Haiwezekani Mungu asimuue Shetani halafu aamuru Watu waue wanaofanya mambo ya kishetani; Haiingii akilini

Haiwezekani Mungu asimuue Shetani halafu aamuru Watu waue wanaofanya mambo ya kishetani; Haiingii akilini

Hapana sijasoma Makerere nimepita MIT kidogo tu miaka miwili nikarudi bongo. Nimepata ka exposure kadogo kupitia Seminary (8 years) na kusoma vitabu vingi. Ndio maana huwa siyumbishwi kifara.
Ingekua uyumbushwi ungekua umeacha legacy kama wakina einstein au newton ambao vizazi na vizazi wanajifunza tofauti na hapo huna uspecial wowote ambao unataka uaminishe watu

Mtu unaona ufahari kusema umesoma MIT alafu unasema huyumbishwi
sisi wafrika tunayumbwishwa ndo maana hata elimu tunayosoma ni kutoka western mfano wewe unajiita francisco huko tayari ni kuyumbishwa kwanin msitumie jina lako la kibantu mwafrika ana safari ndefu sana katika huu ulimwengu
 
HAIWEZEKANI MUNGU ASIMUUE SHETANI ALAFU AAMURU WATU WAUE WANAOFANYA MAMBO YA KISHETANI; HAIINGII AKILINI!

Anaandika, Robert Heriel
Kuhani

Kwenye nyumba za ibada tangu tukiwa Watoto tulifundishwa kuna Wahusika Wawili mahasimu, wakwanza anaitwa MUNGU na wapili anaitwa SHETANI.

Mhusika Mungu huyu tuliambiwa ndiye Muumbaji wa Mbingu na Nchi, na ndiye Baba yetu (Chanzo chetu). Huyu tukaambiwa pia ni Mwema, mwenye upendo, nguvu na uweza. Chanzo chake hatujaelezewa, na hata wanaotuelezea habari zake hawajawahi kumuona. Hii ni kumaanisha hawajui anafananaje.

Mhusika Shetani huyu amepewa uhusika mbaya Kwa kusemekana alimuasi Mhusika MUNGU, asili ya Shetani wapo waliosema ni Jamii ya Malaika waitwao Makerubi, ambaye jina lake ni Lucifer. Wakati wengine wakidai Shetani au Ibilisi asili yake ni Kutoka Koo za majinni. Hii ni kusema Shetani ni kiumbe kilichoumbwa na Mungu. Ingawaje Stori hizi mbili hazijakamilika na zinaacha maswali mengi kuliko kilichoelezwa.

Lusifa kama aliasi, aliasi sheria ipi miongoni MWA sheria za Muumba wake huko Mbinguni?

Kabla hajaasi hiyo sheria ilitamka kuwa adhabu ya kuasi ni ipi?

Stori za Shetani zimeanzia juujuu na kuishia juujuu kama Stori za masela WA vijiweni. Yaani Stori imeanzia Kati na kuishi katikati.

Tukirudi kwenye Hoja.
Wasimulizi WA hizi dini zakuletwa na Waandishi wa vitabu vyao ambavyo vimeandika habari za huyo Mungu na Shetani Kwa uchache Mno, wakaja na sheria, ni kama sheria za biashara ya Market zile za Qnet. Unawekeza Kwa Imani pasipo kuuliza maswali yenye kufikiri, ATI hivyo ndio namna ya Kupata faida kwenye biashara.

Vitabu vya Dini vinaeleza kuwa Shetani ndiye chanzo cha dhambi, inakazia zaidi kuwa kila dhambi ifanywayo na binadamu chanzo chake ni Shetani kwani Shetani ndiye anayeshawishi Watu au viumbe kufanya Uasi.

Ukisoma kwenye Quran au Biblia yapo Makosa MTU akifanya anatakiwa kuuawa kama adhabu.
Mfano WA Makosa hayo ni kama kuua, kuwa Shoga au msagaji, kulala na mnyama, kuzini na mama mzazi au Baba mzazi au mkwe au mtoto wako. Kumkufuru Mungu na kuwa mchawi au mshirikina. Na Makosa mengine mengi yenye kustahili adhabu ya kifo Kwa mujibu wa vitabu vya Dini.

