Hii nguvu si mchezo: Kitenge, Zembwela na Hando wapewa escort ya ving'ora Dubai

Hii nguvu si mchezo: Kitenge, Zembwela na Hando wapewa escort ya ving'ora Dubai

Huhitajika Uongo mwingi sana na nguvu kubwa sana kuhalalisha uovu.


Wao ngoja waipe promoooo tu , Watanzania sio wajinga, na Watanzania wa Sasa wameelimika.
Mkuu watanzania tuna ujinga mwingi sana, let's call a spade its name.
 
Hawa jamaa wanafkr wote tumeishia la Saba , Watanzania tulichobakiza ni jeshi kutuunga mkono , mana hawa wanasiasa wamejificha kwenye nguvu ya jeshi...
Elimu sio msingi mkuu wa kuwa na msimamo wa kizalendo,kuna maprofesa na madkta yana unga mkono dpword,Acha kuwagawa watanzania kwa msingi wa elimu zao.
 
Humaanishi ulichokiandika hapa! Waandishi wako wapi hapo? Kitenge au zimbwela ndio wa kufanya documentary? Kwa uelewa gani na exposure ipi waliyonayo?
Huu ujinga wa kuanzisha vyombo ya habari na kuajiri watu wasio na taaluma ya habari ni janga!
Ulitaka uende wewe? Ungekua wewe una exposure wewe ndiyo ungeenda lkn cha ajabu huna
 
Ulitaka uende wewe? Ungekua wewe una exposure wewe ndiyo ungeenda lkn cha ajabu huna
Ona unavyowaza kimaskini na kizamani! Huu uzalendo mnaohubiri na kuhubiriwa ndio huu wa kuanguliza vinyweo vyenu kwa waarabu kuwadalalia ndugu zenu kwa shs. Milioni sita? Ona aibu unapojibu hoja za kiume wewe! Kabisa na wewe unakubali kuwakilishwa na zembwela yaani! Basi umeoza kichwani!
 
Kuna watu wako hapo kwa kazi maalumu yaani kwa maelekezo kbsa kama kitenge yule ana kazi na kazi nyingine ndani yake pia
 
View attachment 2666300

Nani amefatilia Wasafi media leo asubuhi? Hawa watangazaji watatu tangu juzi wapo Dubai na wanajinasibu Kama ni wageni rasmi wa DP world kutoka Tanzania. Na wanapata escort ya ving'ora Kama wageni wa heshima.

Leo walikuwa wanawahoji watanzania ambao wanafanya kazi hapo bandari ya Dubai. Kiuhalisia wote waliohojiwa ni kutoka kwa ndugu zetu unguja na pemba (Zanzibar).

Mambo mengi mazuri Sana ya DP world yameongelewa,ikiwa pamoja na bandari kupokea meli 30 kwa wakati mmoja na kuhudumia meli sita zenye magari 3k kwa siku mbili tu. Mambo ni mengi.

Lakini Hawa jamaa ni wanajizima data au hawajui kilio Cha wanaowapinga hao DP world kuwa siyo ufanisi wao Bali ni MKATABA mbovu na wa kinyonyaji na wakivhief Mangungo baina yao na Tanzania?

Hata dada yetu wa Jf bi Faiza Fox nae aliandikw uzi wenye mtazamo huu huu wa kina Zembwela kuwa "DP world wapo hadi Uingereza iweje nyie walala hoi watanganyika mnawakataa". Akapigwa maswali haya haya,umeuona mkataba wa Uingereza? Au mkataba wa Uingereza na huu wa kwetu unafanana?

Alafu kingine; hivi ni nani amawafadhili Hawa jamaa watatu? Huko Dubai? Maana wanajimwayamwaya kama wafalme. Na Wana ego balaa,full kujisifu.

Hii nguvu ya DP world kwenye media za bongo siyo mchezo.

Lakini Hawajui kuwa ukimsisitiza Sana Mtu kuwa kitu chako ni ni kizuri ndivyo unavyomfanya astuke kwamba kwa nini jamaa ananilazimisha Sana nione hiki kitu chake kipo sawa? Jamaa wanafosi mpaka kila mtu Sasa anajua kwamba wanalazimisha!!

Hii tabia tunayo Sana sisi mawinga/ wazee wa kulenga hapa kariakoo. Nikiona hiki kiatu ni 'mdosho',nguvu ninayotumia kukuaminisha kwamba ni kiatu genuine ili uingie mkenge siyo ya nchi hii. Ukifungua wallet tu tukamalizana napita hivi,utajijua mbele ya safari. Ukikivaa ukapiga hatua zako 20,mguu unanyanyuka,soli inabaki chini.

