Haiwezekani Mungu asimuue Shetani halafu aamuru Watu waue wanaofanya mambo ya kishetani; Haiingii akilini

Haiwezekani Mungu asimuue Shetani halafu aamuru Watu waue wanaofanya mambo ya kishetani; Haiingii akilini

Kwa hiyo sasa hivi umekubali mungu wako wengi🤣🤣
Mbona unakosa msimamo.

Sihangaiki na Biblia, wewe ndio umeleta Biblia humu ndani. Mada yangu inahusu Mungu na shetani ambao ni Wahusika waliotajwa na vitabu vingi tuu sio Biblia pekeake.

Wewe ndio umeleta Biblia, Mimi nikakujibu kulingana na ulichokileta
Sio kukubali Miungu wako wengi ilo liko wazi kama huangaiki na biblia tutajie huyo Mungu unayesema ni sawa na shetan
 
Kwa hiyo biblia unayosema imeborongwa alafu unaitumia tena kwa kumtuhumu Yahweh ni sawa na shetani samahan unakupaji wa unafki

Wewe ndio umeileta Biblia humu, sasa ninatumia silaha anayoitumia ninayejadiliana naye.
Hujui hata mijadala inavyofanyika au unadhani upo Kanisani hapa?
 
Kama unaamin shetani anahusika kweny maovu kwann serikali hutoa hukum ya kunyongwa kwa muuaji why shetani asihukumiwe?


uongeza. Someni dini ndo mje kureason.
Serikali haimtambui Mungu wala shetani. Haina dini
 
Sio kukubali Miungu wako wengi ilo liko wazi kama huangaiki na biblia tutajie huyo Mungu unayesema ni sawa na shetan

Mungu wa kwenye Vitabu vyenu ambaye hasimu wake ni Shetani kama mada isemavyo. Soma mada vizuri.
Kama Mungu unayemuabudu hasimu wake anaitwa shetani basi ndiye ninayemzungumzia hapa
 
Quran

Al-Hijr 15:26-44

"Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia.
Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,Isipo kuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na walio sujudu.
(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio sujudu?

Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliye muumba kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yenye sura.

(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni! (Waliolaaniwa)

Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.

Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapo fufuliwa.

(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula

Mpaka siku ya wakati maalumu.

Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,ila waja wako waliosafika.

Akasema: hii njia ya kujia kwangu iliyonyooka

Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipo kuwa wale wapotofu walio kufuata.

Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote.

Ina milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu walio tengewa."





 
Mungu yupo na bila shetani dunia ingekuwa inabore, shetani analeta vybez , uwepo wa shetani mitihani wa necta ya mbingu
 
Maisha bila dini inawezekana

Ukikaa ukafikiria, dini ni kitu kilichitengenezwa na binadamu pale ambapo alishindwa kujibu maswali magumu mfano, chanzo cha ulimwengu....

Umeanza kulitambua hilo, big up
Huwa unaandika makala zisizo kichwa wala miguu za kikristo, sasa nimethibitisha kumbe bado huna uelewa wa Mungu. Hoja zako ni za kiwango cha kawaida tu, unahitaji kuelekezwa uelewe, wala hazina ugumu kama unavyodhani. Tutakujibu ili uwe na ufahamu.
 
KISSENDI anaamini Mungu yupo, sio dini, na huyo Mungu ni upendo na matendo mema.
Kissendi Nyanda Ntalima Mpandagoya a.k.a Mkushi, yeye ndio muasisi wa makundi sogozi yanayojulikana kwa jina la Waafrika Tujitambue, ambapo amekuwa akifundisha mambo mbalimbali juu ya historia ya mtu mweusi, namna alivyokuwa kinara wa Mapinduzi ya ustaarabu na teknolojia duniani.

Lakini kutokana na husda na fitna za husda za NYAHUNI au mtu mweupe, akautweza utu wa mtu mweusi na kumsahaulisha kabisa asili yake kwa kutumia dini za Ukristo na Uislam.

NYAHUNI waliwakata mikono watu wote waliotokea kwenye koo za wahunzi.

Hizi harakati zina nia njema sana, lakini sidhani kama zitawafurahisha mabeberu
 
Quran 15:26

Al-Hijr 15:26

"Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia.
Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,Isipo kuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na walio sujudu.
(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio sujudu?

Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliye muumba kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yenye sura.

(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni! (Waliolaaniwa)

Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.

Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapo fufuliwa.

(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula

Mpaka siku ya wakati maalumu.

Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,ila waja wako waliosafishika

Malizia Ile Aya isemayo, aliyemnyoosha Mungu Shetani hawezi mpindisha, na aliyempindisha hawezi kunyooshwa
 
Huyu jamaa ni mfikiriaji mzuri lkn tatizo lake ni moja tu. I mean No offense Robert Heriel Mtibeli

Akipata maswali anajaribu kujibu kwa kufikiria yy mwenyewe, hasomi zaidi wataalam wengine wameandikaje kuhusu anachojiuliza/kufikiria muda huo.