Swali linakuja, Ikiwa mhusika Mungu wa kwenye vitabu hivyo vya Dini, aliamuru Watu kuwaua Watu wenzao wanaofanya Makosa au dhambi nzito kama zilivyotajwa, ni Kwa nini huyu Mungu asingeshughulika na Shetani mwenyewe ambaye ndiye anawafanya Watu WAUE, wawe mashoga, na kufanya zinaa chafu ya kiwango cha juu?

Kwa sababu kama kweli Mungu hakutaka Dunia iwe na uovu kama ni kweli Kabisa basi ni dhahiri angedili na chanzo ambacho vitabu vya Dini vinamtaja ni mhusika Shetani.

Haiingii akilini badala ya kumuua Shetani ambaye ndiye chanzo cha Watu kufanya uovu mkubwa, ATI uwaamuru hao Watu wawaue Watu wenzao wanaofanya Matendo ya kishetani yaani wanaomfuata Shetani ambaye wamezaliwa wamemkuta na watakufa watamuacha. Hakuna mantiki kabisa ya Jambo Hilo.

Nafikiri Vitabu vya Dini vinashindwa kueleza ukweli Kati ya huu;
1. Binadamu ndio Shetani wenyewe. Lakini wametafuta Shetani bandia asiyeonekana ili wamsingizie.
Hoja hii haina nguvu Kwa sababu Mwanadamu hawezi kupambana na Mungu au Shetani yaani hawezi kupambana na matamanio yake yaliyomo katika Akili yake. Kwani matamanio na utashi ndio humuongoza MTU.

2. Mungu na Shetani ni Mhusika mmoja. Yaani Mungu ndiye Shetani na Shetani ndiye huyohuyo Mungu.
Vitabu vya Dini vinashindwa kuelezea ukweli huu labda Kwa kuogopa kuyafanya Maisha yataonekana hayana maana. Jambo ambalo nikweli kuwa Maisha ni ubatili.

Kama Mungu ndiye muumba wa yote na muweza WA yote tafsiri yake Ipo wazi kabisa.
Hii ni kusema, Mungu hawezi kumuua Shetani Wakati yeye ndiye huyohuyo Shetani. Na Shetani hawezi kumuua Mungu Wakati yeye ndiye huyohuyo Mungu.

Hoja hii inanguvu Kwa sababu, hata vitabu vya Dini vinaeleza kuwa Mungu aliumba Mema na Mabaya (ushetani) lakini akamwambia Mwanadamu achague Mema ili aweze kuishi.

Kumaanisha upande mzuri au Mwema wa Muumbaji wetu ndio wanadini waliuita Mungu na upande Mbaya wa Muumbaji wetu wakauita Shetani. Ni kama vile USO na kisogo ambavyo vyote vipo Kwa mhusika mmoja.

Haiwezekani Lusifa Awe Muasi hivihivi, lazima tujiulize huo Uasi ulitoka wapi ikiwa sio Kwa Muumbaji wake? Kwa sababu kiumbe hakina uwezo wa kuumba Jambo lolote liwe zuri au liwe Baya.

Taikon pumzika sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Unafikir mwalimu wako shuleni alishindwa kuwapa matokeo ya A bila kufanya mtihani. Why mlitakiwa kufany mtihani?
 
Yaani isingekuwa kuzikana watu wenye akili timamu wasingekuwa wanaenda kanisani na misikitini
Tunajiunga na hivi vyama vikubwa vya kidini yaani ukristo, uislam na budha kwasababu tunataka kuzikwa kwa heshima sisi pamoja na watoto na ndugu zetu, dini ni kama chama tu kama vile ccm na cuf.
 
HAIWEZEKANI MUNGU ASIMUUE SHETANI ALAFU AAMURU WATU WAUE WANAOFANYA MAMBO YA KISHETANI; HAIINGII AKILINI!

Anaandika, Robert Heriel
Kuhani

Kwenye nyumba za ibada tangu tukiwa Watoto tulifundishwa kuna Wahusika Wawili mahasimu, wakwanza anaitwa MUNGU na wapili anaitwa SHETANI.

