Hapa ndio ninapokuwa na walakini na uwepo wa Mungu

Hapa ndio ninapokuwa na walakini na uwepo wa Mungu

Ushahidi gani unataka na mateso yao unayaona?

Kuteseka kwao ni uthibitisho tosha kwamba Mungu Kashindwa kuwasaidia.

Huyo Mungu angekuwa anasaidia, Kusingekuwa na watu wanao teseka. Duniani.
Kushindwa kusaidia na kutosaidia tu ni tofauti, wewe unatuambia kashindwa kusaidia sasa labda ueleze kashindwa kwa namna ipi? Kwamba hana uwezo wa kusaidia au kaamua tu kutosaidia?
 
Kuna uhusiano gani wa kuwepo Mungu na hayo unayoyasema? Kwamba uwepo wa Mungu unategemea na yeye kutoa msaada?

Hebu nieleweshe.
Anakinzana na sifa zake mnazomwelezea:

1.Mwenye Upendo
Utaacha viumbe ulioumba mwenyewe wateseke ili hali unaweza kuwanasua kwenye huo mkwamo!

2.Mwenye Kusamehe
Alimtupa kuzimu shetani kwa kosa moja tu!

Fikiria hizo mbili, halafu tuambie huyu fictional character wenu kama sio fake ni nini?
 
Sasa akijitokeza hadharani na kila mtu akajua uwepo wake bila utata je hapo itakuwa suala la kuamini tena? Hebu nieleweshe.
Halitakuwa suala la kuamini tena.

Litakuwa suala la kujua kwa uhakika kabisa kwamba Mungu yupo.
 
Kushindwa kusaidia na kutosaidia tu ni tofauti, wewe unatuambia kashindwa kusaidia sasa labda ueleze kashindwa kwa namna ipi? Kwamba hana uwezo wa kusaidia au kaamua tu kutosaidia?
Mungu anaaminiwa kwamba ana uwezo wa kila kitu, Lakini Mungu huyo kashindwa kusaidia chochote kile. Hivyo Mungu mwenye uwezo wa kila kitu, Hayupo.

Mungu anaaminiwa kwamba ana upendo na huruma sana, Kama kaamua kutosaidia, Basi ni makusudi.

Na kwa maana hiyo, Mungu mwenye upendo na huruma, Hayupo.

Sifa za Mungu ndizo zinamfanya asiwepo.
 
Anakinzana na sifa zake mnazomwelezea:

1.Mwenye Upendo
Utaacha viumbe ulioumba mwenyewe wateseke ili hali unaweza kuwanasua kwenye huo mkwamo!

2.Mwenye Kusamehe
Alimtupa kuzimu shetani kwa kosa moja tu!

Fikiria hizo mbili, halafu tuambie huyu fictional character wenu kama sio fake ni nini?
1) Hii hoja ingekuwa na mashiko kama Mungu angekuwa ameahidi kwamba hatoacha wala kuruhusu kiumbe ateseke hapa duniani kwa sababu yeye ana upendo, kwa sababu yapo mambo mengine ambayo huonyesha hiyo sifa ya upendo wa Mungu.

2)Kuna visa vingi sana venye kuonyesha sifa ya Mungu ya kusamehe, na hadi sasa bado ipo ofa ya watu kusamehewa kwa sababu ya hiyo sifa ya kusamehe.

Ndio maana nashangaa kutumia hizo hoja kufanya hitimisho la kusema hakuna Mungu. Hizo sifa za Mungu zipo nyingi hili nalo mlizingatie.
 
Ngoja nukasevu mahali😀
Ebu soma hili andiko kwanza then ukae ujifikilie:



Dunia hii imepitia uongo/utapeli/propaganda kubwa sana na zikapita lakini uongo pekee ulio dumu kwa muda mrefu ni huu

Hebu fikiria unaambiwa kuna MUNGU muweza wa yote yupo sahihi na hajawahi kukosea

Ameumba dunia kwaajili yetu na ataiangamiza dunia kwaajili yetu
Alijua ataiangamiza dunia kabla hata hajaiumba lakini aliiumba hivyo hivyo ili aje kuiangamiza,
Ameumba moto wa jehanamu kwakuwa ametuumba tukosee ili atuchome moto japo alikua na UWEZO wakutuumba tusiwe wakosefu ili atuumbie Pepo tu tukale bata

Anajua tunacho hitaji lakini lazima tumuombe ili atupe, lakini hata tukimuomba hatupi tunavyo taka sisi maana tayari amekwisha tupangia kila mtu atampa nini, ataishije na atakufaje