Mie msomaji wake sana, 70% ya anachodhan ni swali jipya kujiuliza huwa naona lishapatiwa majibu na baadhi ya wanazuoni.

So read more Mr Robert
Ajiangalie asijiaminishe sana katika mawa
 
Twende taratibu huwezi ukaruka ruka tu mada ikiwa kweli unataka mjadala.

Sawasawa.

Embu tuambie Kabla Ibilisi hajaasi Mungu hakujua Ibilisi ataasi?
Kama alijua, ni Nani aliyeweka Uasi ndani ya Ibilisi maana Ibilisi ni kiumbe tuu, ameumbwa.
Ni kama Mimi na wewe
 
Jibu tunalipata kuwa kwanini MUNGU hakumuua ibilis palepale baada ya kumuasi? Ni kuwa Mungu hana desturi ya kuangamiza viumbe tu kwa kuvionea, huwa ana kawaida ya kuvipa muda kwanza ili kuona kama huenda vikarejea katika njia. Iblis nae amepewa muda mara baada ya kuona kuwa amehukumiwa upotovu...hakuona Toba kama adam alivyokuja kukosea na kula tunda la mti aliokatazwa...IBLIS aliomba apewe uhai mrefu tu ili aje kutimiza lengo lake la kuvipoteza vizazi vya adam.

Mungu alilijua hili na alimtaarifu mapema Adam na mkewe Hawa, kuwa Iblis ni adui yenu basi nanyi mfanyeni kuwa ni adui.

Hivyo Iblis bado ana muda mrefu wa kuishi ulimwenguni, sisi tutakufa tutamuacha mpaka wakati wake nae utakapofika wa kufa
 
HAIWEZEKANI MUNGU ASIMUUE SHETANI ALAFU AAMURU WATU WAUE WANAOFANYA MAMBO YA KISHETANI; HAIINGII AKILINI!

Anaandika, Robert Heriel
Kuhani

Kwenye nyumba za ibada tangu tukiwa Watoto tulifundishwa kuna Wahusika Wawili mahasimu, wakwanza anaitwa MUNGU na wapili anaitwa SHETANI.

Mhusika Mungu huyu tuliambiwa ndiye Muumbaji wa Mbingu na Nchi, na ndiye Baba yetu (Chanzo chetu). Huyu tukaambiwa pia ni Mwema, mwenye upendo, nguvu na uweza. Chanzo chake hatujaelezewa, na hata wanaotuelezea habari zake hawajawahi kumuona. Hii ni kumaanisha hawajui anafananaje.

Mhusika Shetani huyu amepewa uhusika mbaya Kwa kusemekana alimuasi Mhusika MUNGU, asili ya Shetani wapo waliosema ni Jamii ya Malaika waitwao Makerubi, ambaye jina lake ni Lucifer. Wakati wengine wakidai Shetani au Ibilisi asili yake ni Kutoka Koo za majinni. Hii ni kusema Shetani ni kiumbe kilichoumbwa na Mungu. Ingawaje Stori hizi mbili hazijakamilika na zinaacha maswali mengi kuliko kilichoelezwa.

Lusifa kama aliasi, aliasi sheria ipi miongoni MWA sheria za Muumba wake huko Mbinguni?

Kabla hajaasi hiyo sheria ilitamka kuwa adhabu ya kuasi ni ipi?

Stori za Shetani zimeanzia juujuu na kuishia juujuu kama Stori za masela WA vijiweni. Yaani Stori imeanzia Kati na kuishi katikati.

Tukirudi kwenye Hoja.
Wasimulizi WA hizi dini zakuletwa na Waandishi wa vitabu vyao ambavyo vimeandika habari za huyo Mungu na Shetani Kwa uchache Mno, wakaja na sheria, ni kama sheria za biashara ya Market zile za Qnet. Unawekeza Kwa Imani pasipo kuuliza maswali yenye kufikiri, ATI hivyo ndio namna ya Kupata faida kwenye biashara.

Vitabu vya Dini vinaeleza kuwa Shetani ndiye chanzo cha dhambi, inakazia zaidi kuwa kila dhambi ifanywayo na binadamu chanzo chake ni Shetani kwani Shetani ndiye anayeshawishi Watu au viumbe kufanya Uasi.

Ukisoma kwenye Quran au Biblia yapo Makosa MTU akifanya anatakiwa kuuawa kama adhabu.
Mfano WA Makosa hayo ni kama kuua, kuwa Shoga au msagaji, kulala na mnyama, kuzini na mama mzazi au Baba mzazi au mkwe au mtoto wako. Kumkufuru Mungu na kuwa mchawi au mshirikina. Na Makosa mengine mengi yenye kustahili adhabu ya kifo Kwa mujibu wa vitabu vya Dini.

