Harusi ya Majizzo, Millard Ayo: Vijana matajiri hawapendi kuchezea pesa zao wala kusumbua watu na michango

Michango ya Harusi ni Janga Kwa Taifa. Ujinga kabisa mtu unataka kuoa weka bajeti yako kusanya pesa usisumbue watu. Mtu anataka Harusi ya M15 wakati mfukoni hata mia hana, halafu watu wamchangie.
 
Mkuu fanya Settings kwenye WhatsApp messenger yako ambapo hakuna yeyote atayeweza kukuunga kwenye group. Binafsi nimewakomesha kwa hilo. No stress za michango!
Tupe elimu boss.....mana waafrika ustaharabu zero kabsa
 
Kuna jamaa yangu mtu wa mbwembwe sana, akafanya harusi, sikuchanga, ghafra tu baada ya harusi namsalimia anakausha, nikajua mchango wangu ndiyo sababu....
 
Pole mkuu. Mi waliniunga group la harusi simjui ata member mmoja wala bwana harusi.

Nikaahidi nitatoa laki 5 hafu nikaleft. Nilitafutwa aisee ova sio SMS sio kupigiwa. Akijitambulisha tu anakula block.
Wakristo mara nyingi ndio wana mambo hayo mi kuna mmoja simjui wala hanijui alikuja ofisini ikawa kila siku anapita kukumbushia nikaona hii noma nikampa elfu 20 akapotea yaani Christian kila kitu kwao ni gharama mazishi gharama harusi gharama mpaka kero halafu wanasumbua watu mtaani na michango.
 
Ni ujinga mwingi mnoo mkuu..
 
Michango kwenye harusi yangu haikuzidi 7mil. Hii ni ile iliyokuwa counted for, mingine niliipiga juu kwa juu. Hii 7mil ilichangiwa na familia zisiozidi 10. Familia moja ilichangia 2mil, wapo waliochaangia 1mil, 500k, etc. Hizi ni familia ambazo nilishajitoa sana kwa hali na mali kwa issues zao bila kutegemea returns zozote.

Nilitangaza mara moja tu kwenye magroup ya primary, secondary na chuo. Sikuwahi mkumbusha mtu mchango, wale wa karibu walinitumia wenyewe bila kukumbushwa, ambao hawakutuma sikuwasumbua kwa message.

Week kabla ya harusi nilituma tena message kwenye magroup hayo kutoa offer ya kadi za bure kwa yule atayekuwa karibu. Waalikuja wachache sababu marafiki wengi wapo Dar na harusi ipo mkoani.


Gharama za harusi zilikuwa almost 6mil. Mainly chakula na vinywaji.
Mapambo 300k, cake 200k, ukumbi 300k, MC free, Camera man 200k, etc

Camera niliokodi Camera 2, moja ya Video, nyingine ya picha, nikawapa Deiwaka vijana wawili, kila mmoja akabeba ya kwake na accessories zake, shughuli ilivyoisha nikanyonya vilivyo vyangu, nikarudisha camera za watu.

Maisha ni kuchagua...Mungu anisaidie mtoto wangu aje kuwa na spirit kali zaidi yangu.
 
Mimi nilikuta nimeungwa kwenye group sijui nani anaoa nikaleft muda huo huo. Kuna jirani yangu anaolewa kanipa kadi nayo sichangii sijui hata nimeitelekeza wapi. Nitachangia misiba na wagonjwa tuu.
 
Mtoa mada una ujumbe mzito sana, vichwa laini hawatokuelewa!
Lakini %99 ya watakaofunga ndoa, wataowa mara moja tu. Hiki ni kipindi cha mpito na Furaha. Harusi kubwa huja n michango mikubwa. Kakaangu alilipa maali ml15, siku ya harusi yake alihongwa taslim ml37,magari mawili, kiwanja kigamboni n mizawad kadha wa kadha anayoijua yeye n mkewe. Kwa ufupi, kama unaweza kujidhatiti kwa kugharamikia ndoa yako, gharamika. Kama hawezi, tumelelewa kwenye jamii ya michango, changisha mpaka uifikie bajeti. Hii ni sherehe yako, pesa makaratasi tu. Furaha ndio kila kitu. Ni upuuzi kuhangaika mithili ya punda kazini, alafu ushindwe kujipa Furaha kwa pesa za jasho lako. Pia, unafikiria kwa harusi ya mil 3, yupo wa kukuzawadi zaidi ya mil1??? Labda kwa ndugu wa karibu. Ila ukigharamika, hata zawadi zitakuja zikiwa n staha. Maisha mafupi, pesa tutaziacha, mkeo aolewe n boya jingine lije kulienjoy jasho lako. Mabibi n mabwana, yolo, enjoy wakati ungali hai. Kila kitu kina mwisho
 
Depal Depal Depal Aikoooooooooooooooooooooo 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 njoo unione nimelazwa Benjamini Mkapa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…