Ndio muumba wa kila kitu(magonjwa, bangi, majini, ulabu nk) na anaweza kudhibiti chochote lakini anamlaumu msaidizi wake muasi(Shetani) kuleta mambo hayo mabaya duniani(magonjwa nk) kwa watu wake aliyewaumba wakati yeye ndiye aliye mtupa msaidizi wake huyo huku duniani
Yaani yeye kashindwana naye huko mbinguni kaja kumtupa kwetu sisi viumbe dhaifu tupambane naye na tukishindwa tutachomwa moto milele, lakini anasisitiza anatupenda sana kama mtu anavyopenda na kujali mboni ya jicho lake

Hebu tafakari hili, kawaumba Adam na Hawa na wakati bado wageni duniani akawatupia Nyoka(Shetani) ili awarubuni, na kwa ugeni wao wakarubunika matokeo yake katupa adhabu ya shuruba watu wote hata ambao tulikua hatupo na hata ambao hawajazaliwa chamoto watakiona...... Not fair

Mungu muweza wa yote hayupo WAZI PASI NA SHAKA kwa watu wote kujua huyu ndio MUNGU badala yake Mungu ndio amekua sehemu kubwa ya mgawanyiko wa watu na kusababisha kuwa na imani za MIUNGU zaidi ya milioni dunia nzima
Na kibaya zaidi unatakiwa to blindly believe him, usihoji wala kuwa na shaka juu ya uwepo wake(ni laana na kufuru) vinginevyo moto wa milele unakuhusu

Yaani kuna Fundi Kapenta mmoja huko Galilaya eti kafa kwaajili ya dhambi za watu wote duniani.... seriously
ADKq_NanOtSrTiofgZ8GKcrlzUppoPN47uaEWRTLnWp5aOLqj1Fw2UVggrKgTMaoQYkbbLqm7AaSh9qlGSTCUjtkL8U=s0-d-e1-ft
?
Akaitwa Mungu lakini Mungu huyu akajaribiwa na shetani
ADKq_NanOtSrTiofgZ8GKcrlzUppoPN47uaEWRTLnWp5aOLqj1Fw2UVggrKgTMaoQYkbbLqm7AaSh9qlGSTCUjtkL8U=s0-d-e1-ft

Fundi kampenta huyu hakuandika kitabu chochote ila wahuni walio kuwa wanampinga ndio wakaja kuandika vitabu kuhusu fundi huyu na vinaitwa “Bibilia Neno la Mungu takatifu”
Mabilioni ya watu dunia kote wanakesha makanisani wakimlilia na kumuomba awape uponyaji, mali, waume/wake nk

Hebu fikiria huko Arabia kuna Maamuma mmoja hajui kusoma wala kuandika alidai anashushiwa maagizo na Mungu kukata vichwa watu wote watakao pinga na kutokutii maagizo yake, “akashushiwa” aya za vitisho na neema kwa watakao tii, yaani ukifa unampigania Mungu unakwenda kupewa mbikra 72 kazi yako ni kuzagamua tu
ADKq_Nbuw1UIZCqE5Y9pLRPZlhZlI-SOFRzVgM7CzwW1Eqs44ilAgX075S52J_2AK051Ru4F1ybI2CJ3ABIuxUe5vxc=s0-d-e1-ft
ADKq_Nbuw1UIZCqE5Y9pLRPZlhZlI-SOFRzVgM7CzwW1Eqs44ilAgX075S52J_2AK051Ru4F1ybI2CJ3ABIuxUe5vxc=s0-d-e1-ft
ADKq_Nbuw1UIZCqE5Y9pLRPZlhZlI-SOFRzVgM7CzwW1Eqs44ilAgX075S52J_2AK051Ru4F1ybI2CJ3ABIuxUe5vxc=s0-d-e1-ft

Mabilioni ya watu duniani wanasujudu mara 5 kwa siku na kushinda njaa mwezi kila mwaka ili wakale naye bata Peponi

Kwamba maisha yako hapa duniani ni ya mpito tu maisha yako yapo baada ya kufa
Unachotakiwa kufanya ni kumuamini na kufanya aliyoa agiza ili ukale bata sana baada ya kufa
😀
 
Habari za siku ya leo WanaJamiiForums?

Kama kichwa cha habari kilivyojitosheleza. Sababu zinazonifanya niwe na mashaka na uwepo wa Mungu ni hizi hapa.

Sina dhambi mi ni mtakatifu haswa,
Lakini nimepitia mambo mazito mno ambayo mtu yeyote lazima angekuwa na mashaka na uwepo wa Mungu.

Sio kwamba simuamini Mungu kwa asilimia mia, Bali nina mashaka na uwepo wake (Nipo DILEMMA).

Ni hayo tu
Mpumbavu husema moyoni, Hakuna Mungu; Ni wafisadi, na wametenda mambo ya kuchukiza, Hakuna atendaye mema. Zab 53:1
 
Mungu anaaminiwa kwamba ana uwezo wa kila kitu, Lakini Mungu huyo kashindwa kusaidia chochote kile. Hivyo Mungu mwenye uwezo wa kila kitu, Hayupo.

