Hili Taifa Vijana wangetumia ⅓ ya Akili zao leo hii tungekuwa Taifa kubwa kiuchumi zaidi ya Taifa la Marekani!

Hili Taifa Vijana wangetumia ⅓ ya Akili zao leo hii tungekuwa Taifa kubwa kiuchumi zaidi ya Taifa la Marekani!

Nsikuchoshe na Usinchoshe,tusichoshane!

Ukiona viongozi wa Serikali wana wang'ang'ania wazee kwenye nafasi nyeti tambua ya kwamba vijana watakuwa na matatizo ya kiakili,Vijana wengi waliopewa nafasi ili waonyeshe uwezo wao wamekuwa wapumbavu kuliko hata wazee waliochokaa!.

Hili Taifa la Tanzania ndilo Taifa linaloongoza duniani kwakuwa na Vijana wapumbavu kuliko Mataifa yote yanayotambulika na Umoja wa Mataifa (UN).

Hebu fikiria kijana anatoka nyumbani au kibaruani kwake kuelekea Airport (JKNIA) kumpokea msanii wa muziki wa kizazi kipya kisa kachukua tuzo huko Marekani,na kibaya zaidi huyo kijana anakimbiza gari lililombeba huyo msanii kitokea Airport hadi Kawe!.

Zaidi ya Km 22 huyu kijana anakimbiza gari kutoka JULIUS KAMBARAGE NYERERE INTERNATIONAL AIRPOT (JKNIA) hadi Kawe huku akitokwa jasho na kunuka kama mbuzi wakati huo huo huyo msanii akiwa anapigwa na AC (Air Condition)!.

Nimetafakari sana namna vijana wa nchi hii (Wengi) walivyo wapumbavu hadi nimekosa majibu!.

Hebu fikiria muda ambao huyo kijana kapoteza katika shughuli za uzalishaji mali!.

Kwanini vijana wasitumie muda kama walioutumia leo wakaandamana kuihoji serikali kuhusu ripoti ya CAG? Nilitamani kuona vijana wanahoji wezi wa mali na
wafuja rasilimali zilizotajwa kwenye ripoti ya CAG lakini hakuna anayehoji zaidi ya kushiriki kwenye mambo ya kipumbavu!.

Hili Taifa bila Vijana kubadilika sidhani kama twaweza kupiga hatua zaidi ya kila siku kuishia kuimba nyimbo za mapambio za kina Lucas mwashambwa mama anaupiga mwingi!

Hebu fikiria jitu lililokuwa linapewa heshima hapa jf kama liokota makopo maarufu la JF Chizi Maarifa nalo limekuwa sehemu ya ujinga huo leo pale Airport to Kawe!

Mdeki vyoo wa pale lugalo GENTAMYCINE yeye alishituka mapema hakwenda huko ila alimuachia mwehu mwenzie Chizi Maarifa amuwakilishe!

Vijana wa hili Taifa wengi ni wapumbavu sana!
Nilikuwepo Airport nilishangaa sana.
 
Yaani wazee waibe mapesa ya Kodi za Wtz afu uje ututukane vijana?,; Escrow, Richmomd, Kagoda vyote hivyo ni wazee wameusika!!. Afu wewe ni mzee au kijana?, Kama ni kijana mabadiliko hayaanzi na watu 19000 anza wewe acha kutushambulia kipumbavu...!.
Mbona hujasema waliokuwa wanadeki mabarbara 2015 kipindi Cha Lowasa?, Mbona hujasema wanaojazana kwa mwamposa?, Kama atatokea mtu akaja na wazo la kwamaba ili Tz iendelee tunahitaji "kufuta kizazi chote Cha CCM aidha kwakuwakataka mapanga au kuwapiga mabomu ndio nitamheshimu nakumuona shujaa!. Haya mengine ni upuuzi tu na kuwachukia watu, yaani mtu asimshangilie mtu anayempenda?, Futa kizazi dhalim Cha CCM uone Kama Tz itakuwa na shida na njaa za kipuuzi!. Naichukia CCM na watu wake....
 
Tumeshazoea kejeli zenu.
Yani mabandiko yao, nasema mabandiko yao kwa sababu ni kundi kubwa tu, lenye makasiriko lenye kudai wao ndio wenye kuleta Salvation, atiii wao ndio wajuaji. Konyo kabisa haya madudu. Huwa hawanishangazi vile bali ni jinsi wanavyopenyeza mabandiko yao yaliyojaa matusi kwa Mtanzania, Mwafrika na mtu yeyote yule mweusi, halafu Uongozi wa JF na Moderatore wanaachia tu kana ni poa!

No, hakuna cha kuzoea haya matusi. Its a No No

Hebu fikiri kwanza, ati kwasababu kijana anakimbiza gari lililombeba msanii ikitokea Airport hadi Kawe, km 22 basi vijana wote Watanzania hawana akili! Yaani hakutumia akili?...

.... Kweli ? mtu aende airport, akimbie km 22 na anamjua anayemkimbiza, iwe ni gari au mtu, halafu useme hana akili?
 
Tanzania izidi nchi ya Marekani kiuchumi?

Hakuna taifa lolote la kiarabu ambalo linaizidi Marekani kiuchumi.

Sasa utakuwa nchi yako ambayo umeme ni wa mgao?

