu akipotosha taifa letu, na kuwazuia watu wasimpe Kaisari kodi, akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo Mfalme."


Kama hawakumjua ni nani, na alishinda porini akisali; walimwonaje akipotosha watu wasilipe kodi?
 
Ikiwa Mungu anafanya mambo yote kwa shauri na mapenzi yake, utasemaje una freewill ya kuchagua unachotaka?
Wewe unapofanya mambo yako kwa uhuru inamaanisha sisi wengine hatupo huru?

Mungu anatumia uhuru wake kufanya mema, sisi nasi tunatumia uhuru wetu kadiri tupendavyo.

Kila mmoja anashinda mechi zake.
 
Tulikuwa na concept ya freewill, tukaingiza predestination; unataka tuongeze concept ya tatu - determinism? Mbona tutakesha sasa. 😁
Hili sio jambo la kuongezwa, ni jambo ambalo lipo na linafungama na sifa za Mungu wako otherwise umpunguze sifa Mungu ili tui exclude hiyo hoja hapa

Kwa sifa za Mungu ni kwamba kila kitu kilishakuwa calculated na hapa tunapita njia aliyotuwekea sisi japo katika fikra zetu tunaweza hisi tunafanya mambo kwa utashi wetu Refer katika ile verse ya ephisians.

Sasa kama kila kitu kinachotokea hakitokei kwa bahati mbaya, ipi nafasi ya mtu kuwa responsible kwa matendo ayafanyayo wakati tayari alikwisha umbwa aje afanye hayo aliyofanya?
 
Wewe kwa mfano kama unajua Juma asiposoma atafeli na akisoma atafaulu kunamzuiaje Juma kusoma na akafaulu au kutokusoma na akafeli?
Mfano wako hauko relevant

Kwasababu ujuzi wangu sio wa uhakika, pili swala la juma kutosoma sio uamuzi wake maana alikwisha pangiwa asije kusoma tangu hata hajazaliwa na hakuweza kuepuka hilo

Niambie kwa namna gani Juma angeweza kutumia freewill ya kusoma na kufaulu ikiwa Mungu alikwisha mpangia tangu hajazaliwa?

Ubaya na wema ni matokeo ya freewill

Sasa mama mjamzito anayetoa mimba kwa kukiua kichanga tumboni halafu Mungu alikwisha kujua hilo na alikuwa na uwezo wa kulizuia lakini akaruhusu litokee kwasababu ya freewill

Kama Mungu anajali freewill, ni ipi nafasi ya hicho kichanga kutumia freewill kati ya kuchagua kuuliwa au kutouliwa?
 
Kama Mungu anaingilia mambo ya wengine na kama hakuna freewill basi kusingekuwa na uovu.

Uovu upo kwa kuwa mnatumia freewill zenu kuamua kuwa waovu.

Hakuna anayekupangia.
Unatumia ubaya kufanya mazuri yaonekane mazuri

Kwani haiwezekani kuwa na freewill yenye kuchagua mazuri pekee?
 
Wewe unapofanya mambo yako kwa uhuru inamaanisha sisi wengine hatupo huru?

Mungu anatumia uhuru wake kufanya mema, sisi nasi tunatumia uhuru wetu kadiri tupendavyo.

Kila mmoja anashinda mechi zake.
Verse haizungumzii uhuru wa Mungu kwenye mambo yake, imnazungumzia nafasi ya Mungu katika kuwapangia watu mambo yote kwa mapenzi yake

Mungu anayewachagulia watu kwa kusudi lake, hao watu waliochaguliwa kwenye mambo fulani utasemaje wametumia freewill kuchagua hayo waliyo chaguliwa?
 
Davinci naona unayachakata mawazo mithili ya Tafakuri na tungo za dan brown ndani ya code ya maria magdalena kukimbilia ulaya/ufaransa na ujauzito wa bwana Yeshua/Yesu Mnazeleti na uzaoo wake upo hadi hivi sasa-holy grail' (Mark 16-8 ):



Project yangu ipo mbioni kumalizika "ALISINA UTACHOMWA MOTO NAKUAPIA"

Huku miaka mitano Ijayo Project ya "FREEDOM FROM RELIGION FOUNDATION -TANZANIA"
 
Kujua kwa Mungu mambo yote hata kabla sijazaliwa kunanizuia kufanya mimi nayo taka unless niwe na option ya kufanya kile ambacho yeye hajakiona au kwenda kinyume na alivyoona

Kupitia mfano wa calvin aliyeua makumi ya watu. Sasa kama mimi tu nimetengeneza madai lakini hakuna mtu yeyote rational ambaye ameweza kuniamini kuwa sihusiki na mauaji hayo aliyosababisha calvin na kuwa sikujua kitachokwenda kutokea baadaye

If this is what people would think about me, then what should we think about God?
Unathibitisha ya kuwa mfano wako si halisi. Swali langu la msingi unalotakiwa kujibu ni kuwa kujua kwake kuna kuzuia nini wewe kufanya unalo taka ?