Nikimwangalia Gerald Hando ni Kama Mtu mwenye kujistukia tofauti na wenzie. Hawa jamaa wawili wanaupepeta mdomo si mchezo. Hawana breki.
Uzi wako ulikuwa uwe mzuri sana hadi ulipokuja mtaja huyo mdini @faizafox nikaishia kutoendelea
 
Ona unavyowaza kimaskini na kizamani! Huu uzalendo mnaohubiri na kuhubiriwa ndio huu wa kuanguliza vinyweo vyenu kwa waarabu kuwadalalia ndugu zenu kwa shs. Milioni sita? Ona aibu unapojibu hoja za kiume wewe! Kabisa na wewe unakubali kuwakilishwa na zembwela yaani! Basi umeoza kichwani!
Hao walioenda wana akili na exposure kuliko ata kama una elimu ya makaratasi unayodhani inakufanya uwe bora zaidi ya hao.
Basi nenda wewe....aaaaah
Eti kufanya udalali...Poverty mentality ina kuumiza eti
 
Kwa hiyo Pemba na Unguja wao hawataki mamilioni ya DP hadi bandari zao ziachwe kwenye huo mkataba wa Mangungo?

Wakati mwingine naona huu muungano ungevunjwa tu kila mtu akae kwao...
 
Hao walioenda wana akili na exposure kuliko ata kama una elimu ya makaratasi unayodhani inakufanya uwe bora zaidi ya hao.
Basi nenda wewe....aaaaah
Eti kufanya udalali...Poverty mentality ina kuumiza eti
Kama kweli elimu uliyonayo bila kujali ni rasmi au ya kitamaduni hebu kaa kitako umtafakari mmojammoja Kati ya waliokwenda huko Dubai Kama Kuna hoja waliyoweza kuijenga kwa wenye kampuni. Akili ya kawaida inakataa siyo?
Nitakushangaa Sana Kama bado unaendelea kutetea upuuzi huo wa kubebeshwa mifuko ya Rambo ughaibuni! Naona kinyaa Kama mzazi.
Walibeba agenda zipi na walirudi na majibu gani mapya? Kitenge aliandika kuwa kule bandarini Dubai huoni watu zaidi ni mitambo tu tofauti na waziri wako aliyesema wataongeza ajira zaidi ya 70,000. Huuoni huo mkanyagano na mkorogano? Na bado unabaki eti ungeenda wewe! Ona aibu dogo na acha kulinganisha elimu humu hazikusaidii! Mkataba ni mbaya na mbovu tu period!
 
WATANGAZAJI WA KISASA NI MBUMBUMBU.

Akina Adam mchomvu.
Zembwela, swebe, seki, JUMA lokole, Dida,

AMA KWELI KAMA NCHI TUNAZIDI KUPOTEA, TAIFA LINAELEKEA KIFO.
Kuna mwamba Masoud Kipanya na Siza wa clouds hata Huyo Gerald Hando ni Bonge ya Watangazaji Wana maswali ya maana yenye mantiki na yenye kukidhi au kukata kiu ya msikilizaji wanakupa unachotaka kusikia wao kuchimba na kutizama kitu Kwa Angle zote huwa Wana karesearch kabisa kabla ya interview (ukiwasikiliza utanielewa), so namtetea...Gerald ana miiko kama ya kina Kp na Siza ndo mana alikuwa kapooza Fulani hivi [emoji16][emoji1] kwahivo alikuwa Hana Chemistry yake pale akili kubwa kuwekwa na vitu vya kipuuzi....
 
Tanzania kuna uhaba mkubwa wa waandishi wa habari na watangazaji wengi ni failure waliookotezwa hapa na pale. Na wachache wenye ufahamu tamaa imetangulia mbele
katangaze wewe mwenye ufahamu.

Dah hizi wivu ni tatizo kuliko Dpw
 
Hiyo ya ving"ora ni uongo, hata ruler wa huko anatembea bila ving'ora, usiwafananishe Dubai na ujinga wa kwetu huku. Mwone Mfalme wao anakula misele amaendesha mwenyewe, hakuna ving'ora wala nini:



Huyo mpaka ofisi za serikali anakwenda kuguwaa mwenyewe kama raia wanapata huduma inavyotakiwa.

Kwanini Watanzanoia mnakuwa waongo namna hii?
 
Back
Top Bottom