Hao wazee wamefanya nini zaidi ya kuuza nchi?

Tatizo umeandika huu uzi ukiwa na mhemuko sana. Kaa kwa kutulia kisha andika upya
Tupitie habari kidogo aisee, siunajua marekani kwasasa ni nchi ya ulimwengu wa tatu au bado tunakariri yazamani. Nchi imeporomoka vibaya sana na inamadeni vibaya mno.
 
Screenshot_20231121-011304_Instagram Lite.jpg
 
Sheria na kanuni za kipambavu zinazoruhusu upigaji kama masilahi ya wabunge, katiba mbovu, matumizi ya anasa ya viongozi n.k zimetungwa kipindi ambacho hao vijana walikua watoto au hawajazaliwa kabisa.

Nyie wazee/wababa mlikua wapi kuandamana zisipitishwe from the first place mpaka mnataka kumrushia kijana mzigo wa kuzipinga?

Mlikua wajinga kuona ubovu? Mliogopa kukinukisha? Hayo maandamano unayotaka vijana tufanye mngeyafanya nyie mliotutangulia leo hii usingekuwepo hapa unalalamika.

Wazee/wababa mmeshindwa kuzuia chanzo cha tatizo kwaiyo hamna uhalali wa kulaumu vijana kwa kushindwa kupambania hayo matatizo yaishe. Actually youths suffer consequences of your ignorance, selfish and cowardness.
Sasa kama wazee walikosea miaka hiyo nyie vijana ambao sasa ni zaidi ya asilimia 70 si ndiyo mnatakiwa mkomae mwanzo mwisho ili kuleta mabadiliko ili muishi vizuri na vizazi vyenu?? Mkiwasusia wazee si ndiyo itazidi kula kwenu mazima?? Konde boy anawaandamanisha bure wakati yeye yuko kazini na anaingiza mkwanja??
 
Jamaa wanaboa, kutwa vijana vijana vijana utafikiri wao enzi zao za ujana waliacha legacy ya maana.
Hivi nyie vijana wa leo mngeweza kweli kupigania uhuru na kumtoa mkoloni kweli? Hebu tuwe wakweli mngeweza nyie?? [emoji12]
 
Sasa kama wazee walikosea miaka hiyo nyie vijana ambao sasa ni zaidi ya asilimia 70 si ndiyo mnatakiwa mkomae mwanzo mwisho ili kuleta mabadiliko ili muishi vizuri na vizazi vyenu?? Mkiwasusia wazee si ndiyo itazidi kula kwenu mazima?? Konde boy anawaandamanisha bure wakati yeye yuko kazini na anaingiza mkwanja??
Ndo watulie sasa tutakinukisha wakati ukifika sio kila siku vijana vijana vijana halafu ukiangalia hao wazee/wababa katiba mbovu wameitunga wao, nchi wameifilisi wao, mifumo mibovu wameiweka wao
 
Mbona yanga day au simba day sioni threads kama hizi

Mbona sijawahi kuona watu wakiponda watu wanaokesha kuangalia ligi za mpira za ulaya

Au tu watu wakiponda bar kujaa weekdays

Kwa nini ikija sekta ya burudani huwa kuna stigma ilhali hata michezo hususani mpira inapoteza muda vile vile

By the way, pamoja na libya kuwa na rasilimali pamoja na uongozi thabiti wa Ghadafi lakini haikuikaribia marekani zaidi ya kuboresha maisha ya wanachi wake. Hapo bado China na teknolojia, productive population na strong government institutions lakini bado haijafikia. Ndio iwe Tz, umekuza vitu mkuu
Kuendekeza mpira kupindukia kuliko kujali your welfare ni ujinga mwingine... ambalo pia ni tatizo la vijana wa kizazi kipya..
 
Usipoteze muda wala nguvu zako ktk kufuatilia maisha ya vijana wa Tz, unaweza kufa kwa presha ya moyo au msongo wa mawazo. Achana nao, akili zao wanazijua wao wenyewe.
Jaribu kufikiria, kampuni moja inatoa tangazo la kazi kwa vijana mtandaoni, tangaxo hilo Lina muda wa miezi mitatu, lakini tangazo hilo limetazamwa na viewers wapatao 35 tu kwa muda wote huo wa miezi mitatu, walati huo huo kuna habari ya udaku kwamba "Wema Sepetu Apata Bwana Mwingine Mpya", na habari hii imewekwa mtandaoni yapata masaa matatu yaliyopita, lakini ukiangalia idadi ya watazaji wa hanari unaona wapo viewers laki tatu ambao wamesoma hanari hiyo. Hii ni ajabu sana, hizi ndio akili walizonazo vijana wa Tz.
Wema Sepetu huko Instagram anaongoza kwa kuwa na followers wengi zaidi ya milioni kumi, ukijiuliza kikubwa au cha kujifunza kwa vijana hukioni...
 
Nyinyi vijana wa kipindi hicho mlifanya nini kwa nyakati zenu ambacho mnaweza jivunia leo
Wewe kwenu kama wazazi walizaliwa na kukulia kwenye umasikini ina maana na wewe ni lazima uwe masikini? Wewe huwezi kuvunja hiyo cycle ya umasikini kwenye familia yenu?
 
Back
Top Bottom