Hii video ina-trend ya namna kijana Ali alivyonyanyaswa na kubaguliwa Zanzibar

Hii video ina-trend ya namna kijana Ali alivyonyanyaswa na kubaguliwa Zanzibar

Mwanzo 21:9 Baadaye Sara alimwona Ishmaeli, mtoto wa Abrahamu aliyezaliwa na Hagari, Mmisri, akicheza na Isaka mwanawe. 10Basi, Sara akamwambia Abrahamu, “Mfukuzie mbali mjakazi huyu na mwanawe.

HAPA NDIPO ASILI YA UZAO WA CHUKI, ULIPAJI VISASI, MAUAJI, UGAIDI ULIPO ANZIA.

WATU WA VISIWANI NI KAMA WATU WA UZAO WA ISHIMAEL WENGINE, USISUMBUKE NAO
"Akicheza na Isaka mwanaye?" Sijawahi ona mbona kwenye maandiko huo mstari, version Gani hiyo mkuu?
 
Huyu jamaa ni muislamu mbona ?
Dhambi ya ubaguzi huwa haiishi kamwe.
Mkimaliza kuwabagua wote waliotofauti nanyi mtaanza kubaguana wenyewe kwa wenyewe kwa rangi au hata maumbo ya miili yenu.
 
Kwa hiyo mkristo ndo mwenye haki ya kufanyiwa ubaguzi na waislamu?
Ulisikia wapi ? kule kuna sheria zao fuateni msipeleke demokrasia yenu sio Tanganyika....

Zanzibar ni jamii nyingin usiforce pambana na maisha serikali yako ya Tz.
 
Dhambi ya ubaguzi huwa haiishi kamwe.
Mkimaliza kuwabagua wote waliotofauti nanyi mtaanza kubaguana wenyewe kwa wenyewe kwa rangi au hata maumbo ya miili yenu.
Unaongea nn? yaani zanzibar inakuhusu nn ? Acha unafiki nchii hapa watu wanauliwa daily na serikali wewe unafautilia ya zanzibar kama sio tabia za kike.

Mtu ana kosa anahojiwa nyie mnaingia udini na ubara, hamuwezi kufanya chochote kile.
 
Hao wazanzibari kama wamejitosheleza wanafuata nini huku Tanganyika?
Ulisikia wapi Zanzibar wanategemea bara wakati wamepokwa mamlaka na bara? , sisi ukanda wa pwani ni ndugu zetu nyie kutoka bara hawahusu .
 
Hao jamaa wana shida wakijua ww ni wabara ata huduma za kawaida sokon wanapandisha bei
 
Hapo nilichoona tatizo kubwa ni shule tu yaani hao jamaa wangekua wamefika hata form two tu wakafeli wasingekua na akili za hovyo namna hio
 
Mtu yoyote kutoka bara akija kuishi Zanzibar, akili za 90% ya wazanzibar wanawaza mojawapo ya haya;
1. Ni mgalatia mwenye hatari ya kuambukiza ugalatia Zanzibar!
2. Amekimbia dhiki bara ili kuja kuneemeka Zanzibar hivyo kuzuia riziki kwa wazanzibar!
3. Ana malengo maalum mabaya ya siri dhidi ya Zanzibar au wazanzibar!

Angalizo
Ukija Zanzibar njoo kwa tahadhari, adabu na hekima.
Na wao wakija bara tuwachukulie hivyo hivyo
 
sio kila kitu ni dini bro mimi nimesema kwa wale wazinzibar shule haikua upande wao kumtendea binadamu mwanzao yale
wewe pia ina expose namna gan una upungufu au ukosefu wa uelewa kwa kufowad malink yasiyohusiana na mada pale juu muwe na utu

Ulikuwepo au unaangalia hiyo clip ya dakika 2 na unahukumu?
Mbona kuna vijana kwa maelfu na hwajakamatwa?


View: https://vm.tiktok.com/ZGex5E9LJ/
 
Ali
Nimeiona hii video ya kijana Ali mwenye ulemavu na tatizo la kifafa.
Nimesikitika sana alichofanyiwa na wananchi wenzetu wa Zanzibar.
Huyu kijana kwa wanaomjua wanasema amekulia Sinza na ni mlemavu kweli na amekua akiishi kwa kupata vibarua na kuomba msaada wa chakula na hela.

Udhalilishaji aliofanyiwa umeniacha na maumivu makubwa moyoni. Mtu hata kwa kumtazama usoni unaona dhahiri hayuko sawa na asiye na siha njema. Nimesawijika sana.

Wanasema amewaibia lakini hakuna uthibitisho wa hilo. Zaidi unaona ni chuki ya kwa kua ni mtu wa bara na zaidi ukisikiliza clip kwa uzuri kuna mtu anaropoka hawezi kua na msalaba huyo? Hiyo baada ya mmoja kumuuliza bwana Ali kuhusu mtu anaitwa Eric Masawe.

Nimekerekwa sana kwa udhalilishaji huu. Hii chuki ya dini ya mtu inatoka wapi? Asilani siwezi kumchukia mtu kwa dini yake hata kama si wa imani yangu na siafiki mambo juu ya imani yake. Kulikua na haja gani kutaja suala la msalaba?

Mimi kwetu Arumeru baba yangu alikua anakodisha ardhi kwa wazanzibari kiroho safi bila kujali dini zao wala utofauti wa makabila. Lakini, wenzetu hii chuki inatoka wapi?

Bwana Ali ametwezwa sana utu wake. Na huyu ni ndugu muislam vipi kwa asiye muislam? Hivi ndio dini inaelekeza? Kama mnaona kuomba anapata sana basi nanyi muombe muone kama ni jambo la kujivunia.

Wazanzibari mkae mkijua kama ni hasira zenu basi muipelekee CCM na sio wananchi wa kawaida. Huyo ndie adui yenu na adui wa kila mmoja wetu.

Ifike wakati mstaarabike. Dini badala ya kutujenga zinatufanya kuwa mafala na majinga.
View attachment 2977699
Ali namfahamu,kijana wa Mbagala huyo:-
1.Ni kweli an ugonjwa wa kifafa na hutumia dawa
2.Ni mlemavu wa mguu mmoja nadhani hutumia magongo kutembea
3.Ni mwizi mzuri sana,mwaka jana September, alilazwa hospitali moja hivi kubwa ya umma,akawa anasinguzia ameibiwa simu kwenye ile wodi aliyelazwa na wafanya usafi alipwe isivyo halali,hadi kutokea "staff" wanaomjua background yake kumuongelea
Ni kweli wazanzibar wana ubaguzi uliopitilizia,lakinj hata watu kutoka bara sio wakamilifu bado wezi,vibaka,matapeli,wazinzi na walevi wapo wa kutosha
 
Back
Top Bottom