Swali linakuja, Ikiwa mhusika Mungu wa kwenye vitabu hivyo vya Dini, aliamuru Watu kuwaua Watu wenzao wanaofanya Makosa au dhambi nzito kama zilivyotajwa, ni Kwa nini huyu Mungu asingeshughulika na Shetani mwenyewe ambaye ndiye anawafanya Watu WAUE, wawe mashoga, na kufanya zinaa chafu ya kiwango cha juu?

Kwa sababu kama kweli Mungu hakutaka Dunia iwe na uovu kama ni kweli Kabisa basi ni dhahiri angedili na chanzo ambacho vitabu vya Dini vinamtaja ni mhusika Shetani.

Haiingii akilini badala ya kumuua Shetani ambaye ndiye chanzo cha Watu kufanya uovu mkubwa, ATI uwaamuru hao Watu wawaue Watu wenzao wanaofanya Matendo ya kishetani yaani wanaomfuata Shetani ambaye wamezaliwa wamemkuta na watakufa watamuacha. Hakuna mantiki kabisa ya Jambo Hilo.

Nafikiri Vitabu vya Dini vinashindwa kueleza ukweli Kati ya huu;
1. Binadamu ndio Shetani wenyewe. Lakini wametafuta Shetani bandia asiyeonekana ili wamsingizie.
Hoja hii haina nguvu Kwa sababu Mwanadamu hawezi kupambana na Mungu au Shetani yaani hawezi kupambana na matamanio yake yaliyomo katika Akili yake. Kwani matamanio na utashi ndio humuongoza MTU.

2. Mungu na Shetani ni Mhusika mmoja. Yaani Mungu ndiye Shetani na Shetani ndiye huyohuyo Mungu.
Vitabu vya Dini vinashindwa kuelezea ukweli huu labda Kwa kuogopa kuyafanya Maisha yataonekana hayana maana. Jambo ambalo nikweli kuwa Maisha ni ubatili.

Kama Mungu ndiye muumba wa yote na muweza WA yote tafsiri yake Ipo wazi kabisa.
Hii ni kusema, Mungu hawezi kumuua Shetani Wakati yeye ndiye huyohuyo Shetani. Na Shetani hawezi kumuua Mungu Wakati yeye ndiye huyohuyo Mungu.

Hoja hii inanguvu Kwa sababu, hata vitabu vya Dini vinaeleza kuwa Mungu aliumba Mema na Mabaya (ushetani) lakini akamwambia Mwanadamu achague Mema ili aweze kuishi.

Kumaanisha upande mzuri au Mwema wa Muumbaji wetu ndio wanadini waliuita Mungu na upande Mbaya wa Muumbaji wetu wakauita Shetani. Ni kama vile USO na kisogo ambavyo vyote vipo Kwa mhusika mmoja.

Haiwezekani Lusifa Awe Muasi hivihivi, lazima tujiulize huo Uasi ulitoka wapi ikiwa sio Kwa Muumbaji wake? Kwa sababu kiumbe hakina uwezo wa kuumba Jambo lolote liwe zuri au liwe Baya.

Taikon pumzika sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Acha makufuru

wewe ni binadamu tu unayekunya na kuharisha limited with time, you are not worthy of questioning an eternal God's wisdom.
 
Mwambie mara ngapi Watu wameambiwa wamlete Shetani au Mungu Mahakamani na wakashindwa,
Kumaanisha wakosaji ni wao wenyewe Ila wanasingizia wengine wasiohusika.
Naomba kujua kwanza

Je unaamini katika uislamu au ukristo

Maana huwezi jadili habari za Mungu na Sheteni ilihali wewe huamini kama kuna Mungu na Shetani!

Na kama unaamini je hujui mipaka ya kuhoji habari za Mungu na Shetani katika dini yako?
 
Sawasawa.

Embu tuambie Kabla Ibilisi hajaasi Mungu hakujua Ibilisi ataasi?
Kama alijua, ni Nani aliyeweka Uasi ndani ya Ibilisi maana Ibilisi ni kiumbe tuu, ameumbwa.
Ni kama Mimi na wewe
Mungu ni mjuzi wa yaliyopita na yajayo. Anajua matendo watakayotenda viumbe wake kabla hata ya kuwaumba.

Wanaadamu na majini wameumbwa ndani yao wakiwa na Roho na Nafsi. Nafsi ndio mimi na wewe....hii nafsi imepewa uchaguzi wa kutenda iwe mema au mabaya, kuamini au kukufuru.

Mungu alichofanya ni kuibainishia nafsi matendo mabaya na mazuri kisha akaipa uhuru wa kuchagua inataka kufata kipi ila akaionya kuwa katika kila chaguzi mwisho wake itakutana na pepo ama moto.

So mwanadamu na jini wana haki ya kutenda wanalolitaka ila mwisho watalipwa kwa yale waliyoyachagua.
 
Back
Top Bottom