Hakuna Taifa linaloitwa Palestina liliwahi exists tangu dunia iumbwe kumbe

Hakuna Taifa linaloitwa Palestina liliwahi exists tangu dunia iumbwe kumbe

Hoja zingine ni za kijinga,kwani kabla ya 1961 kulikuwa na Taifa linaitwa Tanganyika?
Ila kulikuwa na watu katika eneo hilo ambapo badaye walikuja kupata uhuru na kuunda Taifa la Tanganyika.

Haiwezekani ukusanye watu kutoka eneo A uwapeleke eneo B kisha hao watu waunde Taifa,huku watu waliokiwepo hapo toka awali wakataliwe kuunda Taifa.
 
Tunawambiaga uku mtaani sisi bado tunasoma wanatukatalia....... tena sisi uku mtaani masomo yetu ni magumu sana atukalili ila lazima uwelewe🚶
 
Soma biblia kijana. Hawakuwa na nchi au sehemu yao maalum.

Wengine walikuwa wanaharamu wa Tamar ambae eti alizaa na baba mkwe wake alipofanya ukahaba, akaja kusingiziwa ndiyo kizazi cha Yesu.
Ni akheri usitumie Biblia kama unataka kusema hakukuwa na taifa la Israeli. Maana kuna mistari lukuki inayoonesha utaifa wa Israeli.

Sasa mtu kuzaa na baba mkwe umeona haiwezekani au? Mbona ni vitu vinatokea hata hapa Tanzania? Sio kila aliyetajwa kwenye Biblia basi ni kielelezo chetu leo. Hata Rahabu alikuwa kahaba lakini yumo kwenye ukoo wa Yesu, hiyo haina maana watu sasa ni ruksa kuwa makahaba.
 
Hoja zingine ni za kijinga,kwani kabla ya 1961 kulikuwa na Taifa linaitwa Tanganyika?
Ila kulikuwa na watu katika eneo hilo ambapo badaye walikuja kupata uhuru na kuunda Taifa la Tanganyika.

Haiwezekani ukusanye watu kutoka eneo A uwapeleke eneo B kisha hao watu waunde Taifa,huku watu waliokiwepo hapo toka awali wakataliwe kuunda Taifa.
Point
 
Wasamaria


Katika mataifa pia ilitakiwa waisrael wawafukuze kipindi waisrael wanarudi kanaani walikuwa ni wasamaria(palestina ya sasa)

Wao kwa makusudi wakaamua kuwaacha na Mungu aliawaonya kuhusu hilo.

Kwa mujibu wa kitabu biblia.

Japo sihalalishi huo ugomvi wa sasa ila huo ni ukweli.
 
HALIJAWAI KUWAPO TAIFA LINALOITWA PALESTINA! NI HAKI YA WA ISRAEL KUKOMBOA ARDHI YAO! Kama hujapita shule au kufuatilia historia huwezi Jua haya

1. Kabla ya Taifa Kuundwa Upya na kuitwa Israel (1948) Lilikuwapo Taifa linaitwa British mandate yaan eneo Lilikuwa chini ya Uingereza 1920-1948 wala siyo Taifa liitwalo Palestina.

2. Kabla ya British Mandate, sehemu Hiyo ilikuwa ni Ottoman Empire (himaya ya Ottoman) (1517-1917), wala si Taifa la Palestinian.

3. Kabla ya Ottoman Empire,ilikuwapo himaya ya Misri yaan Islamic Mamluk Sultanate of Egypt (1250-1517), siyo Taifa la Palestinian.

4. Kabla ya Islamic Mamluk Sultanate of Egypt, lilikuwapo himaya ya Ayyubid Dynasty (1171-1260), wala si Palestina. Godfrey wa Bouillon alilivamia eneo mwaka 1099.

5. Kabla ya Ayyubid Dynasty, ilikuwapo himaya ya kikristo ya Yerusalemu (Christian Kingdom of Jerusalem 1099-1291), wala si Taifa la Palestina.

6.Kabla ya utawala wa kikristo yaan Christian Kingdom of Jerusalem, alikuwapo Fatimid Caliphate (909-1171), siyo la Palestina.

