Hakuna Taifa lililoendelea kwa kujipendekeza na kujidharau

Paragraph iko wapi wewe mbuzi.


Mimi naona lundo la maandishi. Takataka kabisa
Mropokaji weye! Na mvivu wa kusoma. Kama mimi mbuzi weye utakuwa nani? Heri mbuzi kuliko Binadamu asiye jitambua na mwenye akili fupi. Mbuzi ni moja ya wanyama wenye akili na wasafi.
Kuliko mtu aloumbwa lakini mbuzi anamzidi kwa maarifa. Kwa sababu hujitambui na unadhani kutukana ndo solution katika maisha.
Kwanza kujibizana nawe ni kupoteza muda, mtu alie punguani udhani matusi ndo mtaji.
 
Haya. Tumekusikia. Unanung'unika, kuuma na kupuliza. Mataga na wana-Lumumba mupo na hoja?
Sina haja ya kuwa mataga wala Lumumba. Na sijawahi ikanyaga hata hiyo Lumumba. Na sina utimu. Nipo zangu nje naendelea na maisha yangu. Sihitaji timu yoyote wala ushabiki.
 
Wataishia kukutukana ila haohao ndio watakuwa wa kwanza kulalamika maana wanaishi kwa ndoto hewa
 
Hiyo ipo wazi watanzania mnawatetemekea wakenya. Na wakenya ulijua hilo, ndo maana wanawadharau watanzania. katika mikataba iliyosainiwa unadhani anae enda kufaidi ni nani? Kenya wameshinda.
 
Na Hakuna Taifa litakaloendelea likijingia ndani peke yake kana Kwamba liko kisiwani.

Mataifa yanategemeana katika kuyafikia maendeleo.
 
Na Hakuna Taifa litakaloendelea likijingia ndani peke yake kana Kwamba liko kisiwani.

Mataifa yanategemeana katika kuyafikia maendeleo.
Hakuna alie sema Tanzania ijifungie nadhani ujaelewa mada. Tanzania imekuwa na ushirikiano wa nchi zingine kwa muda mrefu na hata wakati wa Magufuli balozi nyingi zilifunguliwa hadi balozi wa Isarael amabo nyerere aliufunga. Tusipotoshe!
 
labda mkuu wewe ungependekeza afanyaje?!!
au unaijua mipango yake yote kwamba kwanini kenya na baada ya kenya ataenda wapi na kwanini n.k?
 
Hizo enzi unazoziongelea ni takriban miaka 50 iliyopita na pamoja na hayo mengine uliyoelezea hapo juu kwa ufupi nakumbuka na yafuatayo ambayo ni vyema pia yakatumika kuweka sawa muktadha wa zama unazoziongelea:

(i) chama cha siasa kilikuwa ni kimoja peke yake na kilikuwa kimeshika hatamu,
(ii) njia kuu za uchumi zilikuwa chini ya usimamizi wa serikali na wafanyabiashara wachache wenye asili ya mashariki ya kati na Kiasia - tulinunua sukari kwa kibali cha DC na kwa sisi tuliokulia vijijini tulishuhudia mashamba ya ushirika ya vijiji ambayo yalilimwa na wananchi wote ila mazao yake walijua viongozi yalipopelekwa.
(iii) hakukuwa na TV na ilikuwa marufuku kuinunua isipokuwa kwa kibali,
(iv) hakukuwa na radio binafsi,
(v) hakukuwa na magazeti binafsi,
(vi) hakukuwa na mobile phones wala mtandao (internet),
(vii) nchi kadhaa za afrika zilikuwa bado kwenye ukoloni mkongwe,
(viii) TV zilikuwa hakuna pasi na kibali maalum, Magari yalikuwa ya Serikali (Landrover 109 series) na ya wafanya biashara wachache wenye asili ya kiarabu na kiasia,
(ix) Mipaka ya majirani ilikuwa imefungwa; yaani mipaka ya nchi za Kenya Uganda, Rwanda, Burundi, Malawi, Msumbiji sikumbuki vyema kuhusu Zambia kwani ilikuwa nchi rafiki
(x) siasa zilizokuwepo zilikuwa za ujamaa na Kujitegemea.
(xi) nchi likuwa na raia takriban milioni 10.
(xii) Kulikuwa na pande tatu kubwa kwenye siasa za kimataifa - yaani Magharibi ikiongozwa na Marekani (Mabepari), Mashariki ikiongozwa na urusi (Wasoshalisti) na nchi zisizofungamana na upande wowote - nyingi zikiwa nchi za ulimwengu wa tatu na sisi tulikuwa wanachama. Hii ilitumika kama mbinu ya kidiplomasia ya kuweza kushirikiana na pande zote mbili zilizokuwa zinahasimiana.
(xiii) Mashirika ya misaada ya magharibi kama DANIDA, SIDA, USAID yalitamalaki kwenye sekta za elimu, afya, maji etc.