Mhusika Mungu huyu tuliambiwa ndiye Muumbaji wa Mbingu na Nchi, na ndiye Baba yetu (Chanzo chetu). Huyu tukaambiwa pia ni Mwema, mwenye upendo, nguvu na uweza. Chanzo chake hatujaelezewa, na hata wanaotuelezea habari zake hawajawahi kumuona. Hii ni kumaanisha hawajui anafananaje.

Mhusika Shetani huyu amepewa uhusika mbaya Kwa kusemekana alimuasi Mhusika MUNGU, asili ya Shetani wapo waliosema ni Jamii ya Malaika waitwao Makerubi, ambaye jina lake ni Lucifer. Wakati wengine wakidai Shetani au Ibilisi asili yake ni Kutoka Koo za majinni. Hii ni kusema Shetani ni kiumbe kilichoumbwa na Mungu. Ingawaje Stori hizi mbili hazijakamilika na zinaacha maswali mengi kuliko kilichoelezwa.

Lusifa kama aliasi, aliasi sheria ipi miongoni MWA sheria za Muumba wake huko Mbinguni?

Kabla hajaasi hiyo sheria ilitamka kuwa adhabu ya kuasi ni ipi?

Stori za Shetani zimeanzia juujuu na kuishia juujuu kama Stori za masela WA vijiweni. Yaani Stori imeanzia Kati na kuishi katikati.

Tukirudi kwenye Hoja.
Wasimulizi WA hizi dini zakuletwa na Waandishi wa vitabu vyao ambavyo vimeandika habari za huyo Mungu na Shetani Kwa uchache Mno, wakaja na sheria, ni kama sheria za biashara ya Market zile za Qnet. Unawekeza Kwa Imani pasipo kuuliza maswali yenye kufikiri, ATI hivyo ndio namna ya Kupata faida kwenye biashara.

Vitabu vya Dini vinaeleza kuwa Shetani ndiye chanzo cha dhambi, inakazia zaidi kuwa kila dhambi ifanywayo na binadamu chanzo chake ni Shetani kwani Shetani ndiye anayeshawishi Watu au viumbe kufanya Uasi.

Ukisoma kwenye Quran au Biblia yapo Makosa MTU akifanya anatakiwa kuuawa kama adhabu.
Mfano WA Makosa hayo ni kama kuua, kuwa Shoga au msagaji, kulala na mnyama, kuzini na mama mzazi au Baba mzazi au mkwe au mtoto wako. Kumkufuru Mungu na kuwa mchawi au mshirikina. Na Makosa mengine mengi yenye kustahili adhabu ya kifo Kwa mujibu wa vitabu vya Dini.

Swali linakuja, Ikiwa mhusika Mungu wa kwenye vitabu hivyo vya Dini, aliamuru Watu kuwaua Watu wenzao wanaofanya Makosa au dhambi nzito kama zilivyotajwa, ni Kwa nini huyu Mungu asingeshughulika na Shetani mwenyewe ambaye ndiye anawafanya Watu WAUE, wawe mashoga, na kufanya zinaa chafu ya kiwango cha juu?

Kwa sababu kama kweli Mungu hakutaka Dunia iwe na uovu kama ni kweli Kabisa basi ni dhahiri angedili na chanzo ambacho vitabu vya Dini vinamtaja ni mhusika Shetani.

Haiingii akilini badala ya kumuua Shetani ambaye ndiye chanzo cha Watu kufanya uovu mkubwa, ATI uwaamuru hao Watu wawaue Watu wenzao wanaofanya Matendo ya kishetani yaani wanaomfuata Shetani ambaye wamezaliwa wamemkuta na watakufa watamuacha. Hakuna mantiki kabisa ya Jambo Hilo.

Nafikiri Vitabu vya Dini vinashindwa kueleza ukweli Kati ya huu;
1. Binadamu ndio Shetani wenyewe. Lakini wametafuta Shetani bandia asiyeonekana ili wamsingizie.
Hoja hii haina nguvu Kwa sababu Mwanadamu hawezi kupambana na Mungu au Shetani yaani hawezi kupambana na matamanio yake yaliyomo katika Akili yake. Kwani matamanio na utashi ndio humuongoza MTU.

2. Mungu na Shetani ni Mhusika mmoja. Yaani Mungu ndiye Shetani na Shetani ndiye huyohuyo Mungu.
Vitabu vya Dini vinashindwa kuelezea ukweli huu labda Kwa kuogopa kuyafanya Maisha yataonekana hayana maana. Jambo ambalo nikweli kuwa Maisha ni ubatili.