7. Kabla ya Fatimid Caliphate, ilikuwapo himaya ya Byzantine (the Byzantine Empire 330-636), wala si Taifa la Palestina.

8. Kabla ya Byzantine Empire, ilikuwapo tawala ya Rumi, yaan Roman Empire (27 BCE - 476 CE), siyo Palestina.

9. Kabla ya warumi yaan Roman Empire, walikuwapo Hasmonean Dynasty (140-37 BCE), siyo Palestina.

10. Kabla Hasmonean Dynasty,walikuwapo waselekudi yaan Seleucid Empire (312-63 BCE), siyo Palestina state.

11. Kabla ya Seleucid Empire,eneo lilikuwa chini ya Alexander yaan Empire of Alexander the Great (334-323 BCE), wala si Palestina.

12. Kabla ya Alexander the Great, walikuwapo wa pesian the Persian Empire (c. 550-330 BCE), wala si Palestina.

13. Kabla ya hao wa habeshi yaan Persian Empire, walikuwa wa Babylonian Empire (c. 1894-539 BCE),wala si Palestina.

14. Kabla ya Babylonian Empire, eneo lilikuwa chini ya Yusa wa Israel yaan Kingdoms of Israel and Judea (c. 1050-586 BCE), siyo Palestina.

15.Kabla ya Yuda wa Israel yaan Kingdoms of Israel and Judea, eneo lilikuwa himaya ya Israel yaan the Kingdom of Israel (c. 1040-722 BCE), siyo Palestina.

16. Kabla ya Utawala wa Israle yaan kingdom of Israel, yalikuwa makabila 12 ya wa Israel yaan the theocracy of the Twelve Tribes of Israel (c. 1400-1050 BCE), wala si Palestina.

17. Kabla ya Makabila 12 ya Israle yaan theocracy of the Twelve Tribes of Israel, eneo lilikuwa chini ya kanani yaan individual state of Canaan (c. 3000-1200 BCE), wala si Palestina.

Kwa kifupi hakuna Taifa linaloitwa Palestina na halijawai kutokea.

View attachment 3139944

Anaandika TAT kule Twitter (X)
Miaka yote hiyo uliyoitaja ya enzi hizo hakukuwa na taifa lililoitwa Tanzania, leo bila haya mnadai ni nchi yenu na mtailinda kwa udi na uvumba.
Si-support Palestine wala Israel lakini kwa sasa wote wana territories zao na wanastahili haki ya kuishi kwa uhuru.
 
Wasamaria


Katika mataifa pia ilitakiwa waisrael wawafukuze kipindi waisrael wanarudi kanaani walikuwa ni wasamaria(palestina ya sasa)

Wao kwa makusudi wakaamua kuwaacha na Mungu aliawaonya kuhusu hilo.

Kwa mujibu wa kitabu biblia.

Japo sihalalishi huo ugomvi wa sasa ila huo ni ukweli.
Samahani Mkuu!
Unamaanisha Kuwa Wasamaria na Pelishit (Wafilisti) au Wapalestine ni Taifa Moja???

Kama Ni hivyo hauko Sahihi Kulikuwa na Wasamaria na Pia Kulikuw na wafilisti..

Wasamaria walikuwa jamii ya zamani ya Kiyahudi yenye imani zao na mila zao tofauti, na waliishi hasa katika mji wa Samaria na maeneo ya karibu katika Ufalme wa Kaskazini wa Israeli. Na wao Wanaamini Agano la Kale kama sehemu ya maandiko yao, lakini wanatofautiana na Wayahudi wengine katika mambo kadhaa ya kidini, ibada, kama vile wao kuamini kuwa Mlima Gerizimu ni mlima mtakatifu.
 