Kwa ufupi hoja ninayojenga ni kuwa huwezi kuendesha nchi leo kwa kutumia mbinu na falsafa za miaka 50 iliyopita. Lazima tuwe na mbinu za karne hii ikiwemo mahusiano ya kimataifa au diplomasia ya kiuchumi (siyo kubembeleza kama unavyodai) na kuvutia mitaji ya kimataifa kuwekeza nchini wakati tukiwajengea watu wetu mitaji ili washiriki kwenye uwekezaji pia.
 
Watanzania TT unajua kuwa nyinyi na kundi lenu mmeanzisha kampeni ya kupinga kila jambo analo fanya mama Samia.

Ila mkae mkijua kuwa huyu ndiye rais wa JMT hakuna jinsi mtaweza kumkwamisha.

Lugha yako hiyo mbona hukuitumia wakati wa mtangulizi wake?
 
Tangu mwaka 2015 ATCL hadi sasa hasara ya 150+billion
Una ubishi wa kitoto. ATCL ilikuwa imekufa, hata hukumbuki juhudi za kuifufua na kuanza biashara ni lini.
 
Wewe unajua maana ya asilimia 70 hau unaboresha umagufulication ulioandika?

Hayo ni mawazo yako hata wakenya nao wanalalamika Uhuru kaiuza Kenya
 
Hakuna Mtu anayekataa kulipa kodi ila iwe kodi inayolipika, hao matajiri unaosema, wanalalamika pia ila huwezi kusikia, hakuna feza za Serikali, feza ni za wananchi na serikali wameiweka wao, Na ni Wananchi wanasema kodi ni nyingi na Kubwa hazilipiki, Raisi amesikia Wananchi anarekebisha.
 
Una ubishi wa kitoto. ATCL ilikuwa imekufa, hata hukumbuki juhudi za kuifufua na kuanza biashara ni lini.
Kwahiyo kuifufua ndiyo green light ya kuwafanya mpate hasara ya 150 billion?

Huu ni ufisadi wa hali ya juu kuwahi kufanyika hapa nchini tanzania.
 
Siasa za Wapinzani hasa Chadema zimeharibu sana hii Nchi Tuzidi kumuomba Mungu manake Mambo ni mengi muda ni Mchache sana Kila nafsi itaonja umauti!!!
Wapiinzani walichoma moto vifaranga vya kenya, wakapiga mnada ng'ombe za wakenya, wakasababisha mahindi ya tanzania yakazuiwa kuingia kenya, wakawatuma wakuu wa mikoa kuleta ubabe mipakani. ili kuharibu ujirani mwema, mwenyekiti wao akasema tutembee kifua mbere maana sisi ni dona kantre
 
Wamarekani wanajishusha? Huwajui wamarekani wewe.

Hofu ya Marekani kuhusu China ni hofu halisi na wala si utani. China ni economic giant kwelikweli hakuna anachoweza marekani ambachi China hawezi. Advantage pekee waliyo nayo wamarekani ni nguvu ya kidiplomasia kutokana na umaarufu wa Marekani wa zamani. Lakini linapokuja suala la uwezo, kile ambacho mmarekani anaweza, China anaweza pia au zaidi. Leo hii China anaweza kufinance projects kubwa kubwa barani Afrika na duniani kote, kitu amabacho Marekani hawezi. Na hilo linawatisha kweli kweli wamarekani.
 
Kwahiyo tujifungie ndani kwa sababu hatuwezi kusimamia sheria na taratibu zetu zilizopo?!?
 

Ni kwa vipi Tanzania imejipendekeza na kujidharau ?
 
Historia itaongea...Uzuri kuna comparisons na tutaweza kupata njia ya tatu bora zaidi baada ya haya kushindwa au kweza kuwa mema
 
Kwahiyo tujifungie ndani kwa sababu hatuwezi kusimamia sheria na taratibu zetu zilizopo?!?
Tunajifungia kwa muda kujenga misingi...Unless tunataka kuwa wasindikizaji kwenye dunia...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…