Hapa Makongoro Nyerere kaamua kusema ukweli mbele ya Rais bila kupepesa macho

Hapa Makongoro Nyerere kaamua kusema ukweli mbele ya Rais bila kupepesa macho

Makongoro alienda vita ya Uganda bila hata baba yake kujua, Makongoro alijiunga na upinzani NCCR na kupata Ubunge.

Makongoro aliwahi kukataa ubunge wa kuteuliwa na Mkapa.

Kama jina la Nyerere ndio linambeba mbona lisiwabebe hao watoto wengine wa Nyerere?
 
Kaongea tu, lakini Makongoro ni mpambanaji sana tena bila hata kutegemea jina la baba yake.

Alikuwa Jeshini. Akaenda vitani Uganda.

Aligombea Ubunge Arusha kupitia NCCR Mageuzi 1995 baba yake akiwa hai na akashinda.

Na siku zote amekuwa yeye Kama yeye kifikra na Mambo yake.

Hapo kawapelekea ujumbe wenzake wa mbeleko za chuma. Anawauliza wameifanyia nini nchi? Pia kasema ukweli mtoto hachagui Baba. Mbona watoto wa Walimu wakiwa Walimu watu hawapigi kelele wanabakia kusifia yaani huyu kama Baba yake? Au kwa vile wamefaulu mitihani ya uwalimu?
 
Nadhani wengi hamjamuelewa Makongoro. Alicho maanisha ni kwamba kuna mambo mengi wamayafanya lakini hayajulikani, hayaandikwi popote..hivyo watu wanadhani wako hapo walipo kwa sababu ni mtoto wa fulani.
Wewe ndiye umeelewa hivyo? Bila yeye kusema hilo unafikiri hawa wanao ramba asali kwa urefu wa kamba zao wangeweza sema hilo?
 
Halafu Jaji Warioba kama vipi atusaidie kupata Katiba yetu. Tumechoka kupigwa kalenda na Wanasiasa! Na hasa wale wa kutoka CCM.
 
Hii kauli ni kubwa sana. Kuwa watoto wa Viongozi wanapata Nafasi si kwa sababu wamewahi fanya matendo makubwa. Ila ni sababu tu ya Majina ya Watoto wao.

Nadhani alikuwa anamaanisha yeye, riziwani kikwete,januari makamba,nape nnauye n.k

Anasema wao wapo hapo ukisema utafute walichofanya mpaka kuwepo hapo utatafuta mpaka ukome. Ila ndo wapo sababu ya wazazi wao.

Sisi tunaokesha JF kuipigania CCM ni lini tutafika huko? Angalau nasi mtukumbuke jamani MNAPOLAMBA ASALI. KWA SASA MAKAMBA ANASEMA NI KULAMBA ASALI TU KWA KWENDA MBELE.

View attachment 2181892
🤣🤣🤣
KIDUMU CCM

#Siempre JMT🙏
 
Makongoro akiwa anapiga speech live on a national yelevision inahitaji ujasiri maana street language za kutosha
Jamaa kitaa sana na anaweza kutoa boko any moment
Kuna maneno kayasema ni deep street am sure hata rais hakuyaelewa...
The man is funny and free soul creature with a bottle of hennessee in his hand.
Jamaa haaminiki masihara mengi
 
Mwl alizingatia sana suala la uwanadamu na akiona kuwa huna uwanadamu alikuwa hasiti kama akipata nafasi kumuambia mteuaji huyo hana uwanadamu. Katika wateuliwa ni nani hana uanadamu na kwa nini?
 
CCM ni ukoo wa kambale, baba, mama, watoto wote misharubu
 
Mnategemea katiba mpya kwa kuandika mitandaoni?mtasubiri sana kuna tatizo sis wa tz tunalo sijui ni laana au nn mpaka tufunguke kiakili tutakua tumepigwa vya kutosha. Hongereni wanasiasa wa tz mmeshatusoma kua sie mazuzu na waoga mnatumia mwanya huo kama fursa kwa wa tz
Mheshimiwa, hivi unawafahamu vizuri wale form four failures kweli? Wale wapumbavu wanaweza kushindwa kuelezea maana ya PGO! Ila siyo kupiga watu virungu na kuwaua.

Sasa usawa huu unavunjwa miguu, kiuno, au kuuwawa kabisa! Nani atawalea watoto wangu wadogo? Hii ndiyo sababu wengi tunaogopa kuingia mitaani kuidai hiyo Katiba Mpya. Labda wabadilishe mitaala yao kwanza. Hii ya sasa nguvu zinatumika sana kuliko akili.
 
Halafu Jaji Warioba kama vipi atusaidie kupata Katiba yetu. Tumechoka kupigwa kalenda na Wanasiasa! Na hasa wale wa kutoka CCM.
Tupiganie katika constitution iwe inamshitaki mtawala na asiwepo mtu ambaye sheria haimgusi. Hiki kitu muhimu sana. Kapigania katiba ya kwanza hicho kifungu hakikuwepo. Je katiba ya pili kitakuwepo? Bila hicho kifungu kuwekwa katika katiba ni sawa na mechi bila refa.

Halafu mchakato wa katiba ni msamiati wa kupotosha tuu. Wewe weka wasomi wawili tuu wa sheria halafu tuwape imprest na posho ya nguvu. Amin amin nawaambia, wiki moja tuu utapata katiba nzuri sana kupita ya mataifa makubwa.

Hili neno "mchakato wa katiba" halina mantiki yeyote kisheria. Wewe sema kuundwa kwa katiba mpya na wataalamu wa wizara ya sheria linaeleweka.
 
Hii kauli ni kubwa sana. Kuwa watoto wa Viongozi wanapata Nafasi si kwa sababu wamewahi fanya matendo makubwa. Ila ni sababu tu ya Majina ya Watoto wao.

Nadhani alikuwa anamaanisha yeye, riziwani kikwete,januari makamba,nape nnauye n.k

Anasema wao wapo hapo ukisema utafute walichofanya mpaka kuwepo hapo utatafuta mpaka ukome. Ila ndo wapo sababu ya wazazi wao.

Sisi tunaokesha JF kuipigania CCM ni lini tutafika huko? Angalau nasi mtukumbuke jamani MNAPOLAMBA ASALI. KWA SASA MAKAMBA ANASEMA NI KULAMBA ASALI TU KWA KWENDA MBELE.

View attachment 2181892
Watu wanafadhiliana!! Kwa kujuana!! Ujumbe umefika!
 
Mnategemea katiba mpya kwa kuandika mitandaoni?mtasubiri sana kuna tatizo sis wa tz tunalo sijui ni laana au nn mpaka tufunguke kiakili tutakua tumepigwa vya kutosha. Hongereni wanasiasa wa tz mmeshatusoma kua sie mazuzu na waoga mnatumia mwanya huo kama fursa kwa wa tz
Duh!
 
Back
Top Bottom