Miaka yote hiyo uliyoitaja ya enzi hizo hakukuwa na taifa lililoitwa Tabzania, leo bila haya mnadai ni nchi yenu na mtailinda kwa udi na uvumba.
Si-support Palestine wala Israel lakini kwa sasa wote wana territories zao na wanastahili haki ya kuishi kwa uhuru.
Tanzania Umeenda Mbali sana Taifa Linaloitwa Tanganyika tu halikuwepo 🤣🤣

Ambalo Limeanza mwaka 1961 na 1962 Likawa Jamhuri na mwaka 1964 April Taifa la Tanganyika Likafutika 😅😅

Likazaliwa Taifa Jipya la Tanzania..

Na naunga Mkono hoja zamani walikuwa wakiishi pamoja kwa Amani nini kinachofanya sasa Wagombane maana walikuwa pamoja Tangu miaka yote hiyo aliyotaja kwenye historia yake
 
Kuna surah kabisa inaitwa banii israail/wana wa israel,ahadi iliambatana na masharti ambayo hayakutimizwa ukisoma hizo aya,najua umegugo ukakopi tu,halafu Quran Inasema musa alikua muislam si myahudi
Musa alikuwa muislam aaahaahaaa uislam huu wa juz juz hapa ambao muhamad muanzilish aliwakuta hata nduguze wakiwa wakristo aahaah huu huu unaoenezwa kwa mtutu wa bunduki au mwngne
 
Musa alikuwa muislam aaahaahaaa uislam huu wa juz juz hapa ambao muhamad muanzilish aliwakuta hata nduguze wakiwa wakristo aahaah huu huu unaoenezwa kwa mtutu wa bunduki au mwngne
Musa hakuwa Muislam na Jina lake halikuwa Musa
MUSA jina lake Ni Moshe hayo majina mengine ni Yaliyotoholewa..

Musa alikuwa Muisrael aliyefundishwa kwenye Dini ya Misri na kulelewa kama Mwana mfalme..
Na baadae Musa alikuwa ni Miongoni mwa Wakombozi wa BaniIsra..

Ila kama anamaanisha Musa alikuwa Ni Mu'Islam ni kweli Maana Islam maana Yake Ni Mnyenyekevu au Kunyenyekea Ni kweli Musa alikuwa Mnyenyekevu Mbele ya Mungu ila hakuwahi kuwa Muislm kama Dini
 
Musa hakuwa Muislam na Jina lake halikuwa Musa wala Moses..
MUSA jina lake Ni Moshe hayo majina mengine ni Yaliyotoholewa..

Musa alikuwa Muisrael aliyefundishwa kwenye Dini ya Misri na kulelewa kama Mwana mfalme..
Na baadae Musa alikuwa ni Miongoni mwa Wakombozi wa BaniIsra..

Ila kama anamaanisha Musa alikuwa Ni Mu'Islam ni kweli Maana Islam maana Yake Ni Mnyenyekevu au Kunyenyekea Ni kweli Musa alikuwa Mnyenyekevu Mbele ya Mungu ila hakuwahi kuwa Muislm kama Dini

Nani alikwambia Musa alikuwa akiitwa Moshe?. Hujui kuwa Musa alikuwa na jina la kale la Wamisri?.
 
Samahani Mkuu!
Unamaanisha Kuwa Wasamaria na Pelishit (Wafilisti) au Wapalestine ni Taifa Moja???

Kama Ni hivyo hauko Sahihi Kulikuwa na Wasamaria na Pia Kulikuw na wafilisti..

Wasamaria walikuwa jamii ya zamani ya Kiyahudi yenye imani zao na mila zao tofauti, na waliishi hasa katika mji wa Samaria na maeneo ya karibu katika Ufalme wa Kaskazini wa Israeli. Na wao Wanaamini Agano la Kale kama sehemu ya maandiko yao, lakini wanatofautiana na Wayahudi wengine katika mambo kadhaa ya kidini, ibada, kama vile wao kuamini kuwa Mlima Gerizimu ni mlima mtakatifu.
Sijakuelewa?

Kulikuwa na mataifa mengi tu ambayo yote ilipaswa yafukuzwe. Hata ukigoogle now.Palestine ya sasa ndio samaria ya zamani.
 