Mola wetu kwa kutuumba sisi na kutujua vizuri nje ndani anajua cha kabla na baadae, mfano mwepesi sana, wewe lro hii kwa kumjua kwako vizuri mtu fulani basi huwa unajua nini atafanya baada ya jambo fulani.

Sasa hapo ndipo ulipo uhuru kamili wa mwanadamu, Allah anajua kila kitu ana uwezo wa kila kitu, lakini anakuacha ufanye unachotaka sababu amekupa uhuru ila angetaka kuzuia angezuia.
 
Kabla ya kuzaliwa kwako Mungu akijua utaua, una option ya kutoua?

Kama huna option ya kutoua utasemaje sijazuliwa kufanya nachotaka?
Options zipo kibao, kuna kuomba dua Mola akuepusha na madhila. Ndiyo maana huwa tunaomba msamaha kwa makosa tunayofanya na kusamehewa, na dua hubadilisha aliyokupangia Mola.
 
Unathibitisha ya kuwa mfano wako si halisi. Swali langu la msingi unalotakiwa kujibu ni kuwa kujua kwake kuna kuzuia nini wewe kufanya unalo taka ?

Mola wetu kwa kutuumba sisi na kutujua vizuri nje ndani anajua cha kabla na baadae, mfano mwepesi sana, wewe lro hii kwa kumjua kwako vizuri mtu fulani basi huwa unajua nini atafanya baada ya jambo fulani.

Sasa hapo ndipo ulipo uhuru kamili wa mwanadamu, Allah anajua kila kitu ana uwezo wa kila kitu, lakini anakuacha ufanye unachotaka sababu amekupa uhuru ila angetaka kuzuia angezuia.
Unashindwa kuelewa jambo

Ni kwamba katika concept ya freewill na dhana ya Mungu mjuzi wa yote, muweza wa yote na mwenye upendo wote.

Tunasema freewill ni illusion kwasababu kila kitu kilipangwa though the choice may seem very free for you but in reality you're choice cannot be otherwise
 
Options zipo kibao, kuna kuomba dua Mola akuepusha na madhila. Ndiyo maana huwa tunaomba msamaha kwa makosa tunayofanya na kusamehewa, na dua hubadilisha aliyokupangia Mola.
Hapa ndipo unapojichanganya

Kuomba kwako dua kutakuwa ni kitu kipya kitachoweza kubadilisha maono ya Mungu?

Kuomba kwako msamaha nako sio kwa utashi wako, na hata ukibadilishiwa hiyo itaonekana hivyo katika perception yako lakini uhalisia ni kuwa yeye ndiye alitaka iwe hivyo
 
Free will ni uhuru wa kuchagua mema na mabaya, wote tunakubaliana na tafsiri hiyo.

Na kwamba ubaya unatokea kwasababu kuna freewill na bila freewill kusingekuwa na raha kwasababu watu wangeishi kama robots

Anyway. Peponi kuna freewill au haipo?
Nitajibu;

Ndiyoni freewill ni kuchagua mema na yasiyo mema kwetu, kuchagua kwenda left ama right wewe tu na utaendelea kuyapata matokeo kadri ya unavyochagua.

Ndiyo, ubaya ni matokeo ya makosa katika chaguzi zetu, na mda mwingine unatufunza kuwa njia ile ya mwanzo sio sahihi, tubadilike/tubadilishe.

Na ipo popote utakapokuwa utakuwa na freewill [hadi levo fulani za mbinguni] kulingana na mazingira utakayokuwapo [mfano huwezi kuamua tu kupaa ukiwa duniani], free will ni sifa zetu wanaadamu na baadhi ya viumbe wengine wa Mungu. Ndiyo maana kuna mahala Yesu alisisitiza sana kuwa tutumie utashi wetu kuyafanya mapenzi ya baba wa Mbinguni. Kumbe hata yeye angeweza kutotii kukinywa kikombe kama angeamua hivyo ila akaamua kutumia utashi wake kukubali kuyatenda mapenzi ya Baba yake. Maana huo ni mfano mzuri wa kujitoa kwa upendo kusema ukweli hata kama maisha ya matatani.
 
Back
Top Bottom