Kama Mungu ndiye muumba wa yote na muweza WA yote tafsiri yake Ipo wazi kabisa.
Hii ni kusema, Mungu hawezi kumuua Shetani Wakati yeye ndiye huyohuyo Shetani. Na Shetani hawezi kumuua Mungu Wakati yeye ndiye huyohuyo Mungu.

Hoja hii inanguvu Kwa sababu, hata vitabu vya Dini vinaeleza kuwa Mungu aliumba Mema na Mabaya (ushetani) lakini akamwambia Mwanadamu achague Mema ili aweze kuishi.

Kumaanisha upande mzuri au Mwema wa Muumbaji wetu ndio wanadini waliuita Mungu na upande Mbaya wa Muumbaji wetu wakauita Shetani. Ni kama vile USO na kisogo ambavyo vyote vipo Kwa mhusika mmoja.

Haiwezekani Lusifa Awe Muasi hivihivi, lazima tujiulize huo Uasi ulitoka wapi ikiwa sio Kwa Muumbaji wake? Kwa sababu kiumbe hakina uwezo wa kuumba Jambo lolote liwe zuri au liwe Baya.

Taikon pumzika sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Kama unaamin shetani anahusika kweny maovu kwann serikali hutoa hukum ya kunyongwa kwa muuaji why shetani asihukumiwe?


uongeza. Someni dini ndo mje kureason.
 
Unafikir mwalimu wako shuleni alishindwa kuwapa matokeo ya A bila kufanya mtihani. Why mlitakiwa kufany mtihani?
Mkuu kwa hiyo mungu anatufanyia majaribio wakati alituumba mwenyewe, na anajua hatma zetu, hii ina make sense kweli? Yaani mzazi akuzae alafu akujaribu mwanae yaani akuababishie mateso na ana uwezo mkubwa tu wa kukusaidia, nyie pambaneni na huyo mungu wenu mlioaminishwa na wazungu.
 
Kama unaamin shetani anahusika kweny maovu kwann serikali hutoa hukum ya kunyongwa kwa muuaji why shetani asihukumiwe?


uongeza. Someni dini ndo mje kureason.

Nani kasema anaamini hayo?
Mimi nimesema vitabu vya Dini vinasema(vimeandika) wewe unaeleza vitu tofauti na nilichoeleza
 
Ingekua uyumbushwi ungekua umeacha legacy kama wakina einstein au newton ambao vizazi na vizazi wanajifunza tofauti na hapo huna uspecial wowote ambao unataka uaminishe watu

Sisi wafrika tunayumbwishwa ndo maana hata elimu tunayosoma ni kutoka western mfano wewe unajiita francisco huko tayari ni kuyumbishwa kwanin msitumie jina lako la kibantu mwafrika ana safari ndefu sana katika huu ulimwengu
🚮
 
Kama Mungu angefanya hivi ingeonekana ya kwamba Mungu ni dhaifu,na anamhofia shetani,Kwa hiyo Ili Mungu endelee kuonenekana mkuu Kwa viumbe vyake amemwachilia shetani mpaka mwisho wa nyakati
 
Unafikir mwalimu wako shuleni alishindwa kuwapa matokeo ya A bila kufanya mtihani. Why mlitakiwa kufany mtihani?

Wewe unaweza kutengeneza roboti alafu ukalipa mtihani kisha roboti likifeli unaliadhibu. Wakati huohuo unajua matokeo kuwa litafeli au litafaulu.

Hiyo kitu inakuingia akilini kweli?
 
Kama Mungu angefanya hivi ingeonekana ya kwamba Mungu ni dhaifu,na anamhofia shetani,Kwa hiyo Ili Mungu endelee kuonenekana mkuu Kwa viumbe vyake amemwachilia shetani mpaka mwisho wa nyakati

Mwisho wa nyakati ndio nini?
Wewe utajuaje huu ni mwisho wa nyakati wakati mwanzo hauujui?
Kwa mfano, Kwa uelewa wako WA mambo ya Muda unaweza elewa muda uliopo ni muda gani?
 
Back
Top Bottom