Nani alikwambia Musa alikuwa akiitwa Moshe?. Hujui kuwa Musa alikuwa na jina la kale la Wamisri?.
Missile of the Nation

Habar!
Kwakuwa Umeleta Mada Hii na Mimi niko tayari kukueleza Uhalisia wake!
Ni kweli kabisa Jina Halisi la Musa sio Moshe wala Musa yenyewe..

Jina la Musa Halisia alikuwa Akiitwa "Hapimose"
Wakati huo neno "Hapi" lilikuwa linaamisha "Maji" au "Mungu maji" au "Mungu kutoka Maji ya Mto nile"
Na Neno "Mose" Maana yake "Yeye aliyetokana na"
Au unaweza ukasema "mwana wa" au kwa wale wenzetu wa Tanzania Tungetumia majina kama "Mwana...", Kwa watani wangu Wasukuma wangesema "Ng'wana...." kwaKabila zingine kanda ya Ziwa wangesema "Nya..."

kwa Wazungu wangesema "Son of...." au "Child of.." etc..


Sasa Unapata Picha halisi sasa kwamba Jina halisi la musa Lilikuwa "Son of Hapi" au "Child of Hapi" au "The one Come from Hapi" au Simply "Born of Hapi"

Au Kwa tafsiri halisi "The one comes from water" au "the One comes from water God"

Majina ya Maprince wengi wa kimisri yalikuwa Lazima yawe na Root Ms au Mose kwa sababu waliamini Kwamba Prince hawi prince ila Mungu amemteua Kuongoza taifa..

Kina Moses wengine ni kama "Ramses" tafsiri yake "The one comes from God Ra" au Simply "Born of Ra"
Mwingine..Thutmose ("born of Thoth")


SASA ILIKUWAJE HAPIMOSE akawa MOSHE (AMBAYE WENGI WANAMFAHAMU KAMA MUSA/MOSES)

Usisahau kwamba Mlezi wa Hapimose (Yaani Yaya, Au kw Lugha Nyepesi Dada wa Kazi wa Hapimose) Alikuwa ni mama yake Mzazi,

So yeye Alikuwa Anamuita Musa Jina MOSHE kiebrania Na Ambalo ndilo limetumika Hata kwenye Biblia ya Kiebrania Mpaka leo..

Akifupisha Jina Hapimose kwa hiyo yeye alimuita Simply MOSHE akimaanisha "Aliyetolewa" au "Kutoa"

Hakuwahi Malizia Aliyetolewa kwenye Maji kwa sababu ilikuwa Ni kuabudi Miungu Mingine kama Huyo Mungu Hapi wakati wao kama Waebrania Hawakuwahi kuabudu Mungu mwingine kwahyo yeye Alikomea Kuita Moshe tu..

Na hilo ndo likawa Jina La Musa kwa Waebrania wote, Hata alipokuwa Anarudi nyumbani kueleza Kuhusu Jinsi mtoto anavyokuwa Alikuwa Akitaja Moshe na Sio HAPIMOSE..

Na hata Musa alipotoroka Misri alianza Kujiita Moshe badala ya Hapimose..

Nadhani umenielewa Ila kama una swali unaweza Kuniuliza
 
Sijakuelewa?

Kulikuwa na mataifa mengi tu ambayo yote ilipaswa yafukuzwe. Hata ukigoogle now.Palestine ya sasa ndio samaria ya zamani.
KWanini unasema Ilibidi wafukuzwe 😅😅

Wangoni Asili yao ni Afrika ya Kusini,Amakonde asili yao ni Msumbiji, Wamakua Asili yao ni Msumbiji na Zambia, Wamasai asili yao ni Ethipia, Hakuna Kabila Tanzania Lililokuwa na Asili yake hapa..

Swali Baada ya Kupata Uhuru Tanganyika Ilibidi Tuwafukuze makabila ya Nje kwakuwa Yapo kwenye Ardhi yetu??

Pengine Hata Hatukuwahi kuikaa Ardhi hiyo ila Ni ardhi ya Kihistoria??

Nazungumzia Palestine/Paleshit/Ardhi ya wafilisti ni tofauti na Taifa la Samaria ambalo ni wayahudi waliokengeuka
 
Back
Top Bottom