Mungu anaaminiwa kwamba ana upendo na huruma sana, Kama kaamua kutosaidia, Basi ni makusudi.

Na kwa maana hiyo, Mungu mwenye upendo na huruma, Hayupo.

Sifa za Mungu ndizo zinamfanya asiwepo.
Hoja bado dhaifu, wapi Mungu aliahidi kusaidia?
Yani kwa sababu tu ana sifa ya upendo na uwezo ndio analazimika kusaidia kwa kila jambo kisa ana hizo sifa?

Halafu ipo mifano yenye kuonyesha uwepo hizo sifa, sasa utasemaje sifa zinamfanya asiwepo?
 
Halitakuwa suala la kuamini tena.

Litakuwa suala la kujua kwa uhakika kabisa kwamba Mungu yupo.
SUnaona sasa? lengo la Mungu ni imani watu kumuamini ila wewe unataka isiwe imani, ndio maana numekuwa nauliza kipi kinamfanya alazimike yeye kujionyesha?

Ndio maana yanaelezwa faida na hasara za kuamini na kutoamini.
 
Hoja bado dhaifu, wapi Mungu aliahidi kusaidia?
Yani kwa sababu tu ana sifa ya upendo na uwezo ndio analazimika kusaidia kwa kila jambo kisa ana hizo sifa?

Halafu ipo mifano yenye kuonyesha uwepo hizo sifa, sasa utasemaje sifa zinamfanya asiwepo?
Mungu hajawahi kuahidi kusaidia. Mungu hayupo.

Nimekujibu hivyo kulingana na wewe ulivyo niuliza swali lako kwenye post #81.

Uliuliza hivi "Mungu kashindwa kusaidia au kaamua kutosaidia"

Mungu hayupo kwa namna yoyote ile.

Kwanza, Hakuna uthibitisho wowote wa uwepo wake, yeye kama yeye. Ni imani tu zisizo na uthibitisho wowote ule.

Pili, Sifa anazosifiwa na kudaiwa kwamba huyo Mungu anazo, zinapingana waziwazi na uhalisia ulivyo.

Hivyo hakuna Mungu.
 
Hata kama ni mipango ya shetani ila watendaji ni binaadamu wenyewe, shetani hamforce mtu kufanya kitu.
HAA!! 🙄🙄 Hii mpya.

Ikiwa Shetani hamfosi mtu kufanya uovu, Je binadamu ametoa wapi akili ya kufanya maovu?
 
SUnaona sasa? lengo la Mungu ni imani watu kumuamini ila wewe unataka isiwe imani, ndio maana numekuwa nauliza kipi kinamfanya alazimike yeye kujionyesha?

Ndio maana yanaelezwa faida na hasara za kuamini na kutoamini.
Mimi sitaki isiwe imani.

Kuwa na imani na kuamini ni haki yako ya kikatiba kabisa. Unaweza kuchagua kuamini chochote utakacho hata mawe, miti, mapango, majabali n.k

Lakini ukianza kudai kwamba imani yako ina ukweli lazima uthibitishe hilo.
 
Mpumbavu husema moyoni, Hakuna Mungu; Ni wafisadi, na wametenda mambo ya kuchukiza, Hakuna atendaye mema. Zab 53:1
Huyo Mungu, Kwa nini aliumba binadamu wapumbavu wanaosema yeye hayupo?

Huyo Mungu, Alishindwaje kuumba binadamu wema tu watakao sema yeye yupo siku zote na wakati wote?

Hivi huyo Mungu anajielewa kweli?

Huyo Mungu kama aliumba binadamu wenye uwezo wa kusema yeye hayupo, Halafu anataka asemwe yupo, Basi Mungu huyo pia ni Mpumbavu sana.
 
1) Hii hoja ingekuwa na mashiko kama Mungu angekuwa ameahidi kwamba hatoacha wala kuruhusu kiumbe ateseke hapa duniani kwa sababu yeye ana upendo, kwa sababu yapo mambo mengine ambayo huonyesha hiyo sifa ya upendo wa Mungu.

2)Kuna visa vingi sana venye kuonyesha sifa ya Mungu ya kusamehe, na hadi sasa bado ipo ofa ya watu kusamehewa kwa sababu ya hiyo sifa ya kusamehe.

Ndio maana nashangaa kutumia hizo hoja kufanya hitimisho la kusema hakuna Mungu. Hizo sifa za Mungu zipo nyingi hili nalo mlizingatie.
Hakuna hizo hoja kabisa.
Hivyo visa vingi ni vipi?
Hakuna Mungu huu ndio ukweli.
 
Back
Top Bottom